Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,445
SEHEMU YA 05
ILIPOISHIA:
Msisimko nilioupata ulikuwa mkubwa sana, mara mkuu wa kaya akakurupuka kutoka kwenye maficho yake, Mimah akamtazama mkuu wa kaya kisha akanitazama usoni, aibu za kikekike zikiwa zimemjaa, akageuka na kunipa kisogo kisha akamkamata tena mkuu wa kaya na kumuelekeza njia ya kupita huku akiwa ni kama anataka kuokota kitu sakafuni.
SASA ENDELEA...
Kiukweli sikutegemea kama anaweza kufanya kitu kama kile, kwa mara nyingine tukajikuta msambweni, safari hii tukiwa katika mazingira tofauti kabisa. Nilifanya kile nilichotakiwa kukifanya, tena kwa ufanisi mkubwa sana na haukupita muda mrefu, Mimah akapasua tena dafu, akawa ni kama amechanganyikiwa.
“Nakupenda wewe! Nakupenda sharobaro wangu,” alisema huku akinikumbatia kwa nguvu, mapigo ya moyo wake yakimuenda mbio kuliko kawaida. Nadhani alichokipata hakuwa amekitegemea kabisa.
Basi alichukua sabuni na kujipaka mwili mzima, akahamia kwangu, akafanya hivyohivyo kisha akaongeza kasi ya bomba la mvua, tukaoga na baada ya kumaliza, tulirudi kule chumbani kwake.
“Ngoja nipumzike kidogo mume wangu,” alisema, nikawa nashangilia mwenyewe ushindi kwa sababu eti tayari nilishakuwa mume wake, akajifuta maji kwa taulo safi, akanipa na mimi nijifute na harakaharaka akapanda kwenye kitanda kikubwa na cha kisasa na kujilaza.
Baada ya kumaliza, na mimi nilipanda pale juu ya kitanda, akageuka kichovu na kunitazama, huku tabasamu hafifu likiwa limechanua kwenye uso wake.
“Kwani wewe una miaka mingapi?”
“Eeh, mambo ya kuulizana miaka yametoka wapi tena?”
“Mh! Nimekuuliza tu, unajua nilikuwa nakuona kama bado mdogo sana kwangu,” alisema, nikaishia kucheka tu kwa sababu nilikuwa najua anachotaka kukisema, nikabadilisha mazungumzo kwa sababu ni kweli kiumri bado nilikuwa mdogo, niliwahi tu kwenye mambo ya kikubwa na uwezo kweli nilikuwa nao, katika hilo najiamini.
Tuliendelea kupiga stori za hapa na pale, mwisho tukajikuta tena uwanjani, kwa mara nyingine nikakata mzizi wa fitina. Mpaka ngwe hiyo inaisha, Mimah alikuwa hoi bin taabani, akajitupa upande wa pili kama mzigo na haukupita muda mrefu, akaanza kukoroma.
Nilipochungulia nje kwa kupitia dirisha kubwa lililokuwa mle chumbani, niligundua kwamba kigiza cha jioni kilishaanza kuingia, ikabidi nikurupuke harakaharaka kwa sababu sikutaka kuingia matatizoni na baba mdogo kwa sababu angeweza kunifokea sana kama ningechelewa kurudi.
Basi nilijiandaa harakaharaka, nikamuwekea vitu vyote vizuri ikiwa ni pamoja na kuhakikisha yule samaki amekaa vizuri kwenye friji, nikatoka kimyakimya na kuanza kutembea harakaharaka kurudi nyumbani. Nilitembea kwa miguu kwa sababu sikutaka kutumia fedha za mtaji kwa ajili ya kuchukua usafiri, nilijua nitagombana na baba mdogo na hakuna kitu ambacho nilikuwa sikitaki kama kumuudhi.
Kwenye majira ya kama saa mbili kasoro hizi za usiku, tayari nilikuwa nimewasili nyumbani, kwa bahati nzuri baba mdogo hakuwa bado amerejea, kwa hiyo nikamkabidhi mke wake hesabu kisha nikaenda moja kwa moja ‘magetoni’ kwangu, nikajilaza kitandani huku nikiendelea kusherehekea ushindi nilioupata kwa Mimah.
