Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Tukio hilo limetokea uwanja wa ndege wakati msichana wa Kenya (aliyevaa sketi nyeusi katika picha) alijisogeza kwa Chris Brown ili aweze kupiga naye picha, maarufu kama 'Selfie'
Katika hali ambayo iliwashangaza watu walioshuhudia tukio hilo ikiwa pamoja na waandishi wa habari, Mwanamuziki huyo alichukuwa simu ya dada huyo akaitupa chini na kwenda kupanda gari iliyoandaliwa kwa ajili ya kumchukua
Habari inayoendelea hivi sasa kenya ni kuwepo kwa wito kwa wananchi kususia onyesho la Mwanamuziki huyo ikiwa na pamoja na kuzitaka mamlaka za nchi hiyo kumfukuza nchini humo Chris Brown kama zilivyofanya kwa Koffi Olomide miezi michache iliyopita.
Chanzo : Citizen Tv