China imeahidi kuendelea kushirikiana na nchi za SADC katika mapambano dhidi ya COVID19

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,969
IMG_20200429_114024_235.jpg
Serikali ya China imeahidi kuendelea kushirikiana na nchi za SADC katika mapambano dhidi ya COVID19.

Ahadi hiyo imetolewa leo Beijing na Mkurugenzi wa Afrika wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Nd.DAI Bing alipokutana na Mwenyekiti wa Mabalozi wa Nchi za SADC Nd. Mbelwa Kairuki

Katika kutekeleza ahadi hiyo- wiki ijayo Timu ya Madaktari Bingwa walioshiriki katika mapambano dhidi ya COVID19 nchini China itakwenda katika nchi mbili za SADC- Zimbabwe na DRC kwa ajili ya kukutana na madaktari wa nchi hizo kubadilishana uzoefu wa tiba ya COVID19.

Vilevile China itatuma awamu ya pili ya msaada wa vifaa Tiba kwa nchi zote za SADC.
 
Jambo la kheri hili, ila mbona balozi ameshindwa ku-lobby hao madaktari waje na Bongo? Au huku hatuna tatizo kubwa sana kama DRC na Zim?
 
Hao wanatafuta mali ghafi tu kwa ajili ya uchumi wao ulioporomoka. Hawawezi kutupenda kabisa hawa, tumeona majuzi tu kwenye swala la Covid-19 walivyotubagua na kutusingizia ugonjwa ambao wao ndio walikuwa ni chanzo.
Hawa watu ni bure kabisa.
 
Kweli naamini baadhi ya watu weusi ni vema tukaacha wazungu wawatoe kafara kwa sababu moja tuuu UKOSEFU WA MAARIFA.
1. Mchina ni mwanadamu kama watu weusi.
Tusiwakaribishe kwenye nchi zetu kwa sababu wanatuombea mabaya.
2. Tuna madaktari wazuri badala tuwape ushirikiano pamoja na waganga wa jadi ili tuzuie haya maradhi. Bado mnawadhami hao wanyonyaji.
3. Imefika wakati kuwaacha watu weusi watolewe kafara ambao hawataki kutafuta maarifa.
4. Naamini waganga wa jadi wenye dawa za asili za kutukinga au kutibu kabisa maradhi tunayoletewa na hawa watu weupe.
 
Back
Top Bottom