Chuki haitoruhusiwa kwenye hii thread jamani ! (Fulani) Tuachie Chama Chetu !!

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
1196144825_mbowe.jpg


Mbowe tuachie chama chetu
March 12, 2008



Baada ya yeye mwenyewe kukwepa vikwazo kadhaa vya kujibu hoja na mambo mengine anayoulizwa kwa njia ya mtandao au kwa simu za mkono kwa muda mrefu , sasa limekuja swala lingine nalo ni la yeye kufeli masomo yake katika chuo alichokuwa ameenda kujiendeleza .

Kufeli masomo sio kitu kipya hapa duniani au popote pale au kushindwa kitu chochote sio kitu kigeni lakini inategemeana umeshindwa au kuanguka kwa sababu zipi haswa , je kuanguka kwako kutaathiri vipi morani ya wale waliochini yako au unaotarajia kuongoza hapo mbeleni .

Na ndio hapo tunapokuja katika mada yenyewe ya jioni ya leo , habari zinazozidi kusambaa sasa hivi katika vyombo vya habari na duru zingine za habari zinasema kwamba Freeman Mbowe mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani chadema amefeli masomo yake ya chuo .

Kwa kuwa amefeli masomo ya chuo na amekuwa akifeli katika mambo mengine mengi katika uongozi wake ndani ya chadema basi ni vizuri sasa aachie ngazi hata katika chama aachie wale wengine wanaoweza kufanya mambo haya zaidi yake .

Kwa kuanza tu kati kati ya mwaka jana kulitokea vijana machachari katika chadema wakimshutumu mbowe binafsi kwa mambo mbali mbali yaliyochangia katika kukidhoofisha chama yeye kama mwenyekiti hakuwahi kutoa kauli yoyote kuhusu shutuma zile alikaa kimya kama vile hakuna kinachoendelea .

Shutuma zilizotolewa ni pamoja na ukabila ndani ya chama chenyewe pamoja na kuchaguana kwa kujuana bila usawa wowote ule , na sakata hili mpaka leo bado linaivuruga chadema na wanachama wake wengi haswa wale masikini wasiokuwa na uwezo wa kusema .

Katika harakati za uchaguzi wa kiteto napo mwenyekiti huyu ameshindwa kuonyesha cheche zozote badala yake wakashindwa kwa kishindo na baadaye akaja kufeli mitihani yake ya chuo .

Ushauri wangu ni kumuomba ndugu mbowe aachie ngazi katika chadema sasa akafanye mambo mengine naamini katika chadema wako watu wengi wenye uwezo kuliko yeye na waliowazalendo zaidi katika chama na nchi yao ya Tanzania kuliko yeye
 
KadaMpinzani,
Your choice for the title of this thread is not bad in my opinion.


Chuki haitoruhusiwa kwenye hii thread jamani ! (Fulani) Tuachie Chama Chetu !!
 
KadaMpinzani,
Your choice for the title of this thread is not bad in my opinion.

at least that was what i found to be great at the moment, maana wakianza kufurumuka utadhani wametumwa (kwa kushambulia)!
 
Usiwe defensive this much... hii ni sign ya weakness on your part!

diagnosis hizo umefanya wewe kama nani ??

sidhani kuwa defensive is a bad idea, is it ? l!

weakness za mbowe (anayeongelewa kwenye mada) nazo ni zipi since you are able to diagnose anyone ?
 
... kinachokosekana ni maudhuhi ya hii mada yako! Na ndio maana una ianzisha kwa kutojiamini "Chuki haitoruhusiwa kwenye hii thread!!" , maneno yako tu ni CHUKI sasa kwanini wachangiaji wengine wasiweke CHUKI?
 
na kama ulivyosema kufeli sio kitu kipya hapa duniani, so mi naona hata kwa mbowe si kitu kipya. Na tukisema tuanze kuchunguzana waliopasi ndo watuongoze nadhani watabaki wachache sana, coz hata hao kina makamba wanaowabuluza watanzania kwa uongozi mbovu elimu zao ni vichekesho kama si uharo...so think twice
 
katika sifa za kiongozi ndani ya katiba ya chadema hakuna mahali panaposema kiongozi akienda kujiendeleza sharti afaulu masomo.Aidha suala la kuachia chama ama kutoachia sharti lije kidemokrasia, na wakati wa uchaguzi ndani ya chadema haujawadia. Yamkini kuwachia chama chenu unamaanisha aache uanachama? bahati mbaya kwako na matamanio yako, kutofaulu masomo hakutambuliki ndani ya chadema kama sababu ya mwanachama kupoteza uanachama wake.
NB. kama mnashtuka sasa hivi kuhusu elimu yake na uwezo wake katika masomo, mmechelewa, mngeanzia kumwuliza mapema kabla ya kumpa dhamana ya uongozi; kidato cha sita alifaulu au aliangukia pua.
 
katika sifa za kiongozi ndani ya katiba ya chadema hakuna mahali panaposema kiongozi akienda kujiendeleza sharti afaulu masomo.Aidha suala la kuachia chama ama kutoachia sharti lije kidemokrasia, na wakati wa uchaguzi ndani ya chadema haujawadia. Yamkini kuwachia chama chenu unamaanisha aache uanachama? bahati mbaya kwako na matamanio yako, kutofaulu masomo hakutambuliki ndani ya chadema kama sababu ya mwanachama kupoteza uanachama wake.
NB. kama mnashtuka sasa hivi kuhusu elimu yake na uwezo wake katika masomo, mmechelewa, mngeanzia kumwuliza mapema kabla ya kumpa dhamana ya uongozi; kidato cha sita alifaulu au aliangukia pua.

