Chombezo: Nelly Muosha Magari Wa Posta

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,425
MTUNZI: IRENE MWAMFUPE NDAUKA
SEHEMU YA 01


Jumapili moja baada ya kula chakula cha usiku, baba mzazi wa kijana Nelson ambaye wengi walipenda kukatisha jina lake na kumwita Nelly, Mzee Reli ya Uhuru akiwa ameketi sebuleni na kijana wake huyo aliyehitimu kidato cha nne, alimweleza kwamba kwa wakati ule hakuwa na fedha za kuweza kumuendeleza kielimu hivyo ajichanganye mjini kujitafutia maisha.
Wakati mzee huyo aliyepewa jina la utani la Reli ya Uhuru kufuatia kuwa mmoja wa watu waliojenga reli hiyo, akimweleza hivyo, mkewe alikuwa akimsikiliza ambapo alimuunga mkono mumewe kwani hali yao kiuchumi aliielewa vizuri.
“Nelly, ni kweli kabisa kwa hivi sasa baba yako hana fedha na unaona jinsi familia yetu ilivyo kubwa na wote tunamtegemea yeye, mimi nakubaliana na ushauri wake wa wewe kujichanganya mjini kufanya vibarua ambavyo vitakuwezesha kupata riziki yako na yetu,” mama huyo alimwambia kijana wake.
Nelly kijana ambaye tangu udogo wake ni handsome boy kiasi cha kuwavutia wasichana wengi wakiwemo watu wazima, aliposikia kauli hiyo ya wazazi wake aliinamisha kichwa na kuanza kufikiria hatima ya maisha yake ingekuwaje.
“Hivi baba, huwezi kuuza lile shamba la Kimanzichana ili fedha zitakazopatikana niweze kuendelea na masomo nitimize ndoto zangu za kuwa mhasibu?” Nelly alimwuliza baba yake.
Baba yake alimfahamisha kwamba baada ya mambo yake kuanza kumwendea kombo, aliuza nusu ya shamba hilo na nusu iliyobaki asingeweza kuiuza kwani alipanga ije iwasaidie wadogo zake ambao walikuwa wadogo.
Kwa kuwa Nelly alikuwa akielewa ukubwa wa familia yao na jinsi mzazi wake alivyokuwa akihangaika kuitunza, akawa hana jinsi zaidi ya kuingia mitaani kusaka kibarua chochote ambacho kingemuwezesha kupata fedha.
“Oke baba na mama, kwa kuwa naielewa hali halisi ya maisha yetu hapa nyumbani, nitazungumza na fundi Yassin ili niongozane naye kwenye shughuli zake za ujenzi,” Nelly aliwaambia wazazi wake.
Alipotoa kauli hiyo, baba yake licha ya kujiuliza moyoni kama kweli Nelly aliyemlea kimayai angeweza kufanya kazi ya uwashi lakini hakutaka kumuonesha wasiwasi wake, akamwambia sawa.
Baada ya mazungumzo hayo, Nelly aliwaaga wazazi wake na kwenda kwenye chumba alichokuwa akilala na wadogo zake wawili kilichokuwa uani, akawa anatafakari ugumu wa maisha uliokuwa ukiwakabili.
Chumbani kwa wazazi wake, baba na mama yake walimjadili sana kijana wao kama angeweza kufanya kazi ya ujenzi lakini baadaye walikubaliana wasubiri kuona matokeo.
Alfajiri na mapema Nelly alikwenda kumgongea fundi Yassin ambaye alikuwa fundi washi aliyekuwa akisifika sana kwa umahiri wake wa kujenga nyumba maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar.
“Niambie Nelly, naona leo umenivamia alfajiri yote hii, umekwama nini?” fundi Yassin aliyekuwa akimpa fedha Nelly siku moja moja alipokwama alimwuliza.
“Ukiacha kukwama, leo nataka tuongozane huko site unakokwenda kujenga japo nikakusaidie kazi yoyote maana mtoto wa kiume kumtegemea baba kila kitu haipendezi,” Nelly alimwambia fundi Yassin.
“Yaani Nelly na huo usharobaro wako unataka kwenda kufanya kazi ya kukoroga zege au kuranda mbao, utaweza kweli?” fundi Yassin alimwuliza.
 
SEHEMU YA 02

Kufuatia kuambiwa hivyo, kijana huyo mweupe, mrefu wa wastani na mwenye vidimponsi vinavyoonekana kila akiongea au kucheka alimjibu fundi Yassin kwamba kwa kuwa alikuwa mtoto wa kiume alikuwa tayari kufanya kazi yoyote.
Licha ya Nelly kupewa ushauri wa kutafuta kazi yoyote ya kufanya, aliumia sana kufuatia bro mmoja ambaye ni mambo safi kumchukua demu wake Careen kwa vile hakuwa na hela.
Msichana huyo aliyeingizwa kwenye ulimwengu wa kimapenzi na Nelly, alikuwa akimpenda sana Nelly lakini alishindwa kudumu naye kwa sababu kila alipohitaji sapoti ya fedha kutoka kwa mpenzi wake huyo ilikuwa zii.
Kila Nelly alipokuwa akikumbuka tukio hilo la kuporwa demu wake na yule bro anayemiliki kampuni ya kutoa mizigo Bandarini aliumia sana, kwa sehemu ishu hiyo ilimfanya akubaliane na ushauri wa baba yake wa kutafuta kibarua chochote cha kufanya.
“Ila Nelly kwa jinsi ninavyokuona sijui kama utaweza kufanya kazi ngumu, kwa kuwa umeamua basi vizuri jiandae ili kesho twende pamoja,” fundi Yassin alimwambia Nelly aliyekuwa akivaa miwani sababu ya kusumbuliwa na macho kwa mbali.
“Fundi Yassin, haina haja ya kusubiri kesho, hivi unavyoniona nipo full, labda niende nikachukue nguo za kufanyia kazi, nimechoka kukaa nyumbani,” Nelly alimwambia fundi Yassin aliyeishia kucheka.
“Haya bwana, nenda kachukue nguo hizo ili nami nijiandae kisha tuanze safari, ukija nitakwambia tunakokwenda,” fundi Yassin alimwambia Nelly.
Baada ya kuambiwa hivyo, kijana huyo wa Kisukuma alikwenda kwao akachukuwa shati kuukuu, suruali ya zamani na raba ambazo hakuwa akizivaa kwa sababu zilianza kuchoka akaziweka kwenye begi.
Wakati Nelly ambaye nimeshakwambia ni handsome boy haswa akijiandaa, nyumbani kwa fundi Yassin mkewe alimwuliza alikuwa akizungumza na nani.
Fundi Yassin alimsimulia kila kitu mkewe, ambaye hakuamini kama kweli Nelly aliyekuwa akimfahamu kwa usmati wake angeweza kufanya kazi ya ujenzi aliyokuwa akiifanya mumewe.
“Yaani baba Tatu, Nelly huyu sharobaro mvaa miwani ataweza kweli kubeba zege, matofali, kuchota maji au kubeba mbao?” mkewe Yassin alimwuliza mumewe.
“Nami nimemuuliza hivyo kaniambia ataweza, wewe ngoja niende naye halafu tukirudi ndiyo nitakueleza kitakachojiri huko,” fundi Yassin alimwambia mkewe, wakacheka.
Wakati fundi Yassin akizungumza na mkewe, nyumbani kwa akina Nelly, baba yake alipomuona kijana wake kabeba begi muda ule wa alfajiri alihisi huenda alikuwa akitoroka kufuatia kumwambia aanze kujitegemea.
“Nelly mbona na begi alfajiri yote hii, unakwenda wapi?” mzee huyo alimwuliza kijana wake.
Baada mama Nelly kuchangamshwa damu asubuhi ile alimshukuru mumewe, akiwa anachekacheka aliamka na kwenda kuandaa maji ya kuoga, wakaoga pamoja kisha alimwandali kifungua kinywa.
Baba Nelly alipomaliza kunywa chai aliondoka kuelekea kwenye pilika za kutafuta riziki, akiwa njiani akawa anamtafakari Nelly aliyemweleza anakwenda kumsaidia kazi fundi Yassim.
“Kama ataweza nitasema kweli amekuwa lakini kwa jinsi ninavyomjua atakapotoka huko ataniambia hatakwenda tena,” mzee huyo aliwaza.
Nelly akiwa na begi lake alipofika nyumbani kwa fundi Yassin, alimkuta akiwa anamsubiri. Hawakupoteza muda, fundi huyo aliamuga mkewe kisha alichukuwa zana zake za kazi na kuanza safari ya kwenda site.
Kwa kuwa bado ilikuwa ni alfajiri walipofika kituo cha daladala lilifika DCM la Mwenge wakapanda, kwa bahati walikaa siti moja.
Wakiwa wanaendelea na safari fundi Yassin ambaye mpaka muda huo alikuwa aamini kama kweli Nelly aliyekuwa akimfahamu vizuri kwa kupenda mambo ya usharobaro aliamua kwenda kufanya kazi za ujenzi.
“Nelly hivi ni kweli umeamua kwa dhati kufanya kazi ngumu ninazofanya?” fundi Yassin alimwuliza .
“Fundi bwana! Sasa kama wewe unaweza mimi nitashindwaje? Mimi mtoto wa kiume bro!” Nelly alimwambia fundi Yassin aliyeishia kucheka.
Katika daladala walilopanda, kiti cha kushoto alikaa kaka mmoja upande wa dirishani na kufuatia demu mmoja mkali ambaye alfajiri hiyo alikuwa akiangalia mambo ya dunia katika simu yake ya kisasa ‘Smartphone.’
Wakati msichana huyo akiwa bize na simu yake, Nelly alikuwa akimtupia macho kwa chati na kumsifia moyoni kwamba kweli Mungu alijua kumuumba na kuishia kusema kama alikuwa ana boyfriend wake basi alikuwa akila vinono.
Hata hivyo, Nelly ambaye alikuwa akiwapenda watoto wazuri alipanga kama demu huyo atashukia Mwenge amuombe namba yake, alipanga kujaribu tu zali la mentali.
DCM walilopanda lilipofika Mwananyamala Hospitali, Yule dada mkali aliinuka moyo wa Nelly ulipiga pa kwani alijua mahesabu yake ya kuomba namba yalifeli, akajisemea moyoni; kudadeki.’
Wakati Nelly akiwa katika wakati huo mgumu, alimuona Yule kaka aliyekaa upande dirishani na yule msichana mkali akasogea dirishani, moyo wa Nelly ukajaa furaha.
“Vipi Nelly naona upo mbali, unawaza kazi za huko site nini?” fundi Yassin alimshtua Nelly ambaye mawazo yake yalikuwa kwa Yule demu.
“Hapana fundi, mambo mengi tu kichwani si unajua hali ilivyo ngumu siku hizi!” Nelly alimwambia fundi Yassin.
Kwa kuwa muda huo wa hakukuwa na jamu, kufumba na kufumbua walijikuta wamefika Makumbusho abiria wakaanza kuteremka kutoka garini, kwenye siti ya akina Nelly alianza yeye, upande wa kushoto Yule demu,
Kufuatia zana za kazi alizokuwa nazo, fundi Yassin ilibidi watu wote washuke ili asiwabughudhi, Nelly na Yule msichana wakiwa chini, kijana huyo handsome boy aliamua kumsalimia na kumsifia kwa jinsi alivyojaaliwa uzuri na alivyopendeza.
Kama ambavyo nimekuwa nisema mara kwa mara kwamba kama kuna mtu hapa duniani akisifiwa huwa hafurahi ujue ana matatizo, Yule dada alimshukuru Nelly na kuachia tabasamu pana.
Je, Nini?
 
