China yaisaidia Afrika kuingia katika “zama za 5G"

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG41603709553.jpg

Hivi karibuni, China imeweka hatua mpya katika kuzisaidia nchi za Afrika kuendeleza mageuzi ya kidijitali. Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Zambia ya MTN imeshirikiana na Huawei ya China kuzindua mtandao wa majaribio wa 5G, na kuifanya nchi hiyo kuwa miongoni mwa nchi za awali barani Afrika kuwa na mtandao wa 5G. Hapo awali, mtandao huru wa kibiashara wa 5G ambao Huawei ilishiriki katika ujenzi ulianza kutumika nchini Afrika Kusini na Kenya.

Katika sekta ya mawasiliano ya simu duniani, Huawei bila shaka ni mshindani asiyetarajiwa. Marekani ilipotumia nguvu yake kutawala sekta hiyo na kutoza ada kubwa za hataza, Huawei ilivunja ndoto ya Marekani kwa teknolojia bora zaidi ya mawasiliano ya 5G. Tangu wakati huo, Marekani imekuwa ikianza vita vya 5G. Kwa upande mmoja, imeweka vikwazo vya kiteknolojia katika chip dhidi ya Huawei, na kwa upande mwingine, imeweka shinikizo kwa nchi mbalimbali kukataa kutumia vifaa vya mawasiliano vya 5G vya Huawei, kwa kisingizio cha ushauri wa moyo mwema. Lakini, uwongo huu ulifichuliwa hivi karibuni na waziri wa zamani wa biashara wa Uingereza Vince Cable. Alisema uamuzi wa serikali ya Uingereza kupiga marufuku matumizi ya vifaa na huduma za 5G za Huawei "hauna uhusiano wowote na usalama wa taifa", bali ulichochewa na shinikizo la Marekani. Wakati alipokuwa madarakani, idara za ujasusi na usalama za nchi hiyo zilituma maafisa wa ujasusi kufanya kazi ndani ya Huawei, lakini hitimisho linabaki kuwa matumizi ya huduma za Huawei hayaleti hatari yoyote.

Mwezi Disemba mwaka jana, Rais Xi Jinping wa China alitoa hotuba kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 8 wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOFAC, ambapo ushirikiano wa uchumi wa kidijitali unachukua nafasi kubwa. Aliahidi kuwa China itaisaidia Afrika kutekeleza miradi 10 ya uchumi wa kidijitali. Wakati janga la Covid-19 linazuia mtiririko wa biashara duniani huku likileta ongezeko la mahitaji ya huduma za kidijitali, teknolojia na huduma za kidijitali zitakuwa eneo muhimu la ushirikiano kati ya China na Afrika. Kwa Afrika, hii inamaanisha hitaji la dharura la kuboresha miundombinu yake ya kidijitali, na uwepo wa kampuni za teknolojia ya China barani Afrika hufanya bidhaa za China kuwa na soko.

Katika miaka ya hivi karibuni, ushirikiano kati ya China na Afrika katika uvumbuzi wa kisayansi na kiteknolojia umepata maendeleo makubwa. Mjini Dakar, ambako mkutano wa FOFAC ulifanyika, China imejenga kituo cha data kwa ajili ya kuhifadhi data na mifumo ya kidijitali ya serikali ya Senegal, ambayo itahamishwa kutoka kwenye seva nchini Marekani na Ulaya. Rais wa Senegal Macky Sall alisema hatua hiyo itaimarisha uhuru wa nchi yake kidijitali. Vituo kama hicho pia vimejengwa katika nchi nyingi za Afrika kama vile Tanzania, Mali na Madagaska. Hadi sasa, China imetia saini makubaliano ya ushirikiano wa kiteknolojia baina ya serikali na nchi 16 za Afrika.

Mbali na teknolojia, Transsion, kampuni ya simu yenye makao yake makuu mjini Shenzhen, China inayojulikana sana barani Afrika imefungua njia inayowawezesha waafrika kuungana na mtandao wakati wowote. Kulingana na kampuni ya utafiti wa soko ya Marekani IDC, kutokana na uhaba wa vipuri unaowakabili wazalishaji kupunguza ahueni katika soko la simu za kisasa, utoaji wa simu mahiri barani Afrika ulipungua kwa 2.3% katika robo ya tatu ya 2021 kutoka robo iliyotangulia. Hata hivyo, Transsion iliongoza katika mauzo ya simu za mkononi barani Afrika kwa 47.4% katika robo hiyo, wakati Samsung ilikuwa ya pili kwa 21.3% na kampuni nyingine ya simu ya China Xiaomi kwa 6.1%.

Aidha, teknolojia ya China pia imechangia sana kuenea kwa kasi kwa pochi za kidijitali kwa watu kutuma pesa kupitia simu za kisasa barani Afrika. Kwa mfano, M-Pesa, mtoa huduma mkuu wa huduma ya pesa kwa simu za mkononi barani Afrika, imetumia suluhu za biashara za Huawei. Opera, kivinjari cha kampuni ya Beijing Kunlun Technology, imekuwa na ushirikiano na kampuni ya OPay ya biashara ya mtandaoni na malipo ya Nigeria.

Mabadiliko ya kidijitali yanatoa fursa kwa maendeleo ya kiuchumi ya Afrika. Kuanzia ujenzi wa mtandao wa 5G na vituo vya data hadi biashara ya simu za mkononi, kampuni za China zinatoa uungaji mkono wa pande zote. Haishangazi kwamba wahandisi wa Marekani ambao wamebahatika kutembelea historia na maendeleo ya 5G ya Huawei walisema kwamba ikiwa Marekani haikufanikiwa, inawezekana kuwa itakuwa nyuma ya nchi za Afrika.
 
Hakuna msaada hawajafanya kwa bahati mbaya.

Walijenga HQ ya AU Addis Ababa and they install a lot of sound bugs.
 
Hakuna msaada hawajafanya kwa bahati mbaya.

Walijenga HQ ya AU Addis Ababa and they install a lot of sound bugs.
Una siri gani kama kila kitu unategemea misaada tu...........labda awasikilize wale wanao msnitch kwa mabepari
 

Hivi karibuni, China imeweka hatua mpya katika kuzisaidia nchi za Afrika kuendeleza mageuzi ya kidijitali. Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Zambia ya MTN imeshirikiana na Huawei ya China kuzindua mtandao wa majaribio wa 5G, na kuifanya nchi hiyo kuwa miongoni mwa nchi za awali barani Afrika kuwa na mtandao wa 5G. Hapo awali, mtandao huru wa kibiashara wa 5G ambao Huawei ilishiriki katika ujenzi ulianza kutumika nchini Afrika Kusini na Kenya.

Katika sekta ya mawasiliano ya simu duniani, Huawei bila shaka ni mshindani asiyetarajiwa. Marekani ilipotumia nguvu yake kutawala sekta hiyo na kutoza ada kubwa za hataza, Huawei ilivunja ndoto ya Marekani kwa teknolojia bora zaidi ya mawasiliano ya 5G. Tangu wakati huo, Marekani imekuwa ikianza vita vya 5G. Kwa upande mmoja, imeweka vikwazo vya kiteknolojia katika chip dhidi ya Huawei, na kwa upande mwingine, imeweka shinikizo kwa nchi mbalimbali kukataa kutumia vifaa vya mawasiliano vya 5G vya Huawei, kwa kisingizio cha ushauri wa moyo mwema. Lakini, uwongo huu ulifichuliwa hivi karibuni na waziri wa zamani wa biashara wa Uingereza Vince Cable. Alisema uamuzi wa serikali ya Uingereza kupiga marufuku matumizi ya vifaa na huduma za 5G za Huawei "hauna uhusiano wowote na usalama wa taifa", bali ulichochewa na shinikizo la Marekani. Wakati alipokuwa madarakani, idara za ujasusi na usalama za nchi hiyo zilituma maafisa wa ujasusi kufanya kazi ndani ya Huawei, lakini hitimisho linabaki kuwa matumizi ya huduma za Huawei hayaleti hatari yoyote.

Mwezi Disemba mwaka jana, Rais Xi Jinping wa China alitoa hotuba kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 8 wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOFAC, ambapo ushirikiano wa uchumi wa kidijitali unachukua nafasi kubwa. Aliahidi kuwa China itaisaidia Afrika kutekeleza miradi 10 ya uchumi wa kidijitali. Wakati janga la Covid-19 linazuia mtiririko wa biashara duniani huku likileta ongezeko la mahitaji ya huduma za kidijitali, teknolojia na huduma za kidijitali zitakuwa eneo muhimu la ushirikiano kati ya China na Afrika. Kwa Afrika, hii inamaanisha hitaji la dharura la kuboresha miundombinu yake ya kidijitali, na uwepo wa kampuni za teknolojia ya China barani Afrika hufanya bidhaa za China kuwa na soko.

Katika miaka ya hivi karibuni, ushirikiano kati ya China na Afrika katika uvumbuzi wa kisayansi na kiteknolojia umepata maendeleo makubwa. Mjini Dakar, ambako mkutano wa FOFAC ulifanyika, China imejenga kituo cha data kwa ajili ya kuhifadhi data na mifumo ya kidijitali ya serikali ya Senegal, ambayo itahamishwa kutoka kwenye seva nchini Marekani na Ulaya. Rais wa Senegal Macky Sall alisema hatua hiyo itaimarisha uhuru wa nchi yake kidijitali. Vituo kama hicho pia vimejengwa katika nchi nyingi za Afrika kama vile Tanzania, Mali na Madagaska. Hadi sasa, China imetia saini makubaliano ya ushirikiano wa kiteknolojia baina ya serikali na nchi 16 za Afrika.

Mbali na teknolojia, Transsion, kampuni ya simu yenye makao yake makuu mjini Shenzhen, China inayojulikana sana barani Afrika imefungua njia inayowawezesha waafrika kuungana na mtandao wakati wowote. Kulingana na kampuni ya utafiti wa soko ya Marekani IDC, kutokana na uhaba wa vipuri unaowakabili wazalishaji kupunguza ahueni katika soko la simu za kisasa, utoaji wa simu mahiri barani Afrika ulipungua kwa 2.3% katika robo ya tatu ya 2021 kutoka robo iliyotangulia. Hata hivyo, Transsion iliongoza katika mauzo ya simu za mkononi barani Afrika kwa 47.4% katika robo hiyo, wakati Samsung ilikuwa ya pili kwa 21.3% na kampuni nyingine ya simu ya China Xiaomi kwa 6.1%.

Aidha, teknolojia ya China pia imechangia sana kuenea kwa kasi kwa pochi za kidijitali kwa watu kutuma pesa kupitia simu za kisasa barani Afrika. Kwa mfano, M-Pesa, mtoa huduma mkuu wa huduma ya pesa kwa simu za mkononi barani Afrika, imetumia suluhu za biashara za Huawei. Opera, kivinjari cha kampuni ya Beijing Kunlun Technology, imekuwa na ushirikiano na kampuni ya OPay ya biashara ya mtandaoni na malipo ya Nigeria.

Mabadiliko ya kidijitali yanatoa fursa kwa maendeleo ya kiuchumi ya Afrika. Kuanzia ujenzi wa mtandao wa 5G na vituo vya data hadi biashara ya simu za mkononi, kampuni za China zinatoa uungaji mkono wa pande zote. Haishangazi kwamba wahandisi wa Marekani ambao wamebahatika kutembelea historia na maendeleo ya 5G ya Huawei walisema kwamba ikiwa Marekani haikufanikiwa, inawezekana kuwa itakuwa nyuma ya nchi za Afrika.
Trump aliwaweza Huawei aliwalima sunctions mpaka wamepotea
 
5G na hizi bei zetu za data tutaweza? Si itakuwa ukigusa tu, unapata message, umeshatumia 75% ya bando lako.
 
Back
Top Bottom