Chonde Chonde Serikali tupieni upesi ' Jicho lake Kali ' katika huu ' Usanii ' wa uwekezaji wa GSM, Sevilla na la Liga kwa Klabu ya Yanga

Tuache tuache tuache we simba damu tunakujua huwezi kutusumbua na story zako za kuunga unga

Waulize simba na mo wenu kulikuwa na haja ya kuajiri CEO kutoka south wakati kuna madogo kibao wanaiweza hiyo position

Tuache na yanga yetu
 
GSM anataka au anadhani Sisi Wanayanga wote ni Mangumbaru ( Wajinga ) na Mapopoma ( Wapumbavu ) wakati kumbe wenye Akili tupo wengi.
wewe siku zote mbona huwa unajitanabaisha kuwa ni mwana Mbumbumbu SC kindakindaki?
au umetishika na hii mikwara ya Vyura FC nini??
 
Mna
Hapo ID yangu hii ilikuwa ' Hacked ' na Watu wabaya, ila kwa sasa ndiyo ninayo Mimi GENTAMYCINE Mwanayanga ' Kindakindaki ' kabisa Mkuu!!!
[/QUOTMnaMnafiki mkubwa wee sijui unafaidika na nn kwa unafiki wa kujifanya mwana yanga fake
 
Tulia wewe mkuu tunahitaji yanga mpya mimi binafsi sijaona tatizo muacheni GSM afanye manuva kwa manufaa ya klabu na wanachama tumechoka kutembeza mabakuli na kudharauliwa wanajangwani wenzangu ni heri tumshukuru mungu kwa kutufikisha mpaka hapa haina ya kulaumu uongozi wadau
 
Kwani MO keshatoa BIL 20 ALIZOWAAHIDI " TAKO MOKO" FC? Yana waachie yanga pambana na Gabacholi wenu!

Inasemekana ameshatoa kwani ndiyo maana Wachezaji wetu Yanga FC wanaongoza ' Kuwapiga Mizinga ' Wachezaji ' Matajiri ' wa Simba SC Mkuu.
 
Nikiwa kama Mwanachama wa Klabu ya Yanga mwenye Kadi ambayo Namba yake haina ulazima wowote ule kwa Wewe Kuijua naomba niwe wa Kwanza kuiomba Serikali makini inayoongozwa na ' Jemedari ' Rais Dkt. Magufuli kupitia Vyombo vyake ' Nyeti ' kabisa vitupie Macho katika hiki kinachoitwa ni ' Mchakato ' wa Kuipeleka Yanga SC yetu katika Mabadiliko na Mafanikio.

Kwa nilichokiona tu jana pale Serena Hotel nilijua nitaona mambo yenye Kuakisi kabisa yale Mafanikio ambayo ' Muhamasishaji ' wetu Antonio Nugaz alikuwa ' akituhubiria ' kwa Wiki nzima, lakini badala yake nilichokuja Kukiona ni harufu ya ' Usamjo Usamjo ' nikimaanisha ' Uwongo Uwongo / Utapeli Utapeli ' unaotaka kufanywa na huyu ' Tajiri ' wa sasa Gharib Said Mohammed ( GSM )

Tunaambiwa sijui La Liga mara tena Klabu ya Sevilla na hapo hapo tena GSM nao wanahusishwa yaani ni ' Kutuchanganya ' tu Sisi Wanayanga na Wanachama wa Yanga SC ambao ni kwa bahati mbaya mno wengi wetu hata uwezo Wetu tu wa Kupambanua mambo ni mdogo na siyo kama Wanachama wa Simba SC na Mashabiki zao ambao wengi Wao ' wamebarikiwa ' sana Akili ( IQ ) na Mungu.

Hivi Klabu yangu ya Yanga ina ulazima wowote ule wa Kumtafuta ' Consultant ' wa Kuleta Mabadiliko Yanga SC kutokea nchini Hispania ( Spain ) wakati hapa hapa Kwetu nchini Tanzania kuna ' Consultancies Firms ' nyingi tu ambazo zingeweza Kuisaidia Klabu yetu ya Yanga tena kwa Gharama nafuu kabisa na Pesa zingine zingesaida Kulipa Madeni ambayo yanaikabili Klabu yetu?

Na ni kwanini kama Jambo ni la Yanga SC yetu lakini anayeonekana kila mara akiwa ' mbele mbele ' na ' Kiherehere ' ni huyu GSM tu pekee lakini Viongozi Wetu wa Yanga SC ni kama vile ama nao ' Wameshatekwa ' na GSM au hawana tena Sauti kutokana na ' Njaa ' zao na Kutokujiamini Kwao? Nayasema haya kwa Uchungu kabisa kwani GENTAMYCINE sitaki Yanga SC yangu ipotee.

Nilitegemea katika Hafla ya pale Serena Hotel basi nami ningeuona kweli huo ' Uwakilishi ' wa unaoitwa ' Utatu ' wa akina GSM, La Liga na Klabu ya Sevilla ila niliona tu ' Muwakilishi ' asiye na Uzito wowote ule kutokea huko Hispania ( Spain ) huku Wanachana na Wanayanga ' tukidanganywa ' kama Watoto Wadogo tukiwa na Mwanachama Mwenzetu Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete.

Anachokifanya huyu ' Tajiri ' GSM ni kutaka ' Kutuzuga ' tu Sisi Wanayanga hasa baada ya Kutusoma ' Upopoma ' wetu uliotutukuka kujifanya anatutengenezea Mtandao mkubwa wa Mabadiliko na Mafanaikio Sisi Wanayanga ili atuteke Akili kisha baadae aje kuwa ' Main Bidder ' katika ' Uwekezaji ' na baadae aichukue Yanga SC na aanze ' Kujitajirisha ' nayo Kikubwa sana.

Wanayanga hatujaambiwa huu ' Mchakato ' wa GSM, La Liga na Klabu ya Sevilla una Manufaa gani kwa Klabu yetu ya Yanga hasa Kiuchumi, Kimfumo, Kibishara, Kimchezo na Kiuwekezaji kabisa badala yake GSM imetafuta tu Waandishi wa Habari kadhaa ili waendelee ' Kutuhadaa ' Sisi Wanayanga na hatimaye ' Waaminike ' na ' Waiteke ' rasmi Yanga SC na tuje Kujuta rasmi.

Rais wangu Ndugu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Waziri husika Dkt. Mwakyembe, Baraza la Michezo Tanzania, TAKUKURU na hata Watu wa TISS tafadhali msikae mbali na hili linalofanywa na hii Klabu yangu ninayoipenda ya Yanga kwani kuna kila harufu ya ' Upigwaji ' hapa na tusisahau pia kuwa kwa sasa Hispania ndiyo Lango Kuu ya Biashara za Dawa za Kulevya na ni ' Wabaguzi ' Wakuu pia duniani.

Kwa hili kama Wanachama Wenzangu wa Yanga SC msiponielewa naihama Yanga SC na nahamia rasmi ama Azam FC au kule Biashara Mara FC.
Kwanza ww sio Yanga na kama ni mwanchama wa Yanga ww ndio huna iQ
 
Huyu jamaa ni bonge ya jinga fulani, lakini yeye mwenyewe anajiona anauwezo sana, na ukiangalia hizo comment ni kama vile anatumia ID nyinginyingi anajijibu yeye mwenyewe
 
Tuache tuache tuache we simba damu tunakujua huwezi kutusumbua na story zako za kuunga unga

Waulize simba na mo wenu kulikuwa na haja ya kuajiri CEO kutoka south wakati kuna madogo kibao wanaiweza hiyo position

Tuache na yanga yetu

Tanzania ina ' CEO's ' wa Kuendesha mambo mengine tu, ila haina ' CEO's' wa Kuendesha na Kusimamia Mambo ya Mpira. Tuwapongeze Simba SC.
 
wewe siku zote mbona huwa unajitanabaisha kuwa ni mwana Mbumbumbu SC kindakindaki?
au umetishika na hii mikwara ya Vyura FC nini??

Ni lini Mimi GENTAMYCINE nimejitambulisha hapa kuwa ni Mwana Simba SC Mkuu? Hivi kuna JF Member asiyejua kuwa Mimi ni Mwana Yanga SC?
 
Mleta maada akili yako ndogo sana niliwahi kukwambia ukachukia vijana kama nyie mtafanya taifa hili liwe maskini sana,unajua nn kuhusu GSM akili za hivi na mawazo kama yako ndio yamefanya Mo apewe asilimia 49 za hisa wakati wanachama wa simba hawafikishi hata asilimia 22 za hisa zilizobaki.Kumuhusisha raisi na hili niujinga kabisha ww kama una hofu chukua hatu kama kijana nenda TFF au uongozi wa yanga fatilia zaidi ujue nn kinaendelea sio majungu tu dah inasikitisha sana.

Akili yangu ni ndogo kwakuwa nimesema tu ukweli wa ' Kuwashtua ' wana Yanga SC Wenzangu kuwa GSM anaenda ' Kutupiga ' Yanga SC yetu au?
 
Hata mi nimejiuliza huyu jamaa aliyeleta hii habari si mwana simba huyu au ndo muendelezo wa unafiki kama jadi ya waTZ

Ni lini GENTAMYCINE " Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer " amewahi Kujinasibu hapa kuwa ni Mwana Yanga SC?
 
Kwanza ww sio Yanga na kama ni mwanchama wa Yanga ww ndio huna iQ

Futa Kauli yako upesi sana vinginevyo wale ' Waganga ' wote mliowatumia kwa Kuwafunga Simba SC tarehe 8 nawapa Simba SC wawatumie hasa.
 
Huyu jamaa ni bonge ya jinga fulani, lakini yeye mwenyewe anajiona anauwezo sana, na ukiangalia hizo comment ni kama vile anatumia ID nyinginyingi anajijibu yeye mwenyewe

Ungebahatika tu au hata Ukoo wako wote wa Kuume na Kikeni kuwa na angalau hata 5% ya IQ yangu mngeringa na kutamba ila hamjapewa wote.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom