Chimbuko la wazaramo

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,439
Hili ni moja ya kabila ambalo linapatikana hapa hapa Tanzania hasa upande wa mashariki.

Japo habari na historia la kabila hili zilishaandikwa, hasa juu ya asili ya neno Uzaramo au Wazaramo. Kwa kuwakumbusha tu, Wazaramo maana yake ni waamiaji. Naweza kusema kuwa, kwa mujibu wa wataalamu walioandika habari za makabila ya tanzania na Afrika kwa ujumla , wanasema kuwa, Wazaramo ni jumla ya koo mbalimbali zilizofika Pwani ya Afrika mshariki, hasa maeneo ya mwambao wa Dar es salaam hata kabla ya miaka ya 1600.

Koo hizo ambazo zilitokea bara zilikuja Kuzarama yaani kuhamia maeneo ya Pwani kwa lengo la kufanya shughuli mbalimbali za kibaishara na uvuvi kwenye meneo hayo. Ukweli ni kwamba neno Kuzarama ni la kibantu na maana yake ni Kuhamia.

Hivyo mtu anayehamia huitwa Mzaramo na wakiwa wengi wanaitwa Wazaramo. Na wakati wageni hao wanafika pwani, waliuliza nyinyi ni wakina nani na ndipo wenyeji hao walipojibu kuwa wao ni Wazaramo, yaani wahamiaj. Basi kuanzia hapo yaani miaka ya 1840/1850 kipindi wageni wanafika na kuandika habari za waafrika Watu waliofika Pwani walifahamika kama Wazaramo.

Jambo la kufahamu hapo ni kwamba, koo zilizokuja kuzarama ni kutoka maeneo mbalimbali. Hivyo kuna uwezekano wa kuwa , koo za makabila mengi ziliunda kabila hili la kizaramo. Na ndio maana tamaduni nyingi za kizaramo zipo kwenye makabila mengi japo kuna utofauti kidogo ambao ulisababishwa na masuala ya kijiografia.

Mara baada ya kufahamu habari hizo, tupate kufahamu chimbuko au mahali ambapo kabila hili la kizaramo zilianzia. Inafafanuliwa kuwa, kabila la wazaramo lilipata kuchimbukia maeneo ya Moneromango au wengi hutamka Mwanarumango.

Hama kuhusu Maneromango, ni sehemu inayopatika katika wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani. Inafafanuliwa kuwa eneo hili ndio chimbuko la Wazaramo kwa kuwa, kiongozi wa kabila hili Bwana Pazi Kilama alipata kuishi maeneo hayo, na hata mpaka vita kati ya Wazaramo na Wakamba vinatokea, vilipiganiwa maeneo haya.

Hata koo za Kibena kwa mara ya Kwanza walikutana hapo na Wazaramo na kuachana maeneo ya Moneromango. Na zaidi ya hapo, hata zile koo maarufu kama ukoo wa wakina Samatha na ukoo wakina Kawambwa, zilipata kuishi maeneo ya Monerumano au Mwanarumango.

Na pia kulikuwa na habari nyingi za kuvamiwa na simba, inasimuliwa kuwa maeneo hayo ndio yalikuwa maeneo ambayo yalikuwa yakivamiwa sana na simba. Hivyo maeneo ya Monerumango ndio moja ya maeneo ya mwanzo kukaliwa na Wazaramo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili ni moja ya kabila ambalo linapatikana hapa hapa Tanzania hasa upande wa mashariki.

Japo habari na historia la kabila hili zilishaandikwa, hasa juu ya asili ya neno Uzaramo au Wazaramo. Kwa kuwakumbusha tu, Wazaramo maana yake ni waamiaji. Naweza kusema kuwa, kwa mujibu wa wataalamu walioandika habari za makabila ya tanzania na Afrika kwa ujumla , wanasema kuwa, Wazaramo ni jumla ya koo mbalimbali zilizofika Pwani ya Afrika mshariki, hasa maeneo ya mwambao wa Dar es salaam hata kabla ya miaka ya 1600.

Koo hizo ambazo zilitokea bara zilikuja Kuzarama yaani kuhamia maeneo ya Pwani kwa lengo la kufanya shughuli mbalimbali za kibaishara na uvuvi kwenye meneo hayo. Ukweli ni kwamba neno Kuzarama ni la kibantu na maana yake ni Kuhamia.

Hivyo mtu anayehamia huitwa Mzaramo na wakiwa wengi wanaitwa Wazaramo. Na wakati wageni hao wanafika pwani, waliuliza nyinyi ni wakina nani na ndipo wenyeji hao walipojibu kuwa wao ni Wazaramo, yaani wahamiaj. Basi kuanzia hapo yaani miaka ya 1840/1850 kipindi wageni wanafika na kuandika habari za waafrika Watu waliofika Pwani walifahamika kama Wazaramo.

Jambo la kufahamu hapo ni kwamba, koo zilizokuja kuzarama ni kutoka maeneo mbalimbali. Hivyo kuna uwezekano wa kuwa , koo za makabila mengi ziliunda kabila hili la kizaramo. Na ndio maana tamaduni nyingi za kizaramo zipo kwenye makabila mengi japo kuna utofauti kidogo ambao ulisababishwa na masuala ya kijiografia.

Mara baada ya kufahamu habari hizo, tupate kufahamu chimbuko au mahali ambapo kabila hili la kizaramo zilianzia. Inafafanuliwa kuwa, kabila la wazaramo lilipata kuchimbukia maeneo ya Moneromango au wengi hutamka Mwanarumango.

Hama kuhusu Maneromango, ni sehemu inayopatika katika wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani. Inafafanuliwa kuwa eneo hili ndio chimbuko la Wazaramo kwa kuwa, kiongozi wa kabila hili Bwana Pazi Kilama alipata kuishi maeneo hayo, na hata mpaka vita kati ya Wazaramo na Wakamba vinatokea, vilipiganiwa maeneo haya.

Hata koo za Kibena kwa mara ya Kwanza walikutana hapo na Wazaramo na kuachana maeneo ya Moneromango. Na zaidi ya hapo, hata zile koo maarufu kama ukoo wa wakina Samatha na ukoo wakina Kawambwa, zilipata kuishi maeneo ya Monerumano au Mwanarumango.

Na pia kulikuwa na habari nyingi za kuvamiwa na simba, inasimuliwa kuwa maeneo hayo ndio yalikuwa maeneo ambayo yalikuwa yakivamiwa sana na simba. Hivyo maeneo ya Monerumango ndio moja ya maeneo ya mwanzo kukaliwa na Wazaramo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao WAZARAMO (wahamiaji), walipofika hayo maeneo hawakuwakuta wenyeji? Na hao wenyeji ni kabila gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
...kulikuwa na habari nyingi za kuvamiwa na simba, inasimuliwa kuwa maeneo hayo ndio yalikuwa maeneo ambayo yalikuwa yakivamiwa sana na simba. Hivyo maeneo ya Monerumango ndio moja ya maeneo ya mwanzo kukaliwa na Wazaramo
Asante mleta mada.
Hii habari inahitaji mwendelezo...! Baada ya wazaramo kukalia maeneo ya Monerumango...simba walitishika ama waliendelea na timbwili lao?
 
Wazaramo hawanaga chimbuko
Niliposikia wahamiaji kutoka bara...nikajua ni bara kweli...wapi..mleta mada anasema wanatokea Kisarawe! Sasa Kisarawe toka lini ikawa Bara. Nina wasiwasi mleta mada ni mzaramo tena mjukuu wa Chifu Pazi (nimemkumbuka Idd Pazi, golikipa matata sana enzi hizo...mpira tunaufuatilia 'Redio Tanzania-Dar es-Salaam'..watangazaji Omary Jongo na Ahamed Jongo na dereva wa OB van nimemsahau jina). Wazaramo kwa 'kukuza mambo hawajambo'. Eti wahamiaji kutoka bara. Ha ha haaa!
 
