FRANK MICHAEL
Senior Member
- May 17, 2011
- 151
- 46
Kazi kubwa ya mbunge ni kuwaakilisha wananchi wake katika Bunge la jamuhuri ya muungano, mhimili mkuu wa demokrasia nchini ambalo kazi yake kuu ni kutunga sheria, kuisimamia serikali ikiwa ni pamoja na kuratibu mahusiano kati ya wananchi na serikali yao waliyoiweka madarakani kwa kuhakikisha kuwa serikali hiyo inatekeleza matakwa yao.
na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 iko wazi kwa jambo hili katika sehemu yake ya utangulizi kwamba misingi ya uhuru, haki, udugu, amani, tuliyojiwekea, yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye Demokrasia, ambayo serikali yake husimamiwa na bunge lenyewe, wajumbe waliochaguliwa wanawakilishwa (siyo serikali, bali) wananchi.''
kwa mantiki hii wananchi huchaguwa wale wachache bora (aristoi) wanaodhani wanaweza kuwakilisha vema katika kuisimamia Serikali (ya wananchi) waliyoiweka madarakani.
tena kwa mantiki hii"demokrasia" ni serikali ya watu ( wananchi) iliyowekwa madarakani na watu kwa ajili yam watu.
kwa tafsiri hii iliyo sahihi mbunge wa Simanjiro Mh Christopher OLesendeka, amepoteza uhalali wa kuitwa mbunge wa Simanjiro.
Tulivyokuwa kwenye Ziara ya katibu mkuu wa Chadema wilayani Simanjiro, tumejionea mambo mengi ya kushangaza na kuhuzunisha, tumezoea kuona watu wa kilalamikia kero za maji, migogoro ya ardhi, huduma duni za afya, elimu isiyo na viwango vya kuridhisha, ugumu wa maisha, na mambo mengine ya kawaida, lakini ya simanjiro yanashtua kidogo, watu azima wanachapwa viboko na wenyeviti wa vijiji vyao wakijaribu kuhoji masuala yanayohusu maslahi ya watawala hao wa Vijiji, hiyo kama haitoshi watu wanatishiwa kuhamishwa kama wakijarib kupingana na mawazo ya viongozi wa vijiji vyao, mimi nimezaliwa Simanjiro nikakulia Simanjiro nikasoma elimu yangu ya Msingi Simanjiro, lakini Ziara hii ya Katibu mkuu wa Chadema Mh Dr Willbord Slaa imenionyesha sura ya nyingine ya Simanjiro ambayo sikuwa naifahamu huko nyuma.
Naweza kusema Simanjiro haina Mbunge na wala siyo sehemu ya Tanzania.........
simanjiro ni Wilaya ya kwanza kuwa na Barabara mbovu.........
pamoja na na hali hii hatujaahi kumuonana mbunge wetu akilipigia kelele au akitokwa na mapovu mdomoni kama kama tulivyo mzoeya yanavyomtoka akiisifia CCM...........
Naweza kusema Simanjiro ni Sehemu inayongoza Tanzania kwa kuwa na watu wenye maisha duni pamoja na kuwa mungu ametujalia rasilimali nyingi hali wanasimanjiro bado ni mbaya na sijawahi kumuona Mbunge wangu akitokwa na mapovu mdomoni kuoji Tanzanite imebadilishaje maisha ya wanasimanjiro..........
Mh mbunge wangu sikuwahi kusikia ukipaza sauti yako hiyo kama ulivyokuwa ukiipaza juzi kijenge ukimnadi mgombea udiwani wa Kimandolu wa CCM kulalamikia uwonevu wanaofanyiwa wapigakura wako wa Simanjiro na wenyeviti wa Vijiji amoja na kwamba taarifa unazo.........
