China yapata pigo,Tanzania na Kenya zasitisha miradi ya mabilioni

ze kokuyo

JF-Expert Member
Jan 24, 2014
7,418
9,599
China yapata pigo baada ya nchi za Tanzania na Kenya kusitisha miradi ya mabilioni ya dola.

Rais Magufuli wa Tanzania alieleza sababu kuu ya kusitisha mradi wa bandari ya Bagamoyo ambayo ingefadhiliwa na Uchina ni masharti magumu na ya kinyonyaji.

Nchi nyingi zimeanza kupitia upya miradi ya China zikiwemo Malaysia,Pakistan, Ethiopia kufuatia madai ya China kuziingiza nchi kwenye madeni makubwa yasiyolipika kwa lengo la kutwaa rasilimali na maeneo muhimu ya nchi kama vile bandari nk.
Malaysia ilisitisha miradi ya mabilioni ya dola ikieleza kwamba ubora na thamani ya miradi hiyo haiendani na kiwango ambacho China ilipanga kukitumia kuijenga.

Nchi za magharibi pia imekua ikiitupia lawama China kwa kuziweka nchi masikini kwenye lindi la madeni lakini China imekua ikipuuzia tuhuma hizo.

Mwaka 2018 China ilitwaa bandari ya Srilanka ambayo itaimiliki kwa kipindi cha miaka Mia moja sababu nchi hiyo ilishindwa kulipa mkopo iliyochukua toka Uchina.

Nchi za Africa zimetajwa kupendelea mikopo ya Uchina sababu haina masharti magumu kama Ile ya nchi za magharibi
 
vocha za bure vocha za bure kabsa

Utaratibu wa kupata vocha hizo ni huu


1.fungua link hii itakupeleka playstore uta download app hii inaitwa dent


2.baada ya ku install usiifungue kwanza rudi uje ku click link hii upya then link itakupeleka tena kwenye app uliyokwisha download


3.baada ya hapo utaweka namba yako ya simu unayotaka ipate kifurushi


4.uta login baada ya hapo utapewa dent coin ambazo zina viwango mbali mbali za voucher so kuendana na idadi ya dent utachague kiwango cha voucher kwenye app na itatumiwa inbox hapo hapo


kiwango cha coin utakachopewa ni 1600 ambapo utweza kuweka voucher ya 5000

Ila ukijiunga na link unapata kiwango kidogo cha coin
 
Exit China,Enter USA. Balozi wa Marekani akihojiwa citizen Tv ameapa mradi wa NRB Mombasa highway utakuwa wa kupigia mfano.Asilimia 90 waajiriwa Kenyans.
Lakini China miradi yao 95% ya malighafi zinatoka kwao na 90% ya wafanyakazi ni wa wachina na bado ukishindwa kulipa wanakuchukulia bandari au uwanja wa ndege
 
Afrika hawawezi kukwepa demokrasia kwa gharama ya misaada ya China na kujitegemea pia hatuwezi lazima tuweke tu demokrasia hatuna namna. Development is no a bed of roses.
 
EWE UNAOEIPONDA CHINA, JUZI SERIKALI YAKO IMEPEWA BILIONI 60 HUKO, ENDELEA KUIPONDA CHINA WAKATI ROOM YAKO UNAYOLALIA IMEJAA VITU VYA KICHINA NA SIM YAKO PIA NI YA KICHINA, HUWEZI KUISHI BILA YA MCHINA WW ACHA BLABLAAA
Screenshot_20190628_144250_com.gbinsta.android.jpeg
Screenshot_20190628_144242_com.gbinsta.android.jpeg
 
Kwani mitumba inatoka wapi Mkuu kama sio kwa haohao West. Wachina wataletaje mitumba wakati wao wenyewe wana watu wengi sana masikini wanazihitaji hizo nguo.
Sawa kabisa mkuu wangesema lazima terms and conditions zizingatiwe ndio tupatiwe mitumba! Wangekuja wa mwambie Jiwe wewe tunakupa suti safi aliyo vyaa John F. Kennedy na jiwe angefurahia na kutoa Makinikia bure!!!
Hawo jamaa wa Magharibi ni washenzi Kweli kweli!
 
Sawa kabisa mkuu wangesema lazima terms and conditions zizingatiwe ndio tupatiwe mitumba! Wangekuja wa mwambie Jiwe wewe tunakupa suti safi aliyo vyaa John F. Kennedy na jiwe angefurahia na kutoa Makinikia bure!!!
Hawo jamaa wa Magharibi ni washenzi Kweli kweli!
Hahaha ila fundi25 kwani mitumba tumeanza kuvaa leo,si tangu kipindi hicho China haina hata ndoto ya kua superpower jamaa wa west walikua wakitupatia mitumba
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Hahaha ila fundi25 kwani mitumba tumeanza kuvaa leo,si tangu kipindi hicho China haina hata ndoto ya kua superpower jamaa wa west walikua wakitupatia mitumba
Mkuu walikuwa wanaileta mingine kupitia mashirika Yao kama wanavyo tuletea misaada inayoitwa kwa Hisani ya watu wa marekani!! China kaja kupindua kila kitu mkuu Adi leo kama sio mchina ungekuwa na album za picha kama 20 au pengine mia
Umepiga mapicha style kibao !!
Jama wahuni kweli kweli! Simu janja tungezisikia redioni!
 
Lakini China miradi yao 95% ya malighafi zinatoka kwao na 90% ya wafanyakazi ni wa wachina na bado ukishindwa kulipa wanakuchukulia bandari au uwanja wa ndege
Cha kushangaza ni kwa nini viongozi wetu wanakubali Mikataba ya aina hiyo?Rushwa bila kupatiwa dawa vizazi vitatekea kwa uroho wa viongozi wachache.Vifungo virefu
bila fine labda yaweza saidia
 
Mkuu walikuwa wanaileta mingine kupitia mashirika Yao kama wanavyo tuletea misaada inayoitwa kwa Hisani ya watu wa marekani!! China kaja kupindua kila kitu mkuu Adi leo kama sio mchina ungekuwa na album za picha kama 20 au pengine mia
Umepiga mapicha style kibao !!
Jama wahuni kweli kweli! Simu janja tungezisikia redioni!
Hamna kitu kama hicho Mkuu,Hizo teknolojia zote ni za West huko China zilipelekwa kwa ajili ya uunganishwaji sababu ya gharama.

Hata ukiangalia simu za kichina sensor, software na vitu vingine vingi waanagiza toka kampuni za kimagharibi kama vile Sony, Samsung,Google, Qualcomm, Intel,ARM,nk
 
Cha kushangaza ni kwa nini viongozi wetu wanakubali Mikataba ya aina hiyo?Rushwa bila kupatiwa dawa vizazi vitatekea kwa uroho wa viongozi wachache.Vifungo virefu
bila fine labda yaweza saidia
Kutokomeza hilo ni kufanya taasisi za nchi ziwe na nguvu kwa kua Katiba bora. Bunge na Mahakama viwe na nguvu na vijitegemee hapo tutafika. Hata ukiangalia China ukiiba ni shaba tu hata kama ulikua kiongozi mkubwa Serikalini
 
Lakini China miradi yao 95% ya malighafi zinatoka kwao na 90% ya wafanyakazi ni wa wachina na bado ukishindwa kulipa wanakuchukulia bandari au uwanja wa ndege
Balozi amesisitiza mradi mwelekeo wake teach a man to fish zaidi-Give a man a fish, and you feed him for a day. Teach a man to fish, and you feed him for a lifetime.
 
Back
Top Bottom