China na Russia kamwe hawawezi kutumia hiyo chanjo ya mRNA ya kampuni ya Pfizer (Billgate) na BioNTech (Mjerumani): Kwa nini Afrika tulazimishwe?

Sasa kwa nini tusinunue chanjo toka China? Kwanza ni rafiki zetu wa damu na juzi tu Waziri wao wa mambo ya nje alikuwa Chato. Wao kazi yao ni kutupiga ban kwenye nchi zao...
Msipende uongo. Hamna taifa linalolazimishwa kununua chanjo yeyote. Kila mtu anajua kuwa kwa Afrika hizo za Ujerumani na Marekani hazifai kutokana na mahitaji yake ya utunzaji.

Covax inakusudia kununua za Astra Zeneca na hasa zile zitakazo tengenezwa under license India ambazo zitakuwa za bei nafuu. Kama tuna uwezo wa kununua za kichina au kirusi, tununue na hamna atakae tuzuia.

Kama hatutaki kabisa chanjo, hivyo hivyo. Tena wengi watafurahi maana mahitaji ya chanjo ni makubwa kuliko supply. Hizo ambazo hamzitaki watanunua na kuwachanjia raia zao. Ila tusitegemee kuwa watatupa pesa yao ili tununue dawa za kupigia nyungu. Uamuzi ni wetu, tusiwasingizie wengine.

Amandla...
 
Wewe ndio umeleta hii hoja mfu ambayo haipo. Bill Gates anamiliki makampuni gani ya pharmaceuticals na ana hisa asilimia ngapi?....
Wale conspiracy theorist ni wafanya biashara Kama walivyo wengine, kazi ni kuwapotosha watu usipotumia reasoning ya Hali ya juu ndio utakua huyo jamaa anaitwa Patriot

Na safari wamepiga hela mfano wanaposema watu wasitumie vaccine, watupe alternative hawana ndo utawajua ni wababaishaji. Hata jiwe kawafuatilia ndo maana anaongea ujinga ujinga
 
Hiyo tunayoiita chanjo inayotengenezwa na kampuni ya Pfizer ikishirikiana na kampuni ya BioNTech ya ujerumani si sawa na chanjo zinazojulikana ambazo hutumia virusi vya ugonjwa huo huo vilivyopunguzwa makali (attenuated live viruses). Hawa wanatumia genetically engineered manufactured synthetics za genetitically coded mRNA to instruct our DNA in the genes of our cells (nucleas chromosomes) to produce certain proteins which are thought to be protective or curative of certain diseases including cancer diseases.
You are very poor thinker, ni wazi kabisa theory yako imetoka katika kichwa ambacho ni hardheaded, wewe unaambiwa uchukue tahadhari ugonjwa upo na unauwa watu na tayari kila mahali watu wanaona kwa macho yao athari zake sasa theory yako bado inakutuma watu wakae kimya wasiseme mana ukisema ni taharuki sasa dunia na nchi sio kijiko cha chai kama unavyoona wewe na mjomba wako ambao sasa munaipelekesha nchi kama familia yako nyumbani.

Life it is very simply., ukiona Corona is nothing kwako sawa shawishi familia yako na ukoo wako tu usijaribu kumzuia anayeona Corona nihatari kwake, katika nchi kila mtu mawazo yake na mtazamo wake katika kila aspect, kama issue ni PHd tayari PHds zimetapakaa nchi nzima, usivae barakoa lakini anaevaa usimzuie wala kumsema.

Tuna uzoefu mjomba wako kila Corona ikikaza anaenda kuishi kijijini kwao chato, kama barakoa hizi ki-sayansi ni hatari usimzuie anaenona si hatari kwa afya yake, tengeneza za kwako kwenye kampuni yako.

Unapoambiwa upokee chanjo kwa ajili ya watu wako ni kwasababu na wewe bado hujatulia saa zote munatembeza mabakuli ya omba omba kwa hao mabeberu unaosema ili na wewe angalau upate izo buku7 kwa ajili ya maisha yako na familia yako. Mutakapoacha ujuaji na ujinga siku yoyote huko Tanzania ndio mtaanza kupata maendeleo kwa ajili ya watu wenu ili muondokane na huo umasikini uliokubuhu.

