MgungaMiba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2011
- 999
- 815
Bw Rajabu ni kada mzuri wa CCM hapa Igunga, anajihusisha na huduma za Kompyuta akishirikiana na Mke wake. Kipindi hiki cha kampeni, alijitolea kumruhusu Mkewe kipenzi awemo kwenye msafara wa kampeni za CCM zinazoongozwa na Ndg Mwigullu Nchemba, mkewe huyo alikuwa akijihusisha zaidi na huduma za kompyuta katika msafara huo. Kumbe Mwigullu kwa kukosa uadilifu kwake alikuwa akimmezea mate Mke huyo wa kada mwenzake, na bila kujali hisani ya Bw Rajabu, na kwa kutumia ukubwa wake, bila haya wala tone la aibu, akaanza kumpiga miti mke wa mwenzie! Vijana wa Igunga waliomo kwenye convoy hilo walikerwa sana na mchezo huo wa mkuu huyo wa kampeni, kwani pia alikuwa ni Mke wa mwenzao, hivyo walikwenda kumtonya Rajabu wakati Mwigullu akiwa katikati ya Mselebuko, ndipo Rajabu alipokwenda na kumfumania Mwigullu Live bila chenga, tena kavu bila Kinga! Rajabu kwa hasira na uchungu alianza kumpa kipondo cha nguvu Mkewe hadi kumjeruhi vibaya, wakati akifanya hivyo, Mwigullu alipata mwanya wa kukurupuka na kujinusuru akiwa na nguo zake mkononi. Mke huyo kutokana na majeraha aliyopata ilibidi akapate Form ya Polisi (PF3) ndio akatibiwe, na ile haitolewi bila maelezo. Hali imeshakuwa mbaya ndani ya kambi ya Kampeni ya CCM, imebidi wakuu wa chama walimalize kiaina ili kunusuru hali. Yamezimwa lakini Rajabu bado moyo unamuuma, ingekuwa busara zaidi kwa wakuu wa CCM wakamuondoa Mwigullu kwa kisingizio chochote ili kupunguza harufu mbaya aliyoileta. Kama hawamuondoi Mwigullu kwenye kampeni za Igunga, basi tutasaidiana na Rajabu tukamshitaki kwa Mungu, hata ikibidi kumsomea Albadiri ili alaaniwe na Mungu, na hakika laana aliyoileta Mwigullu kwa CCM itaonekana dhahiri tar 2/10/2011.