China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

Mkuu heshima kwako kwa kushea uzoefu wako, big up. Nilitaka kupata mtazamo wako wa uzoefu wa bidhaa zinazolipa kutoka huko uchina kwa mtu ambaye anaanza (beginner) na kwa mtaji mdogo say 10m, mfano bidhaa kama handbag za akina dada? Waonaje?. Nimesikia pia ukinunua bidhaa huko china unawapa wauzaji adress ya kampuni ya usafiri (eg silent ocean) kisha wao wanapeleka kwa wasafirishaji, unalipia (usafirishaji)ukishachukua bongo. Je hii ndio tratatibu? Na pia huwa nasikia pia bangkok, vp huko kuna bidhaa nzuri pia? Ushauri wowote kwa beginner asie na uzoefu wowote
Kuhusu bidhaa zinazolipa, naweza kusema bidhaa yoyote inalipa ISIPOKUWA inategemea tu na soko lako ulilolikusudia likoje huku nyumbani Tanzania.
Cha muhimu ANZIA SOKONI ndio uende kiwandani. Hakikisha unajua soko linataka nini kwa muda husika.
Kwa hali ya sasa ya kiuchumi Tanzania, sishauri sana (mtazamo wangu) kwa anaeanza biashara aingie kwenye bidhaa za fasheni na urembo kama nguo na mikoba au viatu.
Kwa sasa "purchasing power" ya watanzania wengi imeshuka kwenye bidhaa za nguo, viatu na mikoba.
Mabadiliko ya kiuchumi, watu wengi wameanza kujiongeza na kufikiria kuwekeza kwenye ujasiriamali mdogo mdogo.
Kwa hiyo kwa sasa ukiuza bidhaa ambayo itatatua changamoto za watu basi utakuwa umejihakikishia soko lako. Kwa mfano: sasa hivi wajasiriamali wadogo wamejikita katika kilimo, ufugaju na usindikaji. Pia wamejikita katika kuongeza thamani ya bidhaa ambazo zimeshazalishwa. Kwa hiyo ukija na bidhaa mfano packaging materials utauza sana kwa sababu hiyo ni moja ya changamoto ya wajasiriamali wengi hawana parking materials kwa ajili ya bidhaa zao. Kwa hiyo utakuwa umetatua matatatizo ya wengi na unaweza ukawa general supplier mikoani (usifocus DSM tu, angalia pia mikaoni).
Bidhaa za nguo na fasheni watu wamepunguza kuvaa "vyuma vimekaza" unless labda utumie mbinu ya kukopesha ambayo nayo ni risk sana na mtaji unaweza ukazama huku unajiona!
Kingine kuhusu bidhaa za nguo na mikoba ni kuwa biashara hiyo inaendeshwa kwa nguvu ya fashion iliyopo, hivyo unaweza kununua mzigo china, mpaka unafika TZ (Kama ni meli umetumia siku 45 hivi) unaweza kukuta nguo au mikoba uliyoleta iloshaingia kariakoo kitambo (wakati mzigo wako ukiwa majini) na bei haipo kama ulivyotarajia, mwisho wa siku unajikuta unauza kwa hasara.
Pia ni muhimu kujikita kwenye biashara ambayo ushindani wake si mkubwa . Biashara ya nguo na mikoba ipo kila baada ya nyumba kadhaa. Kuna maduka ya madera, viatu kila kona! Shangwe za kuvaa siku hizi sio kiviiiileeee...hali si hali.
Biashara ya nguo na viatu ukiwa wewe ndio unaanza itakulazimu ushushe bei uweke "penetrating price" ili uweze kuingia sokoni vizuri mana tayari sokoni kuna wenzio ambao wapo kitambo, unless wewe uje na kitu cha kipekee sana.
Kuhusu usafirishaji, hiyo ni moja ya taratibu lakini binafsi nashauri uwe na mtu kule ambaye atasimama katikati yako na muuzaji ili kuondoa risk mana wachina nao si wote wa kuwaamini. Kuwa na mtu alieko kule yeye akague bidhaa kiwandani, kisha malipo fanya mwenyewe kwenye akaunti ya muuzaji (ambayo iko secured na incase of anything unaweza kuclaim refund na hela yako ikarudi mf. kupitia paypal/alibaba trade assurance nk nk) kisha mzigo ukifika kwenye Ghala la wasafirishaji basi huyo mtu wako aende akaukague na ajiridhishe kuwa ndio ule ule alioukagua kiwandani)
Kuhusu Bankok sina uzoefu napo. wenye uzoefu na huko wataongezea.
NB: Ni maoni yangu tu na yanaweza yasiwe mujarab kwa wengine
 
Kuhusu bidhaa zinazolipa, naweza kusema bidhaa yoyote inalipa ISIPOKUWA inategemea tu na soko lako ulilolikusudia likoje huku nyumbani Tanzania.
Cha muhimu ANZIA SOKONI ndio uende kiwandani. Hakikisha unajua soko linataka nini kwa muda husika.
Kwa hali ya sasa ya kiuchumi Tanzania, sishauri sana (mtazamo wangu) kwa anaeanza biashara aingie kwenye bidhaa za fasheni na urembo kama nguo na mikoba au viatu.
Kwa sasa "purchasing power" ya watanzania wengi imeshuka kwenye bidhaa za nguo, viatu na mikoba.
Mabadiliko ya kiuchumi, watu wengi wameanza kujiongeza na kufikiria kuwekeza kwenye ujasiriamali mdogo mdogo.
Kwa hiyo kwa sasa ukiuza bidhaa ambayo itatatua changamoto za watu basi utakuwa umejihakikishia soko lako. Kwa mfano: sasa hivi wajasiriamali wadogo wamejikita katika kilimo, ufugaju na usindikaji. Pia wamejikita katika kuongeza thamani ya bidhaa ambazo zimeshazalishwa. Kwa hiyo ukija na bidhaa mfano parking materials utauza sana kwa sababu hiyo ni moja ya changamoto ya wajasiriamali wengi hawana parking materials kwa ajili ya bidhaa zao. Kwa hiyo utakuwa umetatua matatatizo ya wengi na unaweza ukawa general supplier mikoani (usifocus DSM tu, angalia pia mikaoni).
Bidhaa za nguo na fasheni watu wamepunguza kuvaa "vyuma vimekaza" unless labda utumie mbinu ya kukopesha ambayo nayo ni risk sana na mtaji unaweza ukazama huku unajiona!
Kingine kuhusu bidhaa za nguo na mikoba ni kuwa biashara hiyo inaendeshwa kwa nguvu ya fashion iliyopo, hivyo unaweza kununua mzigo china, mpaka unafika TZ (Kama ni meli umetumia siku 45 hivi) unaweza kukuta nguo au mikoba uliyoleta iloshaingia kariakoo kitambo (wakati mzigo wako ukiwa majini) na bei haipo kama ulivyotarajia, mwisho wa siku unajikuta unauza kwa hasara.
Pia ni muhimu kujikita kwenye biashara ambayo ushindani wake si mkubwa . Biashara ya nguo na mikoba ipo kila baada ya nyumba kadhaa. Kuna maduka ya madera, viatu kila kona! Shangwe za kuvaa siku hizi sio kiviiiileeee...hali si hali.
Biashara ya nguo na viatu ukiwa wewe ndio unaanza itakulazimu ushushe bei uweke "penetrating price" ili uweze kuingia sokoni vizuri mana tayari sokoni kuna wenzio ambao wapo kitambo, unless wewe uje na kitu cha kipekee sana.
Kuhusu Bankok sina uzoefu napo. wenye uzoefu na huko wataongezea.
NB: Ni maoni yangu tu na yanaweza yasiwe mujarab kwa wengine

Mkuu nashukuru kwa majibu mazuri. Nakubaliana na wewe purchasing power imeshuka sana watu wanatumia pesa kwenye 'needs' kuliko 'wants'. Hilo la packaging pia niliwahi kulifanyia upembuzi haswa kutengeneza mifuko ya karatasi lakini nikagundua mashine nyingi zinapatikana india na ni za pesa ndefu zaidi ya $60k. Sijui hapo kwenye vifungashio kama una abc za kushea.
 
Mkuu nashukuru kwa majibu mazuri. Nakubaliana na wewe purchasing power imeshuka sana watu wanatumia pesa kwenye 'needs' kuliko 'wants'. Hilo la packaging pia niliwahi kulifanyia upembuzi haswa kutengeneza mifuko ya karatasi lakini nikagundua mashine nyingi zinapatikana india na ni za pesa ndefu zaidi ya $60k. Sijui hapo kwenye vifungashio kama una abc za kushea.
Kwenye suala la mashine ni kweli, mashine zipo ghali na hata sisi tunaozileta huku Tanzania, bado watanzania wanataka mashine NZURI ila za bei rahisi kitu ambacho hakiwezekani 100%.
Watanzania tunapata tabu moja kwenye "kuyatoa maisha"! Yaani kila mtu anataka aminyane yeye kama yeye yaani peke yake ili atoke! Vijana wa nchi zilizoendelea/makampuni makubwa yaliyoendelea yalianza chini lakini baadae yaliunganisha nguvu, yaani mfano mwenye wazo la biashara aliunganisha nguvu na mwenye mtaji wa pesa, mwisho wa siku wote mnatoka. Wengi bado tuko nyuma katika kuamini vitu kama patnership (inayotambulika kisheria) na sio ya "kishkaji"! wengi hawaamini kwa kuwa flani na flani walifanya kisha wakadhulumiana! kwa hiyo kila mtu anatoa mfano huo ambao labda ukiangalia haukuwa hata na mikataba ya kisheria nk.
Kwa hiyo nitoe wito kwa vijana KUUNGANISHA NGUVU ya pamoja kuwekeza kwenye viwanda vidogo vidogo ili kuweza kumudu kununua hizo mashine ulizosema nk.
Packaging ni mfano tu nimetoa lakini vipo vimashine vidogo vidogo ambavyo unaweza kwenda china ukanunua na ukaja navyo ukauza kwa bei ya kawaida na ukawa mkombozi kwa wengi na pia hata wewe mwenyewe badala ya kuziuza lakini ukaamua kuzitumia. mfano wa mashine (small scale):
1. Mashine ya kusaga vitu vikavu kama viungo
2. Mashine za kukamua mafuta
3. mashine za kubana mifuko
4. mashine za kushona viroba
5. mashine za kupalilia
6. mashine za kupukuchua mazao ya nafaka kama mahindi, mtama, maharage nk
7. Mashine za kuvuna mpunga nk.
8. mashine za kuponda unga wa ngano
9. Mashine za kuchanganya vyakula vya mifugo
10. Mashine za kusaga/kukata majani kwa ajili ya mifugo
11. vyerehani vya umeme
12. mashine za kukoroga sabuni
13. Mashine ya kuprint label kwenye vifungashio

Pia unaweza kuuza vigungashio ambavyo tayari vimeshatengenezqa kama mifuko, chupa za aina mbali mbali nk. ukizinunua hizi china kutoka kiwandani moja kwa moja na kuzileta Tanzania utauza sana tu hasa hasa kama utanunua na kisha ukija Tanzania unatengeneza label kulingana na mahitaji ya mteja ili mteja auze bidhaa yenye brand name yake. Tsh 10M ni mtaji mkubwa saba kama utaamua kuwekeza kwenye hili la vifungashio.
 
Habari!nahitaji mshine ya kukamua mafuta ya alizeti na peanuts medium size,je naweza pata bei gani mpaka hapa Bongo?
 
Habari!nahitaji mshine ya kukamua mafuta ya alizeti na peanuts medium size,je naweza pata bei gani mpaka hapa Bongo?
mkuu, asante kwa swali. ili uzi huu tusiuchanganye kidhima, nashauri ubakie kama ulivyo uwe ni ushauri tu tena wa BUREEEEEE na nitaendelea kuutoa BUREEE kadri MUNGU atakavyoniwezesha. Kuhusu mashine hizo ulizouliza na nyingine naomba ingia kwenye hii link hapa utaona
Niulize kuhusu mashine za ujasiriamali na upatikanaji wake
 
Mkuu kinachofanyika hapa ni sawa tu kununua vitu China na kuuza kwenye masoko makubwa hapa nchini kama Nakumatt, The Game, Pick and Pay, n.k. Tofauti ni kuwa badala ya kuuza hapa nchi unaviuuza kwenye masoko makubwa AmAZON AU eBAY duniani. Tofauti nyingine ni kuwa huendi China wala USA/UK kuuza. Amazon wana mfumo unaokuwezesha kusafirisha vitu kwako mpaka kwao unaitwa FBA-Fulfillment By Amazon. Ukishanunua vitu vyako China wanakusafirishia mpaka Amazon kisha wanavitunza kwenye store yao. Kazi yako wewe nikuvi list kwenye Amzano.com kuonyesha picha na maelezo yake nakuanza kufanya marketing. Kikubwa hapa ni kupata reviews za bidhaa zako ili ziweze ku rank higher na kuanza kupata wateja.

Vintage_Retro_Pu_Leather_Stand_mobile_phone.jpg_220x220.jpg
Mfano hii ni Iphone 6 cover, Alibaba wanauza US $1-5 / Piece( FOB Price) na min order ni 500 negotiable
21MCB6oHOWL.jpg
. Ukienda Amazon.com, cover ile ile
Phone 6 Case, Spigen [HEAVY DUTY] Tough ArmorCase for iPhone 6 (4.7-Inch) - Gunmetal (SGP11022) wanaiuza $ 17. Walichofanya hapa ni wamei brand tu


Unaweza kuona potential iliyopo kwenye masoko haya. Na ukifanya marketing vizuri unaweza kuuza hapa piece 20 kwa siku. Assume una biashara kama hizo 3 au nne hivi. Haya yanafanyika kwenye computer bila hata kunyanyuka nyumbani kwako.

Lakini kama nilivyosema inahitaji kujifunza na watu hasa watumiaji wa mitandao wasitumie kwa kutumiana vichekesho tu ila watumie kwa kufanya biashara za uhakika. Wanachuo na watu wenye muda wa ziada na mtaji kidogo say $ 200 wanaweza kuanza biashara hii.

P.S Watu wanadhani bidhaa za China zina quality ndogo lakini siyo kweli, China wanakuuzia quality unayotaka. Kwa USA na Ulaya huwezi ingiza kama hizi zinazokuja kwetu.

PPS. Watu watafikiri ni mtaji mkubwa, hata unaweza kujaribu kwa kuleta sample na kuuza katika masoko yetu hapa nchini, Nakumatt, The game n.k kuna fursa hiyo ili product yako uijue vizuri.

PPPS. Bandiko hili linaweza kusomwa pamoja na lingine lililoko humu ndani linalosema kununua vitu Amazon. Somo ni refu sana ila inawezekana hakuna pesa rahisi.

Samahani kwa mwandiko mbaya, I am not so much used to the writing stuff.
NSamahani nlikuwa naomba kwamba natawezaje kuanza biashara hiyo na process inakuaje kwa sababu naamini ni fursa nzuri kwa upande wangu...!!
 
nami nasubiri...japo mkuu hujaainsha ni aina gani ya biashara ili wachangiaji watoe data vizuri!
 
kama umesha wahi fanya biashara yoyote kuchukua mzigo china na kuleta TZ, naomba mrejesho wa garama na changamoto
Mkuu naleta kila siku mizigo Tanzania. Gharama nimeeleza hapo juu mwanzo kabisa wa uzi huu. Changamoto pia zimejadiliwa sana humu ndani. Tafadhali chukua muda kupitia huu uzi kuanzia mwanzo hadi mwisho na naamini hutajuta bando lako utakalitumia. You will never be the same ! utapata cha kujifunza na majibu ya maswali yako
 
Huu uzi nimeusoma kwa wakati muafaka.Nataka kufungua shop la kuuza phone accessories&phone but nataka niagize kutoka China.Sina uzoefu hata kidogo nimesoma nimepata primary information lakini najiona bado nina inferior
 
Mkuu, hili bandiko aliweka mwenzetu humu ndani, ila linaelezea kununua tu Amazon, nimeziba mwanya kwa kuonesha unaponunua Amazon wao wanaokuuzia hununua Alibaba.com China. Hivyo tuwe makini na bidhaa hizi, tunaambiwa kuna ni za USA au Ulaya kumbe nao baadhi ya bidhaa zao hunuunua China. Unaweza kusoma kwa pamoja ili kupata uelewa zaidi.