Akili inabidi uitume iweze kuchanganua mambo sio kila siku kulishwa munayolishwa halafu munakuja hapa na porojo ndefu kila mtu anaona umepwaya.
 
Leo mnajilinganisha na China na Russia? Kwa taarifa tu hao "marafiki" zenu huwa hawapokei misaada mpaka ya ARV toka kwa mabeberu, na kama kweli hamtaki bidhaa za mabeberu zile Bombardier mnazoringia zimetoka wapi? Mnachekesha sana kwa huu utoto wenu mnaolazimisha muonekane "mnajiweza"

Bidhaa za mchina kwenye haya mataifa ya dunia ya tatu haziaminiki, nyingi ni feki, wanazitengeneza kwa viwango vya chini kwasababu wanajua wakituletea original hatuwezi ku- afford kununua, original watazipeleka S.A, America na ulaya; nendeni mkalete hizo pipi za mchina mmumunye kwa raha zenu.
Humu kuna watu wameleweshwa propaganda za vijiweni. Hata kwa mabeberu kuna watu wamelewa hizo conspiracy theories na wanaziamini ... hivyo Africa tusiwashangae.

Imagine siku zote tumepokea chanjo a bado tunaendelea kupokea hizo chanjo tena kwa misaada. Sasa kama kulikuwa na mpango wa kutuua kwani ni lazima tu waje au wasubiri Corona au watengeneze Corona. Bill Gates amekuwa mbele sana kusaidia Africa kwenye Ukimwi na Malaria, kama ni kweli kwa nini asitumie hizo project kutumaliza. Tena hizo project zimelenga zaidi Africa.

Ukiingia madukani, vitu vyote vya kutengengezwa hata vyakula vinatoka kwa hao Mabeberu. Africa hatuzalishi chakula cha kututoshelea. Sasa kwa nini watumie technolojia kubwa kutuangamiza wakati wanaweza kutumia haa tu unga wa yanga au mafuta ya kupikia.
 
Wewe ndio umeleta hii hoja mfu ambayo haipo. Bill Gates anamiliki makampuni gani ya pharmaceuticals na ana hisa asilimia ngapi?

Ujuaji wa kipuuzi utakuja kuwafanya mfe kwa stress. Pfizer, Moderna, AstraZeneca, Johnson & Johnson na BionTech wapi ambako Gates kahusika. Watu kama nyinyi huwa mnaishi kwa shemeji hamna hata kazi mnajikuta genius kumbe vilaza tu.
Mtu ni philanthropist kwenye sekta ya afya, tiyari mnamuita mtengeneza madawa. Mtu akigawa magodoro shuleni mtasema ana kiwanda cha magodoro?
JIsomee bhana! Kwa nini hutaki kusoma ujue makampuni ya biotech na wacahangiaji ni akina nani? Hapa siyo darasa la 4 usubilie notisi ubaoni bhana!
 
Sasa kwa nini tusinunue chanjo toka China? Kwanza ni rafiki zetu wa damu na juzi tu Waziri wao wa mambo ya nje alikuwa Chato. Wao kazi yao ni kutupiga ban kwenye nchi zao.

Bidhaa zetu nyingi zinatoka China. Kwa nini hii bidhaa ya mRNA tulazimishwe kuinunua kutoka kwa mabeberu hawa trna kwa bei yao kubwa mara 100 ukilinganisha na ile chanjo ya China? Halafu ya China ni original, haina RNA.
Umejuaje kua ya china ni original? Never trust that much
 
Hao rafiki zenu wa damu wameshindwa kuwapa ARV, condoms, chanjo ya polio, chanjo ya TB (BCG) na hata logistic ya kusambaza chanjo ya COVID ni UNICEF ndiyo wasambazaji.
Dada yangu tunapaswa kuzinduka kuhusiana na hivi vitu tunazopewa za bure bure. Unadhani wanatupenda kweli kwa kutusambazia mikondomu ya lukuki ya bure? Tunajua walichoweka katika hiyo mifuta ya mikondomu? Mbona bombadier na dreamline hawatupi bure? Kwa nini Mchina na Mrusi haruhusu mikondomu yao kuingia nchini kwao?

Dada yangu hawa jamaa wana lao kuhusu sisi watu wa Afrika. Hii kampuni ya Pfizer ndiyo mtengenezaji na msambazaji pekee wa Viagra kwenye nchi za Afrika. Kwa nini? Madhara ya viagra ni makubwa. Tumekuwa tukishuhudia wanaume wakifia guest kwa sababu ya viagra. Combination ya viagra na kakorona na ka mRNA mwanaume huchomoki nakuambia!

Wewe dada yangu unadhani ni kwa nini sasa hivi asilimia 52% ya wanaume wa Tanzania wana Erectile Dysfunction (ED)? Unakuta kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 25 hajiwezi hadi atumie viagra. Huu ndiyo mchezo wa kuletewa vitu vya bure bure. Hizo ARVs tunazoletewa bure kwao hazitumiki. Wao wana dawa kabambe zaidi zinazoua kabisa virusi hivyo, sisi tunapewa za kuvifubaisha tu! Kwao ukimwi haupo na kama upo ni kidogo sana na hauwauwi na kodomu hawavai tena.
 
Dada yangu tunapaswa kuzinduka kuhusiana na hivi vitu tunazopewa za bure bure. Unadhani wanatupenda kweli kwa kutusambazia mikondomu ya lukuki ya bure? Tunajua walichoweka katika hiyo mifuta ya mikondomu? Mbona bombadier na dreamline hawatupi bure? Kwa nini Mchina na Mrusi haruhusu mikondomu yao kuingia nchini kwao? Dada yangu hawa jamaa wana lao kuhusu sisi watu wa Afrika. Hii kampuni ya Pfizer ndiyo mtengenezaji na msambazaji pekee wa Viagra kwenye nchi za Afrika. Kwa nini? Madhara ya viagra ni makubwa. Tumekuwa tukishuhudia wanaume wakifia guest kwa sababu ya viagra. Combination ya viagra na kakorona mwanaume huchomoki nakuambia!
Waliopata chanjo awamu ya kwanza Ulaya ni wafanyakazi wa afya. Wengi walipata Pfzer na Biotech pia ya Oxford. Kama chanjo ingekua na madhara kwa Waafrika ingeshawaua hawa waliopata awamu ya kwanza.
 
“China sasa hivi wanatumia kipimo cha kinyesi au rectal swab which is easier and more convinient”

mkuu rectal swab iko easier and convenient????
Rectal swab unajifanyia tu mwenyewe na haiumi bali inaleta raha. Kama vipi mke wako au mpenzi wako anakufanyia hiyo swab kwa raha zaidi (inaitwa double plessure)! Kajaribu ujionee.
 
Hivi bill gates anahusikaje na Pfizer au biotech kampuni ya ujerumani, mnamuongelea as if yeye ndo mmiliki wa kampuni zote za pharmaceutical, Kama ndo hivyo angekua ni trillionaire
Wee vipi unauliza u trillionaire wa Bill Gate. Kwenye hizi vaccine za mRA za korona kupitia kampuni zake za Pfizer na Moderna hadi sasa ameshauza chanjo za thamani ya USD 23 trillion.

Na hii ni ndani ya mwezi mmoja tu! Si mchezo. Hii biashara ya dawa na chanjo huwezi kuilinganisha na biashara nyingine yo yote hapa duniani kwa kutengenezq fweza. Kampuni za kutengeneza madege na magari ni nothing ukilinganisha na chanjo au dawa au hata kondomu tu.
 
