China kwa mtazamo wa mwafrika anayeishi China kwa karibu miongo miwili: China ya sasa ina mambo mengi ya kujifunza kuliko uchumi peke yake

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
1638321591560.png

kasri ya kifalme mjini Beijing (Forbidden City)

1638321609595.png

mandhari ya kisasa mjini Shanghai​

Kwa muda wa muongo mmoja sasa China imekuwa inatajwa kama nchi yenye uchumi wenye nguvu ambao unakaribia kuupita ule wa Marekani. Kwa watu wengi wa Afrika picha ya China kidogo ina mchanganyiko wa yale waliyofahamu kupitia filamu na vyombo vya habari vya nchi za magharibi, na hivi karibuni kupitia mji wa Guangzhou ambao kutokana na ushirikiano wa kibiashara umekuwa ni mji unaojulikana zaidi kwa waafrika. Lakini hali halisi ni kuwa China ya sasa ni zaidi ya hapo.

Kwa mtu anayetoka nchi yoyote inayoendelea, iwe ni ya Afrika, Asia au Amerika ya Kusini au hata katika baadhi ya nchi za Ulaya, akitembelea miji ya Beijing, Shanghai, Tianjin au Guangzhou anaweza kujiuliza mara mbili ni kwanini China inawekwa kwenye kundi moja na nchi zinazoendelea. Ukiiangalia miji hii, kwenye upande wa miundo mbinu unaweza kuona ni ya kisasa, sawa au hata zaidi ya nchi za magharibi katika baadhi ya maeneo. Kwa mfano mfumo wa Subway wa miji hiyo, ni bora na ya kisasa zaidi kuliko hata ya miji mikubwa ya nchi nyingi zilizoendelea.

Tukiangalia kwenye upande wa uchumi, mara nyingi tunasikia kuwa China ni nchi ya pili kwa nguvu ya kiuchumi duniani. Lakini tukiangalia kwa ndani na kuangalia hali ya miji au mikoa mbalimbali ya China tunaweza kuwa na picha ya kina zaidi. Kwa mfano GDP ya mji wa Shanghai ni dola za kimarekani bilioni 608, wakati GDP ya Sweden ni dola bilioni 550. GDP ya mji wa Beijing ni dola za kimarekani bilioni 458, wakati ile ya Denmark ni dola bilioni 325.

Licha ya kuwa hali halisi inaonyesha kuwa kuna maeneo ya China ambayo bado yako nyuma, na China inasema maeneo hayo yanaifanya China isiwe kwenye kundi la nchi iliyoendelea, hali halisi ni kuwa maendeleo katika maeneo hayo yanapiga hatua ya kasi. Ni suala la muda tu miji ambayo leo inatajwa kuwa iko nyuma kimaendeleo, kesho ikawa na maendeleo makubwa.

Tukumbukue kuwa suala la maendeleo halipo kwenye miundo mbinu na vitu peke yake. Mambo mawili makubwa yanayotakiwa kujulikana zaidi kuhusu maendeleo ya uchumi wa China ni kuwa maendeleo hayo hajaishia kwenye GDP kubwa, miundombinu mizuri peke yake au kubadilisha maisha ya wachina wa kawaida. Kwanza ni kuwa, kutokana na mafanikio iliyopata China, sasa imekuwa ni nchi inayojiamini kuwa inaweza kufanya mipango na maamuzi yake, na kuyatekeleza na kuyasimamia.

Katika maeneo mengine duniani, jambo hili ni kama janga. Kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa jambo lolote si zuri, au haliwezi kufanyika kama nchi za magharibi hazijasema jambo hilo ni zuri. China imevuka hatua hiyo, inafanya maamuzi, kuyatekeza na kuyasimamia kwa kujiamini, bila kusubiri au kuhofu watu wengine wasema jambo hilo ni zuri au si zuri. Kwa sasa ni nchi chache sana duniani zinazoweza kufikia hatua kama hii. Siku zote kabla ya kufanya uamuzi zinajiuliza nchi za magharibi zitasema nini.
 
daaah inashangaza sana.............njia walizotumia china kudevelop kwa kasi kubwa
 
China pongezi kwao kwa maendeleo ya haraka, kubwa Sera Yao kufungulia uchumi na kuchangamana na dunia. Wamekuwa wazalishaji wa dunia kwa miongo kadhaa 3-4 ( miaka 30-40)
Habari mbaya baada ya kutumia Sehemu kubwa ama kumaliza Malighafi za asili wanaanza kuhaha Africa na Asia.
Jitihadi kuhamia high tech bado Zina changamoto nyingi kufuatia Tabia ya Mchina kutoaminika.Japo miji Kama Shanghai wanajaribu viwanda vya high tech kuondokana na viwanda bidhaa.
Hivyo huenda China ikaporomoka kwa kasi miaka 2050; Kufuatia nchi nyingi kuwa na Sera protectionism malighafi na kuvutia viwanda bidhaa kuzalishwa ndani nchi husika.
 
Back
Top Bottom