Jifunze njia nzuri ya kufanya manunuzi kwenye mtandao (Ebay, Amazon, Bestbuy)


Imekuwa ni shida sana kwa watanzania wengi kununua bidhaaa katika masoko haya ya mtandaoni kwani mengi huwa hayakupi fursa ya kutumiwa mzigo wako moja kwa moja Tanzania. baadhi ya thread zilianzishwa na zimeelezea mengi sana kuhusiana na manunuzi haya ya mtandaoni, ila tulipata ufumbuzi mdogo. Nimejaribu kupitia pitia forums nyingi nichanganue namna mbadala ya kupata mizigo bila ya kutumia gharama nyingi. hii ni kwa kutumia FOWARDING COMPANIES ambazo kazi yake ni 1: Kukupatia anuani ya Marekani (au popote iliopo ila nashauri marekani au uingereza UK) au US Shipping Address 2:Kupokea mzigo kwenye soko ulilotumia (eidha amazon,ebay au lolote lile lisilo ship Tanzania) 3:Kukutumia mzigo wewe hapo ulipo kwa wakala kama DHL,FEDEX,UPS,USPS NK baada ya kujua kazi ya fowarding company unahitaji kuwa na vigezo vifuatavyo (kwa wageni wasiofahamu/hawajapitia previous threads:

1:CREDIT CARD (KADI YA BENKI) INAYOFANYA ONLINE PURCHASES;
Hii inapatikana almost bank zote hapa Tanzania (kasoro NMB sina uhakika), ni kadi yeyote ya visa au mastercard unachotakiwa ni kwenda kwenye tawi la benki yako na kuomba fomu ya kuruhusu kadi yako ifanye malipo ya mtandaoni(online purchases) na mara nyingi huchukua maximum 24hours kuactivate.

2:KUJIUNGA NA PAYPAL
Hiii ni kampuni inayolinda malipo yako kwa kutomuonesha muuzaji details (nyaraka) za kadi yako kama number na css ambayo vitampa muuzaji access ya kuchukua pesa zako. Ila kwa paypal utalindwa na kurudishiwa pesa pale panapotokea shida au huduma mbaya.

3:KUJIUNGA NA FOWARDING COMPANY

Hii hatua ni ya wewe kwenda kwenye website (tovuti) za hizi fowarding company na kujiunga (sighnup) nazo/nayo ili zianze kukupatia huduma... nitaelezea chini zaidi kuhusu ipi ni ipi na huduma zao zikoje na faida na hasara za kila moja ili ujichagulie wewe mwenyewe binafsi

4:KUTAMBUA SOKO BORA LENYE HUDUMA NZURI(ONLINE MARKET)
Hapa tunazungumzia website za masoko kama ebay,amazon, bestbuy, apple.com, dell.com, toshiba.com nk.. masoko haya ndipo utakapo nunua bidhaa yako.

PROCESS NZIMA KUANZIA UNANUNUA MPAKA MZIGO UNAKUFIKIA IKOJE?
hii iko hivi.... 1:Ingia katika soko lako ulilolichagua au unalopendelea, hapa nasuggest kutumia sana amazon(ndilo ninaloliamini) amazon ukiingia utakuta bidhaa nyingi ila kuwa makini kuchukua zile bidhaa zilizo na alama ya prime chini...alama hiyo inamaanisha kuwa huo mzigo unauzwa, utapakiwa, na kutumwa na amazon wenyewe, so no utapeli hapo, yani u get what u wanted. 2:Nunua na kuagiza kitu kwenda kwenye address ya fowarding company ulioichagua, hivyo mzigo ulioununua utaenda moja kwa moja kwenye company yako, wao wakishaupata watakutumia e-mail uthibitishe au uchague courier wa kukutumia mzigo wako, hapo ndio utachagua either dhl,ups,fedex nk.wao watakutumia na kuchukua kiasi chao cha pesa ya huduma na kukutumia mzigo pamoja na kukupatia tracking number ya kujua mzigo wako ulipo na utaupokea vyema.

FOWARDING COMPANIES ZENYEWE:

1: MYUS.COM link- MyUS.com - #1 International Shipping, Mail and Package Forwarding Service - MyUS.comhii ni company niliyoitumia na nina expirience nayo ya mizigo miwili, hawa ni waaminifu wana charge pesa kidogo na huwa hawachukui muda kukutumia mzigo wako. yaani unafika leo hata ukitaka utumwe leo unatumwa, na utafika upesi sana bila ya zengwe lolote.
Ubaya wao: wanatumia sana DHL ambayo kwa mizigo mikubwa ni gharama sana kwa mtanzania wa kawaida, kiasi cha dola kumi kujiunga na huduma zao
Uzuri wao: watakutumia mzigo hata kama utakuwa hauna pesa kwenye account yako, watakujulisha ni duka lipi lina discount ya kutumia huduma zao, watakukumbusha kulipa deni lao, utapewa muda wa miezi miwili kulipa pesa yao,

