Chonde chonde CHADEMA, wasameheni wabunge wenu 19 wa viti maalumu kwa maslahi ya chama na taifa

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Jan 26, 2020
3,674
11,585
Wakati wa utawala wa dola ya Rumi, adhabu ya kusulubiwa msalabani ilikuwa ni adhabu kwa ajili ya wahalifu sugu, watu kama wauaji, majambazi na wahaini. Ilikuwa adhabu ya kudhalilisha, ya kikatili na iliyo hakikisha mateso makuu kabla ya kifo. Mtu aliye tundikwa msalabani alikuwa anaomba afe haraka ili kusitisha maumivu makali aliyokuwa anayapitia.

"Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui walitendalo", hii ilikuwa ni kauli ya Yesu Kristo mwana wa Mungu, mara baada ya kuwa ametundikwa msalabani na askari wa Rumi. Pamoja na ukatili wa hali ya juu waliokuwa wanamtendea, lakini bado aliwaombea kwa Mungu wasamehewe.

Kusamehe ni lango kuu la kuponya maumivu na mifarakano katika jamii yoyote ile, na ndio maana Yesu alifundisha umuhimu wa kusamehe tena na tena, na hata kuonesha kwa mfano pale alipowasamehe na kuwaombea msamaha wale waliomtendea uovu.

Nichukue nafasi hii kuuomba uongozi wa CHADEMA, wasameheni wabunge 19 wa viti maalum, najua 'usaliti' walioufanya umewaumiza sana ukizingatia mateso mliyoyapitia kutoka kwa mwendazake, vituko vya uchaguzi wa mwaka 2020 na hata mateso mnayoyapitia leo hii baada ya mwendazake kunyakuliwa.

Baada ya kifo cha JPM, ni vema nchi nzima tufungue ukurasa mpya ili tuweze kusongo mbele. Nawashauri CDM wapeni adhabu ya kuwavua nyadhifa za uongozi ndani ya chama lakini waacheni wawe wanachama wenu na muwape baraka zote kuwepo bungeni.

Wabunge wale 19 wamekuwa kama watoto yatima, hawawezi kutoa hoja kali bungeni kwakuwa hawana support ya chama chao, uwepo wao ni kwa fadhila za Ndugai, hivyo basi wanalazimika kuwa wapole wasimuudhi kwani anaweza kuwafukuza muda wowote kwa kigezo kuwa amepokea barua ya CDM ya kuwavua uanachama.

Kwenye kuliponya taifa hata ninyi CDM mnao wajibu wa kukiponya chama chenu. Tunaponya majereha kwa kusameheana na kushikamana zaidi, na sio kuwindana na kutesana.

Najua ndani ya CMD kuna watu wana itikadi kali (extremists), hawa wapo kwenye vyama vyote. Msikubali ushauri wao wa kuendelea kutowatambua wabunge wale, that is extreme! Si mmeshuhudia kilichoipata nchi yetu baada ya CCM kumpa nchi 'extremist' mwaka 2015?. Kaeni mbali na ma extremists.

Lakini pia, nanyi wabunge 19, kuweni wapole, tafuteni suluhu na chama chenu, ninyi ni watoto wa CDM, mmekosea lakini mtabaki kuwa watoto wa CDM. Nendeni ukonga mkamtembelee mwenyekiti wenu kule mahabusu, muanze kutafuta njia za kuyatibu majeraha ya siasa za chuki zilizopandwa na mwendazake.

Kuliponya taifa sio kazi ya SSH peke yake, kila mtu kwa nafasi yake aangalie namna ya kuboresha na kurekebisha palipo vurugwa na siasa zile za chuki.
 
Wakati wa utawala wa dola ya Rumi, adhabu ya kusulubiwa msalabani ilikuwa ni adhabu kwa ajili ya wahalifu sugu, watu kama wauaji, majambazi na wahaini. Ilikuwa adhabu ya kudhalilisha, ya kikatili na iliyo hakikisha mateso makuu kabla ya kifo. Mtu aliye tundikwa msalabani alikuwa anaomba afe haraka ili kusitisha maumivu makali aliyokuwa anayapitia.

"Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui walitendalo", hii ilikuwa ni kauli ya Yesu Kristo mwana wa Mungu, mara baada ya kuwa ametundikwa msalabani na askari wa Rumi. Pamoja na ukatili wa hali ya juu waliokuwa wanamtendea, lakini bado aliwaombea kwa Mungu wasamehewe.