Niliposikia wahamiaji kutoka bara...nikajua ni bara kweli...wapi..mleta mada anasema wanatokea Kisarawe! Sasa Kisarawe toka lini ikawa Bara. Nina wasiwasi mleta mada ni mzaramo tena mjukuu wa Chifu Pazi (nimemkumbuka Idd Pazi, golikipa matata sana enzi hizo...mpira tunaufuatilia 'Redio Tanzania-Dar es-Salaam'..watangazaji Omary Jongo na Ahamed Jongo na dereva wa OB van nimemsahau jina). Wazaramo kwa 'kukuza mambo hawajambo'. Eti wahamiaji kutoka bara. Ha ha haaa!
Mkuu mimi nimefahamu kwamba amesema Manerumango inapatikana Wilaya ya Kisarawe. Au sikumuelewa sawasawa?
 
Hao WAZARAMO (wahamiaji), walipofika hayo maeneo hawakuwakuta wenyeji? Na hao wenyeji ni kabila gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Zamani pwani zote za Africa ziliogopwa waafrica kuweka makazi, hawakuishi watu, sababu kubwa ni kuwa waliogopa kukamatwa na kuuzwa utumwani kirahisi. wachache walowahi pata ishi ni wale watumwa walio choka kuendelea na misafara kwa sababu mbalimbali km kuugua. Afya mbovu, kuvuja damu sana, walitelekezwa maeneo ya pwani, hata ukiugua watakwambia jikaze ufike pwani km wakikupenda! wasipokupenda wanakuulia kwa mbali! hkna kesi unakuwa chakula cha Mbweha, fisi! nk

Wapagazi tu yaani(vibaraka weusi tu tuseme km madalali) ndiyo walikuwa wanaweka kambi pwani ili Waarabu wakija wawapatikane kirahisi na kuwapeleke kwa machifu wakorofi waliokamata mateka wengi vitani ili wauzwe! na hawa wapagazi walikuwa wanapewa nguvu za siraha naujira kwa Mabwana zao Waaarabu wafanya bisahara kubwa mfano TIPTIP alikuwa na kambi kabambe pwani ya Mombasa-Kenya.

Kumbuka Waarabu walifanya Biashara hii haramu kwa Jumla ya Miaka 1300 Net!!! bila kupumzika! Mzungu alipojiunga ndiyo biashara ikakolea zaidi! pale wafanya biashara waarabu waliporudia mzigo wa pembe na Watumwa Africa, bahati mbaya wakakuta wapagazi wazoefu hawapo waliwasubiria kwenye ngome za wapagazi walizo jijengea kwa muda. na huduma walipewa na hawa wazaramo dhaifu.

Kwa hiyo wapagazi hawakujishughulisha sana na watumwa waliotelekezwa kwenye vijiji vya pwani sababu waliwapatia huduma muhimu kama chakula, mapenzi, upepelezi nk, pia miaka ya mwanzoni pwani haikuwa na watu wengi, kama wale wa Bara walopatikana vitani, na afya zao zilikuwa mgogoro siyo za kuvumilia mwendo, mpaka leo, Mzaramo hana Afia anaweza ishi kwa chai ya rangi na kitumbua tu na akaridhika!!!

Wapagazi na maafisa wao wakuu baadhi yao waliwaza mbali zaidi wakawa wanaleta vimada vyao hapo kutokea Bara kama wanavo fanya leo Madereva wa Malori makubwa humo barabarani kila kituo ana kimada, na kwa upande wa watumwa toka Bara ili kupata favour ya Mpagazi Baba wakati ule ilikuwa ni heshima kubwa, kwanza ujue ulikuwa uuzwe utumwani na kubeba mizigo, ilikuwa ni neema wakati huo! hasa wanawake ndiyo walipewa kipaumbele!!

Waarabu walinunua sana wanawake kuliko wanaume na kule waliolewa kwa nguvu na watu wenye nguvu kimasrahi kama vile wafalme waliwaweka sehemu maalum kama zizi zinazo julikana kama ''Harlem'' hapo walikuwa wanajichagulia tu wanavo taka na kuzaa nao watoto! ndo maana waarabu wapemba huko Uarabuni ni wengi tuna unganiko la damu ila wao ndiyo wana roho mbaya dhidi yetu kuliko Muarabu Mwenyewe! Mfano Tip tip!
 