SEHEMU- 3
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale Nelly alipomsalimia yule dada waliyepanda kwenye gari moja na kumsifia jinsi alivyokuwa mzuri na alivyopendeza, ambapo dada huyo alimshukuru na kuporomosha tabasamu pana.
Baada ya dada huyo kuachia tabasamu, Nelly hakumuangusha, alimshukuru naye akaachia tabasamu pana vilevile mtoto wa kike akaziona dimponsi zake na kubaini Nelly alikuwa handsome boy.
“Huyu kaka nilikuwa sijamwangalia vizuri, kumbe ni handsome boy namna hii, yaani alivyotabasamu dimponsi zake zimempendeza,” yule dada akajisemea moyoni.
Kama vile Nelly alikuwa akijua alichokuwa akikiwaza yule mrembo, akajisemea moyoni kwamba ‘kama unampata mtoto mzuri kama huyu… mbona dunia utaiona tamu!’
Kwa kuwa Nelly ambaye kichwa chake kushika vitu kilikuwa kama kompyuta, fasta alimuomba yule dada amtajie namba yake ya simu, kwa kuwa Nelly hakuwa na simu yule dada akamwuliza kama angeweza kuikariri.
“Hiyo mbona kazi ndogo sana, kichwa changu kwa kukariri ndiyo chenyewe,” Nellya akamwambi.
Haya, sifuri, saba, moja, mbili, Sabini, sabini na sita mwisho thelathini, Nelly aliikariri nyema namba hiyo, alipomuuliza jina akamwambia akimpigia au kumtumia ujumbe atamtajia.
Wakati Nelly anamaliza kuzungumza na yule binti mkali, fundi Yassin aliwasikia akaishia kutabasamu na kujisemea moyoni kwamba; “Hawa vijana wa siku hizi wana mambo mengi, kwa muda mfupi tayari amezoeana na mrembo!”
Yule msichana akiwa kama alikuwa akisubiri kuambiwa jambo na Nelly, fundi Yassin akamwita Nelly na kumwambia auchukue ule mfuko uliokuwa na chepe na vifaa vingine vya kujengea.
Kuhofia kupata aibu ya kuonekana na yule mrembo kama alikuwa fundi washi licha ya kuonekana kijana wa kisasa, Nelly alijifanya hakumsikia na kumuaga yule mrembo.
“Poa, tutawasiliana si unajua mida ya kazi hii!” yule msichana ambaye hakuelewa chochote baina ya Nelly na fundi Yassin alimwambia Nelly ambaye naye alimjibu poa.
“Ila wewe dogo unatisha kama moto wa gesi, mara hii umempata mrembo, kweli sikuwezi,” fundi Yassin alimwambia Nelly.
“Kawaida tu bro, sisi vijana unapomuona mtoto mzuri kama yule siyo vyema kumuacha bila kumsalimia na kumsifia, si hata wewe umemuona alivyoumbika?” Nelly alimwambia fundi Yassin na kutabasamu.
Fundi Yassin ambaye licha ya kwamba umri wake ulikwenda lakini naye alikuwa mzoefu wa mambo ya mjini, akaishia kucheka na kusema haya bwana!
Maongezi hayo yalijiri wakati fundi Yassin na Nelly wakisubiri basi la kwenda Tegeta Kibaoni, haukupita muda mrefu lilifika wakapanda ambapo fundi aliuweka mfuko wa zana zake za kazi nyuma ya kiti cha dereva, kama ilivyokuwa awali pia waliketi siti moja.
Wakati safari ikiendelea mtaalam Nelly ambaye kichwa chake kilikuwa kama kompyuta akaanza kuzitaja zile namba za yule mrembo kimoyomoyo, sifuri, saba, moja, mbili, Sabini, sabini na sita, thelathini na kuishia kutabasamu kwani alikuwa ana uhakika hakukosea.
“Mwenzangu vipi mbona unatabasamu?” fundi Yassin alimwuliza Nelly.
“Kanifurahisha huyo kondakta kwa staili yake ya Kata K, yaani ukivuta kidogo hiyo suruali atabaki na boksa tu!” Nelly alimchomekea fundi Yassin wakati si kweli alifurahishwa na jambo hilo.
“Huo si ndiyo uvaaji wenu vijana wa karne hii, huwa nashindwa kuelewa, hivi kijana huwezi kuvaa vizuri ukaonekana wa kileo mpaka uoneshe nguo yako ya ndani?” fundi Yassin alimwuliza Nelly.
Nelly aliishia kucheka na kumwambia hayo ni mambo ya vijana japo yeye hakuwa na tabia hiyo, ambapo fundi Yassin alikubaliana na kusema hata yeye (Nelly) alikuwa na ugonjwa wake.
“Mh fundi, ugonjwa gani?” Nelly alimwuliza fundi Yassin huku akicheka.
 
