Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 8,940
- 6,853
Msipende uongo. Hamna taifa linalolazimishwa kununua chanjo yeyote. Kila mtu anajua kuwa kwa Afrika hizo za Ujerumani na Marekani hazifai kutokana na mahitaji yake ya utunzaji.Sasa kwa nini tusinunue chanjo toka China? Kwanza ni rafiki zetu wa damu na juzi tu Waziri wao wa mambo ya nje alikuwa Chato. Wao kazi yao ni kutupiga ban kwenye nchi zao...
Covax inakusudia kununua za Astra Zeneca na hasa zile zitakazo tengenezwa under license India ambazo zitakuwa za bei nafuu. Kama tuna uwezo wa kununua za kichina au kirusi, tununue na hamna atakae tuzuia.
Kama hatutaki kabisa chanjo, hivyo hivyo. Tena wengi watafurahi maana mahitaji ya chanjo ni makubwa kuliko supply. Hizo ambazo hamzitaki watanunua na kuwachanjia raia zao. Ila tusitegemee kuwa watatupa pesa yao ili tununue dawa za kupigia nyungu. Uamuzi ni wetu, tusiwasingizie wengine.
Amandla...