commonmwananchi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 3,377
- 1,952
Mama Mheshimiwa Spika Anna Makinda,nikiwa raia mtanzania na mpenda ukweli,sina uhakika kama utapata wasaa au hata kama huwa unapata muda wa kupita ndani ya hii JF,ingawa nina uhakika huku si marafiki zako sana.
Naandika ili wewe na wengine ambao mnayo dhamana ya kuruhusu mchakato wa hizi kura za kutokuwa na imani na waziri mkuu uendelee kama taratibu zinazopaswa kufuatwa kihalali.hatua yoyote ile mtakayoichukua na kutumia rungu la chuma kuizuia aidha kwa kuahirisha bunge kabla ya jumatatu,basi mjue matokeo yake yanaweza kuwa historia ambayo ccm na serikali yake wataendelea kuijutia kwa muda mrefu sana.
Elewa watanzania wamechoka kuhangaika huku jasho lao likifaidiwa na wachache wasiostahili,tunapenda kuona haki ikitawala nchini bila fitna na ufisadi hu tunaouona.maamuzi yako mazuri ndio yatakaayoiokoa ccm na aibu hii,pia maamuzi yako mabaya ndio yatakayoimaliza ccm mbele ya umma wa watanzania wapenda haki nchini kote.
Nakuomba kupitia forum yetu pendwa JF mungu akubariki akurudishie busara na utende haki,tumeambiwa ulikuwa ukiteta na katibu mkuu ikulu Bw Sefue,hatujui kama alikuja kukushauri yenye wema au yenye maslahi kwa watu fulani.tunaomba mungu akuongoze kwa hili ututendee haki.
AMEN.
Naandika ili wewe na wengine ambao mnayo dhamana ya kuruhusu mchakato wa hizi kura za kutokuwa na imani na waziri mkuu uendelee kama taratibu zinazopaswa kufuatwa kihalali.hatua yoyote ile mtakayoichukua na kutumia rungu la chuma kuizuia aidha kwa kuahirisha bunge kabla ya jumatatu,basi mjue matokeo yake yanaweza kuwa historia ambayo ccm na serikali yake wataendelea kuijutia kwa muda mrefu sana.
Elewa watanzania wamechoka kuhangaika huku jasho lao likifaidiwa na wachache wasiostahili,tunapenda kuona haki ikitawala nchini bila fitna na ufisadi hu tunaouona.maamuzi yako mazuri ndio yatakaayoiokoa ccm na aibu hii,pia maamuzi yako mabaya ndio yatakayoimaliza ccm mbele ya umma wa watanzania wapenda haki nchini kote.
Nakuomba kupitia forum yetu pendwa JF mungu akubariki akurudishie busara na utende haki,tumeambiwa ulikuwa ukiteta na katibu mkuu ikulu Bw Sefue,hatujui kama alikuja kukushauri yenye wema au yenye maslahi kwa watu fulani.tunaomba mungu akuongoze kwa hili ututendee haki.
AMEN.