Dp800
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 1,755
- 3,608
Chama cha demokrasia na Maendeleo CHADEMA, kipo na kinaendelea na maandalizi ya uchaguzi mkuu bila ya uwepo wa Katibu wake mkuu mheshimiwa sana Dr. Slaa hili ni jambo ambalo sisi kama wanachama wake tunapata mashaka kidogo hasa kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi ya ukatibu katika shughuli za kila siku za Chama cha siasa. Ombi langu kwa viongozi wakuu wa Chama chetu ni kulitazama jambo hili kwa makini ili kuhakikisha umoja na mshikamano wetu katika kipindi hichi kigumu unaimarishwa zaidi na nafasi hiyo inazibwa mapema iwezekanavyo.