SEHEMU-4
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale fundi Yassin na Nelly walipokuwa wapo ndani ya daladala wakielekea site ambapo fundi huyo alimwambia alikuwa akielewa ugonjwa wake ndipo kijana huyo aliyejua alichokimaanisha fundi akaangua kicheko na kusababisha abiria wengine wamwangalie.
Je, kilifuatia nini? Songa mbele…
Baada ya Nelly kubaini watu walimshangaa alivyoangua kicheko akamwambia fundi Yassin kwamba wayaache mazungumzo yale kwanza hadi watakapofika site.
“Haya tubadili mada, lakini dogo leo nimekuvulia kofia kwa jinsi ulivyomzoea yule mrembo,” fundi Yassin alimwambia Nelly.
“Fundi bwana, mbona mambo ya kawaida tu kwa sisi vijana!” Nelly alimwambia fundi wake, wakacheka.
Basi walilopanda lilipofika kituo cha Africana Mbezi waliteremka kama abiria sita wakapanda wengine wakiwemo wasichana wawili wazuri naliovaa kwa mpangilio.
Mmoja wa wasichana hao alikaa siti iliyokuwa mbele ya akina Nelly na mwingine ambaye alikuwa mweupe, mwenye shepu ya kimisi alikaa siti ya kushoto iliyokaribiana na Nelly.
“Dogo umeyaona mambo yako?” fundi Yassin alimtania Nelly.
“He bwana siyo mchezo, yaani nimeamiani mida hii ya asubuhi kwenye madaladala kunakuwa na watoto wakali aisee!” Nelly alimwambia fundi Yassin kwa sauti ya chini, wakacheka.
Wakati akitoa kauli hiyo kumbe yule msichana aliyekuwa amekaa siti ya kushoto alimsikia Nelly, akaachia tabasamu lililoona na kijana huyo mwenye dimponsi.
Nelly alimbinya pajani fundi Yassin na kumweleza yule msichana aliwasikia, ambapo fundi huyo akacheka na kumsifia kwamba kweli alikuwa ma masikio shapu!
Basi lilipofika njia panda ya kwenda Bahari Beach, wale wasichana walishuka kitendoa mabcho hakikumpendeza Nelly akaishia kusikitika moyoni.
“Da! Watoto wazuri kumbe wanashukia hapa,” Nelly aliwaza lakini hakuweza kuwazuia na kubaki kusonya ndani kwa ndani.
Kama vile fundi Yassin alijua Nelly hakupenda wale watoto wazuri washuke, akamtania kwamba licha ya kujifanya mjanja hakuweza hata kuwapa hi wale waremboa.
“Yaani bro wewe acha tu kama umejua nilivyoumia warembo kushuka pale, kama wangeshukia Tegeta ndiyo ungejua mimi ndiyo Nelson Mzamba kijana wa Kisukuma,” Nelly alimwambia fundi Yassin wakacheka.
Kutokana na kunogewa na stori, walishtukia basi limesimama Tegeta waliteremka ambapo fundi Yassin alichukuwa mfuko uliokuwa na zana za kazi na kumfahamisha Nelly kwamba walitakiwa kupanda mabasi yanayokwenda Kisauke.
“Kisauke ndiyo wapi?” Nelly ambaye ndiyo mara yake ya kwanza kusikia jina hilo alimwuliza fundi Yassin.
Fundi Yassin alipoulizwa hivyo aliishia kucheka na kumfahamisha Nelly kwamba ni mbele ya Madale ambako wenye nazo wengi wameporomosha mahekalu ya nguvu.
“ Ndiyo huko ambako Diamond Platnumz kajenga mjengo wake?” Nelly alimwuliza fundi Yassin.
“Yap! Ila Kisauke ipo kwa mbele lakini hatutafika mwisho,” fundi Yassin alimwambia Nelly.
Kwa kuwa walikuwa wanazungumza huku wanatembea walifika kituo cha mabasi ya Kisauke wakakuta kuna hiace inakaribia kujaa wakaingia na baada ya dakika chache gari likaondoka.
Njiani Nelly ambaye alikuwa hajawahi kufika pande za Tegeta akawa anashangaa jinsi watu walivyojenga nyumba na walipofika Kiwanda cha Twiga Simenti alishangaa sana kwani aliakuwa akikisikia tu!
“Hiki ndiyo kiwanda cha simenti cha Wazo?” alimwuliza fundi Yassin ambaye alimjibu ndiyo.
Baada ya kutoka Wazo gari liliendelea na safari hadi walipofika sehemu waliyopaswa kushuka, walipoteremka Nelly alishangaa kumuona kijana mmoja akija kumpokea fundi Yassin ule mfuko wa kazi.
“Shikamoo bro?” yule kijana alimsalimia kisha akanisabahi kwa kusema vipi mambo?
Baada ya kuitikia salamu, fundi Yassin alinitambulisha kwamba yule kijana alikuwa ni mmoja wa vijana waliokuwa wakimsaidia kazi na kuniambia alikuwa anaitwa Zakayo.
“Aliponitajia jina hilo na jinsi kijana huyo alivyokuwa mfupi, nikammkumbuka Zakayo wa kwenye Biblia, nikatabasamu.
“Zakayo, huyu anaitwa Nelly tutakuwa pamoja kwenye kazi zetu,” fundi Yassin alinitambulisha kwa Zakayo.
“Yaani naye atakuwa anakoroga zege kama sisi?” Zakayo alimwuliza fundi Yassin.
“Ndiyo tutakuwa naye,” fundi Yassin alimwambia.
 
SEHEMU-5
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale fundi Yassin alipomtambulisha Nelly kwa Zakayo aliyekuwa akimsaidia kazi na kwamba wangekuwa wote kazini jambo ambalo Zakayo hakuamini kufuatia muonekano wa kisharobaro wa Nelly. Je, kilifuatia nini? Songa mbele…
Baada ya utambulisho huo, fundi na vijana wake waliendelea na safari ya kwenda site lakini Zakayo alikuwa bado aamini kama Nelly aliyeonekana sharobaro angefanya kazi ya kubeba zege.
Walizidi kupiga stori za hapa na pale huku Nelly akistaajabu majumba makubwa ya kisasa yaliyojengwa ambapo fundi Yassin akawa anamuonesha majengo kadhaa ambayo alikuwa amechangia kuyajenga.
Baada ya kutembea kama dakika saba hivi, Nelly alishangaa wakiwa wapo kwenye bonge ya jumba lenye geti kubwa jeusi, fundi Yassin akamwambia walikuwa wamefika site.
Kauli ya fundi huyo ilimshangaza Nelly kwa sababu hakuona nyumba iliyokuwa ikijengwa lakini hakumwuliza hadi fundi Yassin alipobonyeza kengele ya getini ndipo alitokea binti mmoja mrembo akafungua, Nelly alipomuona moyo wake ulipiga paa!
“Kumbe ni wewe fundi umekuja, karibuni!” mrembo huyo alimwambia fundi Yassin huku akimtupia macho Nelly.
“Asante Doreen, vipi bosi yupo?” fundi Yassin alimwuliza Doreen.
Baada ya kuulizwa hivyo, msichana huyo ambaye alikuwa akimwangalia Nelly kwa kuibia alimfahamisha kwamba baba na mama yake walisafiri alfajiri ya siku hiyo kwenda Arusha.
“Eh! Mbona jana hakuniambia na vipi kuna maagizo aliyokuachia?” Fundi Yassin alimwuliza Doreen.
“Kaniambia kila kitu mtazungumza kwenye simu,” Doreen alimfahamisha fundi.
Baada ya kuambiwa hivyo fundi alimtambabulisha Nelly kwa Doreen na kumwambia watakuwanaye pale kazini kisha akamtambulisha Doreen kwa kijana huyo mwenye dimponsi.
“Yaani naye ni fundi au amekuja kutembea ni ndugu yako?” Doreen alimwuliza fundi kwani kwa jinsi alivyomuona Nelly hakufanana kabisa na kazi za ujenzi alizokuwa akizifanya fundi Yassin.
“Yeah! Atakuwa ananisaidia kazi kama wanavyofanya akina Zakayo na wenzake,” fundi Yassin alimfahamisha Doreen bila kujua ni namna gani Nelly aliumia moyoni.
“Da yaani fundi badala ya kusema mimi ndugu yake nimekuja kutembea anaweka wazi kila kitu kwa huyu mtoto mkali, kaharibu kinoma!” Nelly alizungumza kimoyomoyo.
Baada ya fundi kutoa kauli hiyo, Doreen ambaye hakuamini kama ni kweli Nelly alikuwa fundi alifunga geti kisha alimwambia fundi Yassin alikuwa ndani na kama watahitaji kitu wamwite Anne ambaye alikuwa msichana wao wa kazi.
Wakati fundi Yassin akitoa utambulisho huo, Zakayo alikuwa amekwisha zunguka nyumba ya nyumba hiyo ambako kulikuwa na jengo lingine lililokuwa likijengwa.
“Nelly hapa ndipo site ninapofanya kazi mwezi wa pili sasa, nyumba yah ii nyumba bosi wangu anaangusha mjengo mwingine,” fundi Yassin alimwambia Nelly.
Fundi alimwongoza Nelly hadi eneo hilo ndipo kijana huyo mwenye dimponsi ambaye akili yake ilikuwa kwa Doreen alibaki akishangaa ukubwa wa jumba la yule bosi na ingine aliyokuwa akijenga kwa nyuma yake.
“Kweli kuna watu wana fedha jamani, mijengo yote hii ya mtu mmoja?” fundi Yassin alimwuliza fundi.
“Wewe unashangaa nyumba hii, ukienda huko mbele ndiyo balaa watu wamefanya kufuru balaa,” fundi Yassin alimwambia Nelly.
Walipofika kwenye nyumba ya pili ambayo ilikuwa ikiwekwa malumalu, walimkuta kijana mwingine akipanga malumalu, alipomuona fundi Yassin alimwamkia.
Baada ya kumwamkia, alimtazama kwa makini Nelly na kumwambia; “Vipi Mambo?”
“Poa, za kazi?” Nelly alimsabahi.
“Nzuri, karibu!” kijana huyo alimkaribisha Nelly aliyesema asante.
“Hatuni, huyu hapa anaitwa Nelson Nzamba lakini tunapenda kulikatisha jina lake na kumwita Nely, ni jirani yangu tutakuwanaye pamoja kwenye kazi zetu,” fundi Yassin alimtambulisha Nelly kwa Haruni.
Kufuatia utambulisho huo, kama ilivyokuwa kwa Zakayo, Haruni hakuamini kwa muonekano wa Nelly kama alifanana na kazi za kukoroga zege, akamwuliza:
“Fundi bwana kwa masihara umezidi, yaani atakuwa akikoroga zege na kukubeba matofali, malumalu kama sisi?”
“Ndiyo, kwani unamuonaje?” fundi alimwuliza Haruni.
“Hata mimi nimemuuliza kama wewe kaniambia hivyohivyo,” Zakayo akadakia.
“Kama nilivyowaleza naye tutakuwa tunafanya naye kazi,” fundi Yassin aliwaambia.
Kule ndani, Doreen kama ilivyokuwa kwa akina Harunu na Zakayo, akawa haamini kabisa kama Nelly ni fundi.
“Huyo kijana piga ua garagaza siyo fundi, nahisi atakuwa kaja kumpeleleza baba yangu, sijawahi kumuona sharabaro tena anayevaa miwani na mwenye dimponsi anafanya kazi za ujenzi,” Doreen aliwaza.
 