Nikawasha kiredio changu kidogo kinachotumia flashi na kuweka wimbo niliokuwa naupenda sana, wa tipwatipwa tetema, nikawa naburudika. Japokuwa nilikuwa najikaza, ukweli ni kwamba nilikuwa nimechoka sana, sikutamani hata kula usiku huo, hisia tamu juu ya Mimah zikawa zinaendelea kupita ndani ya kichwa changu, baadaye nikapitiwa na usingizi mzito.
Nilipokuja kuzinduka, tayari muda ulikuwa umeenda sana, nilipotazama saa, ilikuwa inaonesha ni saa tisa kasoro za usiku, nikachukua kisimu changu ambacho tangu niliporudi sikuwa nimeshughulika nacho, nikagundua kwamba kilikuwa kimezima, bila kuuliza nikajua kuwa lazima itakuwa kimeisha chaji.
Nilikichomeka kwenye chaji na kukiwasha, nikarudi kitandani na kujilaza, mara meseji zikaanza kuingia mfululizo. Niliinuka kichovu na kukichukua, nikashtuka kugundua kwamba kumbe Mimah alikuwa amenipigia sana na pengine ndiyo maana kisimu kikazima. Kulikuwa na ‘missed’ call kama kumi hivi, zote zikiwa zimetoka kwa Mimah lakini pia kulikuwa na meseji kibao, ikabidi nianze kuzifungua na kusoma moja baada ya nyingine. Zote zilikuwa ni kutoka kwa Mimah. Alikuwa ananiuliza nimeondoka saa ngapi, kwa nini nimeondoka bila kumuaga, mbona sipokei simu na kadhalika.
Maswali yalikuwa mengi kiasi kwamba hata sikujua nijibu lipi, nikaamua kurudi kulala kwa sababu bado sikuwa nimepumzika vya kutosha. Haukupita muda mrefu, nikapitiwa na usingizi.
Kelele za mlango uliokuwa unagongwa na baba mdogo, ndizo zilizonizindua kutoka usingizini, harakaharaka nikakurupuka na kwenda kumfungulia, nikamsalimu kwa adabu.
“Nasikia jana ulitoka mchana hata chakula hukula na ukarudi usiku, na chakula pia hukula. Kwa nini unakuwa na tabia za ajabuajabu? Haya niambie ulikuwa umeenda wapi?” baba mdogo alianza kuwaka. Kiukweli nilikasirika kwa sababu nilijua mtu anayetugombanisha ni mama mdogo, kwa nini anichunge kama mtoto mdogo?
Sikutaka kubishana naye kwa hiyo nilimjibu tu kwa kifupi kwamba nilikuwa nimeenda kukusanya madeni, nikamuona akipoa ghafla. Akanihesabia fedha za kwenda kununulia mzigo na kunisisitiza kuwa makini na kazi.
Aliporudi ndani kwake, nilitoka harakaharaka na kwenda bafuni kuoga, nikarudi na kuanza kujiandaa huku bado nikiwa na kinyongo na mama mdogo. Kwa nini anichonganishe na baba? Basi baada ya kumaliza kujiandaa, nilichukua kapu langu na kutoka mpaka kituoni, nikakalia daladala na safari ya kuelekea Feri ikaanza.
Mara simu yangu ilianza kuita, haikuwa kawaida simu yangu kupigwa alfajiri kiasi hicho, harakaharaka nikaitoa mfukoni na kuitazama, alikuwa ni Mimah.
“Wewe!”
“Ooh! Mimah, za asubuhi mama.”
“Mbaya! Uko wapi?”
“Naenda Feri.”
“Una tabia mbaya sana, ndiyo nini ulivyonifanya jana? Yaani ume...” alisema lakini kabla hajamaliza,kwa kuwa nilikuwa kwenye daladala, ilibidi nimkatishe.
“Kwani leo huendi kazini?”
“Kwa gwaride ulilonichezesha unafikiri nitaweza kwenda kazini kweli? Nimejilalia zangu, njoo!”
“Hapana, nafuata mzigo kwanza.”
“Ukitoka huko uje basi, ujue yule samaki tangu jana sijamtengeneza. Uje unitengenezee nimpike na sili kitu mpaka uje,” alisema Mimah kwa sauti ya kudeka, nikajikuta nacheka tu mwenyewe. Alipokata simu, nilianza kumfikiria Mimah, kiukweli ujasiri wangu ulikuwa umezaa matunda matamu sana.
Wakati safari inaendelea, dereva alifungulia redio mle kwenye daladala, akaweka wimbo wa Tetema, tena kwa sauti ya juu, basi wakati mziki huo unapigwa, na mimi nikawa nafuatisha maneno yake huku nikivuta kumbukumbu za jana yake nilivyokuwa na Mimah, nikajikuta nacheka tu mwenyewe.
“Mbona unacheka mwenyewe?” abiria mwenzangu niliyekuwa nimekaa naye, aliniuliza, nikahisi nimemkwaza, harakaharaka nikauchuna kisha nikamjibu kwa kifupi ‘naupenda tu huu wimbo.’
“Mh! Unapenda wimbo au unapenda hayo maneno yake? Sisi wanawake wanene tunapata sana shida, kila unakopita unasikia wahuni wanakuimbia ‘tipwatipwa tetema...’ hadi kero,” alisema yule abiria mwenzangu ambaye kwa sababu alikuwa amejitanda ushungi na kuvaa gauni kubwakubwa, kwanza nilidhani ni mama mtu mzima laini pia sikuweza kumgundua haraka kwamba kumbe na yeye ni ‘tipwatipwa’.
Nikashusha macho yangu na kuanza kumchunguza vizuri huku mapigo ya moyo wangu yakianza kunienda mbio. Aligundua kwamba nilikuwa nikimtazama kwa macho ya kuibia, basi akanigeukia na kunitazama, macho yangu na yake yakagongana, nikaachia tabasamu pana, na yeye akaachia tabasamu.
“Ujue nyie masharobaro wa siku hizi hamna adabu kabisa, si ajabu hapo unaimba huo wimbo kwa sababu umeniona mimi,” alisema, nikacheka sana huku nikiendelea kumtathmini jinsi alivyokuwa mzuri.
Je, nini kitafuatia?
ILIPOISHIA:
Msisimko nilioupata ulikuwa mkubwa sana, mara mkuu wa kaya akakurupuka kutoka kwenye maficho yake, Mimah akamtazama mkuu wa kaya kisha akanitazama usoni, aibu za kikekike zikiwa zimemjaa, akageuka na kunipa kisogo kisha akamkamata tena mkuu wa kaya na kumuelekeza njia ya kupita huku akiwa ni kama anataka kuokota kitu sakafuni.
SASA ENDELEA...
Kiukweli sikutegemea kama anaweza kufanya kitu kama kile, kwa mara nyingine tukajikuta msambweni, safari hii tukiwa katika mazingira tofauti kabisa. Nilifanya kile nilichotakiwa kukifanya, tena kwa ufanisi mkubwa sana na haukupita muda mrefu, Mimah akapasua tena dafu, akawa ni kama amechanganyikiwa.
“Nakupenda wewe! Nakupenda sharobaro wangu,” alisema huku akinikumbatia kwa nguvu, mapigo ya moyo wake yakimuenda mbio kuliko kawaida. Nadhani alichokipata hakuwa amekitegemea kabisa.
Basi alichukua sabuni na kujipaka mwili mzima, akahamia kwangu, akafanya hivyohivyo kisha akaongeza kasi ya bomba la mvua, tukaoga na baada ya kumaliza, tulirudi kule chumbani kwake.
“Ngoja nipumzike kidogo mume wangu,” alisema, nikawa nashangilia mwenyewe ushindi kwa sababu eti tayari nilishakuwa mume wake, akajifuta maji kwa taulo safi, akanipa na mimi nijifute na harakaharaka akapanda kwenye kitanda kikubwa na cha kisasa na kujilaza.
Baada ya kumaliza, na mimi nilipanda pale juu ya kitanda, akageuka kichovu na kunitazama, huku tabasamu hafifu likiwa limechanua kwenye uso wake.
“Kwani wewe una miaka mingapi?”
“Eeh, mambo ya kuulizana miaka yametoka wapi tena?”
“Mh! Nimekuuliza tu, unajua nilikuwa nakuona kama bado mdogo sana kwangu,” alisema, nikaishia kucheka tu kwa sababu nilikuwa najua anachotaka kukisema, nikabadilisha mazungumzo kwa sababu ni kweli kiumri bado nilikuwa mdogo, niliwahi tu kwenye mambo ya kikubwa na uwezo kweli nilikuwa nao, katika hilo najiamini.
Tuliendelea kupiga stori za hapa na pale, mwisho tukajikuta tena uwanjani, kwa mara nyingine nikakata mzizi wa fitina. Mpaka ngwe hiyo inaisha, Mimah alikuwa hoi bin taabani, akajitupa upande wa pili kama mzigo na haukupita muda mrefu, akaanza kukoroma.
Nilipochungulia nje kwa kupitia dirisha kubwa lililokuwa mle chumbani, niligundua kwamba kigiza cha jioni kilishaanza kuingia, ikabidi nikurupuke harakaharaka kwa sababu sikutaka kuingia matatizoni na baba mdogo kwa sababu angeweza kunifokea sana kama ningechelewa kurudi.
Basi nilijiandaa harakaharaka, nikamuwekea vitu vyote vizuri ikiwa ni pamoja na kuhakikisha yule samaki amekaa vizuri kwenye friji, nikatoka kimyakimya na kuanza kutembea harakaharaka kurudi nyumbani. Nilitembea kwa miguu kwa sababu sikutaka kutumia fedha za mtaji kwa ajili ya kuchukua usafiri, nilijua nitagombana na baba mdogo na hakuna kitu ambacho nilikuwa sikitaki kama kumuudhi.
Kwenye majira ya kama saa mbili kasoro hizi za usiku, tayari nilikuwa nimewasili nyumbani, kwa bahati nzuri baba mdogo hakuwa bado amerejea, kwa hiyo nikamkabidhi mke wake hesabu kisha nikaenda moja kwa moja ‘magetoni’ kwangu, nikajilaza kitandani huku nikiendelea kusherehekea ushindi nilioupata kwa Mimah.
Nikawasha kiredio changu kidogo kinachotumia flashi na kuweka wimbo niliokuwa naupenda sana, wa tipwatipwa tetema, nikawa naburudika. Japokuwa nilikuwa najikaza, ukweli ni kwamba nilikuwa nimechoka sana, sikutamani hata kula usiku huo, hisia tamu juu ya Mimah zikawa zinaendelea kupita ndani ya kichwa changu, baadaye nikapitiwa na usingizi mzito.
Nilipokuja kuzinduka, tayari muda ulikuwa umeenda sana, nilipotazama saa, ilikuwa inaonesha ni saa tisa kasoro za usiku, nikachukua kisimu changu ambacho tangu niliporudi sikuwa nimeshughulika nacho, nikagundua kwamba kilikuwa kimezima, bila kuuliza nikajua kuwa lazima itakuwa kimeisha chaji.
Nilikichomeka kwenye chaji na kukiwasha, nikarudi kitandani na kujilaza, mara meseji zikaanza kuingia mfululizo. Niliinuka kichovu na kukichukua, nikashtuka kugundua kwamba kumbe Mimah alikuwa amenipigia sana na pengine ndiyo maana kisimu kikazima. Kulikuwa na ‘missed’ call kama kumi hivi, zote zikiwa zimetoka kwa Mimah lakini pia kulikuwa na meseji kibao, ikabidi nianze kuzifungua na kusoma moja baada ya nyingine. Zote zilikuwa ni kutoka kwa Mimah. Alikuwa ananiuliza nimeondoka saa ngapi, kwa nini nimeondoka bila kumuaga, mbona sipokei simu na kadhalika.
Maswali yalikuwa mengi kiasi kwamba hata sikujua nijibu lipi, nikaamua kurudi kulala kwa sababu bado sikuwa nimepumzika vya kutosha. Haukupita muda mrefu, nikapitiwa na usingizi.
Kelele za mlango uliokuwa unagongwa na baba mdogo, ndizo zilizonizindua kutoka usingizini, harakaharaka nikakurupuka na kwenda kumfungulia, nikamsalimu kwa adabu.
“Nasikia jana ulitoka mchana hata chakula hukula na ukarudi usiku, na chakula pia hukula. Kwa nini unakuwa na tabia za ajabuajabu? Haya niambie ulikuwa umeenda wapi?” baba mdogo alianza kuwaka. Kiukweli nilikasirika kwa sababu nilijua mtu anayetugombanisha ni mama mdogo, kwa nini anichunge kama mtoto mdogo?
Sikutaka kubishana naye kwa hiyo nilimjibu tu kwa kifupi kwamba nilikuwa nimeenda kukusanya madeni, nikamuona akipoa ghafla. Akanihesabia fedha za kwenda kununulia mzigo na kunisisitiza kuwa makini na kazi.
Aliporudi ndani kwake, nilitoka harakaharaka na kwenda bafuni kuoga, nikarudi na kuanza kujiandaa huku bado nikiwa na kinyongo na mama mdogo. Kwa nini anichonganishe na baba? Basi baada ya kumaliza kujiandaa, nilichukua kapu langu na kutoka mpaka kituoni, nikakalia daladala na safari ya kuelekea Feri ikaanza.
Mara simu yangu ilianza kuita, haikuwa kawaida simu yangu kupigwa alfajiri kiasi hicho, harakaharaka nikaitoa mfukoni na kuitazama, alikuwa ni Mimah.
“Wewe!”
“Ooh! Mimah, za asubuhi mama.”
“Mbaya! Uko wapi?”
“Naenda Feri.”
“Una tabia mbaya sana, ndiyo nini ulivyonifanya jana? Yaani ume...” alisema lakini kabla hajamaliza,kwa kuwa nilikuwa kwenye daladala, ilibidi nimkatishe.
“Kwani leo huendi kazini?”
“Kwa gwaride ulilonichezesha unafikiri nitaweza kwenda kazini kweli? Nimejilalia zangu, njoo!”
“Hapana, nafuata mzigo kwanza.”
“Ukitoka huko uje basi, ujue yule samaki tangu jana sijamtengeneza. Uje unitengenezee nimpike na sili kitu mpaka uje,” alisema Mimah kwa sauti ya kudeka, nikajikuta nacheka tu mwenyewe. Alipokata simu, nilianza kumfikiria Mimah, kiukweli ujasiri wangu ulikuwa umezaa matunda matamu sana.
Wakati safari inaendelea, dereva alifungulia redio mle kwenye daladala, akaweka wimbo wa Tetema, tena kwa sauti ya juu, basi wakati mziki huo unapigwa, na mimi nikawa nafuatisha maneno yake huku nikivuta kumbukumbu za jana yake nilivyokuwa na Mimah, nikajikuta nacheka tu mwenyewe.
“Mbona unacheka mwenyewe?” abiria mwenzangu niliyekuwa nimekaa naye, aliniuliza, nikahisi nimemkwaza, harakaharaka nikauchuna kisha nikamjibu kwa kifupi ‘naupenda tu huu wimbo.’
“Mh! Unapenda wimbo au unapenda hayo maneno yake? Sisi wanawake wanene tunapata sana shida, kila unakopita unasikia wahuni wanakuimbia ‘tipwatipwa tetema...’ hadi kero,” alisema yule abiria mwenzangu ambaye kwa sababu alikuwa amejitanda ushungi na kuvaa gauni kubwakubwa, kwanza nilidhani ni mama mtu mzima laini pia sikuweza kumgundua haraka kwamba kumbe na yeye ni ‘tipwatipwa’.
Nikashusha macho yangu na kuanza kumchunguza vizuri huku mapigo ya moyo wangu yakianza kunienda mbio. Aligundua kwamba nilikuwa nikimtazama kwa macho ya kuibia, basi akanigeukia na kunitazama, macho yangu na yake yakagongana, nikaachia tabasamu pana, na yeye akaachia tabasamu.
“Ujue nyie masharobaro wa siku hizi hamna adabu kabisa, si ajabu hapo unaimba huo wimbo kwa sababu umeniona mimi,” alisema, nikacheka sana huku nikiendelea kumtathmini jinsi alivyokuwa mzuri.
Je, nini kitafuatia?