China yasema iko tayari kushirikiana na Serikali ya Wataliban

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
9,147
33,299
Dunia imejaa fitina, wakati Marekani kafungasha virago vyake huko Afghanistan na kuwaachia Wataliban wakijitwalia ushindi mnono na kujiandaa kuunda serikali, China yasema iko tayari kushirikiana na Serikali ya Wataleban.

Wakati nchi kadhaa zikiwa kwenye hatihati za kufunga balozi zao, Urusi yasema Ubalozi wake utaendelea kuwepo Kabul. Wakati hayo yakitokea Ujerumani yajuta na kusema yanayotokea Afghanistan kwa sasa Ni aibu kubwa Sana kwa NATO.

Wanazuoni tunajiuliza Marekani alifuata Nini Huko? Je malengo yake yametimia?

Watalibani wanarudi Tena madarakani baada ya kufurushwa miaka takriban 20 iliyopota. Marekani aliondoka Vietnam kiajabu, aliondoka Korea kiajabu, aliondoka Cuba kiajabu, aliondoka Somalia kiajabu, aliondoka Iraq kiajabu, aliondoka Syria kiajabu.

Kwa hiyo Marekani karidhia aliowaita magaidi kurudi Tena Ikulu? Kwangu Mimi Wataleban hawakuwa magaidi Ila walimkaribisha gaidi Osama bin Laden na kundi lake la Al Qaida.

Wakati huo Wataliban wakiongozwa na Mullah Omar Mohamed na Osama bin Laden Raia wa Saud Arabia/yemen akiongoza kundi la Al Qaida.

Bin laden ndio aliyesimamia shoo ya kulipua balozi za Marekani zilizopo Dar es salaam na Nairobi, kulipua meli ya Marekani Yemen na kuteketeza majengo marefu zaidi mawili duniani WTC wakati ule, kulipua makao makuu ya Jeshi yanayolindwa zaidi duniani pentagon na kusudio lililoshindwa la kulipua majengo muhimu ya Marekani.

Osama bin laden alipewa hifadhi na Watalaban huko Afghanistan na ndio ikapelekea Marekani kwenda huko kumsaka na hatimae kumuua.

Marekani ilikusudia kuwafuta kabisa wafadhili wa maficho ya Osama Wataliban ili asije akatokea Osama mwingine akapewa hifadhi huko.

Marekani ilimuandama rafiki kipenzi wa Osama Mkuu wa Watalaban ndugu Mullar Omar Mohamed kiongozi wa Kiroho wa Talaban hatimae inasemekana alifia mafichoni.

Lakini watalibani bado wapo,na Leo hii wamerudi madarakani. Malengo ya Marekani yametimia au ilikua Ni kuchoma noti tu, na kupoteza vijana wa kimarekani?

"Lone survivor"
 
Ahmad Shah Massoud aliyekuwa assassinated na Taliban mwaka ambao ndiyo USA ilishambuliwa na Osama, alikuwa anafavour mfumo wa maisha ya kidemokrasia ikiwemo kuwapa wanawake haki sawa na wanaume.

USA ilienda kuwatwanga Taliban kwasababu ya kumhifadhi Osama lakini pia siasa za Masoud ziliivutia USA ndiyo maana wakausaidia upande wa Masoud kuunda serikali ya Afghanistan.

Lakini waafghanistan wanaume waliowengi hawakupenda huo mfumo wa maisha ,ulionekana unakinzana na dini. Walikuwa ni masnitch wakikamua mkwanja wa USA kwa kuimarishiwa jeshi lao hata kulipwa mishahara kutoka USA.

Biden ana haki ya kuwaacha wataliban wachukue nchi kwani inaonyesha serikali ya Afghanistan ilikuwa inawaunga mkono Taliban. Haiingii akilini ,,serikali yenye jeshi(trained soldiers) na vifaa vya kisasa zikiwemo ndege kushindwa kurusha hata risasi moja dhidi ya wanamgambo wenye siraha duni hadi ikulu inatekwa.

Naona Biden kaonya Taliban wasijaribu kumgusa mmarekani yeyote. Kawambia atawajibu kwa haraka na kwa kishindo.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Unao ufahamu lakini hautoshi kuzungumzia suala la "ugaidi".

Hayo unayoyasema kuhusu Osama bin laden ni yale ambayo umeaminishwa tu. Hakuna sehemu Marekani na NATO wakaenda "kulinda/kurudisha" amani halafu sehemu hiyo isivurugike.

Sasa na hawa ndugu zetu Chadema na waendelee kudhani kwamba Marekani ndio mtetezi wa mambo yao hapa nchini.
 
Dunia imejaa fitina, wakati Marekani kafungasha virago vyake huko Afghanistan na kuwaachia Wataliban wakijitwalia ushindi mnono na kujiandaa kuunda serikali, China yasema iko tayari kushirikiana na Serikali ya Wataleban...
Huyo muvi uliyoitaja hapo mwisho nikikumbuka huyo Shaah alivyokua anachinja vichwa vya watu duh
 
Kwani Marekani nani anampa kibali cha kwenda kulinda nchi za watu? Kuna majeshi gani ya nchi zingine ndani ya mipaka ya Marekani?
Mzee shule iliingia vzur kwel...hebu soma vzur marekan china.russia uingereza na wengne wan role gan umoja wa mataifa halaf ndio uulize tena swal lako
 
Ahmad Shah Massoud aliyekuwa assassinated na Taliban mwaka ambao ndiyo USA ilishambuliwa na Osama, alikuwa anafavour mfumo wa maisha ya kidemokrasia ikiwemo kuwapa wanawake haki sawa na wanaume...
Uko sahih sana...biden kawashtukia..kaona isiwe tabu...na uskute hata huyo rais wa afghan anakaa meza moja na wa tali...wao ni kwamba hawatak US aendelee kuwepo eneo hilo.

wakichkua mlungula kutoka russia na kwengne wameona eeeh bwana eeh liwalo na liwe..jeshi la serikal limeambiwa, tulien tulieni msijib mashambuliz jifanyen mme sarenda..hahaha...asiee michezo hii
 
Kufanya biashara ya madawa ya kulevya.
Halaf watu weng hawajui...marekan huko afghan..iraq..na kwengneko ambajo wanaonekana wanajeshi wao...zile ni private companies yaan watu binafsi wanakua na makampuni ya ulinz.

Yaan jeshi kamili kabisa na silaha zotee. Ni makampun ya ma bilionea wa kimarekan..wanafanyaga michezo michafu tu huko...yaan marekan akishaingilia nchi flan..baada ya vita...bas hzo private companies huomba hzo tenda za ulinzi huko ndio maana wale askar wa jesh wanaokwenda huko huwa hawaish sabab ni donge nono

Askar analipwa mara 10 zaid anavyolipwa na serikal..ndomana unaona hawaish kwenda huko unajiuliza wamarekan hawachoki? Yaan sawasawa serikal ya Tz iseme tunaruhusu makampuni binafsi yawe na walinz level ya jeshi halaf muende mkasaidie vita congo na sehem zingne zenye migogoro. .mshahara ni donge nono...uone jins watu watakavyo changamkia fursa...mshahara unalipwa 15m. Hata ni ntaenda
 
Hiyo nchi ina Pia utajiri wa maliasli unaokadiliwa kufikia trilion 3 za marekani hivyo kuna kitu wamevuna wanaondoka
Sio kweli ni Opiem tu na ishu za ugaid na ujasus ..ujue afghan iko karib sana na russia so unatembea tu ya mguu..marekan kafukia na ku install nukes kwenye milima kule inayoangalia russia...mda wowote anauwezo wa kuishambulia russia kikinuka
 
China anataka awakopeshe hao magaidi wakishindwa kulipa watatandikwa wasahau makobazi uani
 
Unao ufahamu lakini hautoshi kuzungumzia suala la "ugaidi".

Hayo unayoyasema kuhusu Osama bin laden ni yale ambayo umeaminishwa tu. Hakuna sehemu Marekani na NATO wakaenda "kulinda/kurudisha" amani halafu sehemu hiyo isivurugike
Sasa ww humu Chadema imekujaje wakati tunaelewa anayeharibu Amani yetu ni chama chetu cha CCM na Police
 
Back
Top Bottom