SEHEMU-6
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale kama ambavyo Zakayo na Haruni walivyokuwa hawaamini kama kweli sharobaro Neely angeweza kufanya kazi ya ujenzi, Dorren naye kushangazwa na jambo hilo ambapo moyoni alisema:
“Huyu kijana piga ua garagaza siyo fundi, nahisi atakuwa kaja kumpeleleza baba yangu, sijawahi kumuona sharabaro tena anayevaa miwani na mwenye dimponsi anafanya kazi za ujenzi.”
Wakati Doreen anawaza hayo, fundi Yassin na Nelly walibadilisha nguo na kuvaa za kufanyia kazi kisha fundi huyo alimwambia Zakayo amwelekeze Nelly kazi ya kufanya.
Baada ya Zakayo kuambiwa hivyo na kumuona Nelly akiwa kabadili nguo na kuvaa za kazi ambazo hata hivyo hazikuwa chakavu kama walizokuwa wakifanyia yeye na Haruni, kidogo aliamini kwamba Nelly pia alikuwa pale kikazi.
Kufuatia fundi kumwambia amwelekeze Nelly kazi ya kufanya, hakutaka siku hiyo ya kwanza kumpa kazi ngumu akamwelekeza ya kuzoa mchanga uliokuwa pembeni ya nyumba kubwa waliyoishi akina Doreen.
“Kaka wakati sisi tunaendelea na kazi ya kuweka malumalu ndani, wewe zoa huu mchanga na kuusogeza pale kwani kesho tunataraji kuanza kuweka malumalu hapa pote,” Zakayo alimwambia Nelly.
Kwa kuwa eneo ambalo ulikuwepo mchanga ambao Nelly aliambiwa hauzoe lilikuwa karibu na chumba alichokuwa akilala Doreen, msichana huyo mrembo alisikia maongezi yao.
Baada ya Zakayo kumwelekeza Nelly kazi ya kufanya akaingia nyumba kubwa walikokuwa wakiweka malimalu na kumkuta fundi Yassin akimwelekeza kazi ya kufanya Haruni.
“Vipi umemwelekeza?” fundi Yassin alimwuliza Zakayo.
“Tayari bro ila mpaka dakika hii siamini kama huyo kijana anaweza kufanya kazi hii ngumu tunayofanya, yule amekaa kimayaiyai,” Zakayo alimwambia fundi Yassin, wakacheka.
“Kwa kuwa kapigika kimaisha, kwa hiyari yake kanifuata na kuniambia anataka kuja kunisaidia kazi ili aweze kupata fedha, si unaelewa maisha ni fedha?” fundi Yassin aliwaambia.
“Ni kweli bro lakini kwa huyo kijana akimaliza siku tatu hapa nitajua kweli amedhamirilia,” Haruni alichagiza, wakacheka.
Wakati fundi Yassin akizungumza na wasaidizi wake hao wa kazi kazi, kule nje Nelly alianza kuchota mchanga kwa kutumia chepe na kuurushia eneo aliloelekezwa na Zakayo bila kujua Doreen alikuwa akimchungulia kupitia dirishani.
“Yaani siamini, huyu kaka na uhandsome wake wote huu na miwani juu anafanya kazi hii, lazima kaja hapa kumpeleleza baba yangu tu maana watu wa usalama wa taifa ni balaa,” Doreen aliwaza.
Wakati mrembo huyo anawaza hivyo, Nelly aliyechota mchanga kama chepe ishirini hivi alipozi na kujinyoosha mgongo kutokana na ugumu wa kazi aliyokuwa akifanya.
“Huyu siyo fundi mbona anaonekana kuchoka haraka,” Doreen aliyekuwa bado anamchungulia Nelly pale dirishani aliwaza.
Baada ya kupita kama dakika arobaini hivi tangu aanze kazi, Nelly alihisi kiu akaingia ndani walikokuwa wakifanya kazi fundi Yassin na akina Zakayo.
“Vipi Nelly, unaendeleaje? Hii kazi yetu haina udogo lakini utazoea kadiri siku zinavyokwenda,” fundi Yassin alimwambia.
“Sawa bro, ila nimebanwa na kiu sijui nitapata wapi maji ya kunywa?” Nelly alimwambia fundi Yassin.
Kwa kuwa mafundi hao walipokuwa wanahitaji maji ya kunywa waliwasaliana na Anne msichana wa kazi wa akina Doreen, Haruni alitoka na Nelly, akaanza kumwita Anne.
Licha ya kumuita mara kadhaa, Anne hakuitika ndipo Doreen alifungua dirisha na kumfahamisha kwamba Anne alikuwa ametoka kidogo.
“Poa dada, huyu fundi mgeni anahitaji maji ya kunywa,” Haruni alimwambia Doreen.
Baada ya kuambiwa hivyo, Doreen alimwambia sawa na kumtaka Nelly apite mlango wa uani kisha aingie jikoni.
Kwa kuwa Nelly hakufahamu mlango huo, alimuomba Zakayo ambaye alikuwa mwenyeji amuoneshe ndipo fundi huyo akamuonesha.
Nelly alizunguka nyuma ya nyumba hiyo na kuuona mlango wa kuingia jikoni alipotembea hatua kama mbili hivi mlango ulifunguliwa na Doreen, macho yao yalipogongana, kila mmoja akaachia tabasamu bila kujua sababu za kufanya hivyo.
“Samahani unataka maji ya baridi au ya moto?” Doreen alimwuliza Nelly ambaye tayari akili yake ilihama baada ya kuona shepu nzuri ya Doreen.
“Kwa hiki kijoto yabaridi yatakuwa mazuri,” Nelly alimwambia Doreen.
“Karibu usubiri ndani wakati nakuandalia,” Doreen alimwambia Nelly.
“Hapana sista wewe niletee tu hapa nje,” Nelly aliyekosa kujiamini alimwambia Doreen.
“Jamani wewe kaka ingia ndani unaogopa nini?” Doreen ambaye alikuwa akilindwa sana na wazazi wake asitoke nyumbani kuhofia wanaume wakware alimwambia Nelly.
 