Waliopata chanjo awamu ya kwanza Ulaya ni wafanyakazi wa afya. Wengi walipata Pfzer na Biotech pia ya Oxford. Kama chanjo ingekua na madhara kwa Waafrika ingeshawaua hawa waliopata awamu ya kwanza.
Kwa taarifa yako dada Ulaya hawatumii hizo chanjo za mRNA zinazotengenezwa na makampuni ya Pfizer na Moderna ya USA. Chanjo wanayotumia ni ya AstraZeneca. Hii chanjo imebuniwa na kutengenezwa na watalaamu wa Oxford Univerity ya Uingereza kwa kushirikiana na kampuni ya madawa (biopharmaceutical company) ya Ufaransa inayoitwa AstraZenecca. Chanjo hii inatumia kirusi cha mafua ya sokwe (chimpanzee adenovirus).

Huyu adenovirus wa sokwe waliomchukua kutoka kwenye misitu yetu ya Afrika walimfanyia biotechnical modification kumpunguza makali na kupata hiyo chanjo. Chanjo hiyo ya Oxford- AstraZeneca ni rahisi kuitunza, inahitaji jokofu tu la kawaida (36 to 46 degrees F) badala ya freezing temperatures za negative 94 F zinazotakiwa kutunza mRNA za Pfizer. Bei yake ni rahisi kiasi cha USD 4 kwa dose badala ya USD 33 kwa dose ya Moderna au Pfizer.

Kwa taarifa yako haya mashindano ya utengenezaji chanjo za covid sasa hivi ni makubwa na ni ya kibiashara zaidi. USA imekataa kuiidhinisha chanjo hiyo ya Uingereza na Ufaransa kutumika nchini kwao Amerika. Chanjo hii ni nzuri kuliko hizo za Amerika na uwezo wake ni 70% to 90% sawa na hizo za mRNA za USA. Hivyo ulaya nao hawazitaki hizo chanjo za waamerika.

Sisi Afrika tunaishi na hao sokwe na nyani wengine wakiwemo tumbili ambao wana hizo adenoviruses tuna share nao. Hawatuzuru wala hatuhitaji kuwafanyia modifications. Hivyo tuna hiyo 70% to 90% kinga tuliyoipata kwa hao nyani. Ni neema ya Mungu.
 
Screenshot_20210202_160812_com.android.chrome.jpg

100% sijawahi muamini beberu aliye muuaji wa Gadaffi
 
ilikuwaje corona ikapungua maambukizi mwaka jana June to July?
Haya magonjwa ya coronavirus na mengineyo ya mafua hususani influenzavirus tangia zamani huwa ni ya msimu ie seasonal diseases. Na msimu wake huwa kuanzia mwezi Novemba hadi Machi. Na milipuko ya magonjwa hayo yamekuwa yakitokea kipindi hicho. Bado miezi 2 hali itakuwa shwari tena.
 
Hiyo tunayoiita chanjo inayotengenezwa na kampuni ya Pfizer ikishirikiana na kampuni ya BioNTech ya ujerumani si sawa na chanjo zinazojulikana ambazo hutumia virusi vya ugonjwa huo huo vilivyopunguzwa makali (attenuated live viruses). Hawa wanatumia genetically engineered manufactured synthetics za genetitically coded mRNA to instruct our DNA in the genes of our cells (nucleas chromosomes) to produce certain proteins which are thought to be protective or curative of certain diseases including cancer diseases.

Utafiti wa kutumia synthetic mRNA kutibu au kukinga magonjwa ya cancer, rabies, zika etc ni wa siku nyingi. Hata hivyo dawa au chanjo za magonjwa hayo zinazotumia genetic mRNA hazikuweza kupata approval ya kutumika kwa binadamu kutoka FDA. Kwa sababu ya taharuki, hofu na wasiwasi wa janga hili la covid - 19 FDA imezipa emergency approval dawa/ chanjo hizo za mRNA. Hazijapitia hatua zote za kimchakato za usalama kama inavyotakiwa kisayansi. Inaelekea waafrika baada ya kujazwa hofu na pesa kupenyezwa walitumika kama guine pigs katika utafiti wa usalama na uwezo wa dawa hizi. Utafiti huo haukuoneshwa kwani ulikuwa unethical.

Chanjo za covid 19 zinazotengenezwa China na Urusi ndizo chanjo halisi zinazotumia live attenuated sars- cov-2, kirusi kinachosababisha covid-19. Urusi na Uchina kamwe haziwezi kutumia hizo chanjo za mRNA kutoka Pfizer/ BioNTech. Ni kipi cha ajabu Tanzania chini ya rais mwanasayansi wa level ya PhD kuzikataa au kuzitilia mashaka hizo chanjo zao za mRNA. Kama tutaamua kuchanja tutatumia chanjo toka China au Russia kwani hizo hazichezi na DNA zetu. Chanjo zinazotumia live attenuated viruses ni rahisi kuzi verify. Hizo za mRNA huwezi ukatambua code (ujumbe) zilizobebeshwa hizo RNA.

Halafu ukweli ni kuwa Afrika ugonjwa huu si tishio hata kidogo. Takwimu ambazo tumelazimishwa na WHO kwamba hata wale ambao hawana ugonjwa lakini wame test positive kwa baadhi ya antigens za cov-2 tuwahesabu kama ni wagonjwa (covid-19), ni kitu ambacho si sahihi na hakikubaliki kisayansi. Unachokonolewa pua kutafuta kama una hizo antigen wakati antigen hizi ungaliweza kuzipata kwenye kinyesi au kwa kuchokonolewa kwenye mkundu. China sasa hivi wanatumia kipimo cha kinyesi au rectal swab which is easier and more convinient. Halafu WHO inatulazimisha tupimane sana na vipimo hatupewi bure, ni za ghari takribani Tsh laki moja kila kipimo - wanatukopesha.

Takwimu wanazozitaka siyo za prevalence wala incidence ya ugonjwa au wa virusi hao wa cov-2 kiepidemolojia nakisayansi. Ndiyo maana Trump aliiondoa USA kwenye shirika hili la WHO kwa kuvurunda kwake kuhusu suala hili. Kama ni kutaka kujua prevalence ya virusi hivi ni vyema a scientific prevalance survey of an unbiased sample population ikafanyika. Si hizi takwimu za kujumlisha contact tracing, patients and carriers.Virusi hivi vimekuwapo duniani tangia zaidi ya miaka million 50 iliyopita. Binadamu amekuwapo hapa duniani kwa miaka million tano tu. Dunia imekuwapo kwa miaka billion tano (after the Big - Bang)!

Hata kwa hizo takwimu tulizolazimishwa kukusanya bado Afrika corona si tatizo la kutufanya tutaharuki. Kwa mfano Kenya ambayo population yake ni 55 million kwa kipindi cha mwaka mmoja ni watu elfu 90 tu ndiyo wame test kuwa na antigen za corona kwenye pua zao, yaani elfu nane tu kwa mwezi! Na wanaofikiriwa kufa kwa corona (kama primary cause of death) hawazidi elfu moja kwa mwaka. Na wengi wa hawa waliokufa walikuwa na magonjwa yao mengine kama kisukari, pressure, congestive cardiac failure, renal failure, cor pulmonary, bronchoathma (pumu) etc. Wala corona haikuwa the primary cause of death. Kwa sababu ya woga na taharuki iliyojengwa kuhusu corona wagonjwa wote hawa wenye changamoto la upumuaji (dypsnoea and tachpnoea) wamekuwa wakikimbiwa au kuogopwa na wauguzi/ madaktari na kupelekea wasipate huduma sahihi ya magonjwa yao na kusababisha vifo vyao. Tumeshuhudia hadi migomo ya wauuguzi, madaktari na watoa huduma za afya wengine.

Taharuki hii kwa nchi za Afrika ndiyo wazungu wanataka ili wapate watu wa kujaribia dawa au chanjo za ugonjwa huu na pia kupiga pesa. JPM kawagusa penyewe. Ndiyo maana hawakuchelewa kuwawaya - mara oh jiandae kupokea chanjo za msaada (lakini mkopo) za mRNA etc.

