China yatajwa zaidi katika ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani barani Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,008
1,030
1637542862954.png

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Anthony Blinken, amemaliza ziara yake katika nchi tatu za Afrika, baada ya kutembelea Kenya, Nigeria na Senegal. Ziara ya Bw. Blinken inafanyika wakati Marekani inajaribu kuonyesha kuwa inarudi kwenye ulingo wa siasa za kimataifa kuhusu Afrika baada ya aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump, kuiweka Afrika
pembeni.

Kurudi kwa Marekani japo kunaonekana kama ni jambo zuri ambalo linaweza kutoa mchango wa kuhimiza maendeleo na utulivu barani Afrika, kunakaribishwa kwa uangalifu kwani bado haiko wazi kama Marekani itakuwa na mtazamo mpya kuhusu Afrika, au kama mtazamo wake utaendelea kuwa kama uleule uliokuwepo kabla ya Rais Donald Trump.

Mara nyingi Afrika imekuwa ikipewa umuhimu mdogo kwenye sera za kidiplomasia za Marekani, sio siri kipaumbele cha Marekani kwenye sera yake ya mambo ya nje kiko Ulaya, Asia na Amerika kusini. Afrika inakumbukwa na Marekani pale inapoona kuwa Afrika inaweza kutumiwa kama jukwaa la kuhatarisha usalama wake. Hali hii inatajwa na baadhi ya wachambuzi kuwa imetoa mwanya kwa wadau wengine kimataifa, kuziba ombwe linalotokea kutokana na kutokuwepo kwa Marekani.

Hali hii ni tofauti sana na China ambayo kwa karibu miaka 50 mfululizo, Afrika imekuwa moja ya vipaumbele muhimu katika sera ya mambo ya nje ya China. Kwa zaidi ya miongo mitatu sasa waziri wa mambo ya nje wa China amekuwa akifanya ziara yake ya kwanza barani Afrika kila mwaka, hali hii imeonyesha kuwa sera ya China kuhusu Afrika, ni endelevu na mambo yanayohusu ushirikiano yamekuwa yakiongezeka.

Katika hali ya kushangaza, karibu kila kipengele kinachotajwa kuhusu ziara ya Bw. Blinken barani Afrika, kinahusishwa na China. Kwa mfano tovuti ya usnews.com imesema ziara ya Bw. Blinken ina lengo la kuonyesha kuwa Marekani ni mdau muhimu wa kikanda na wa kimataifa katika kulinda amani na kuhimiza demokrasia, wakati ikishindana na China. Kama ni kweli Marekani ameipa umuhimu Afrika kutokana na kutaka kushindana na China, basi nchi za Afrika zitakaribisha kurudi kwa Marekani, kushirikiana na nchi jumuiya ya kimataifa kutatua changamoto zilizopo。

Jambo lingine ambalo pia limevutia ufuatiliaji, ni jinsi ya kuutangaza mpango unaoitwa “Build Back Better”, (BBB) mpango ambao umetangazwa kama ni mbadala wa pendekezo la “Ukanda mmoja, njia moja” (BRI). Lakini undani wa mpango huo hadi sasa ni utata, hauko wazo kama pendekezo la “ukanda mmoja, njia moja”. Tovuti ya usnews.com imefikia hatua ya kudhihaki mpango huo, kuwa hata Rais Joe Biden mwenyewe haielewi vizuri mpango huo mpya wa Marekani utatekelezwa vipi. Badala ya kuita mpango huo BBB, tovuti hii imefikia hatua ya kuita mpango wa uharibifu wa haraka ya RRR – (Ruin Republic Rapidly).

Pamoja na kuwa kila nchi inatakiwa kuangalia maslahi yake wakati inashirikiana na nchi nyingine, kilichoifanya sera ya China kwa Afrika ipate uungaji mkono na kuwa na ushawishi barani Afrika, ni pande mbili kujadiliana. Mpango wa “Ukanda mmoja, njia moja” sio mpango wa China kushindana na nchi nyingine Afrika na sio mpango wa China kutekeleza nia yake barani Afrika. Ni mpango ambao pande mbili zinakaa na kujadiliana kwa usawa kuangalia miradi gani inatakiwa kutekelezwa, na pande mbili zinajaribu kuangalia maslahi ya pande zote mbili kwenye mradi huo.

Ukweli ni kwamba nchi za Afrika zimepiga hatua kubwa kwenye maswala ya usalama na demokrasia, licha ya changamoto za hapa na pale zinazoendelea kujitokeza. Changamoto kubwa kwa nchi za Afrika ziko kwenye suala la maendeleo ya kiuchumi. Ushirikiano kati ya China na Afrika unaolenga kutatua changamoto zinazowakabili moja kwa moja watu wa Afrika ndio siri ya mafanikio ya sera ya China kwa Afrika.

Kama sera ya Marekani ikiendelea kufuatilia mambo yake ambayo hayasaidii kutatua changamoto zinazowakabili watu wa Afrika, basi ijue nafasi yake barani Afrika itaendelea kuwa finyu, na nafasi ya wale wanaojali itaendelea kuwa kubwa.
 
Hali hii ni tofauti sana na China ambayo kwa karibu miaka 50 mfululizo, Afrika imekuwa moja ya vipaumbele muhimu katika sera ya mambo ya nje ya China. Kwa zaidi ya miongo mitatu sasa waziri wa mambo ya nje wa China amekuwa akifanya ziara yake ya kwanza barani Afrika kila mwaka, hali hii imeonyesha kuwa sera ya China kuhusu Afrika, ni endelevu na mambo yanayohusu ushirikiano yamekuwa yakiongezeka.
Of course China haiwezi kuwa na influence popote duniani zaidi ya wajinga Afrika. China haiwezi kuna influence Ulaya be it West or East. Asia wanamuona China kama masikini mwenzao, nina uzoefu na Thailand kuhusu China.

South America huko ndiko hajulikanni kwa lolote la maana be it politically, econmically or socially hakuna mwenye ushawishi naye.

Ni kwa washenzi Afrika ndiko anakotamba na bidhaa cheap and below standards rubbishes.
 
Back
Top Bottom