China now 3rd Biggest World Economy

Mfwatiliaji

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
1,323
67
Habari za CNN zinasema China

1. Wamewapiku Germany na sasa wapo nyuma ya Japan na USA in terms of economic volume/gross domestic product.
2. Uchumi wao umekua 10-fold tangu 1979 (i.e. within 30 yrs period).
3. Wamefuta umaskini kwa watu 200 million, more than 90% of the total population lifted out of poverty in the world.
4. Kama uchumi wao ukikukua tena 2 times-wakati wa USA ukiwa stagnant-watawapiku na USA.
5. Mwaka 1979 uchumi wao wote ulikuwa unatawaliwa na serikali (state owned) lakini wamebadilika na kufanikiwa kuwa wajasiriamali (private economy).

Question:
1.Tanzania tumekwama wapi, maana umaskini umeongezeka badala ya kupungua na mambo kwa ujumla ni opposite kabisa na China.
 
MFWATILIAJI,sisi wengine ni ma LAYMAN,hivyo ukitwambia china wameendelea to third biggest economy in the world hatuelewi,kwa kuwa wewe mwenzetu umeelewa,tunaomba tufahamishe je in terms of standard of living katika table wako wapi? au labda haya maendeleo hayaendi sambamba na hali ya maisha.niambie mkuu maana naona kama jibu litaniridisha iko haja ya mimi kuhamia CHINA kwenye maendeleo
 
Yaani Son of Alaska mpaka leo hujui dunia maendeleo yake kama yameamia CHINA? Hapa Toronto masela kibao wameanza kuzamia China .Si wazungu si weusi.Mimi mwenyewe nimepata niko mbioni kwenda kuishi kule.Naenda kuishi SHENZHEN au SANYA
 
Habari za CNN zinasema China
Question:
1.Tanzania tumekwama wapi, maana umaskini umeongezeka badala ya kupungua na mambo kwa ujumla ni opposite kabisa na China.


Mkuu fisadi China ananyongwa, huku kwetu hata kuwafikisa mahakamani
mgogoro unategemea nini? Waho wachache wanaofika kwa pilato watu wengi wa watu wenye 'influence' ktk jamii wanapinga "Oo, nchi itapata machafuko" Ktk hali kama hiyo unategemea uchumi ukue.

China aidha hawakuwasikiliza WB & IMF kugenisisha kila kitu; hadi sasa Serikali bado ina nguvu ktk masuala ya Uchumi ilhali Bongo mmeuza kila 'factory' halafu wakazifanya maghala; hapo kuna uchumi kukua mkuu wangu?

Mchumi kukua hadi apatikane raisi mwendawazimu kwa kuipenda nchi yake hapo ndio utegemee maendeleo.

Kipupwe (winter) njema
 
The notion "we are poor" have been eating us slowly like a cancer, unless we learn it hard way, economic liberation is no where to be found!!!!! Mi naona tanzania tuache kudhani tunaweza jenga bila kutoa jasho tuache ujanja ujanja. Tuangalie hawa tunaowabudu kama miungu namna walivyo toka, wengi wao ni kwa mijeledi na damu ndio matunda wajukuu wanayofaidi leo, nasi tukitaka tanzania ya kesho iwe kama " First world" hakuna short cut hapo, hawata kuruhusu kirahisi kuwa kama wao bila wewe mwenyewe kujitoa sadaka. Tuache ujanja ujanja.
 
Ufisadi ni Economic Sabotage, Especially ufisadi wa Tanzania ni mbaya sana.

Kenya baadhi ya viongozi waliopora wamewekeza nchini mwao, exampe Airkenya, Consumer industries (cooking oil like Kimbo, Kasuku, Cowboy e.t.c; soap, juice - which is found in most supermarkets in Tanzania, Dairy Milk industries like KCC, Transport and more.

So these make processing of agricultural products, creates employment to people. Farmers have markets of their harvests, so people engage in Agriculture as there is good income.
Angalia kwenye maduka makubwa, utakuta juice za nanasi, maembe, machungwa. Lita moja ni shs 2000.
Angalia maziwa ya brookbond, ni mazuri na yanauzwa TZ.

Lakini Tanzania Mafisadi wakiiba wanakwenda kuficha pesa kwenye akaunti za Nje, Example New Jersey UK, Swiss, Malta e.t.c. Na nyingine wanawawekea watoto wao billions of money.

Unaona Bwana/bibie, Pesa hizo zimetokana na Jasho la watanzania wote kwa maana wameiba pesa za Serikali. Serikali inapata mirahaba kutokana na Rasilimali zetu kama madini, utalii. Pia kila mwananchi analipa kodi, kwa maana unaponunua bidhaa yoyote, tayari umelipa kodi -kodi ya ongezeko la thamani. Pia wafanyakazi wanalipia kodi ya mapato.

Sasa kama Jasho la watanzania wote linachukuliwa na watu wachache, in maana hatuendelei, ni kutia maji kwenye debe lililotoboka. Uchumi hautakuwa kamwe.

Huo ni uhujumu uchumi.

kama hizo pesa zisingeibwa, ina maana tungeboresha kilimo, mifugo, barabara, Elimu. Tungejenga viwanda vya kuongezea thamani bidhaa zetu, kilimo na ufugaji ungekuwa na tija.

Mfano, angalia msimu huu ni wa matunda, mananasi, maembe na hata machungwa. Hata tuleje, mengine yataoza. Pia bei yake haimpi tija mkulima. Yanaoza tuuu, kama kungekuwa na kiwanda cha kutengeneza juice, tungeepuka hasara, pia kipato cha mkulima kingeongezeka. Na Serikali ingepata kodi.

Yapo mambo mengi ya mfano, angalia nyanya huko Kilolo iringa zinaoza, angalia maparachichi Mkoa wa kilimanjaro, Arusha, Morogoro yanaoza.

Vitunguu mang'ula manyara.

Angalia bei za uwindaji kitalu dola 27,000, its very little. Inatakiwa iwe dola 80, 000 angalau.

Madini, hatupati kitu. Kodi tumewasamehe, madini wanachota

Uvuvi, wanavua wanakwenda kuuza Norway, swiss Europe yote.

Yaani wacha tu nisiendelee kutaja. Mimi naona hii nchi iuzwe Whole sale halafu kila mtanzania agawiwe chake. Halafu kila mtu achague ataenda wapi.

mimi nitachagua Botswana, Huo ni mfano kwa africa. Tanzania tunayo rasilimali kama au zaidi ya botswana, lakini Botswana wameendelea maradufu.

Hata kenya wametuzidi kwa sababu angalau mafisadi wa huko wamewekeza huko huko kenya.

Ndio maana kenya wanatucheka, tunastahili kwa hilo.

China hakuna ufisadi wacha waendelee.

Hata hivyo hatujachelewa, tupinge ufisadi, we can!
 
Kazi kweli kweli Kuna haja hao walio nunuliwa suti kwenda nje kusoma itabidi waturudishie pesa yetu pamoja na Mshahara, Kwani Idea ilikuwa nzuri naona wenzetu baada yakurudi wametusaliti
Mfano Hizi huyu Chenge Baba yake alikuwa nani huko Shinyanga kasomeshwa kwa pesa za wananchi leo hii anatusaliti
 
Tz tuachane na sheria na utaratibu wa Waingereza...tuwe na utaratibu wa Wachina kwa kama miaka 10 au 20 hivi kuleta discipline and order ya ktk kazi..tuachane na 'demokrasi ya Magh' ni luxury ktk Afrika...nguvu kwanza.

Lee Thesis ni jawabu..Authoritarianism kama Singapore, Malaysia na post 1979 China...ndo jawabu Afrika...nguvu kwanza...then demokrasy then maendeleo! Tofauti na hivi mimi nipo persmistic!

Mungu ibariki Tz!
 
Last edited:
Meanwhile, The country's per capita income is classified in the lower middle category by world standards, at about $2,000 (nominal, 107th of 179 countries/economies), and $7,800 (PPP, 82nd of 179 countries/economies) in 2006, according to the IMF.
 
Yaani Son of Alaska mpaka leo hujui dunia maendeleo yake kama yameamia CHINA? Hapa Toronto masela kibao wameanza kuzamia China .Si wazungu si weusi.Mimi mwenyewe nimepata niko mbioni kwenda kuishi kule.Naenda kuishi SHENZHEN au SANYA

Ni kweli watu wengi sasa hivi macho yao yameelekezwa China. Wamarekani pia wanakimbilia huko. Inabidi tuwahi na sisi kwenda kwa maana hatuishi kisiwani. Lakini ninasikia tayari kuwa wa-tz wako huko wanafanya biashara.
 
Ndugu Pundamilia,

Sipo China, ila kama una habari yoyote kuhusu ufisadi wa china tueleze hapa JF.

Kwa ufahamu wangu ni kuwa hakuna mtu kamili duniani, mapungufu yapo.

ILa kama china ufisadi upo, inawezekana. Ila kumbuka Adhabu kwa FIsadi china ni Kubwa.

Mfano angalia Waziri Mkuu wa Thailand alishtakiwa.

Huku huku Jf nimesoma kuwa fisadi china ni mhujumu uchumi na akithibitika ni kifo.
 
Meanwhile, The country's per capita income is classified in the lower middle category by world standards, at about $2,000 (nominal, 107th of 179 countries/economies), and $7,800 (PPP, 82nd of 179 countries/economies) in 2006, according to the IMF.

RD ni kweli average annual income yao bado iko chini-$2,800-ukilinganisha na western countries, lakini speed yao ya kufuta umaskini imekuwa kubwa mno. Fikiria, asilimia 90 ya umaskini uliofutwa duniani katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita umefanyika kwa hawa jamaa.
 
