China haitakiwi kulaumiwa kwa kusaidia nchi za Afrika kuwachunguza watu wake kupitia ushirikiano wa kidigitali

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
Na Fadhili Mpunji

VCG41N1047669026.jpg


Katika miaka ya hivi karibuni bara la Afrika limekuwa na maendeleo makubwa kwenye sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano (ICT) na mambo ya kidigitali kwa ujumla, na sekta hii inatajwa kuwa ni moja ya sekta zenye maendeleo ya kasi zaidi katika nchi za Afrika, na kuwa sekta inayoleta fursa nyingi na changamoto nyingi kwa pamoja kwa nchi za Afrika.

Kuna ushahidi mkubwa unaoonesha kuwa mambo ya kidigitali barani Afrika yamekuwa na maendeleo makubwa, ikiwa ni pamoja na kwenye sekta ya TEHAMA. Sababu kubwa ya maendeleo hayo inaweza kuwa mahitaji ya wakati na nia ya nchi za Afrika kwenda sambamba na dunia, lakini uwekezaji mkubwa wa serikali za Afrika, makampuni binafsi, na hata serikali washirika za nje ya Afrika zimesaidia kuboresha hali hiyo.

China imekuwa mchangiaji mkubwa wa maendeleo ya sekta ya digitali barani Afrika. Baadhi ya maeneo ya ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika yaliyohimiza maendeleo haya, ni pamoja na ujenzi wa mkonga wa mawasiliano (optic fiber) uliosaidia kuongeza asilimia ya watu wanaofikiwa na huduma za internet, (internet penetration), upatikanaji wa vifaa vya kidigitali vyenye bei nafuu na ubora wa juu. Kutokana na ushirikiano huo, kwa sasa ni jambo la kawaida kuona mwafrika wa kawaida ana simu aina ya smartphone iliyounganishwa na internet, au kwa wale wenye uwezo wa kati kuwa na vifaa kama Kamera za usalama au hapa kompyuta zilizounganishwa na internet.

Maendeleo ya mambo ya digitali yamefungua sekta ya uchumi wa kidigitali ambayo inaendelea kwa kasi. Kwa sasa vijana wengi wa nchi za Afrika wamejiajiri kwenye sekta za sanaa, habari na burudani kutokana na maendeleo ya kidigitali. Imekuwa kawaida kuona televisheni za mtandao, na hata biashara zimeanza kufanywa kwa njia ya mtandao wa internet kati ya watu wa nchi za Afrika, na kati ya watu wa Afrika na nchi nyingine duniani. Na sekta hii imekuwa ni chanzo cha mapato kwa serikali za nchi za Afrika.

Manufaa ya maendeleo haya yameonekana zaidi hivi karibuni hasa kwenye kipindi cha janga la COVID-19. Kupitia mtandao wa internet, wafanyabiashara wa Afrika wameweza kufanya biashara kati yao na nchi nyingine bila kuhitaji kusafiri.

Hata hivyo kumekuwa na maoni kuwa ushirikiano kati ya China na Afrika kwenye sekta hii umeimarisha uwezo wa serikali za nchi za Afrika kufanya upelelezi dhidi ya watu wake, na kufikia kuitaja hali hiyo kuwa ni hali ya utawala kiimla kwa kutumia mambo ya kidigitali (digital authoritarianism). Pamoja na ukweli kwamba nchi za Afrika zimenunua vifaa vya usimamizi wa Internet kutoka China, kila mtu anajua kuwa China ni mmoja wa wauzaji wa vifaa hivyo, na sio mdau pekee au muuzaji pekee anayeuza vifaa hivyo kwa nchi za Afrika.

Ukweli ni kwamba nchi za magharibi zilipuuza fursa za maendeleo ya sekta ya TEHAMA barani Afrika, lakini makampuni ya China yalitambua mapema fursa na kuona mbali kuhusu fursa zilizopo kwenye eneo hilo. Kwa hiyo shutuma na malalamiko, zinaonesha kutofurahishwa na kukosa fursa ya biashara kwa baadhi ya nchi za magharibi.

Lakini ni kweli kuwa kuna changamoto nyingi kwenye usimamizi wa teknolojia za kidigitali barani Afrika. Hii ni kutokana na kuwa maendeleo ya sekta hii yamekuwa ya kasi kuliko maandalizi ya sheria na kanuni za kusimamia teknolojia hizo. Watu wa Afrika wanapata vifaa hivyo kwa urahisi sana, lakini hawajui kwamba kuwa wajibu fulani kwenye kumiliki na kutumia vifaa hivyo. Ni sasa watu wanaanza kutambua kuwa simu za mkononi na internet vikitumiwa vibaya vinaweza kuwa chanzo cha udhalilishaji au ubabe mitandaoni, wizi wa kimtandao, au hata kueneza chuki na kuhatarisha usalama wa nchi.

Mamlaka zinapotambua hatari inayotokana na hali hii, zinachukua hatua za ghafla ambazo baadhi ya watu wanatafsiri kuwa hatua za kikandamizaji za serikali, na wanajaribu kutupia lawama wengine.
 
Na Fadhili Mpunji

View attachment 1949361

Katika miaka ya hivi karibuni bara la Afrika limekuwa na maendeleo makubwa kwenye sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano (ICT) na mambo ya kidigitali kwa ujumla, na sekta hii inatajwa kuwa ni moja ya sekta zenye maendeleo ya kasi zaidi katika nchi za Afrika, na kuwa sekta inayoleta fursa nyingi na changamoto nyingi kwa pamoja kwa nchi za Afrika.

Kuna ushahidi mkubwa unaoonesha kuwa mambo ya kidigitali barani Afrika yamekuwa na maendeleo makubwa, ikiwa ni pamoja na kwenye sekta ya TEHAMA. Sababu kubwa ya maendeleo hayo inaweza kuwa mahitaji ya wakati na nia ya nchi za Afrika kwenda sambamba na dunia, lakini uwekezaji mkubwa wa serikali za Afrika, makampuni binafsi, na hata serikali washirika za nje ya Afrika zimesaidia kuboresha hali hiyo.

China imekuwa mchangiaji mkubwa wa maendeleo ya sekta ya digitali barani Afrika. Baadhi ya maeneo ya ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika yaliyohimiza maendeleo haya, ni pamoja na ujenzi wa mkonga wa mawasiliano (optic fiber) uliosaidia kuongeza asilimia ya watu wanaofikiwa na huduma za internet, (internet penetration), upatikanaji wa vifaa vya kidigitali vyenye bei nafuu na ubora wa juu. Kutokana na ushirikiano huo, kwa sasa ni jambo la kawaida kuona mwafrika wa kawaida ana simu aina ya smartphone iliyounganishwa na internet, au kwa wale wenye uwezo wa kati kuwa na vifaa kama Kamera za usalama au hapa kompyuta zilizounganishwa na internet.

Maendeleo ya mambo ya digitali yamefungua sekta ya uchumi wa kidigitali ambayo inaendelea kwa kasi. Kwa sasa vijana wengi wa nchi za Afrika wamejiajiri kwenye sekta za sanaa, habari na burudani kutokana na maendeleo ya kidigitali. Imekuwa kawaida kuona televisheni za mtandao, na hata biashara zimeanza kufanywa kwa njia ya mtandao wa internet kati ya watu wa nchi za Afrika, na kati ya watu wa Afrika na nchi nyingine duniani. Na sekta hii imekuwa ni chanzo cha mapato kwa serikali za nchi za Afrika.

Manufaa ya maendeleo haya yameonekana zaidi hivi karibuni hasa kwenye kipindi cha janga la COVID-19. Kupitia mtandao wa internet, wafanyabiashara wa Afrika wameweza kufanya biashara kati yao na nchi nyingine bila kuhitaji kusafiri.

Hata hivyo kumekuwa na maoni kuwa ushirikiano kati ya China na Afrika kwenye sekta hii umeimarisha uwezo wa serikali za nchi za Afrika kufanya upelelezi dhidi ya watu wake, na kufikia kuitaja hali hiyo kuwa ni hali ya utawala kiimla kwa kutumia mambo ya kidigitali (digital authoritarianism). Pamoja na ukweli kwamba nchi za Afrika zimenunua vifaa vya usimamizi wa Internet kutoka China, kila mtu anajua kuwa China ni mmoja wa wauzaji wa vifaa hivyo, na sio mdau pekee au muuzaji pekee anayeuza vifaa hivyo kwa nchi za Afrika.

Ukweli ni kwamba nchi za magharibi zilipuuza fursa za maendeleo ya sekta ya TEHAMA barani Afrika, lakini makampuni ya China yalitambua mapema fursa na kuona mbali kuhusu fursa zilizopo kwenye eneo hilo. Kwa hiyo shutuma na malalamiko, zinaonesha kutofurahishwa na kukosa fursa ya biashara kwa baadhi ya nchi za magharibi.

Lakini ni kweli kuwa kuna changamoto nyingi kwenye usimamizi wa teknolojia za kidigitali barani Afrika. Hii ni kutokana na kuwa maendeleo ya sekta hii yamekuwa ya kasi kuliko maandalizi ya sheria na kanuni za kusimamia teknolojia hizo. Watu wa Afrika wanapata vifaa hivyo kwa urahisi sana, lakini hawajui kwamba kuwa wajibu fulani kwenye kumiliki na kutumia vifaa hivyo. Ni sasa watu wanaanza kutambua kuwa simu za mkononi na internet vikitumiwa vibaya vinaweza kuwa chanzo cha udhalilishaji au ubabe mitandaoni, wizi wa kimtandao, au hata kueneza chuki na kuhatarisha usalama wa nchi.

Mamlaka zinapotambua hatari inayotokana na hali hii, zinachukua hatua za ghafla ambazo baadhi ya watu wanatafsiri kuwa hatua za kikandamizaji za serikali, na wanajaribu kutupia lawama wengine.
Kichwa cha habari tofauti na kilichomo ndani
 
Back
Top Bottom