Chunga sana........ Fedha!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,900
21,987
Chunga sana........ Fedha!

Linapokuaja sula la fedha, kwa ndoa mpya wakati mwingine fedha ni kama mtungi wa gas ambao unasubiri kushika moto na kuwaka siku mambo yakiwa ovyo.
Kwenye ndoa linapokuwa suala la pesa mara nyingi mambo makubwa yanayotokea na kusababisha matatizo ni kufanya makosa yanayohusu pesa (maamuzi), bills kubwa (hasa nchi za magharibi) na madeni hasa banks.
Kwa mfano!
James na Jane (as usual) baada ya kuoana wakaamua kununua nyumba mpya kwa (mortgage), nunua fanicha mpya na vifaa vingine vya ndani kwa mkopo, wakaamua kuweka madirisha na milango mipya yote kwa kukopa pesa bank pia wakaamua kujenga garage mpya kwa ajili ya kuhifadhi gari lao na kuweka fence kuzunguka nyumba vyote kwa mkopo.

James anafanya kazi na mkewe Jane naye anafanya kazi na kutokana na plan zao kila kitu kilikuwa shwari ingawa ili kulipa kila kitu ilimpasa James kuongeza kazi siku za weekend na muda wa ziada kila jioni (parttime) pia ili kuhakikisha baada ya mapato yote angalau wanabakiwa na kiasi kidogo cha fedha bada ya kulipa bills zote na madeni ya bank.

James huondoka kazini saa kumi na mbili asubuhi na kurudi saa tano na nusu usiku siku saba kwa wiki miezi 12 kwa mwaka.
Jane naye anapata mimba na kuzaa mtoto na inampasa Jane kuacha kazi pia mtoto naye akaja na pressure zake za matumizi ya pesa.
Sasa kipato kimepungua na loans zipo palepale.

Mama yupo busy na mtoto na anachoka, pia kazi za pale nyumbani list haiishi na ukifika usiku analala bila hoi na baba ndo yupo busy na kazi kwani sasa inabidi ahangaike kuhakikisha bills zote zinalipwa, nyumba, fanicha, fence, garage nk.

Ukweli ni kwamba James anarudi nyumbani kwa ajili ya kuoga, kulala na kuvaa na kuondoka asubuhi kumi na mbili na kurudi usiku saa tano na nusu amechoka na anaishia kwenda pangoni.

Jane anajikuta mpweke na disconnected na mume wake James na hakuna mapenzi tena. Nyumba nzuri lakini haina raha na hawaifaidi kwa chochote kwani bila kufanya kazi hawezi kulipa madeni yote.

Kazi kubwa ambayo James anafanya ni kumtumikia pesa kwa nguvu zote, akili zote na mawazo yote ili kila kitu kiende, hatakiwi kuugua wala kuwa na likizo maana akikosa pesa vitu vyako vyote anapoteza kwani alinunua kwa mikopo.
Mapenzi hakuna, furaha hakuna, kupumzika hakuna na muda wa pamoja kama mke na mume hakuna kisa ni kuwa na pesa ili kulipa madeni yote na hatimaye mwisho wa mwezi ufike.
Tatizo si kutokuwa waaminifu kwa pesa zao bali ni mismanagement na maamuzi mabaya bila kufikiria mbali.

Kumbuka maisha tunaishi sasa na si baadae, mawazo kwamba tujifunge mkanda tutafaidi baadae kwanza tuwekeze inabidi kubalance kwani utafaidi kitu gani baada ya kuwa mzee, uzee ni wakati wa kutoa wosia kwa wajukuu.
Ua utafaidi kitu gani kama utapoteza mke au mume au familia ambayo kwako ni kitu cha thamani.
Issue hapa ni kuwa makini si kukopa bank ili uwe na vitu vya msingi katika maisha yako.
Issue ni kuwa na muda wa kazi, mume, mke au familia na kufurahia maisha.

Hivyo kabla ya kufanya jambo lolote fikiria kwa makini.
 
Back
Top Bottom