China yabeba jukumu muhimu la kuwa nchi inayohimiza amani katika Afrika na dunia kwa ujumla

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
1642724292037.png
China inaendelea kuonesha umuhimu wake duniani hasa katika bara la Afrika baada ya kutangaza kwamba itateua mjumbe maalumu katika pembe ya Afrika, ambayo imekuwa ikikabiliwa ni migogoro kila uchao. Hii pia inaonesha kwamba nchi hii kubwa ya Asia ina wasiwasi na hali ya usalama katika kanda hiyo.

Katika ziara yake iliyomalizika hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi ameweka mbele Mpango wa China wa kuhakikisha Maendeleo ya Amani katika Pembe ya Afrika. Ikiwa ni pamoja na kuimarisha mazungumzo ya kikanda ili kuondokana na changamoto za kiusalama, kuharakisha ufufuaji wa kikanda ili kuondokana na changamoto za maendeleo na kutumia njia muafaka ili kuondokana na changamoto za kiutawala.

Ili kuisaidia kanda hiyo kutimiza amani na ustawi wa muda mrefu, Bw. Wang alisema China itachagua mjumbe maalumu atakayeshughulikia masuala ya Pembe ya Afrika kwa lengo la kutoa uungaji mkono wa lazima kwenye suala hili, na kusisitiza kuwa China haitaingilia kati mambo ya pembe hiyo, badala yake amezishauri nchi za kanda hiyo kuamua hatma yao na kuzitaka Ethiopia, Somalia na Sudan kufanya mazungumzo ya amani kwa ajili ya kuhimiza ujenzi wa amani.

Pembe ya Afrika ina eneo maalumu la kimkakati na lenye uwezo mkubwa wa maendeleo, lakini bahati mbaya katika miaka ya karibuni, migogoro imekuwa ikiibuka mara kwa mara. Hali hii haiendani kabisa na maslahi ya watu wa kanda hiyo na haipaswi kuendelea zaidi.

Mwaka 2007, serikali ya China iliteua Mwakilishi maalumu wa Masuala ya Afrika. Mwakilishi huyo alishiriki kikamilifu kwenye juhudi za upatanishi katika Afrika na kubeba jukumu kubwa barani humo katika masuala ya kuleta amani na usalama. Wakati China imeshakuwa na uzoefu wa uwakilishi wake katika Afrika, mjumbe huyu mpya pia anatarajiwa kusaidia kuboresha amani na maendeleo ya Afrika.

Kanda hiyo ambayo imeonekana kuzidi kuumiza vichwa vya watu katika siku za karibuni, imekuwa ikipokea wawakilishi maalumu mbalimbali ili kuhakikisha utulivu na amani wa eneo hilo, lakini inaoonekana kama “donda ndugu ambalo ni vigumu kutibika”.

Tangu kuzuka kwa mgogoro wa Tigray, Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy amekuwa akikataa kile kinachoitwa "mgogoro wao kuufanya wa kimataifa". Amelikataa jopo la watu mashuhuri waliopendekezwa na Umoja wa Afrika kuhimiza mazungumzo na kukataa maombi mawili ya Mwakilishi maalumu wa Marekani katika kanda hiyo Bw. Feltman ya kuwa na mazungumzo ya pande mbili.

Juhudi za Mjumbe wa AU Bw. Obasanjo zilionekana kugonga mwamba, licha ya kwamba rais huyo wa zamani alisafiri kwenda nchi nyingi duniani zikiwemo Marekani na Ulaya, kwa lengo la kutaka kuungwa mkono katika juhudi zake za upatanishi, ambazo Waethiopia wanaona hiyo ni njia ya kuingilia kati mambo ya nchi yao. Kwa Ethiopia, ufumbuzi wa mgogoro wake na kundi la TPLF ni hadi pale jamii ya kimataifa itakapoacha kuishinikiza nchi hiyo na badala yake ilichukulie hatua kundi la TPLF.

Hadi sasa mgogoro huo umesababisha vifo vya maelfu ya watu, mbali na kuwalazimisha mamilioni ya watu kuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi. Pande hizo mbili zinazozozana nchini Ethiopia kwa miezi kadhaa sasa zimekataa katakata upatanishi wa jumuiya za kikanda na kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.

Ni matarajio yetu kwamba China ambaye ni mshirika mkubwa wa kiujenzi wa nchi za Afrika, ambaye siku zote anaweka mbele sera ya kutoingilia mambo ya nchi nyingine, itafanikiwa katika kuleta amani ya kanda hiyo. China pia inafuata misingi yake ya kwamba waafrika wajiamulie masuala yao wao wenyewe, na kuunga mkono haki ya nchi za Afrika na Umoja wa Afrika kubeba jukumu la uongozi katika masuala ya amani na usalama wa Afrika.
 
Marekani na NATO vimemshindwa Mchina kwa sababu wao wamemudu kutuliza political gimmicks za kukimbizana kila baada ya miaka michache kwenye harakati za uchaguzi ambazo kimsingi ni njia ya kuharibu fedha, kuvuruga amani, kupandikiza chuki na kusambaratisha maendeleo yaliyokuwa yameanza kustawi hadi hapo--just in the name of an animal called DEMOCRACY!
 
China inaendelea kuonesha umuhimu wake duniani hasa katika bara la Afrika baada ya kutangaza kwamba itateua mjumbe maalumu katika pembe ya Afrika, ambayo imekuwa ikikabiliwa ni migogoro kila uchao. Hii pia inaonesha kwamba nchi hii kubwa ya Asia ina wasiwasi na hali ya usalama katika kanda hiyo.

Katika ziara yake iliyomalizika hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi ameweka mbele Mpango wa China wa kuhakikisha Maendeleo ya Amani katika Pembe ya Afrika. Ikiwa ni pamoja na kuimarisha mazungumzo ya kikanda ili kuondokana na changamoto za kiusalama, kuharakisha ufufuaji wa kikanda ili kuondokana na changamoto za maendeleo na kutumia njia muafaka ili kuondokana na changamoto za kiutawala.

Ili kuisaidia kanda hiyo kutimiza amani na ustawi wa muda mrefu, Bw. Wang alisema China itachagua mjumbe maalumu atakayeshughulikia masuala ya Pembe ya Afrika kwa lengo la kutoa uungaji mkono wa lazima kwenye suala hili, na kusisitiza kuwa China haitaingilia kati mambo ya pembe hiyo, badala yake amezishauri nchi za kanda hiyo kuamua hatma yao na kuzitaka Ethiopia, Somalia na Sudan kufanya mazungumzo ya amani kwa ajili ya kuhimiza ujenzi wa amani.

Pembe ya Afrika ina eneo maalumu la kimkakati na lenye uwezo mkubwa wa maendeleo, lakini bahati mbaya katika miaka ya karibuni, migogoro imekuwa ikiibuka mara kwa mara. Hali hii haiendani kabisa na maslahi ya watu wa kanda hiyo na haipaswi kuendelea zaidi.

Mwaka 2007, serikali ya China iliteua Mwakilishi maalumu wa Masuala ya Afrika. Mwakilishi huyo alishiriki kikamilifu kwenye juhudi za upatanishi katika Afrika na kubeba jukumu kubwa barani humo katika masuala ya kuleta amani na usalama. Wakati China imeshakuwa na uzoefu wa uwakilishi wake katika Afrika, mjumbe huyu mpya pia anatarajiwa kusaidia kuboresha amani na maendeleo ya Afrika.

Kanda hiyo ambayo imeonekana kuzidi kuumiza vichwa vya watu katika siku za karibuni, imekuwa ikipokea wawakilishi maalumu mbalimbali ili kuhakikisha utulivu na amani wa eneo hilo, lakini inaoonekana kama “donda ndugu ambalo ni vigumu kutibika”.

Tangu kuzuka kwa mgogoro wa Tigray, Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy amekuwa akikataa kile kinachoitwa "mgogoro wao kuufanya wa kimataifa". Amelikataa jopo la watu mashuhuri waliopendekezwa na Umoja wa Afrika kuhimiza mazungumzo na kukataa maombi mawili ya Mwakilishi maalumu wa Marekani katika kanda hiyo Bw. Feltman ya kuwa na mazungumzo ya pande mbili.

Juhudi za Mjumbe wa AU Bw. Obasanjo zilionekana kugonga mwamba, licha ya kwamba rais huyo wa zamani alisafiri kwenda nchi nyingi duniani zikiwemo Marekani na Ulaya, kwa lengo la kutaka kuungwa mkono katika juhudi zake za upatanishi, ambazo Waethiopia wanaona hiyo ni njia ya kuingilia kati mambo ya nchi yao. Kwa Ethiopia, ufumbuzi wa mgogoro wake na kundi la TPLF ni hadi pale jamii ya kimataifa itakapoacha kuishinikiza nchi hiyo na badala yake ilichukulie hatua kundi la TPLF.

Hadi sasa mgogoro huo umesababisha vifo vya maelfu ya watu, mbali na kuwalazimisha mamilioni ya watu kuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi. Pande hizo mbili zinazozozana nchini Ethiopia kwa miezi kadhaa sasa zimekataa katakata upatanishi wa jumuiya za kikanda na kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.

Ni matarajio yetu kwamba China ambaye ni mshirika mkubwa wa kiujenzi wa nchi za Afrika, ambaye siku zote anaweka mbele sera ya kutoingilia mambo ya nchi nyingine, itafanikiwa katika kuleta amani ya kanda hiyo. China pia inafuata misingi yake ya kwamba waafrika wajiamulie masuala yao wao wenyewe, na kuunga mkono haki ya nchi za Afrika na Umoja wa Afrika kubeba jukumu la uongozi katika masuala ya amani na usalama wa Afrika.

Why Africa?
 
Mchina ba amani ya afrika..give me a break..hao jamaa ni zaidi ya mabeberu..wanatamani hata kuitawala afrika sema hawawezi..ila ni wezi na wahuni wa kutupa..wapo kuvuna mali afrika.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hao jamaa wa fursa tu Amani na DEMOKRASIA sio swagga zao
Nami nataka kushangaa! China ishobokee kuleta amani Afrika wakati wao wanafanya kazi mpaka na madikteta na wauaji wa Afrika! Sera ya Mchina ni biashara kwanza, regardless wanafanya na nani.
 
China haiingilii mambo ya nchi nyingine?!! What a laugh!
Hakuna nchi inayoijali Afrika kwasababu ina mapenzi ya dhati. Kila "mshirika" anajali interests zake tu! Period! Nothing more, nothing less!
 
Back
Top Bottom