Mimi kama mmoja wa watu unawowangoza mpiga kura na mwananchi wa Wilaya ya Simanjiro, kwa kuzingatia haki yangu ya kikatiba ibara ya 18 (a) na (c) ninakutaka ujiuzulu mara moja kwa kushindwa kutambua majukumu yako ya kiungozi vyinginevyo tutaitisha mkutano wa Jimbo ya kukupigia kura ya kutokuwa na Imani na wewe!
na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 iko wazi kwa jambo hili katika sehemu yake ya utangulizi kwamba misingi ya uhuru, haki, udugu, amani, tuliyojiwekea, yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye Demokrasia, ambayo serikali yake husimamiwa na bunge lenyewe, wajumbe waliochaguliwa wanawakilishwa (siyo serikali, bali) wananchi.''
kwa mantiki hii wananchi huchaguwa wale wachache bora (aristoi) wanaodhani wanaweza kuwakilisha vema katika kuisimamia Serikali (ya wananchi) waliyoiweka madarakani.
tena kwa mantiki hii"demokrasia" ni serikali ya watu ( wananchi) iliyowekwa madarakani na watu kwa ajili yam watu.
kwa tafsiri hii iliyo sahihi mbunge wa Simanjiro Mh Christopher OLesendeka, amepoteza uhalali wa kuitwa mbunge wa Simanjiro.
Tulivyokuwa kwenye Ziara ya katibu mkuu wa Chadema wilayani Simanjiro, tumejionea mambo mengi ya kushangaza na kuhuzunisha, tumezoea kuona watu wa kilalamikia kero za maji, migogoro ya ardhi, huduma duni za afya, elimu isiyo na viwango vya kuridhisha, ugumu wa maisha, na mambo mengine ya kawaida, lakini ya simanjiro yanashtua kidogo, watu azima wanachapwa viboko na wenyeviti wa vijiji vyao wakijaribu kuhoji masuala yanayohusu maslahi ya watawala hao wa Vijiji, hiyo kama haitoshi watu wanatishiwa kuhamishwa kama wakijarib kupingana na mawazo ya viongozi wa vijiji vyao, mimi nimezaliwa Simanjiro nikakulia Simanjiro nikasoma elimu yangu ya Msingi Simanjiro, lakini Ziara hii ya Katibu mkuu wa Chadema Mh Dr Willbord Slaa imenionyesha sura ya nyingine ya Simanjiro ambayo sikuwa naifahamu huko nyuma.
Naweza kusema Simanjiro haina Mbunge na wala siyo sehemu ya Tanzania.........
simanjiro ni Wilaya ya kwanza kuwa na Barabara mbovu.........
pamoja na na hali hii hatujaahi kumuonana mbunge wetu akilipigia kelele au akitokwa na mapovu mdomoni kama kama tulivyo mzoeya yanavyomtoka akiisifia CCM...........
Naweza kusema Simanjiro ni Sehemu inayongoza Tanzania kwa kuwa na watu wenye maisha duni pamoja na kuwa mungu ametujalia rasilimali nyingi hali wanasimanjiro bado ni mbaya na sijawahi kumuona Mbunge wangu akitokwa na mapovu mdomoni kuoji Tanzanite imebadilishaje maisha ya wanasimanjiro..........
Mh mbunge wangu sikuwahi kusikia ukipaza sauti yako hiyo kama ulivyokuwa ukiipaza juzi kijenge ukimnadi mgombea udiwani wa Kimandolu wa CCM kulalamikia uwonevu wanaofanyiwa wapigakura wako wa Simanjiro na wenyeviti wa Vijiji amoja na kwamba taarifa unazo.........
Mimi kama mmoja wa watu unawowangoza mpiga kura na mwananchi wa Wilaya ya Simanjiro, kwa kuzingatia haki yangu ya kikatiba ibara ya 18 (a) na (c) ninakutaka ujiuzulu mara moja kwa kushindwa kutambua majukumu yako ya kiungozi vyinginevyo tutaitisha mkutano wa Jimbo ya kukupigia kura ya kutokuwa na Imani na wewe!