Inasikitisha sana Kanisa katoliki kupitia Padre wake machachari wa Baraza la Maaskofu Tanzania, anayeitwa Kitima, bila ushahidi wa kisayansi wala ridhaa ya malaka husika, ghafla kwa taharuki limeamua kuvunja utulivu wa nchi yetu uliokuwapo dhidi ya virusi hivi. Nchi ilikuwa imetulia chini ya ulinzi wa Mungu kwa kutambua kuwa ugonjwa huu hauna tiba wala kinga na kwamba kinachoua kwenye ugonjwa huu hasa ni ile hofu na taharuki na si ukali wa virusi hivi. Hizo barakola, social distancing na lockdown hazisaidii cho chote (useless) na hapa kwetu zina madhara zadi (dangerous) au haviwezekani. Wazungu wamefanya hivyo hazikusaidia chochote. Sweden hawakufanya hivyo kama sisi and are much better! Waafrika waliouawa kwa risasi kwa sababu ya kukiuka masharti ya lockdown ni wengi kuliko waliouawa na corona.

Hata hizo barakola za grade ya juu zinazouzwa Sh elfu kumi kwa moja ambazo zinapaswa kubadilishwa kila baada ya nusu sasa, bado uwezo wake wa kuzuia virusi hivi ni 60% tu. Hivi vya nguo vikibadilishwa kila nusu saa uwezo wake ni 20%. Ukikaa nayo muda murefu (zaidi ya saa)yenyewe ndiyo inakuwa source ya kukuambukiza. Hizo PPEs wanazotakiwa kuvaa watoa huduma wa afya bei yake ni sh laki tano, na zinatakiwa kubadilishwa kila saa moja (disposable).

Na bado udhibiti wake wa virusi hivi ni kama 80% tu! Haya mambo si rahisi scientifically. Isitoshe barakola nyingi zinazoingizwa nchini zinaelekea zilishapandikizwa virusi vya corona. Barakola hizi zinasaidia tu kupunguza hofu kwa wasiojua lakini ni more risk na hatari sana hasa zinapotumika visivyo. Kumuamini Mungu kunatoa hofu hii bila risk yo yote. Na hichi ndicho rais wetu alichokuwa amekifanya kuanzia mwezi April 2020. Vifo vya corona vilitoweka baada ya wananchi kuondokewa na hofu. Walimuamini Mungu, waliamini nyungu na dawa zingine za asili. Sasa kanisa katoliki limeturudisha tulikotoka - kwenye hofu na taharuki. Vyama vya upinzani na mabeberu wame take advantage. Tusikubali.

Social distancing kwa mazingira yetu ni next to impossible na lockdown ndiyo balaa zaidi.

Vita vya dunia ya sasa zinatumia silaha za kibiolojia za mRNA.


Umejieleza kwa ufasaha kabisa, na wenye akili za kujitambua watakuelewa, lakini wale wenye akili za kushikiwa, na kuaminishwa kuwa sisi hatujiwezi kwa chochote bila "kutegemea kitonga", ndio kabisa utawaacha gizani, wakisubiri maelekezo kutoka kwa mabeberu na vibaraka wao tunaoishi nao viungani!
 
Hivi bill gates anahusikaje na Pfizer au biotech kampuni ya ujerumani, mnamuongelea as if yeye ndo mmiliki wa kampuni zote za pharmaceutical, Kama ndo hivyo angekua ni trillionaire
Read widely to understand Bill and Merinda Gate Foundation involvement in these scandalous engagement!
 
Wee vipi unauliza u trillionaire wa Bill Gate. Kwenye hizi vaccine za mRA za korona kupitia kampuni zake za Pfizer na Moderna hadi sasa ameshauza chanjo za thamani ya USD 23 trillion. Na hii ni ndani ya mwezi mmoja tu! Si mchezo. Hii biashara ya dawa na chanjo huwezi kuilinganisha na biashara nyingine yo yote hapa duniani kwa kutengenezq fweza. Kampuni za kutengeneza madege na magari ni nothing ukilinganisha na chanjo au dawa au hata kondomu tu.
Mbona utajiri wa bill gates hujakua Kama kweli anaumiliki wa hisa kwenye hizo kampuni za pharmaceutical acha uongo ndugu
 
Back
Top Bottom