Mkuu chopa inasaidia sna kwenye kulinda kura.Nakumbuka uchaguzi wa arumeru ccm walitaka kuchomeka kura lakini vijana walipowashtukia wakaanza kuwafukuza wao wakiwa na land cruiser na vijana wa cdm wakiwa na magari ya kawaida.Wakawapa taarifa watu wa chopa wakawa wanafukuza kwa juu manake inakuwa rahisi aloyeko juu kukuona hata ukienda wapi.Jamaa kuona hivyo wakaacha gari wakakimbia.inamaana ukizunguka na chopa angani utazuia wizi wa kura, acheni kutudanganya jamani??
Dah! Kura zinalindwa kwa Chopa! Only in Tanzania
Dah! Kura zinalindwa kwa Chopa! Only in Tanzania
Katika mchakato wa kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge unaoendelea mkoani Iringa katika jimbo la Kalenga.RPC wa mkoa huo Kamanda Mvungi ametoa onyo kwa CHADEMA kurusha chopa yao katika anga la mkoa huo siku ya uchaguzi yaani jumapili hii ya tar16.
Kauli ya Kamanda huyu inafuata baada ya kauli ya CHADEMA kuwa watatumia Chopa kulinda kura zao zisiibwe siku hiyo kama ilivyozoeleka kuwa CCM wamekuwa wakijihusisha na uwizi wa kura.
Kamanda Mvungi hakupaswa kutoa kauli hii,inaonesha dhahiri jeshi la polisi nchini lipo upabde fulani kisiasa na linatetea chama kilichopo madarakani,sidhani kama huwepo wa chopa angani unaathiri amani ya eneo husika,kwa namna hipi hasa?
Jeshi la polisi mnapaswa kufanya wajibu wenu na yale yanayowahusu ili kujenga imani kwa wananchi,hampaswi kujihusisha na siasa na ndio mana hata vitu flani hamruhusiwi mfano kujiunga na vyama vya wafanyakazi.
Polisi Tanzania tendeni kazi zenu kufuata misingi ya kazi zenu si kukengeuka.
Nafikiri kama helkopta haina uwezo wa kuzuia uibaji wa kura,basi waruhusiwe kutumia.inamaana ukizunguka na chopa angani utazuia wizi wa kura, acheni kutudanganya jamani??