SEHEMU-7
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale mtoto mkali Doreen alipombembeleza Nelly kwa sauti nyonyoro kwamba aliogopa nini kuingia ndani na kumsihi aingie kwani hakukuwa na tatizo. Je, baada kijana huyo sharobaro kuambiwa hivyo alisemaje? Tuwe pamoja kwenye utamu huu…
Kutokana na sauti nyororo ya kuhamasisha aliyoitoa Doreen, Nelly alijikuta akiwa jikoni mwa akina Doreen ambapo msichana huyo alimuongoza mpaka sebuleni kwao, kutokana na nguo aliyovaa kuchafuka kwa mchanga akawa hajui aketi wapi.
“Karibu ukae kwenye kiti,” Doreen alimwambia Nelly.
“Hapana sista wewe nipe nitakunywa wima, si unaona nilivyochafuka!” Nelly alimwambia Doreen.
Licha ya Nelly kutoa jibu hilo, Doreen ambaye ghafla alitokea kuvutiwa na kijana huyo kimapenzi kutokana na kupita muda mrefu bila kuduu alimlazimisha Nelly kukaa na kusisitiza kwamba hata sofa zingechafuka angemwambia Anne azifute.
Kitendo cha kubembelezwa kukaa na mtoto huyo ‘mtamu,’ Nelly alikaa sofani kitendo kilichomfurahisha sana Doreen ambaye alikwenda sehemu ya kulia chakula palipokuwa na jokofu na kuchukua jagi pamoja na glasi.
Alipofika alipoketi Nelly alizogeza stuli iliyokuwa pembeni ya kochi na kuiweka glasi, akafungua jagi na kumimina juisi nzito ya embe, akachukua glasi na kumkabidhi Nelly aliyebakia kaduwaa.
“Wewe si ulitaka maji, mimi nimependa unywe hii juisi,” Doreen mtoto aliyeumbwa haswa na kujaliwa kuwa na makalio f’lani hivi ya kiuchozi alimwambia Nelly.
“Da! Sikutegemea kama leo nitakutana na sapraizi ya namna hii, sina cha kuongezea zaidi ya kushukuru kwa ukarimu huu ambao sijapata kuuona,” Nelly alimwambia Doreen.
Wakati Nelly na Doreen wakipiga stori ndani, si fundi Yassin, Zakayo wala Haruni aliyekumbuka habari za Nelly kwani wakati huo walikuwa bize kwa kazi ya kuweka malumalu.
“Kuwa huru tu kaka, hapa nyumbani tumebaki wawili tu mimi na dada,” Doreen alimwambia Nelly huku akiwa anakwenda sehemu ya kulia chakula palipokuwa na kabati kubwa la vioo lililokuwa na vyombo.
Kwa kuwa muda huo, msichana huyo alivaa pensi iliyombana vyema na kusababisha wowowo lake la kiuchokozi kuonekana na bla nyepesi mfano wa singilendi iliyoonesha viembe sindano vyake, Nelly akachanganyikiwa kabisa.
“Aaa…duuu…aaa…,” Nelly alijikuta akiguna akiwa amelitumbulia macho eneo la nyuma la Doreen na kushindwa kuendelea kunywa juisi.
Doreen ambaye hakuwa na habari na kilichokuwa kikijiri nyuma yake, alipolifikia kabati la vyombo alisukuma vioo vya kusilaidi na kutoa glasi lakini ile anageuka Nelly alijifanya anakunywa juisi.
“Ngoja na mimi nikusaidie,” Doreen alimwambia Nelly wakati akimimina juisi juisi kwenye glasi yake kisha akaketi kwenye sofa aliloketi Nelly.
Kitendo cha msichana huyo kuketi karibu na sharobaro Nelly, kijana huyo alizidi kuchanganyikiwa ndipo Doreen alimwuliza kama kweli alikuwa fundi au alikuja pale kumpeleleza baba yake.
“Hapana sista, mimi nije kumpeleleza baba yako ili iweje wakati simfahamu na ndiyo mara yangu ya kwanza kufika hapa,” Nelly alimwambia Doreen.
“Ulivyo na kazi unayoifanya vitu viwili tofauti lazima nikutulie shaka,” Doreen alimwambia Nelly.
“Naomba usinifikirie hivyo, mimi siyo mpelelezi,” Nelly alimwambia Doreen.
Baada ya Nelly kumhakikishia hivyo Doreen, msichana huyo alitabasamu na kumwambia kama ni kweli itakuwa vizuri ndipo alimwuliza sababu za kuchagua kazi ya ufundi.
“Maisha tu dada, ila nilitamani sana kukaa ofisini niwe nafanya kazi kwa kutumia kompyuta lakini ndiyo hivyo,” Nelly alimwambia Doreen.
Kufuatia kijana huyo kumwambia hivyo Doreen, msichana huyo alimwuliza alifika kidato cha ngapi, Nelly alimwambia cha nne na kumweleza kila kitu hadi kufikia hatua ya kuwa pale.
“Unataka kuniambia leo ndiyo kwa mara yako ya kwanza kufanya kazi ya ufundi?” Doreen ambaye alimuonea huruma Nelly alimwuliza.
“Ndiyo hivyo,” Nelly alimjibu.
Baada ya kijana huyo kujibu hivyo, Doreen alikubaliana naye kwani alimuona jinsi alivyokuwa akijinyoosha kila alipochota mchanga na kuutupia eneo aliloelekezwa na Zakayo.
“Oke, sasa sina shaka na wewe, naomba nikuongeze juisi,” Doreen ambaye alipania kufikia hatua f’lani na Nelly alimwambia.
“Nashukuru sista inatosha,” Nelly alimwambia Doreen.
Licha ya kukataa, Doreen alimimina juisi na kujaza glasi aliyokuwa akitumia Nelly, lengo lake lilikuwa kumchelewesha kwani aliamini kitendo cha kuwa pamoja na Nelly angemtongoza tu!
“Ila wewe dada ni mkarimu sana, nashukuru kwa kunijali,” Nelly alimwambia Doreen.
 
SEHEMU-8
Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale Nelly alipomshukuru Doreen kwa ukarimu wake huku moyoni akipania kumtongoza dada huyo mrembo kwa sababu hakuwa na sera za kuwaacha watoto wazuri kama huyo. Je, baada ya Nelly kumshukuru, Doreen alisemaje? Tuwe pamoja kwenye utamu huu…
“Usijali kaka fundi, kuwa huru tena nilisahau kukuuliza, hivi ulikunywa chai?” Doreen alimwuliza.
“Kwa kuwa nimekunywa hii juisi nzito nimeshiba sihitaji chai,” Nelly alimwambia Doreen.
“Hakuna kitu kama hicho ngoja nikuandalie maziwa na sambusha ili utakapokwenda kuendelea na kazi uwe na nguvu,” Doreen alimwambia Nelly akainuka na kuelekea jikoni.
Kwa kuwa alipania kumpagawisha kijana huyo, wakati akielekea huko aliyatingisha kimitego makalio yake mapana kitendo kilichomchanganya kabisa sharobaro Nelly.
“Hakika nikiondoka hapa bila ya kumsomesha huyo mtoto mkali dhamira yangu itanisuta sana, siwezi kufanya upuuzi huo hata siku moja ukinzingatia wanawake wameletwa duaniani kwa ajili yetu wanaume,” Nelly aliwaza.
Wakati akiwaza hivyo, Doreen alirejea akiwa na sahani iliyokuwa na sambusa tatu na katika mkono wake wa kulia alibeba chupa ya wastani akajua ilikuwa ya maziwa.
“Huyu mtoto ninavyomuona kanikubali hata nielewa kabisa kama name sitaonesha uanaume wangu, tena akizubaa tu analambwa bakora leo hiihii,” Nelly alijisemea moyoni.
“Ukila hizi sambusa na maziwa ndiyo nitakuruhusu ukaendelee na kazi lakini kinyume chake sitajali cha fundi Yassin wala cha nani nitakufungia humu ndani hadi jioni,” Doreen alimwambia Nelly.
“Sista bwana unaonesha una vituko sana, haya ngoja nile sambusa kisha nikawajibike, jamaa wasije kusema nategea kazi,” Nelly alimwambia Doreen.
Nelly akiwa anatafuna sambusa ya kwanza kwa kutumia staili yake ya kuwalainisha mademu, alimwangalia Doreen kisha akamkonyeza kimtindo, si Doreen akaachia tabasamu.
Kufuatia Doreen kufanya hivyo, Nelly alimsifia kwamba alikuwa mzuri na alijaaliwa kuwa na shepu ya usumbufu ambayo ni wanawake wachache wanazo.
“Jamani shepu ya usumbufu ndiyo shepu gani hiyo?” Doreen alimwuliza Nelly kwa kumtega japo alijua alichomaanisha.
Baada ya kuambiwa hivyo, Nelly alimwambia Doreen asimame ili amuoneshe si mrembo huyo alisimama ndipo Nelly naye akasimama akazishika nyonga zake na kusema:
“Unaona kiuno kama hiki kilivyo? Hebu angalia na hipsi kama hizi, hakika Doreen umeumbika mno, nikutajie vingine?”
Kijana huyo ambaye wakati huo damu zilianza kumwenda mbio na kusahau kabisa kilichompeleka kule site alimwuliza Dorren ambaye alimwambia aendelee kwani hicho ndicho alichokuwa akikihitaji.
“Kingine hizi embe bolibo zako, mwanaume yeyote aliyekamilika akizigusa au kuzishika kabisa, atachanganyikiwa na hayo macho ni balaa tupu!” Nelly alizidi kumfagilia.
“Hivi kwa mfano nikikuruhusi uzishike utanganyikiwa?” Doreen alimwuliza Nelly.
“Siyo kuzishika tu, kwa kuziangalia tu hapa sipo sawa,” Nelly alimweleza Doreen na msichana huyo alipotupia macho kwenye eneo analokaa ‘mkuu wa kaya’ wa Nelly alitabasamu kwani mkuu huyo alikuwa kachangamka.
Kufuatia hali hiyo, Doreen aliyegundua tayari Nelly alipagawa, kumchanganya kabisa alimruhusu ashike embe bolibo yake ya kushoto aone kama kweli atachanganyikiwa.
Baada ya sharobaro Nelly kuambiwa hivyo, ilikuwa sawa na mbuzi kwenda kujilaza miguuni mwa mpika supu au embe dodo kuangukia miguuni mwa mtu, hakuchelewa hata sekunde moja.
Nelly alivamia chesti a.k.a kifua kitamu cha mrembo huyo na kuishika vizuri embe bolibo ya kushoto akaanza kuiminyaminya taratibu kwa staili ya nataka staki, Doreen akaanza kuhema na macho yake kumlegea.
Mpenzi msomaji, si unajua inavyotokea kichaa akiwa amepewa rungu kitakachofuatia, licha ya Nelly kupewa ruhusa ya kuishika embe bolibo moja Doreen, si akazitoa zote ‘out’ zikawa zinamtazama kama vile zilimwambia ‘shindwa mwenyewe.’
Kijana huyo aliyejaaliwa utundu wa malovee, mkono wake wa kushoto akawa anaichezea embe bolibo moja na kwa kutumia kinywa chake akawa anaifyoza nyingine, acha Doreen achachawe.
Kwa kuwa msichana huyo naye alikuwa amemisi sana mambo yetu yale, naye si akayavamia makazi ya mkuu wa kaya wa Nelly, sijui akawa anayafanye bwana, Nelly akaanza kuhema kwa kasi.
Wawili hao ambao wakati huo walikuwa wamehamia kwenye ulimwengu mwingine, waliendelea kufanyiana vurugu zote za mambo ya chumbani zaidi kwani Nelly alimpogusa hapa Doreen alimgusa pale.
Nelly alipogundua ile ilikuwa ni nafasi ya dhahabu ambayo hakuitegemea alimvutia Doreen kwenye sofa walilokalia awali lakini alipotupia macho kwenye stuli akaaishia kucheka baada ya kuona sambusa mbili na maziwa yakiwa nusu kwenye glasi.
“Kweli kila kitu na wakati wake, maziwa yatabaki kuwa maziwa, sambusa zitabaki kuwa sambusa, hapa ni kupeana raha tu na mtoto mkali,” Nelly alijisemea moyoni wakati huo alikwisha inyonyoa pensi ya Doreen na kumuacha mtoto huyo na nguo ambayo nashindwa kuitaja live.
Kwa kuwa nyumba hiyo ilikuwa kimya, Nelly aliamua kumchinjia baharini mtoto huyo mzuri palepale sofani lakini ile anamalizia kutoa kiwalo chake cha mwisho, akasikia akiitwa na Zakayo.
 
