China yaendelea kulinda na kudumisha utamaduni wake usioonekana

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
996
1,016
VCG111334583179.jpg
Leo tarehe 14 Juni ya mwaka huu ni Sikukuu ya mbio za mashua ya Dragon au sikukuu ya mbio za mashua ya joka, ambayo ni sikukuu ya jadi ya China. Sikukuu hii ambayo imewekwa kwenye orodha ya urithi wa utamaduni usioonekana ya Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO, si ngeni kwa watu wa Afrika Mashariki. Kabla ya kuibuka kwa Janga la COVID-19 ilifanyika nchini Uganda mwaka 2017, 2018 na 2019 na kuwaleta pamoja wachina na watu wa nchi za Afrika Mashariki wa nchi zinazolizunguka ziwa Victoria.

Mwaka 2004 China iliposaini mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu kulinda urithi wa utamaduni usioonekana, ilikuwa ni moja ya nchi yenye hazina kubwa ya urithi huo. Na sensa moja iliyofanyika kati ya mwaka 2005 hadi 2009, ilionyesha kuwa China ilikuwa na raslimali zaidi ya laki 8.7 za utamaduni usioonekana. Kuanzia hapo China ilirasimisha taratibu mbalimbali za kuhakikisha kuwa urithi huo unalindwa, unadumishwa na unarithishwa. Sasa China imekuwa na jumla ya vitu 42 vya urithi wa utamaduni usioonekana vilivyoidhinishwa na UNESCO.

VCG111334522637.jpg

Pamoja na kuwa China ina utamaduni wenye nguvu wenye historia ya zaidi ya miaka 5000, kulinda utamaduni wake (hasa urithi wa utamaduni usioonekana) kwenye mazingira ya sasa ya dunia ya utandawazi, si jambo rahisi, ni kazi ngumu inayohitaji juhudi za mtu mmoja moja, jamii nzima na hata serikali. Lakini ni kwanini tunatakiwa kulinda utamaduni usioonekana, na utamaduni huu una umuhimu gani kwetu?

Kwanza tunatakiwa kukumbuka kuwa utambulisho wetu (identity) hautokani na mwonekano wetu au eneo la kijiografia tunaloishi peke yake, bali pia unatokana na mila, desturi na sanaa tulizorithi kutoka kwa mababu zetu vizazi kadhaa vilivyopita, kwa hiyo kulinda vitu hivyo kuna maana kuwa tunalinda utambulisho wetu na asili zetu. Leo tunaweza kusema China inatajwa sana duniani kutokana na nguvu kubwa ya kiuchumi, lakini inawezekana kuwa kungfu/Taiji, chakula cha kichina, matamasha ya jadi China, ndio utambulisho mkubwa wa China na wachina katika nchi nyingine duniani kwa muda mrefu hata kabla ya China kuwa na nguvu ya kiuchumi.

Pili, tunatakiwa kukumbuka kuwa kwa sasa tunaishi kwenye dunia ambayo ni kuna hatari kubwa ya urithi wa utamaduni usioonekana kuweza kupotea kirahisi. Kutokana na kupanuka kwa miji na watu kujihusisha na shughuli za kujiingizia vipato kama ajira za viwandani, kwenye makampuni, au hata kuhamia kwenye maeneo ya miji ambayo hakuna mvuto mkubwa wa kuendeleza urithi wa utamaduni usioonekana, kazi ya kutunza urithi wa utamaduni inakuwa ngumu zaidi. Kwa hiyo tunatakiwa kutumia njia mbalimbali za kisasa na hata za jadi kuhakikisha urithi wa utamaduni wa jadi unarithishwa

Tatu, tunatakiwa kukumbuka kuwa uanuai wa utamaduni usioonekana ni furaha ya sisi binadamu. Kwa kawaida binadamu anakuwa na furaha zaidi anapoona mambo mapya na kujifunza mambo mapya. Tukiangalia sababu za watu kwenye kutalii katika miji na sehemu nyingine duniani, tunaweza kuona kuwa kubwa zaidi ni kujionea vitu tofauti na hata kujaribu uzuri wake. Kama utamaduni wa dunia nzima ungekuwa wa aina moja, basi dunia yetu ingekuwa ya namna moja na isingekuwa ya kufurahisha.

Hali ya kufurahisha ni kuwa China inatambua umuhimu wa urithi wa utamaduni usioonekana, imekuwa inachukua hatua mbalimbali za kulinda urithi wa utamaduni usioonekana kwa kutumia sheria, kama vile kutambua sikukuu maalum za jadi kisheria, au kuwawezesha watu wanaorithisha utamaduni usioonekana. Lakini vile vile imekuwa ikihimiza ushirikiano na nchi za nje katika mambo ya utamaduni kwa ujumla.

China pia imekuwa mshirika mkubwa wa UNESCO, na kuunga mkono juhudi za shirika hilo, ikitambua kuwa tunatakiwa kujitahidi kujenga jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja, ambayo urithi wa utamaduni usioonekana wa kila jamii, unadumishwa, unarithishwa na unakuwa na manufaa kwa dunia nzima.
 
Hayo yote ni kama matambiko ya chinese magic ama chinese shamanism...

Unless kama uchawi nao uitwe ni utamaduni
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom