ruaharuaha
JF-Expert Member
- Feb 14, 2018
- 3,555
- 3,749
Watanzania waelewe, serikali haina vyanzo vingine vya mapato zaidi ya kodi ya watanzania.
Watanzania tunataka maendeleo,barabara nzuri,reli,umeme, shule,hospitali, miji iliyopangika,maji, serikali yenye ufanisi,ulinzi na usalama,lakini ili upate vitu hivyo lazima ugharamikie kwa tozo na kodi, sisi hatutaki kugharamikia vitu hivyo,hatutaki kugharamikia maendeleo.
Hii naifananisha na mtoto, hakuna mtoto anayeanza shule anakubali kirahisi kuamka asubuhi,atalia sana, ila akishapata digrii na kupata mapesa, atakumbuka wema was mzazi, serikali ni mzazi,anafanya jambo jema, kamwe asiache kumpa lililo jema mwanae kisa analia sana.
Unaacha kumlisha mtoto chakula kisa analia? Unataka familia yako wale kuku na biriani wafurahi na ukisema uwajengee nyumba wanalia na wewe unawasikiliza?
Tugharamie maendeleo na tujivunie, unajivuna unaporudi kijijini unakuta kituo cha afya,tena kina umeme na dawa na daktari, unaenda kijijini kwa barabara safi, maji yanapatikana, madarasa safi yana umeme,maabara zipo.
Tunaenda China,Marekani na Ulaya tunamwaga sifa kuwa zimeendelea, hao wamepita njia hii hii tena kwa uzalendo mkubwa na jasho.
Leo ndio tunakopa fedha huko, hao wamejitoa sadaka!
Napendekeza nchi yetu isikubali tabia ya kulialia, tuchukue au tuige mfumo wa China na urusi kiasi kuhusu demokrasia, demokrasia isiwe ukuta was kuzuia maendeleo. Linapokuja suala LA maendeleo mengine ya wanasiasa yawekwe pembeni, kinataka kujengwa kituo cha afya mwanasiasa anapinga kisa demokrasia!
Nchi inataka shule watu waelimike waendane na dunia,mwanasiasa anapinga.
Nchi inataka reli mizigo isafiri kwa haraka ipatikane fedha ya maendeleo,mwanasiasa anapinga!
Yote huyapati bila kodi na tozo.
Kwa kuzaliwa mtanzania tayari una jukumu na wajibu kushiriki katika maendeleo, unataka nani akuletee maendeleo? Unataka mzungu wa London akatwe kodi ili barabara ya kwenda kwenu ijengwe? Halafu wewe ambae huko ni kwenu hutaki kutoa tozo ili ujengewe barabara ya kwenda kwenu!
Wakina mama wamezaa watoto, nchi inahitaji watu wenye afya na elimu, tena wengine ni watoto wako na wa ndugu zako, unaambiwa changia watoto wapate huduma bora za afya na elimu,hutaki, unasubiri Bill Gates aje asomeshe na kutibu watoto wako!
China na Urusi wameweza, system iibadili nchi ifate mfumo huo, viongozi wenye nia njema wasikwamishwe na vikelele, China hawakubali ujinga huu hata Urusi na nchi zinasonga mbele!
Kwa pamoja tulikuwa tunaimba ubeberu mbaya, njia ya kuukwepa ni nchi kujitegemea, halafu hutaki kulipa kodi na tozo! Unasema deni LA taifa linaongezeka, haya, hatukopi,lipa kodi,hutaki!
Samoa usisikilize kelele za wasiopenda maendeleo, hakuna aliyeleta maendeleo aliyefata kelele za aina hiyo
Kuna watu watasema katiba mpya, hivi tukishatunga katiba mpya ndio kila mtu atawekewa fedha mfukoni, barabara zitajijenga,hospitali zitajijenga, tutalala nyumbani na fedha zitajileta zenyewe!
Mfumo wetu unategemea sana Kiongozi mmoja. Akiwa dhaifu, asiye na maono na uthubutu nchi yote inakuwa dhaifu.
Kuna umuhimu mkubwa wa katiba mpya. Kinga kuondelewa, viongozi kuwajibishwa na sheria wasipowajibika. Mahakama, Bunge na jeshi la polisi kuwa huru.
Uteuzi ufuate taaluma ya mtu, weledi na maadili. Pia kuwepo na confirmation hearing.
CV, historia ya mteuliwa itajadiliwa na kuchunguzwa na kuthibitishwa na baadaye kukubaliwa au kukataliwa. Hapo tutapata watu makini kwenye uongozi.