  • SEHEMU YA 9
  • Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale kama ambavyo Zakayo na Haruni walivyokuwa hawaamini kama kweli sharobaro Nelly angeweza kufanya kazi ya ujenzi, Dorren naye kushangazwa na jambo hilo ambapo moyoni alisema:
  • “Huyu kijana piga ua garagaza siyo fundi, nahisi atakuwa kaja kumpeleleza baba yangu, sijawahi kumuona sharabaro tena anayevaa miwani na mwenye dimponsi anafanya kazi za ujenzi.”
  • Wakati Doreen anawaza hayo, fundi Yassin na Nelly walibadilisha nguo na kuvaa za kufanyia kazi kisha fundi huyo alimwambia Zakayo amwelekeze Nelly kazi ya kufanya.
  • Baada ya Zakayo kuambiwa hivyo na kumuona Nelly akiwa kabadili nguo na kuvaa za kazi ambazo hata hivyo hazikuwa chakavu kama walizokuwa wakifanyia yeye na Haruni, kidogo aliamini kwamba Nelly pia alikuwa pale kikazi.
  • Kufuatia fundi kumwambia amwelekeze Nelly kazi ya kufanya, hakutaka siku hiyo ya kwanza kumpa kazi ngumu akamwelekeza ya kuzoa mchanga uliokuwa pembeni ya nyumba kubwa waliyoishi akina Doreen.
  • “Kaka wakati sisi tunaendelea na kazi ya kuweka malumalu ndani, wewe zoa huu mchanga na kuusogeza pale kwani kesho tunataraji kuanza kuweka malumalu hapa pote,” Zakayo alimwambia Nelly.
  • Kwa kuwa eneo ambalo ulikuwepo mchanga ambao Nelly aliambiwa hauzoe lilikuwa karibu na chumba alichokuwa akilala Doreen, msichana huyo mrembo alisikia maongezi yao.
  • Baada ya Zakayo kumwelekeza Nelly kazi ya kufanya akaingia nyumba kubwa walikokuwa wakiweka malimalu na kumkuta fundi Yassin akimwelekeza kazi ya kufanya Haruni.
  • “Vipi umemwelekeza?” fundi Yassin alimwuliza Zakayo.
  • “Tayari bro ila mpaka dakika hii siamini kama huyo kijana anaweza kufanya kazi hii ngumu tunayofanya, yule amekaa kimayaiyai,” Zakayo alimwambia fundi Yassin, wakacheka.
  • “Kwa kuwa kapigika kimaisha, kwa hiyari yake kanifuata na kuniambia anataka kuja kunisaidia kazi ili aweze kupata fedha, si unaelewa maisha ni fedha?” fundi Yassin aliwaambia.
  • “Ni kweli bro lakini kwa huyo kijana akimaliza siku tatu hapa nitajua kweli amedhamirilia,” Haruni alichagiza, wakacheka.
  • Wakati fundi Yassin akizungumza na wasaidizi wake hao wa kazi kazi, kule nje Nelly alianza kuchota mchanga kwa kutumia chepe na kuurushia eneo aliloelekezwa na Zakayo bila kujua Doreen alikuwa akimchungulia kupitia dirishani.
  • “Yaani siamini, huyu kaka na uhandsome wake wote huu na miwani juu anafanya kazi hii, lazima kaja hapa kumpeleleza baba yangu tu maana watu wa usalama wa taifa ni balaa,” Doreen aliwaza.
  • Wakati mrembo huyo anawaza hivyo, Nelly aliyechota mchanga kama chepe ishirini hivi alipozi na kujinyoosha mgongo kutokana na ugumu wa kazi aliyokuwa akifanya.
  • “Huyu siyo fundi mbona anaonekana kuchoka haraka,” Doreen aliyekuwa bado anamchungulia Nelly pale dirishani aliwaza.
  • Baada ya kupita kama dakika arobaini hivi tangu aanze kazi, Nelly alihisi kiu akaingia ndani walikokuwa wakifanya kazi fundi Yassin na akina Zakayo.
  • “Vipi Nelly, unaendeleaje? Hii kazi yetu haina udogo lakini utazoea kadiri siku zinavyokwenda,” fundi Yassin alimwambia.
  • “Sawa bro, ila nimebanwa na kiu sijui nitapata wapi maji ya kunywa?” Nelly alimwambia fundi Yassin.
  • Kwa kuwa mafundi hao walipokuwa wanahitaji maji ya kunywa waliwasaliana na Anne msichana wa kazi wa akina Doreen, Haruni alitoka na Nelly, akaanza kumwita Anne.
  • Licha ya kumuita mara kadhaa, Anne hakuitika ndipo Doreen alifungua dirisha na kumfahamisha kwamba Anne alikuwa ametoka kidogo.
  • “Poa dada, huyu fundi mgeni anahitaji maji ya kunywa,” Haruni alimwambia Doreen.
  • Baada ya kuambiwa hivyo, Doreen alimwambia sawa na kumtaka Nelly apite mlango wa uani kisha aingie jikoni.
  • Kwa kuwa Nelly hakufahamu mlango huo, alimuomba Zakayo ambaye alikuwa mwenyeji amuoneshe ndipo fundi huyo akamuonesha.
  • Nelly alizunguka nyuma ya nyumba hiyo na kuuona mlango wa kuingia jikoni alipotembea hatua kama mbili hivi mlango ulifunguliwa na Doreen, macho yao yalipogongana, kila mmoja akaachia tabasamu bila kujua sababu za kufanya hivyo.
  • “Samahani unataka maji ya baridi au ya moto?” Doreen alimwuliza Nelly ambaye tayari akili yake ilihama baada ya kuona shepu nzuri ya Doreen.
  • “Kwa hiki kijoto yabaridi yatakuwa mazuri,” Nelly alimwambia Doreen.
  • “Karibu usubiri ndani wakati nakuandalia,” Doreen alimwambia Nelly.
  • “Hapana sista wewe niletee tu hapa nje,” Nelly aliyekosa kujiamini alimwambia Doreen.
  • “Jamani wewe kaka ingia ndani unaogopa nini?” Doreen ambaye alikuwa akilindwa sana na wazazi wake asitoke nyumbani kuhofia wanaume wakware alimwambia Nelly.
 
SEHEMU YA 10

Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale sharobaro Nelly alipoiweka soda yake ya kopo juu ya dirisha bila kujua kama Doreen ambaye wakati huo alikuwa hajiwezi kufuatia kijana huyo kumpandisha joto la mahaba alikuwa dirishani kwa ndani akimwangalia. Je, kilifuatia nini?” Songa mbele na utamu huu…

Baada ya kuchota mchanga kama chepe kumi na kuzirushia eneo aliloelekezwa na Zakayo, Nelly alipozi kisha akajishika kiuno na kujinyoosha, kitendo hicho kilimhuzunisha sana Doreen.
“Jamani huyu kaka anaumia bure tu, ngoja kama ataendelea kuja hapa lazima nifanye mpango wa kumpa sapoti yoyote,” Doreen aliwaza.

Wakati Nelly akiendelea na kazi, Zakayo alifika kumwangalia, alivyomkuta akiwa kasimama akatabasamu na kujisemea moyoni ‘huyu kazi hii haiwezi na sijui kama kesho atakuja.’

Zakayo aliwaza hivyo bila kujua kama Nelly alipanga kufika pale site kila siku kwa vile palikuwa na mtoto mkali Doreen ambaye wao walikuwa wakimwangalia tu kama dada yao.