Una hakika mkuu kuwa hiyo hoja imeandikwa na wana chadema?
 
katika sifa za kiongozi ndani ya katiba ya chadema hakuna mahali panaposema kiongozi akienda kujiendeleza sharti afaulu masomo.Aidha suala la kuachia chama ama kutoachia sharti lije kidemokrasia, na wakati wa uchaguzi ndani ya chadema haujawadia. Yamkini kuwachia chama chenu unamaanisha aache uanachama? bahati mbaya kwako na matamanio yako, kutofaulu masomo hakutambuliki ndani ya chadema kama sababu ya mwanachama kupoteza uanachama wake.
NB. kama mnashtuka sasa hivi kuhusu elimu yake na uwezo wake katika masomo, mmechelewa, mngeanzia kumwuliza mapema kabla ya kumpa dhamana ya uongozi; kidato cha sita alifaulu au aliangukia pua.

kwani unafikiri chadema wanamatatizo na mbowe?
matatizo yapo kwa CCM so kuandika wenyewe hii thread wanashindwa thats why wamemtumia mtu kufanya kibarua hiki...
 
MWAKRIKA WA KIKE KWANI ALIKWENDA KUSOMA WAPI?

Off all things I do... kufuatilia shule za watu wanazosoma sasa hivi ni jambo la mwisho kabisa kwenye list.

Samahani kama nitakudissapoint kwa kutojua kuwa Mbowe au wana JF kibao hapa wanasoma wapi sasa hivi. Mtoto wa Makamba ndiye alianzisha hii issue mwaka jana kwa kutumia watu email kibao kwenye hili jambo. Katika hili, wana ccm wana nafasi nzuri zaidi ya kujibu swali lako.
 
Off all things I do... kufuatilia shule za watu wanazosoma sasa hivi ni jambo la mwisho kabisa kwenye list.

Samahani kama nitakudissapoint kwa kutojua kuwa Mbowe au wana JF kibao hapa wanasoma wapi sasa hivi. Mtoto wa Makamba ndiye alianzisha hii issue mwaka jana kwa kutumia watu email kibao kwenye hili jambo. Katika hili, wana ccm wana nafasi nzuri zaidi ya kujibu swali lako.
NO KAMA HUJUI HUJUI HUWEZI UKATOA USICHO NACHO THANKS KWA KUJIBU KULINGANA NA KIWANGO CHAKO
 
Waridi, Mwafrika wa kike na wengine wote mnaojitahidi kumwelimisha Kada Mpinzani.........


Poleni kwa bidii zenu.,.!!!

Sidhani kama mnafahamu kuwa mnaongea na mtu aliyeko kazini. Ameajhiriwa huyu. Huwezi kuwa mtanznaia katika zama hizi bado ukatumia nguvu nyingi kama KM kuwashambulia watetezi wa nchi.

Mkakati wa cham cha mafisadi kuisambaratisha CHADEMA unafahamika kwa undani. Wanachofanya mafuisadi sasa ni kuondoa nguvu za CHADEMA. Kwanza wamekipa chama black brand ya ukabila, sasa wako kwenye mkakati wa kuwaondoa viongozi wanaowaogopa (wasionunulika wala kutishika na wenye ujuzi mkubwa wa siasa) mkakati wao unaofeli sana ni wa kuwaondoa vijana watafiti katika chama.

Mkakati huu unatekelezwa na jopo la wanamikakati wa CCM ambao wanalenga kuvitumia vyombo vya habari kwa wingi kuvuruga mshikamano wa wana-CHADEMA na pia kuwanyima CHADEMA kupanga mikakati yao bali wabakie kujibu tuhuma za magazetini na kuangaliana kwa jicho la husuda.

KM na wenzako mlioko katika ajira ya mafisadi: mnajulikana kwa kazi mnayofanya. Tumieni mbinu nzuri zaidi hii ya sasa ni ya kizamani mno!!!!!

Kamende
 
Waridi, Mwafrika wa kike na wengine wote mnaojitahidi kumwelimisha Kada Mpinzani.........


Poleni kwa bidii zenu.,.!!!

Sidhani kama mnafahamu kuwa mnaongea na mtu aliyeko kazini. Ameajhiriwa huyu. Huwezi kuwa mtanznaia katika zama hizi bado ukatumia nguvu nyingi kama KM kuwashambulia watetezi wa nchi.

Mkakati wa cham cha mafisadi kuisambaratisha CHADEMA unafahamika kwa undani. Wanachofanya mafuisadi sasa ni kuondoa nguvu za CHADEMA. Kwanza wamekipa chama black brand ya ukabila, sasa wako kwenye mkakati wa kuwaondoa viongozi wanaowaogopa (wasionunulika wala kutishika na wenye ujuzi mkubwa wa siasa) mkakati wao unaofeli sana ni wa kuwaondoa vijana watafiti katika chama.

Mkakati huu unatekelezwa na jopo la wanamikakati wa CCM ambao wanalenga kuvitumia vyombo vya habari kwa wingi kuvuruga mshikamano wa wana-CHADEMA na pia kuwanyima CHADEMA kupanga mikakati yao bali wabakie kujibu tuhuma za magazetini na kuangaliana kwa jicho la husuda.

KM na wenzako mlioko katika ajira ya mafisadi: mnajulikana kwa kazi mnayofanya. Tumieni mbinu nzuri zaidi hii ya sasa ni ya kizamani mno!!!!!

Kamende

Kamende umesikika loud and clear!

Haya yote yanajulikana yalikoanzia na thanks GOD huwa hayapewi bureki hata kidogo hapa JF.

Asante!
 
Back
Top Bottom