China inavyoshikana mkono na wenzake wa Afrika katika kuinua huduma za afya

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,033
Ikiwa dunia bado ipo kwenye taharuki ya ugonjwa thakili la COVID-19, nchi mbalimbali zinaendelea kufanya juhudi ya kupambana na ugonjwa huu ili kuhakikisha unatokomezwa kabisa. Mbali na hatua mbalimbali zinazochukuliwa za kuzuia janga hili, nchi za Afrika bado zinaendelea kusuasua na kuonekena kuelemewa zaidi.

Nchi kama Afrika Kusini, Algeria na Misri zimekuwa zikiongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi wa virusi vya Corona. Hata nchi ambazo haziongozi kwa maambukizi bado hali si shwari na zinasumbuliwa sana na ugonjwa huu. Kwa kuonelea hili, China imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha ndugu na rafiki zao wa Afrika wanaweza angalau kumudu chanjo pamoja na kuwapatia misaada mingine ya vifaatiba ili kuokoa maisha ya mamilioni ya watu wa Afrika.

Hivi majuzi tu, Misri imeanza kutoa chanjo ya CoronaVac ya China ambayo imetengezwa humohumo nchini Misri. Hii ni hatua kubwa sana na ya kupigiwa mfano kwa nchi ya Afrika kuweza kutengeneza chanjo chini ya uungaji mkono wa China.

Tunafahamu kuwa mifumo na miundo mbinu imara ya afya, inawezesha kutoa hudumua bora kwa watu wote wakati watakapozihitaji huduma hizo. Na mlipuko wa Corona umedhihirisha wazi nini kinaweza kutokea wakati juhudi za kushughulikia majanga kwenye mifumo ya afya ambayo imeshaelemewa na kushindwa kutoa huduma nyingine muhimu kama za vipimo na matibabu ya saratani, chanjo na huduma kwa kina mama na watoto.

Hivi sasa ujenzi wa Makao Makuu ya Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa cha Afrika (Africa CDC) unaendelea vizuri kama ulivyopangwa. Ujenzi huu unaogharimu dola za Kimarekani bilioni 80, unatokana na juhudi za China katika kuimarisha ushirikiano wake na Afrika kwenye sekta ya afya ya umma. Ujenzi wa kituo hicho ulioanza Disemba mwaka jana katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, unatarajiwa kuchukua miezi 25 hadi kukamilika kwake, na kitakuwa na majengo ya kisasa ya ofisi na maabara ya kiwango cha juu.

Fantahun Hailemichael, mratibu wa mradi wa Makao Makuu ya Africa CDC kwenye Umoja wa Afrika AU, anasema mradi huo unatazamiwa kuboresha huduma za afya ya umma katika Afrika, hasa katika kuongeza uwezo wa Afrika kudhibiti na kusimamia magonjwa ya maambukizi.

"Mradi huu ni matokeo ya moyo mwema wa China kuiunga mkono Afrika kama mshirika wa kweli na wa kuaminika wa nchi za Afrika na Umoja wa Afrika," alisema Hailemichael

Nchi nyingi za Afrika hazina uwezo wa kutosha, ambapo ushahidi kamili unaonekana kwenye janga hili la virusi vya Corona. Hivyo serikali ya China imekuja kama rafiki mwema kuisaidia Afrika kupambana na virusi, ikiwemo kujenga kituo hiki, huku ikifahamu kwamba nchi hizi zina changamoto kubwa ya kuwalinda wananchi wao na kuwapatia huduma muhimu za afya.

Wazo hili la kujenga kituo cha Africa CDC likiwa limependekezwa na rais wa China Xi Jinping, kwenye mkutano uliofanyika mwaka jana kati ya China na Afrika, linapaswa kuenziwa na kuheshimiwa, kwani kiongozi huyu amethibitisha ule msemo wa waswahili kwamba “Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli”. Wakati Waafrika wakiendelea kukosa hata chanjo za kutosha, kituo hicho kitakapokamilika kitabeba jukumu kubwa na muhimu kwenye mapambano haya na labda kutakuwa na ahueni kwenye masuala ya huduma afya.

Tangu miaka ya 1960 China imekuwa ikiwekeza kwa wingi barani Afrika hususan kwenye miundombinu ya barabara, reli na majengo. Na cha kufurahisha ni kwamba China haiwekezi katika miradi isiyo na maana, bali inalenga kulisaidia bara la Afrika na kulifanya liondokane na dhiki mbalimbali.

Mbali na kituo cha Africa CDC, China pia imejikita kwenye ujenzi wa hospitali za Urafiki kati ya China na nchi za Afrika, mfano mzuri ni kule nchini Zimbabwe ambako imejengwa hospitali ya Mahusekwa. Hospitali hii ya kisasa inatoa huduma bora za afya na matibabu kwa watu wa Zimbabwe. Huu ndio moyo wa China kumnyanyua rafiki pale inapoona amedondoka na hatimaye kuendelea naye na safari, lakini yule anayenyanyuliwa, naye anatakiwa kujikaza ili safari iwe nyepesi huko mbele.
VCG11464180689.jpg
 
Wahuni hao wanaweza hata kuvuna internal organs na kuziuza kwao kwa bei mbaya sana. Wana chuki za kutisha dhidi ya Waafrika.
Wanatuita HEI REN yaani watu weusi..hilo neno kwao ni neno la dharau sana . na viungo sio uongo wanavivuna kwa wingi mno
Ninapatwa na hasira sana ninapoona viongozi wanavyowanyenyekea na kuwakenulia meno
 
Back
Top Bottom