Kusamehe ni lango kuu la kuponya maumivu na mifarakano katika jamii yoyote ile, na ndio maana Yesu alifundisha umuhimu wa kusamehe tena na tena, na hata kuonesha kwa mfano pale alipowasamehe na kuwaombea msamaha wale waliomtendea uovu.

Nichukue nafasi hii kuuomba uongozi wa CHADEMA, wasameheni wabunge 19 wa viti maalum, najua 'usaliti' walioufanya umewaumiza sana ukizingatia mateso mliyoyapitia kutoka kwa mwendazake, vituko vya uchaguzi wa mwaka 2020 na hata mateso mnayoyapitia leo hii baada ya mwendazake kunyakuliwa.

Baada ya kifo cha JPM, ni vema nchi nzima tufungue ukurasa mpya ili tuweze kusongo mbele. Nawashauri CDM wapeni adhabu ya kuwavua nyadhifa za uongozi ndani ya chama lakini waacheni wawe wanachama wenu na muwape baraka zote kuwepo bungeni.

Wabunge wale 19 wamekuwa kama watoto yatima, hawawezi kutoa hoja kali bungeni kwakuwa hawana support ya chama chao, uwepo wao ni kwa fadhila za Ndugai, hivyo basi wanalazimika kuwa wapole wasimuudhi kwani anaweza kuwafukuza muda wowote kwa kigezo kuwa amepokea barua ya CDM ya kuwavua uanachama.

Kwenye kuliponya taifa hata ninyi CDM mnao wajibu wa kukiponya chama chenu. Tunaponya majereha kwa kusameheana na kushikamana zaidi, na sio kuwindana na kutesana.

Najua ndani ya CMD kuna watu wana itikadi kali (extremists), hawa wapo kwenye vyama vyote. Msikubali ushauri wao wa kuendelea kutowatambua wabunge wale, that is extreme! Si mmeshuhudia kilichoipata nchi yetu baada ya CCM kumpa nchi 'extremist' mwaka 2015?. Kaeni mbali na ma extremists.

Lakini pia, nanyi wabunge 19, kuweni wapole, tafuteni suluhu na chama chenu, ninyi ni watoto wa CDM, mmekosea lakini mtabaki kuwa watoto wa CDM. Nendeni ukonga mkamtembelee mwenyekiti wenu kule mahabusu, muanze kutafuta njia za kuyatibu majeraha ya siasa za chuki zilizopandwa na mwendazake.

Kuliponya taifa sio kazi ya SSH peke yake, kila mtu kwa nafasi yake aangalie namna ya kuboresha na kurekebisha palipo vurugwa na siasa zile za chuki.
Rubbish.
 
Ww unaesema leo wasamehewe ndio ww utakaekuja kuwacheka Chadema baada ya kuwasamehe
Hakutakuwa na jambo la kucheka. CCM pamoja na utopolo wao lakini hua wanajitahidi kukiweka chama pamoja kwa kuwasamehe wanachama wake. Wale wabunge 19 wana faida zaidi wakiwa CDM kuliko kuwa nje ya chama.
 
Hakutakuwa na jambo la kucheka. CCM pamoja na utopolo wao lakini hua wanajitahidi kukiweka chama pamoja kwa kuwasamehe wanachama wake. Wale wabunge 19 wana faida zaidi wakiwa CDM kuliko kuwa nje ya chama.
Sera ya Chadema ni tofauti na Chama tawala, hao wanaosamehewa huwa ni useless wanarudi ccm coz huwa hawana pakwenda
 
Wana kiburi sana wacha tuwaone
Hawapaswi kushupaza shingo, wafanye diplomasia chinichini wayajenge na chama chao. Ni ngumu sana ku survive ukiwa nje ya chama. Lakini CDM ni vizuri ikiwa na sauti bungeni hata kama ni kidogo tu, kwa maslahi ya taifa.

Wabunge wa CCM hawasomi chochote kinachopelekwa pale, mwisho wa siku wanaumia watanzania.
 
Sera ya Chadema ni tofauti na Chama tawala, hao wanaosamehewa huwa ni useless wanarudi ccm coz huwa hawana pakwenda
Hii miaka 4 tukienda bila sauiti ya CDM pale bungeni basi wananchi wahesabu maumivu tu, wabunge wa CDM ndiyo wanaosoma kinachopelekwa pale na kuibua hoja, CDM iwatumie hawa 19 kwa maslahi ya nchi.

Ndugu zetu wa CCM wao ni wazee wa kupigapiga meza na kuunga mkono hoja.
 
Wakati wa utawala wa dola ya Rumi, adhabu ya kusulubiwa msalabani ilikuwa ni adhabu kwa ajili ya wahalifu sugu, watu kama wauaji, majambazi na wahaini. Ilikuwa adhabu ya kudhalilisha, ya kikatili na iliyo hakikisha mateso makuu kabla ya kifo. Mtu aliye tundikwa msalabani alikuwa anaomba afe haraka ili kusitisha maumivu makali aliyokuwa anayapitia.

"Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui walitendalo", hii ilikuwa ni kauli ya Yesu Kristo mwana wa Mungu, mara baada ya kuwa ametundikwa msalabani na askari wa Rumi. Pamoja na ukatili wa hali ya juu waliokuwa wanamtendea, lakini bado aliwaombea kwa Mungu wasamehewe.

Kusamehe ni lango kuu la kuponya maumivu na mifarakano katika jamii yoyote ile, na ndio maana Yesu alifundisha umuhimu wa kusamehe tena na tena, na hata kuonesha kwa mfano pale alipowasamehe na kuwaombea msamaha wale waliomtendea uovu.

Nichukue nafasi hii kuuomba uongozi wa CHADEMA, wasameheni wabunge 19 wa viti maalum, najua 'usaliti' walioufanya umewaumiza sana ukizingatia mateso mliyoyapitia kutoka kwa mwendazake, vituko vya uchaguzi wa mwaka 2020 na hata mateso mnayoyapitia leo hii baada ya mwendazake kunyakuliwa.

Baada ya kifo cha JPM, ni vema nchi nzima tufungue ukurasa mpya ili tuweze kusongo mbele. Nawashauri CDM wapeni adhabu ya kuwavua nyadhifa za uongozi ndani ya chama lakini waacheni wawe wanachama wenu na muwape baraka zote kuwepo bungeni.

Wabunge wale 19 wamekuwa kama watoto yatima, hawawezi kutoa hoja kali bungeni kwakuwa hawana support ya chama chao, uwepo wao ni kwa fadhila za Ndugai, hivyo basi wanalazimika kuwa wapole wasimuudhi kwani anaweza kuwafukuza muda wowote kwa kigezo kuwa amepokea barua ya CDM ya kuwavua uanachama.

Kwenye kuliponya taifa hata ninyi CDM mnao wajibu wa kukiponya chama chenu. Tunaponya majereha kwa kusameheana na kushikamana zaidi, na sio kuwindana na kutesana.

Najua ndani ya CMD kuna watu wana itikadi kali (extremists), hawa wapo kwenye vyama vyote. Msikubali ushauri wao wa kuendelea kutowatambua wabunge wale, that is extreme! Si mmeshuhudia kilichoipata nchi yetu baada ya CCM kumpa nchi 'extremist' mwaka 2015?. Kaeni mbali na ma extremists.

Lakini pia, nanyi wabunge 19, kuweni wapole, tafuteni suluhu na chama chenu, ninyi ni watoto wa CDM, mmekosea lakini mtabaki kuwa watoto wa CDM. Nendeni ukonga mkamtembelee mwenyekiti wenu kule mahabusu, muanze kutafuta njia za kuyatibu majeraha ya siasa za chuki zilizopandwa na mwendazake.

Kuliponya taifa sio kazi ya SSH peke yake, kila mtu kwa nafasi yake aangalie namna ya kuboresha na kurekebisha palipo vurugwa na siasa zile za chuki.
Wao wajiuzulu ubunge kwanza halafu waombe msamaha. Msamaha hutolewa kwa anayeomba.
 
Wajiuzulu kwanza ubunge wa fadhila.

Then kama Chama kitakuwa na sababu za kuwasamehe its okay.
Viongozi wa chama walio 'moderate' hawawezi kudai hatua kali kiasi hicho.

What is the alternative? wabaki na ubunge wao wa fadhila na CDM inabaki bila sauti yoyote bungeni.

Hasara anaipata mtanzania na nchi kwa ujumla. Ni wajibu wa CDM kuweka maslahi ya taifa mbele kuliko ya chama.
 
Wakati wa utawala wa dola ya Rumi, adhabu ya kusulubiwa msalabani ilikuwa ni adhabu kwa ajili ya wahalifu sugu, watu kama wauaji, majambazi na wahaini. Ilikuwa adhabu ya kudhalilisha, ya kikatili na iliyo hakikisha mateso makuu kabla ya kifo. Mtu aliye tundikwa msalabani alikuwa anaomba afe haraka ili kusitisha maumivu makali aliyokuwa anayapitia.

"Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui walitendalo", hii ilikuwa ni kauli ya Yesu Kristo mwana wa Mungu, mara baada ya kuwa ametundikwa msalabani na askari wa Rumi. Pamoja na ukatili wa hali ya juu waliokuwa wanamtendea, lakini bado aliwaombea kwa Mungu wasamehewe.

Kusamehe ni lango kuu la kuponya maumivu na mifarakano katika jamii yoyote ile, na ndio maana Yesu alifundisha umuhimu wa kusamehe tena na tena, na hata kuonesha kwa mfano pale alipowasamehe na kuwaombea msamaha wale waliomtendea uovu.

Nichukue nafasi hii kuuomba uongozi wa CHADEMA, wasameheni wabunge 19 wa viti maalum, najua 'usaliti' walioufanya umewaumiza sana ukizingatia mateso mliyoyapitia kutoka kwa mwendazake, vituko vya uchaguzi wa mwaka 2020 na hata mateso mnayoyapitia leo hii baada ya mwendazake kunyakuliwa.

Baada ya kifo cha JPM, ni vema nchi nzima tufungue ukurasa mpya ili tuweze kusongo mbele. Nawashauri CDM wapeni adhabu ya kuwavua nyadhifa za uongozi ndani ya chama lakini waacheni wawe wanachama wenu na muwape baraka zote kuwepo bungeni.

Wabunge wale 19 wamekuwa kama watoto yatima, hawawezi kutoa hoja kali bungeni kwakuwa hawana support ya chama chao, uwepo wao ni kwa fadhila za Ndugai, hivyo basi wanalazimika kuwa wapole wasimuudhi kwani anaweza kuwafukuza muda wowote kwa kigezo kuwa amepokea barua ya CDM ya kuwavua uanachama.

Kwenye kuliponya taifa hata ninyi CDM mnao wajibu wa kukiponya chama chenu. Tunaponya majereha kwa kusameheana na kushikamana zaidi, na sio kuwindana na kutesana.

Najua ndani ya CMD kuna watu wana itikadi kali (extremists), hawa wapo kwenye vyama vyote. Msikubali ushauri wao wa kuendelea kutowatambua wabunge wale, that is extreme! Si mmeshuhudia kilichoipata nchi yetu baada ya CCM kumpa nchi 'extremist' mwaka 2015?. Kaeni mbali na ma extremists.

Lakini pia, nanyi wabunge 19, kuweni wapole, tafuteni suluhu na chama chenu, ninyi ni watoto wa CDM, mmekosea lakini mtabaki kuwa watoto wa CDM. Nendeni ukonga mkamtembelee mwenyekiti wenu kule mahabusu, muanze kutafuta njia za kuyatibu majeraha ya siasa za chuki zilizopandwa na mwendazake.

Kuliponya taifa sio kazi ya SSH peke yake, kila mtu kwa nafasi yake aangalie namna ya kuboresha na kurekebisha palipo vurugwa na siasa zile za chuki.
Katika mapambano yoyote yale, waheshimu wanaokuponda maana wanakupa motisha, ila kaa mbali na wanaokurudisha kwa kudhoofisha harakati zako au kuuza siri zako.

Kina Mdee walikuwa recruited fresh from chuo, wakanolewa, wakalelewa na chama. Ila kwa tamaa binafsi wakasaliti chama. Binafsi naona ni rahisi kuwasamehe kina Nassari, Mashinji, Silinde au Lijualikali maana waliamua kujitoa kwenye chama (japo sababu walizotoa ni za uongo), hawakuhujumu misimamo ya chama. Ila hawa kina Mdee wanaenda mbele ya Umma kujinadi kuwa wamepata baraka za chama ndio maana wameenda Bungeni. Kiufupi waliamua kutumia tamaa zao kutaka kugombanisha wanachama na Chadema. Wasiojua msoto ni ngumu sana kuvumilia shida

Snitch hawezi kuwa rafiki, hata akitubu
 
CDM haina mgogoro na hao wabunge, CDM iliwavua uanachama na kilichopaswa kufuata ni wao kupoteza nafasi zao za ubunge kama katiba ingeheshimiwa.Chadema ambacho haitaki ni wao kuendelea kujitambulisha kama wanachama wake wakati sivyo. RejeaSakata la Hamza kutambuliwa kama mwanachama wa CCM na Raia mwema ilisababisha gazeti hilo kufungiwa.
Unadhani kuna faida gani kwa CDM kendelea na mgogoro wa uanachama wa wanachama wabunge wake 19?
 
Back
Top Bottom