“Vipi, leo huu mchanga utaisha kweli?” Zakayo alimwuliza Nelly.
Nelly bila kumficha alimwambia kwa siku ile alichoka sana hivyo angemalizia siku iliyofuata, kufuatia kauli hiyo, Zakayo akacheka na kuingia ndani kumweleza fundi Yassin.

“Kwa kuwa ni mwanaume ataweza, si unajua hizi kazi unapoanza siku ya kwanza zinakuwa ngumu!” fundi Yassin alimwambia Zakayo.

Kufuatia kuelezwa hivyo, Zakayo alipinga na kumwambia fundi Yassin kwamba Nelly akimaliza wiki pale site atampatia shilingi elfu kumi, fundi Yassin akaishia kucheka.
Zakayo alipoingia ndani, Nelly alimalizia soda yake kisha akawafuata wenzake waliokuwa ndani na kushangaa jinsi walivyoweka marumaru katika vyumba viwili.
“Da! Nyie mnapiga kazi sana, kazi hii yote mmeifanya leo?” Nelly aliwauliza.

Fundi Yassin amjibu kwamba mbona walifanya kazi kidogo sana siku hiyo, Nelly akabaki akishangaa, fundi Yassin alipomuuliza kama alimaliza kuhamisha mchanga, akacheka sana na kumwambia atamalizia kesho yake.

Kwa kuwa fundi huyo alikuwa anauelewa usharobaro wa Nelly, hakumsema vibaya kwani alijua atazoea taratibu lakini kwa upande wa Zakayo alijisemea moyoni kwamba Nelly hakuwa mfanyakazi, sijui kwa nini hakumpenda kijana wa watu.

Baada ya kufanya kazi hiyo, Nelly hakuendelea tena na kazi ya kuhamisha mchanga hadi wenzake walipomaliza kazi na baada ya kuoga kwenye bafu la nje, fundi Yassin alikwenda kuonana na Doreen ambaye alimpa bahasha iliyokuwa na hela.

Baada ya kukabidhiwa alimpatia Zakayo shilingi 30,000 halikadhalika Haruni kisha akaiweka ile bahasha mfukoni, Nelly hakuwa na wasiwasi kwani alielewa kingeeleweka mbele ya safari.

Hata hivyo, Nelly alipenda kabla ya kuondoka amuone Doreen akawa anaplani kuhakikisha anafanikisha hilo, fundi Yassin alipowaambia waondoke akamwambia alihisi kiu hivyo ngoja akaombe maji ya kunywa.

“Wewe huna lolote, unataka umuone tu Doreen,” fundi Yassin alimwambia Nelly ambaye alicheka sana na kusema:

“Siyo hivyo bro hayo ni mawazo yako tu mbona mimi nina demu wangu mkali kumpita sijui huyo Doreen halafu mimi mtoto wa kishua kama huyo nitampa nini?” Nelly aliwaambia, wote wakacheka.

“Jamani muda unakwenda, hayo maji nitaenda kukununulia mbele ya safari, halafu kumbuka wewe hapa ni mgeni usije ukaleta picha mbaya bure,” fundi Yassin alimwambia Nelly bila kujua kama sharobaro huyo ilibakia kiduchu kula tende tamu za mtoto wa kishua.

“Haya mkubwa nimekuelewa, twendeni jamani,” Nelly aliwaambia.
Baada ya kutoa kauli hiyo, fundi Yassin aliwaambia waondoke wakatoka lakini wakiwa nje fundi Yassin aliyekuwa kamzoea Anne, dada wa kazi, alimwita ili amuage.
Licha ya kumwita Anne, aliitika Doreen ambaye alitoka nje fasta, na kumwuliza fundi; “Fundi ndiyo mnaondoka?”

“Yeah! Kesho tutafika mapema kuendelea na kazi,” fundi Yassin alimwambia Doreen bila kujua msichana huyo alikuwa na furaha moyoni ya kumuona Nelly.
“Hakuna shida, nawatakia safari njema,” Doreen ambaye alikuwa amevaa kama alivyovaa awali aliwaambia.

Baada ya kumuaga msichana huyo, fundi Yassin, Zakayo na Haruni wakatangulia Nelly alibaki nyuma ambapo aligeuka na kumkonyeza Doreen aliyeachia tabasamu pana.
Mafundi hao walipotoka getini walishika njia hadi ilipokuwa barabara kubwa ambapo Haruni ambaye alikuwa akiishi maeneo hayo aliwaaga wenzake kwamba wangekutana siku iliyofuata.

Baada ya kuagana haukupita muda mrefu daladala iliyotokea Kisauke lilifika, wote watatu walipanda, kwa kuwa siti zilikuwa wazi fundi Yassin na Nelly waliketi pamoja.
Kutokana na uchovu wa kazi, wakiwa kwenye daladala hilo hawakuwa na stori nyingi zaidi ya Nelly kuwatupia macho mademu wazuri aliowaona nje na wawili waliokuwemo ndani ya basi.

Walipofika njia panda ya Wazo Hill maarufu kama Kibaoni, Zakayo aliyekuwa akiishia Bunju alimuaga Yassin na Nelly ambapo fundi Yassin alimsisitiza kuwahi kufika kazini siku iliyofuata.
 
SEHEMU YA 12


Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale Nelly alipomwambia yule mrembo kwamba alikuwa na hela za kununulia simu ya kisasa hivyo dada huyo kubaini kwamba, Nelly alikuwa na kiasi kisichopungua shilingi laki mbili, akaamua kumpa namba zake kwa lengo la kumpiga mizinga mpaka akome. SONGA MBELE…

“Sasa hiyo namba utaindika wapi?” yule mrembo akamuuliza Nelly.
Nelly alicheka na kumwambia amtajie ataikariri, ndipo mrembo akamuuliza kama kweli anaweza kuikariri, Nelly akamwambia amtajie tu wala asihofu angeiweka kichwani.

Baada ya yule msichana kumtajia Nelly alimwambia alishaidaka na asingeisahau, mrembo alipomwambia amtajie Nelly akaitaja bila kukosea, mrembo akaishia kumpongeza kwa kuwa na kichwa chepesi.

Safari iliendelea ndipo fundi Yassin alibaini huko mbele ya safari dogo ambaye hakuwa na fedha kabisa angeumbuka, akageuka na kumwambia Nelly kwamba akifika Tandika atakwenda kumuona yule Mwarabu aliyemletea simu yake.
Nelly alijua nini kilikuwa kikiendelea baina yake na fundi wake, akamwambia sawa ndipo fundi akafungua pochi yake akachomoa wekundu watatu wa msimbazi na kumwambia aweke mfukoni.

Nelly alichukua fedha hizo akiwa anatabasamu na kuzisunda mfukoni huku akimsifia sana fundi wake kwa kujiongeza, basi lilipofika kwenye Mataa ya Veta, yule mrembo alimwambia Nelly kwamba, anasogea mbele kwani alikaribia kufika.

Baada ya kusema hivyo, sharobaro Nelly alimwambia asiwe na wasiwasi naye atashukia hapo kwani alikuwa akihitaji kwenda kumuona rafiki yake Mitaa ya Keko, Fundi Yassin alipomsikia Nelly akitoa kauli hiyo, akajisemea moyoni;
“Mrembo ameshaumia leo, sharobaro ana wekundu watatu mfukoni!”
Kweli gari lilipofika Kituo cha Keko Bora, Nelly alimuaga Fundi Yassin kwamba anakwenda kumuona jamaa yake watakutana nyumbani kisha wakateremka na yule mrembo.

Wakiwa wamesimama kituoni, Nelly alimuuliza yule mrembo kama alikuwa na haraka sana ya kwenda nyumbani, mrembo akamwambia siyo kivile kwa sababu dada yake alikuwa amesafiri.
“Yap! Habari kama hizi ndiyo napenda kuzisikia,” Nelly alijisemea moyoni.
“Kwa hiyo tunaweza kutafuta sehemu japo tupate kinywaji kisha kila mmoja aendelee na safari zake?” Nelly alimuuliza yule mrembo.

Kufuatia yule mrembo kumuona Nelly alikuwa yupo vizuri kifedha, alimwambia hakukuwa na ubaya ndipo kijana huyo ambaye alikuwa na usongo wa yale mambo yetu baada ya kumkosa Doreen akamwambia amfuate.
Wawili hao walivuka barabara na kuanza kurudi walikotokea kisha wakakata kulia na kuingia kibarabara cha mtaani ambapo hawakutembea umbali mrefu wakakuta baa, wakazama ndani.

Msichana huyo ambaye mpaka muda huo Nelly hakulifahamu jina lake, hakuelewa kama baa waliyoingia kwa nyuma ilikuwa na vyumba a.k.a machinjio, walipoketi tu mhudumu alifika na kuwauliza aliwahudumie nini!
Nelly aliagiza kilevi yule mrembo aliagiza soda, kabla mhudumu hajaondoka Nelly alimuuliza kama alikuwa hatumii kilevi, mrembo akamwambia huwa anatumia lakini kwa siku ile hakujisikia tu!
“Kufuatia kauli hiyo, Nelly alimwambia anapojisikia vizuri anakunywa kilevi gani akamtajia ndipo akamwambia mhudumu amletee kilevi hicho na kuachana na soda.