2:COMGATEWAY
link-Shop US Stores and Ship Internationally | comGateway hawa pia ni fowarding company nzuri sana (thanks tu Mwl.RCT), nimepitia site yao na uona wana policy nzuri sana,cha kwanza ni sales tax-free U.S. online shopping yaani punguzo la kodi ya kufanya manunuzi marekani,hii inapelekea huduma zao kuwa nafuu zaidi,pia wana ushirika na shipping courie DHL na FEDEX hivyo kufanya huduma zao kuwa rahisi zaidi.pia wanakupa habari kuhusu discount za masoko mbalimbali kama myus..

3:BORDERLINX
link- Buy in the USA, ship to Belgium with Borderlinx hawa pia ni wazuri sana na hawana tofauti sana na stackry ... wanawiana ingawa ni competitors wakubwa hivyo inakupa urahisi wa kuwatumia..hawa pia hawana registration fee na wanakupa option tofauti tofauti za kutumiwa mzigo wako.

4:SHIPITO
link-USA Address & Mail Forwarding &[HASHTAG]#8211[/HASHTAG]; Shipito.com | English hii pia ni kampuni kongwe ya fowarding na wao gharama zao ni nafuu sana ingawa wanapokea malalamiko mengi sana kutoka kwa wateja wao ukiangalia kwenye forums nyingi.ila kiujumla ni wazuri kwasababu malalamiko ni madogo kulinganisha na ufanisi na pia wanajua na ni wazoefu sana na kazi yao

5:STACKRY
link- Stackry - US shopping, global shipping hii nayo haina tofauti na myus isipokuwa hawa wao hawana kiasi cha kulipia kujiunga nao na wao pia wanakupa option nyingi za kutumia mizigo yako na mabo yao pia ni mazuri kulinganisha na comment wanazopokea kutoka kwa wateja wao. waungwana ni hayo tu niliyo nayo, kazi kwenu ni kufanya utafiti na pia kuangalia na kuchunguza mabo kabla ya kuchukua uamuzi. STACKRY na BORDERLINX walikuwa recommended sana na wanasifiwa mno angalia hii link -http://tech-vise.com/10-parcel-forwarding-services-for-international-shoppers/ pitia hizo websites na ujionee mwenyewe chagua moja na utazame kama wanakufaa.

HUU NI MTAZAMO WANGU BINAFSI WAKUU please evaluate kindly.

nilikuwa nataka kuonyesha steps ila naona thread haitoshi . maana nimeagiza mzigo na nimechukua hatua zote ili mpate kuona ila ithink there r limits.. help Mwl.RCT
Last edited by JZHOELO; 6th November 2014 at 23:17.​
safi
 
Huu uzi nimeusoma kwa wakati muafaka.Nataka kufungua shop la kuuza phone accessories&phone but nataka niagize kutoka China.Sina uzoefu hata kidogo nimesoma nimepata primary information lakini najiona bado nina inferior
soma tena
 
Mkuku sasa sisi wengine sio wapenzi wa safari kivile na tunatamani kuagiza baadhi ya vitu kutoka china ila sasa confidence level ni ndogo hasa kutokana na ukweli kamba bado hatuna uzoefu.Nimewahi fanya window shopping kwenye tovuti mbalimbali za china ningependa kufahamu iwapo mtu anaweza agiza mzigo wake online tokea china na akaletewa kama ambavyo tunafanya na magari kwenye hizo local offices zao

Asante
 
Mkuku sasa sisi wengine sio wapenzi wa safari kivile na tunatamani kuagiza baadhi ya vitu kutoka china ila sasa confidence level ni ndogo hasa kutokana na ukweli kamba bado hatuna uzoefu.Nimewahi fanya window shopping kwenye tovuti mbalimbali za china ningependa kufahamu iwapo mtu anaweza agiza mzigo wake online tokea china na akaletewa kama ambavyo tunafanya na magari kwenye hizo local offices zao

Asante
Ndio mkuu unaweza kuagiza na mzigo kukufikia ulipo. Pitia comments za wadau kuanzia mwanzo, michango ni mingi sana inayoelezea hilo. ukishindwa kabisa nitafute nitakusaidia kupata unachohitaji.
 
Back
Top Bottom