SASA hawa wachina,wanaopigana vikumbo na wamachinga mjini kuuza maua etc etc,wengine wako kwenye ukahaba dar vipi?au huu mgao wa national cake kwao umewapita kando.halafu kwenda Hong kong which is a part of their country restriction kali.It seems posperity is a damn long way away
 
Kuna rafiki yangu mchina ni contractor nilimuuliz nini essence ya maendeleo yao.
Akanijibu seriuos leaders and seriuous government,mambo ya kipumbavu pumbavu mtu ananyongwa.
Discipline ni ya hali ya juu.
Anasema ndo maana hawana dini bse wanaiabudu na kuitukuza serikari yao iliyowatoa toka umaskini mpaka utajiri.
Tz kuna cha kujifunza apo,serious leaders forming a serious government.
Ivi ulishawai sikia China wanafanya uchaguzi countriwise as a whole?
Nasikia wawakilishi tuu wa watu ndo wanamchagua raisi.
 
Yaani Son of Alaska mpaka leo hujui dunia maendeleo yake kama yameamia CHINA? Hapa Toronto masela kibao wameanza kuzamia China .Si wazungu si weusi.Mimi mwenyewe nimepata niko mbioni kwenda kuishi kule.Naenda kuishi SHENZHEN au SANYA

ukitaka kujua uchumi wa china ulivyokua nenda kariakoo, maana watanzania ndo tunaonunua yale matambara ambayo hayana quality bado wanaweza ku export, while korosho za mtwara zinavunjwavunjwa ili kuangalia ubora na kama iko below standard inarudishwa wachina wanatengeneza belowww standard special for tz, kila mahali hata mikoani china imetawala hivi hata vibanio vya nywele vinavyochuja rangi Tanzania hatuwezi kutengeneza bado kidogo tutaletewa na umeme wa kichina, kama ule wa kaka Lowasa.
 
Habari za CNN zinasema China

Question:
1.Tanzania tumekwama wapi, maana umaskini umeongezeka badala ya kupungua na mambo kwa ujumla ni opposite kabisa na China.

1. Kula sana kuliko kuzalisha
2. Kuiba chakula cha watoto hadi kukomba mboga (Ufisadi x Ufisadi x Ufisadi)
3. Kuzalisha watoto wengi kuliko vitu vya kuwahudumia (busy making children while they are busy making wonders)
4. Kutumia akili kiduchu katika mambo yetu (bongo ziko kama za mataahira)
5. Kulala sana na kufanya kazi kidogo tu. Hata tukifanya kazi hatuna malengo au mwelekeo. Mfano kutumia jembe la mkono mwaka 2009 kuzalisha chakula cha watu karibia millioni
6. Kila aina ya ujinga na upuuzi katika mambo ya msingi ....n.k.
 
Habari za CNN zinasema China

1. Wamewapiku Germany na sasa wapo nyuma ya Japan na USA in terms of economic volume/gross domestic product.
2. Uchumi wao umekua 10-fold tangu 1979 (i.e. within 30 yrs period).
3. Wamefuta umaskini kwa watu 200 million, more than 90% of the total population lifted out of poverty in the world.
4. Kama uchumi wao ukikukua tena 2 times-wakati wa USA ukiwa stagnant-watawapiku na USA.
5. Mwaka 1979 uchumi wao wote ulikuwa unatawaliwa na serikali (state owned) lakini wamebadilika na kufanikiwa kuwa wajasiriamali (private economy).

Question:
1.Tanzania tumekwama wapi, maana umaskini umeongezeka badala ya kupungua na mambo kwa ujumla ni opposite kabisa na China.

Sina tatizo na China kuwa ya 3; tatzo langu kubwa ni bidhaa feki zao yaani wamepitiliza kiasi cha kuwafanyizia hata Wachina wenzao (Rejea maziwa yenye melamine).

Tanzania hatujakwama popote ila tunajikwamisha sisi wenyewe kwa bora uongozi, tukiachana na fikra z kutegemea misaada na kupnguza ufisadi tutafika mbali.
 
Habari za CNN zinasema China

1. Wamewapiku Germany na sasa wapo nyuma ya Japan na USA in terms of economic volume/gross domestic product.
2. Uchumi wao umekua 10-fold tangu 1979 (i.e. within 30 yrs period).
3. Wamefuta umaskini kwa watu 200 million, more than 90% of the total population lifted out of poverty in the world.
4. Kama uchumi wao ukikukua tena 2 times-wakati wa USA ukiwa stagnant-watawapiku na USA.
5. Mwaka 1979 uchumi wao wote ulikuwa unatawaliwa na serikali (state owned) lakini wamebadilika na kufanikiwa kuwa wajasiriamali (private economy).

Question:
1.Tanzania tumekwama wapi, maana umaskini umeongezeka badala ya kupungua na mambo kwa ujumla ni opposite kabisa na China.
Ten years later imekuwa ya 2 na inaongoza duniani kwa ppp kama Tanzania inavyoongoza afrika mashariki kwa ppp
 
Back
Top Bottom