“Yaani besti mimi ninywe kilevi wewe unywe soda wapi na wapi? Wewe leo kunywa tani yako suala la fedha siyo tatizo,” Nelly alimwambia yule mrembo kisha akamwita mhudumu wa jikoni.
“Mimi niletee mchemsho wa kuku, wewe utapenda kula nini?” Nelly alimwagiza mhudumu na wakati huohuo akamuuliza mrembo wake alihitaji kula nini.

“Kama ulivyoagiza wewe,” mrembo akamwambia Nelly ambaye alifurahi sana kwani alijua jioni ile ya saa moja angemuua tembo kwa bua.“Mimi nafikiri ungeagiza tofauti na mimi ili kila mtu aonje chakula cha mwenzake, unaonaje?” Nelly alimuuliza yule mrembo.

“Oke, basi mimi niletee ulimi na ndizi mbili, ndimu na pilipili weka pembeni,” yule mrembo aliagiza.
Baada ya kutoa oda hiyo, Nelly alimwambia alifanya vizuri, wakaendelea kunywa pombe waliyoagiza na kuendelea na stori za hapa na pale ndipo mhudumu wa jikoni akaleta msosi.
Alipowanawisha wakaanza kula na kupiga stori huku moyoni Nelly akisema: “Wewe leo lazima nikugaragaze kwani mla vya watu na vyake huliwa.”

Nelly alikata kipande cha mnofu wa kuku na kutaka kumlisha yule mrembo ambaye alikwepesha mdomo na kumwambia ampe mkononi, kijana huyo akafanya hivyo.

“Lakini unajua umenikosesha raha, mimi nilitaka kukulisha wewe umekwepesha mdomo?” Nelly alimwambia.
“Sijapenda tu si unajua mambo hayo hufanyiana wapenzi na si kila mtu?” yule mrembo alimwambia Nelly bila kujua kama kauli yake ilimuumiza sana.
“Najua sana ila sioni kama kuna tatizo mimi kukulisha si namna ya kupoteza mawazo baada ya kazi,” Nelly alimwambia.

Wakati wawili hao wakizungumza, mhudumu wa vinywaji alifika na kuchunguza chupa zilizokuwa na kilevi na kubaini vilibaki kidogo akavimimina kwenye glasi na kumuuliza Nelly kama aongeze.
“Hicho ndicho kilichotuleta hapa, kuepusha usumbufu leta mbili kwa kila mmoja, zote ziwe za moto kama ulizoleta mwanzo,” Nelly alimwambia.
 
SEHEMU YA 13



Mpenzi msomaji, wiki iliyopita niliishia pale mhudumu alipofika katika meza waliyokaa Nelly na Atu kisha kutikisa chupa zilizokuwa na kilevi na kubaini kilibaki kidogo ndipo alimuuliza Nelly kama awaongeze, kijana huyo akamwambia alete mbili kwa kila mmoja na ziwe za moto kama za mwanzo.


Je, nini kilifuatia?


SONGA MBELE NA UTAMU HUU…



Yule mrembo aliposikia Nelly kaagiza aletewe bia nyingine mbili na kwa vile alikaa muda mrefu bila kupata ‘gambe’, akafurahi na kujisemea moyoni akimaliza kinywaji alichoagiza asingeendelea.
Bia zilipoletwa wakaendelea kula na kukata maji, kwa kuwa mlo walioagiza ulikuwa tofauti, kila mmoja akawa anachanganya, Nelly akichukua kipande cha ulimi, yule mrembo naye akawa ananyofoa mnofu wa kuku, ikawa burudani ya aina yake.


Walipomaliza kula, wakaendelea kukata maji ndipo bia za moto walizokuwa wakinywa zikaanza kupanda kichwani kwani mrembo akaongeza spidi ya maongezi na kuchekacheka hata kama Nelly hakuongea ishu ya kuchekesha.
“Yap! Chezea bia wewe, hivyo ndivyo nilikuwa nataka lazima ulipe fadhila za mfadhiliwa, mimi ndiyo Nelson a.k.a Nelly,” Nelly alijisemea moyoni.


Kijana huyo alipobaini mrembo maji yameanza kuchanganya kichwani alimuomba asogeze kiti chake karibu yake kwani alitaka kumwambia jambo f’lani.


“Wewe si uniambie tu jamani hilo jambo kwani mpaka tusogeleane?” msichana huyo aliyeitwa Atuganile aliyependa kukatisha jina lake na kujiita Atu alimwambia Nelly kwa sauti iliyozidiwa kwa kilevi.
“Kwani Atu kuna tatizo gani ukisogea hebu sogea bwana,” Nelly alimwambia msichana huyo mwenye shepu f’lani hivi ya kiuchozi.


Atu alipoambiwa hivyo akasema isiwe tabu akasogeza kiti chake na kukigusanisha na cha Nelly ndipo Nelly akampiga kibao cha mahaba shavuni ambacho kilimfurahisha Atu.
“Ila wewe unajua ni mchokozi sana, sawa tu!” Atu alimwambia Nelly.


“Mimi wala siyo mchokozi ila ukitaka nikuchokoze nitakuchokoza, unaniruhusu?” Nelly alimuuliza Atu.
“Hebu nichokoze niuone huo uchokozi wako,” Atu alimwambia Nelly na kuanza kucheka.
Nelly aliyekuwa amebanwa na haja ndogo aliinuka na kumwambia ngoja akajisaidie kwanza akitoka huko ndiyo atajua uchokozi wake, akaenda uani.


“Hana ujanja, ngoja nifanye fasta asije akatokea mtu akaenda kumsomesha nawaelewa sana wanaume wakware wa hili jiji,” Nelly aliwaza.Baada ya kumaliza kupunguza maji, alirejea walipokuwa wameketi na kusimama nyuma ya Atu aliyekuwa na kifua kilichobeba viembe bolibo vitamu sana, si akamwinamia mabegani na kuingiza mkono wake wa kulia ndani ya kitopu alichovaa Atu na kuishika embe bolibo ya kulia.


Kutokana na embe hiyo kuwa ya moto, Atu alipata raha sana na kwa upande wa Nelly ilikuwa hivyo, kijana wa Kisukuma alilitumia vyema giza lililokuwepo kuichezea embe hiyo hasa ncha yake, Atu akaanza kutoa mhemko wa raha!


Nelly alipogundua mashetani ya Atu yalikuwa eneo hilo, akaingiza mikono yake kifuani, akaanza kuzishika embe zote kwa pamoja na kuanza kuzipekecha, hapo ndipo mdada wa watu akaanza kuachia mayowe f’lani hivi yalioashiria alikuwa anahisi raha kuliko kawaida!


Kufuatia mihemko hiyo, Nelly aligundua kwamba mashetani ya dada huyo yalikuwa jirani hivyo kama angeendelea kumpagawisha, angeweza hata kuangua kilio na watu kupigwa butwaa!


Alichokifanya kijana huyo sharobaro, alichomoa mikono yake kifuani kwa Atu ambaye licha ya kuwepo kigiza Nelly aliweza kuyaona macho yake yalivyokuwa yamelege na kwenda kukaa kwenye siti yake.
Baada ya kukaa aliupitisha mkono wa kushoto maungoni mwa Atu na kumpa pole kwa alichomfanyia ndipo msichana huyo akamwambia muda ule alikuwa yupo katika hali mbaya.
“Hali mbaya kivipi?” Nelly alimuuliza swali la kizushi.


“Eti unaniuliza hali mbaya kivipi, kwani ulikuwa unafanyaje na kifua changu?” Atu alimuuliza.
Kufuatia dada huyo kutoa kauli hiyo, Nelly naye alimwambia hata yeye alikuwa katika wakati mgumu ndipo aliuchukua mkono wa Atu na kuupeleka kwenye makazi ya ‘mkuu wa kaya’.


Mtoto wa kike alipomgusa mkuu huyo wa kaya, akapatwa na hali ambayo nashindwa kuilezea kwani alipitisha muda mrefu bila ya kukutana naye, akaishia kusema: “Jamani wewe mbona mtundu namna hiyo!”
Nelly alipogundua kwamba hata kwa namna gani kwa hatua aliyofikia Atu asingeweza kumchomolea kama angehitaji mkomboti, alimuaga kwamba anakwenda msalani na kwenda moja kwa moja upande uliokuwa na vyumba a.k.a machinjio ambako alilipia rumu.


Baada ya kufanya hivyo alimfuata Atu na kumuomba msamaha kwamba wahamie eneo la ndani ambalo lilikuwa tulivu kwa wao kufanyiana chochote kuliko pale walipokuwa wamekaa.


Kutokana na pombe kumpanda kichwani, kujumlisha na namna ambavyo mwili ulikuwa umemchemka kihisia, dada wa watu hakubisha, alinyanyuka na kumfuata nyuma Nelly kama mwanakondoo aliyekuwa akipelekwa malishoni.
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom