China yaendelea kujiamini katika kutimiza ustawi wa Xinjiang licha ya nchi za Magharibi kujaribu kuipaka matope

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,006
1,026
VCG111314654336.jpg

Na Pili Mwinyi

China Jumapili ilitoa waraka mweupe ukilenga mahsusi kuonesha mwenendo wa idadi ya watu wa mkoa wa Xinjiang, ambapo kwa mujibu wa takwimu za sensa ya saba ya taifa, idadi ya watu wa makabila madogo mkoani humo imeongezeka haraka sana kwa wingi pamoja na watu wake kuwa na maisha bora, na pia kuonesha kuwa idadi ya watu wa kabila la Uygur imeongezeka kutoka milioni 3.61 ya mwaka 1953 hadi milioni 11.62 katika mwaka 2020. Ushahidi huu unadhihirisha uongo na kukanusha shutuma zinazotolewa na nchi za magharibi ikiwemo Marekani kwamba eti China imefanya “mauaji ya halaiki” huko mkoani Xinjian.

Waraka huo ambao umepewa jina la" Mwenendo wa Idadi ya watu na Takwimu mkoani Xinjiang," ni wa kwanza kutolewa na Ofisi ya Habari ya Baraza la Taifa tangu mwaka 2015 ambao unabainisha wazi maendeleo ya idadi ya watu mkoani Xinjiang katika kipindi cha miaka saba. Pia ni wa 10 kutolewa na Ofisi ya Xinjiang, ambapo waraka wa awali uliotolewa uligusia maeneo ya mafanikio ya haki za binadamu, mafunzo ya ufundi na vituo vya elimu, ajira na hatua za kupinga ugaidi.

Waraka huu umetolewa ili kuonesha hali halisi ya Xinjiang kutokana na maneno ya uzushi na minong’ongo kutoka nchi zisizoipendelea China kwa lolote lile inalofanya. Miongoni mwa watu hao kuna wasomi kadhaa ambao wana mitazamo hasi juu ya Xinjiang na kuongea mambo ambayo hayapaswi kuongewa na wataalamu kama hao. Mathalan msomi Adrian Zenz, yeye alitaja takwimu za kiwango cha ukuaji cha Wauygur kutoka 2017 hadi 2018, ambacho kinaonesha kupungua na kusema kwamba China, inadidimiza viwango vya uzazi vya watu wa makabila madogo. Kauli kama hizi zinaonesha chuki za waziwazi, kwani akiwa kama msomi ambaye hana utaalamu wa idadi ya watu, alipaswa kukaa chini na kufanya utafiti ndipo atoe maelezo yake, na sio kutafuta ushahidi wa kijuujuu tu ili kuipaka matope China.

Ni ukweli usiofichika kwamba maendeleo ya uchumi na ya kijamii huwa yanapelekea kupungua kwa kiwango cha uzazi. Na ukiangalia viwango vya uzazi vya China nzima sasa vimepungua na kuwa 1.6‰ mwaka 2018 na ndio maana China imebadili tena sera yake ya uzazi na kuruhusu wazazi kuzaa watoto watatu kwani awali ilikuwa mtoto mmoja, baadaye ikabadilika kuwa wawili.

Mabadiliko ya idadi ya watu wa China pia yanaakisi mwenendo wa mabadiliko duniani, mathalan ukiangalia Marekani, kwa mujibu wa sensa ya hivi karibu viwango vya uzazi vya nchi hiyo vimepungua kwa miaka sita mfululizo. Na mwenendo wa hali ya Xinjiang, kama sehemu nyingine za China na dunia, umebadilika kutoka viwango vikubwa vya uzazi na vifo hadi viwango vidogo vya uzazi na vifo, na mabadiliko hayo yanachangiwa na mambo mengi.

Sababu moja muhimu ni maendeleo ya kiuchumi na kijamii mkoani Xinjiang, ambayo yanaweza kuonekana kwa wakazi katika viwango vya elimu, hasa kwa wasichana. Awali wasichana wenye umri wa miaka 15 walipomaliza shule ya sekondari ya chini walikuwa wakiolewa, na kuzaa watoto hadi watatu. Lakini kutokana na elimu inayotolewa kwa wanawake katika miaka ya hivi karibuni, sasa wasichana wachache sana wenye umri kati ya miaka 15 na 19 ndio wanaolewa na kuzaa.

Hatua za Xinjiang za kupambana na ugaidi na itikadi kali pia zimesaidia kuwakomboa wanawake kwani wengi wao sasa wanatoka majumbani na kwenda kufanya kazi ili kujipatia pesa. Hivyo madai kama haya ambayo “hayana kichwa wala miguu” yanalenga kuipaka sifa mbaya China. Watafiti na wanaharakati kutoka China, Pakistan na Uingereza pia wamekemea vikali na kukosoa kauli mbaya kuhusu Xinjiang. Wataalamu wanakubaliana na takwimu kuhusu maendelo ya Xinjiang na kushadidia ule msemo kwamba “ukweli ukidhihiri uongo hujitenga” hivyo takwimu hizo zinajionesha wazi hasa katika kukua kwa idadi ya watu, kuboreka kwa viwango vya maisha, afya na elimu kwa watu wa makabila madogo.

Carlos Martinez, mtafiti wa kujitegemea na mwanaharakati wa mambo ya kisiasa, amesema madai haya yanayotoka kwa Adrian Zenz, na Taasisi ya Mikakati ya Sera ya Australia (ASPI), yanalenga vita baridi na mambo ya kijeshi ya Pacific. Vyanzo vyake si vya kuaminika kabisa. Ni vyombo vya “vita vya habari” vinavyotumiwa na Marekani na washirika wake.

Historia na hali halisi vimethibitisha kuwa siku hizi Xinjiang inafurahia kipindi kizuri zaidi cha ustawi na maendeleo katika historia. Ni vigumu kwa mtu ambaye hajawahi kufika mkoani humo na hasa kwa wale wanaosikiliza kauli zinazotolewa na upande mmoja tu yaani nchi za Magharibi wanaweza kuamini kirahisi, lakini kwa wale waliobahatika kwenda na kujionea jinsi maisha ya watu wa Xinjiang yalivyobadilika kwa kiasi kikubwa, watakubali kuwa Xinjiang ya miaka ya nyuma sio ya sasa. Serikali ya China imewapatia wakazi wa huko uhuru wa kuabudu bila kujali ni kabila gani, kuwajengea nyumba, kuondoa familia za wafugaji kwenye umasikini ambapo sasa zimekuwa zikifanya kazi na hata kumiliki nyumba na magari ya kifahari.

Hivyo bila kujali nchi au watu wasioitakia mema China wanasema nini, serikali ya China itaendelea kuhimiza umoja, maelewano na maendeleo ya utamaduni, na kujitahidi kuifanya Xinjiang iwe na ustawi na kuelekea kuwa mkoa wa kisasa, mambo ambayo hayatazuiwa na nguvu yoyote ile ya nje, na mustakabali wake unaong’ara uko salama salimini.
 
Baada ya kufuatili mada zako kadhaa, sasa nimejua una uhusiano na ubalozi china tanzania, sio kwa hii propaganda.....umetumwa kivingine...
sisi tunaona kila kukicha jinsi waislamu wa uyghur wanavyofanywa na serikali ya china...
Utakuwa unalipwa wewe kufanya hivi..si bure...

1661608691274.png

1661608718928.png

1661608785513.png

1661608816317.png

1661608845505.png
 
Back
Top Bottom