Chombo cha Orion baada ya kutua kutoka mwezini

Mzawa_G

JF-Expert Member
Feb 27, 2014
667
1,467
Muonekano wa chombo cha orion baada ya kurudi duniani umekuwa ni tofauti kabisa na vile kilivyokuwa kinaonekana mwanzo kabla ya kwenda huko anga za mbali

Mara baada ya kupita katika matabaka mbalimbali ya anga hewa na kupata ule msuguano mkali wa matabaka ambayo yana mgandamizo mkubwa wa hewa hupelekea chochote kile kinapita happo kuweza kusababisha msuguano baina ya chombo na matabaka hayo ya anga hewa

Msuguano ukizidi huzalisha moto mkali ambao huunguza rangi mbalimbali zilizo nje kabisa ya chombo hicho ila kikubwa cha kushukuru ni kwa material yake yenye uwezo wa kuhimili kiasi kikubwa cha joto ambayo yamewekwa kwa nje ndio yanafanya wanaanga na vifaa mbalimbali vya ndani kuwa salama muda wote

geraldchristopher1@gmail.com
Tanzaniascienceyetu
Elimuyaangazambali
Gerald
 
_127972941_epa.jpg.jpeg
 
Chombo hiki kilienda na mwanaanga au peke yake?
Hakikuwa na mwanaanga yeyote coz kilienda kwa majaribio ili chombo kijacho ndicho kitaondoka na kundi la wanasayansi na raia wengine.
 
Yawezekana kuna jambo hatuambiwi mbona serikali zinatumia mabilioni kama sio matrilioni kisa tafiti tu?(vi doubt) tunacho ambiwa ni kuwa chombo kimetua salama baada ya hapo wanapiga kimyaaaa baadae wanaibuka na kusema chombo kilicho kuwa angani sasa kinarudi(kilikuta nini huko? Kimaaa kimeleta nini kutoka huko kimyaaa)
 
Hakuna kitu cha kifala kama huu uwongo wa vibehewa used wanaotaka kutulisha saa sita mchana, kule Mwigulu naye anatudanganya kama wajinga ambao hatukuwahi kwenda shule, eti hata nyumba zetu tulizojenga kwa mikopo ni sehemu ya deni la Taifa
Yaani nyumba yangu niliyoijenga kwa jasho langu ni mkopo 🤧🤧🤧🤒🤒🤒😟😟
 
Hakikuwa na mwanaanga yeyote coz kilienda kwa majaribio ili chombo kijacho ndicho kitaondoka na kundi la wanasayansi na raia wengine.
Kundi la wanasayansi na raia wengine..? Hapana boss ikitokea wakaenda hawatazidi wanne
 
Yawezekana kuna jambo hatuambiwi mbona serikali zinatumia mabilioni kama sio matrilioni kisa tafiti tu?(vi doubt) tunacho ambiwa ni kuwa chombo kimetua salama baada ya hapo wanapiga kimyaaaa baadae wanaibuka na kusema chombo kilicho kuwa angani sasa kinarudi(kilikuta nini huko? Kimaaa kimeleta nini kutoka huko kimyaaa)
Usiwe TU mtu wa kufuatilia taarifa za mtandaoni juu juu.. na wewe uwe unasoma soma itakupa uelewa mpana wa mambo mengi hapa duniani
 
Hakikuwa na mwanaanga yeyote coz kilienda kwa majaribio ili chombo kijacho ndicho kitaondoka na kundi la wanasayansi na raia wengine.
Nadhani nia na lengo la kupeleka chombo huko anga za mbali ni kufanya tafiti na kukusanya taarifa za mahali husika (iwe mwezini, sayari, nk). Baada ya chombo (kilichoenda bila mwanaanga) kukamilisha safari yake, waliokituma chombo hicho wanapataje taarifa zilizokusanywa ilhali chombo hicho kinaporudi hutua baharini na inasemekana wakati mwingine hupotelea baharini? Kuna njia nyingine yoyote ya kupata taarifa hizo?
 
Muonekano wa chombo cha orion baada ya kurudi duniani umekuwa ni tofauti kabisa na vile kilivyokuwa kinaonekana mwanzo kabla ya kwenda huko anga za mbali

Mara baada ya kupita katika matabaka mbalimbali ya anga hewa na kupata ule msuguano mkali wa matabaka ambayo yana mgandamizo mkubwa wa hewa hupelekea chochote kile kinapita happo kuweza kusababisha msuguano baina ya chombo na matabaka hayo ya anga hewa

Msuguano ukizidi huzalisha moto mkali ambao huunguza rangi mbalimbali zilizo nje kabisa ya chombo hicho ila kikubwa cha kushukuru ni kwa material yake yenye uwezo wa kuhimili kiasi kikubwa cha joto ambayo yamewekwa kwa nje ndio yanafanya wanaanga na vifaa mbalimbali vya ndani kuwa salama muda wote

geraldchristopher1@gmail.com
Tanzaniascienceyetu
Elimuyaangazambali
Gerald

FB_IMG_1670868156598.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom