China yajibu mapigo-Yapandisha kodi kwa bidhaa za USA

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,034
28,201
China yalipiza kisasi kwa kuongeza ushuru kwa bidhaa za Marekani

China imesema leo kuwa itaongeza ushuru kwa bidhaa za Marekani za thamani ya dola bilioni 60 kuanzia Juni mosi, katika hatua ya kujibu duru ya karibuni ya Marekani kuongeza ushuru kwa bidhaa za China na mipango ya Marekani kuzilenga bidhaa zote zinazoingizwa nchini mwake kutoka China.

Tangazo hilo limekuja baada ya mazungumzo ya karibuni kabisa ya biashara kati ya Marekani na China kumalizika Ijumaa bila makubaliano, na baada ya Marekani kuongeza ushuru kwa bidhaa za China za thamani ya dola bilioni 200.

Licha ya hatua hiyo ya kulipiza kisasi, China imeonekana kutoa muda zaidi wa hadi Juni mosi. Ushuru mpya utazilenga bidhaa kadhaa za Marekani kuanzia asilimia tano hadi 25. Jibu la China limetangazwa mara tu baada ya Trump kuionya kutolipiza kisasi.

Awali, msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya China Geng Shuang alisema kuwa China hitawahi kusalimu amri kwa shinikizo la kimataifa.

==================

China has decided to impose tariffs of 25 percent, 20 percent and 10 percent on certain U.S. products starting June 1, announced the Customs Tariff Commission of the State Council in a statement issued Monday.
The tariffs will be targeting U.S. goods worth 60 billion U.S. dollars, the statement said, adding that the products under five percent tariff cap would not be affected by this round of tariffs.

SOURCE: CGTN
 
Hapo ni sawa na israel na palestina, mwenzako ameua watu wako ishirini wewe uliyeua mmoja ndiyo unashangilia ushindi, marekani wameweka tariffs za zaidi ya 460 billions of dollars na wamesema china wakilipa kisasi wataweka tariffs kwenye bidhaa zote za china sasa hapo nani ataumia
 
Hapo ni sawa na israel na palestina, mwenzako ameua watu wako ishirini wewe uliyeua mmoja ndiyo unashangilia ushindi, marekani wameweka tariffs za zaidi ya 460 billions of dollars na wamesema china wakilipa kisasi wataweka tariffs kwenye bidhaa zote za china sasa hapo nani ataumia
Tatizo la wana ccm wanajinasibisha na china wakidhani kwamba china akifanikiwa ndo Tanzania kafanikiwa kupitia CCM, hawajui kwamba wote ni mabeberu tu na wao ni mbuzi jike
 
sasa inatusaidia nini sisi watanzania.
Next time we have to engage our minds when thinking about strategic issues which are related to our economies.
Kila mwamba ngozi huvutia kwake. It is all about surving, and for a very long time
 
China has decided to impose tariffs of 25 percent, 20 percent and 10 percent on certain U.S. products starting June 1, announced the Customs Tariff Commission of the State Council in a statement issued Monday.
The tariffs will be targeting U.S. goods worth 60 billion U.S. dollars, the statement said, adding that the products under five percent tariff cap would not be affected by this round of tariffs.

SOURCE: CGTN
Hapo ni sawa na mwenzako anakohoa kidogo ili kurekebisha koo lakini wewe unajamba kwa nguvu ili kumkomoa
 
China has decided to impose tariffs of 25 percent, 20 percent and 10 percent on certain U.S. products starting June 1, announced the Customs Tariff Commission of the State Council in a statement issued Monday.
The tariffs will be targeting U.S. goods worth 60 billion U.S. dollars, the statement said, adding that the products under five percent tariff cap would not be affected by this round of tariffs.

SOURCE: CGTN
The Chinese are meaningless!

Msuli wao wa uchumi bado haujajaza kama wa USA!
 
Ila mkuu unajua China hata asipouza nje bidhaa zake watu wake tu wanaweza kununua na uchumi ukaendelea kukua kama kawaida

Si kweli mzazi

Export kubwa kabisa ya China inaenda USA na wala sio Africa au Europe au Asia kama unavyodhani..

Wakinyimwa USA basi taabu tupu itafuata na EU maana EU ni vijakazi wa USA,akisema ruka vinasema how high!

Soko la USA is the biggest to Chinese!
 
Si kweli mzazi

Export kubwa kabisa ya China inaenda USA na wala sio Africa au Europe au Asia kama unavyodhani..

Wakinyimwa USA basi taabu tupu itafuata na EU maana EU ni vijakazi wa USA,akisema ruka vinasema how high!

Soko la USA is the biggest to Chinese!
Najua mkuu kuanzia magari simu kuku mavyuma ya viwandani hadi maji ya kunywa mkuu
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom