Chonde chonde Watanzania tuchukue tahadhari ya COVID 19 mikononi mwetu. Kumbe marehemu Idd alikuwa anafuatiliwa na Serikali na hakupatikana!

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Marehemu Idd nimethibitisha kuwa alikuwa akifuatiliwa na serikali kwa muda wa wiki mbili kwa kudaiwa kuonana na muathirika wa COVID 19 aliyetoka nje ya nchi. Cha ajabu marehemu alishindikana kupatikana mbali na kuwa alikuwa ndani ya jiji la Dar tena akifanya shughuli zake kama kawaida.

Marehemu kabla ya kufariki mwanzoni mwa wiki, wiki iliyopita siku ya alhamisi mchana alitinga ndani ya bohari kuu ya madawa MSD na kujinunulia sanitizer za kutosha kwa ajili ya kuzisambaza. Mbaya zaidi marehemu alikuwa akiugua mafua muda huo. (Tunaambiwa kuwa wafanyakazi wa MSD walioonana na marehemu tayari wametengwa lakini ni baada ya kusambaa taarifa za kifo cha Idd)

Weekend yote kabla ya kuzidiwa siku ya jumapili usiku Idd alikuwa akila bata kwenye baa kadhaa ndani ya viunga vya Tabata, pia tayari alishapita zahanati kutokana na mafua yaliyokuwa yakimkabili.

Idd alipelekwa Aghakan akiwa kazidiwa na ndipo alipopimwa Corona na kukutwa positive. Wakati taarifa zake zinapelekwa serikalini ili ahamishwe ndipo serikali nayo ikagutuka eti walikuwa wakimfuatilia! Too late!

Tukicheza tutaisha! Serikali inaonyesha udhaifu mkubwa. Mtu katoroka karantini kaenda kukamatwa Iringa tena akiwa ameshaishi na wenyeji siku zaidi ya nne! Huko Mbeya watu 80 wametoroka South Afrika wameingia mpaka katikati ya jiji kwa basi ndipo wanagutuka! Chonde chonde. Serikali lazima izibe mipaka kati ya mikoa na ile ya kimataifa! Tusijifanye hamnazo! Tutajimaliza aslani!
 
hatari kwa hao wenye visukari na mapresha kwa sababu ndio wao wenye mamlaka .....
 
Watu wenyewe ni wabishi na tunajifanya tunajua sana na hata tukiambiwa tuchukue tahadhari hatufanyi hivyo ina kuwa taabu sana maana tupo milioni 50.
 
Idadi kubwa ya maambukizi itakaporipuka ndipo wabongo tutajua huu ugonjwa ni balaa! Ukipita sehemu za starehe, vijiweni, kwenye chombo vya usafiri n. k watu wanajazana kama kumbikumbi hata hatujal, kama taarifa hizo ni za kweli tutakufa kama nzige kwa kuto kujali kwetu na kuchukulia poa kila kitu! Nchi zilizo kwenye maambukizi makubwa zilikuwa hivihivi sasa hivi ni majuto na vilio lakini hatujifunzi!!.
 
hapo kwenye kuturoka ndio pameniacha midomo wazi, yaani mtu mmoja wa kawaida anaitoroka serikali serikali inayojigamba ina magari ina mafuta ina bunduki ina wafanyakazi...ina rasilimali zote.

Hata kama wamepokea rushwa kutoka kwa huyo mtuhumiwa ...je hiyo rushwa inawasaidia sana hadi msababishe watanzania milioni 50 wafe kabisa?. hata huyo aliyetoroka ana nia mbaya na ndugu zake pamoja na tanzania nzima ni muuaji.

ingekuwa ni mimi ningemuweka karantini alindwe na jeshi alafu akipimwa corona akagundulika hana nitampeleka gerezani akalime
 
hapo kwenye kuturoka ndio pameniacha midomo wazi, yaani mtu mmoja wa kawaida anaitoroka serikali serikali inayojigamba ina magari ina mafuta ina bunduki ina wafanyakazi...ina rasilimali zote. Hata kama wamepokea rushwa kutoka kwa huyo mtuhumiwa ...je hiyo rushwa inawasaidia sana hadi msababishe watanzania milioni 50 wafe kabisa?. hata huyo aliyetoroka ana nia mbaya na ndugu zake pamoja na tanzania nzima ni muuaji
ingekuwa ni mimi ningemuweka karantini alindwe na jeshi alafu akipimwa corona akagundulika hana nitampeleka gerezani akalime
Hivyoulivyotaja vinawaona chadema ila sio mgonjwa wa corona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka waambiwe chadema wanasambaza Corona ndiyo watachukua hatua, nakumbuka slow slow alisema Corona ni CHADEMA
 
Huku kwetu wanasema huu ugonjwa ni wa matajiri.
Sisi hohehahe hauwezi kutushika.
 
Back
Top Bottom