Hao WAZARAMO (wahamiaji), walipofika hayo maeneo hawakuwakuta wenyeji? Na hao wenyeji ni kabila gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Zamani pwani zote za Africa ziliogopwa waafrica kuweka makazi, hawakuishi watu, sababu kubwa ni kuwa waliogopa kukamatwa na kuuzwa utumwani kirahisi. wachache walowahi pata ishi ni wale watumwa walio choka kuendelea na misafara kwa sababu mbalimbali km kuugua. Afya mbovu, kuvuja damu sana, walitelekezwa maeneo ya pwani, hata ukiugua watakwambia jikaze ufike pwani km wakikupenda! wasipokupenda wanakuulia kwa mbali! hkna kesi unakuwa chakula cha Mbweha, fisi! nk

Wapagazi tu yaani(vibaraka weusi tu tuseme km madalali) ndiyo walikuwa wanaweka kambi pwani ili Waarabu wakija wawapatikane kirahisi na kuwapeleke kwa machifu wakorofi waliokamata mateka wengi vitani ili wauzwe! na hawa wapagazi walikuwa wanapewa nguvu za siraha naujira kwa Mabwana zao Waaarabu wafanya bisahara kubwa mfano TIPTIP alikuwa na kambi kabambe pwani ya Mombasa-Kenya.

Kumbuka Waarabu walifanya Biashara hii haramu kwa Jumla ya Miaka 1300 Net!!! bila kupumzika! Mzungu alipojiunga ndiyo biashara ikakolea zaidi! pale wafanya biashara waarabu waliporudia mzigo wa pembe na Watumwa Africa, bahati mbaya wakakuta wapagazi wazoefu hawapo waliwasubiria kwenye ngome za wapagazi walizo jijengea kwa muda. na huduma walipewa na hawa wazaramo dhaifu.

Kwa hiyo wapagazi hawakujishughulisha sana na watumwa waliotelekezwa kwenye vijiji vya pwani sababu waliwapatia huduma muhimu kama chakula, mapenzi, upepelezi nk, pia miaka ya mwanzoni pwani haikuwa na watu wengi, kama wale wa Bara walopatikana vitani, na afya zao zilikuwa mgogoro siyo za kuvumilia mwendo, mpaka leo, Mzaramo hana Afia anaweza ishi kwa chai ya rangi na kitumbua tu na akaridhika!!!

Wapagazi na maafisa wao wakuu baadhi yao waliwaza mbali zaidi wakawa wanaleta vimada vyao hapo kutokea Bara kama wanavo fanya leo Madereva wa Malori makubwa humo barabarani kila kituo ana kimada, na kwa upande wa watumwa toka Bara ili kupata favour ya Mpagazi Baba wakati ule ilikuwa ni heshima kubwa, kwanza ujue ulikuwa uuzwe utumwani na kubeba mizigo, ilikuwa ni neema wakati huo! hasa wanawake ndiyo walipewa kipaumbele!!

Waarabu walinunua sana wanawake kuliko wanaume na kule waliolewa kwa nguvu na watu wenye nguvu kimasrahi kama vile wafalme waliwaweka sehemu maalum kama zizi zinazo julikana kama ''Harlem'' hapo walikuwa wanajichagulia tu wanavo taka na kuzaa nao watoto! ndo maana waarabu wapemba huko Uarabuni ni wengi tuna unganiko la damu ila wao ndiyo wana roho mbaya dhidi yetu kuliko Muarabu Mwenyewe! Mfano Tip tip!
 
Wazaramo ni waluguru waliohamia Pwani kwenda kupigana vita, wakaungana na wandengereko. Kzaramo na kiluguru ni kitu kimoja.
Ukisema walitokea Bara unakuwa haupo specific kwa sababu watu waliotokea bara na kuja Pwani ni waswahili. Wazaramo siyo waswahili.
 
Asili ya wazaramo NI mkoa WA Iringa . Walipokuja Dar walipitia Milima ya Uluguru then kundi moja likabaki Uluguruni ambao ndio hao wanaitwa waluguru na jingine likaja pwani na Darusalama ndio hao wazaramo. So wazaramo na waluguru ni kabila moja. Wazaramo asili Yao NI iringa
 
Wazaramo ni waluguru waliohamia Pwani kwenda kupigana vita, wakaungana na wandengereko. Kzaramo na kiluguru ni kitu kimoja.
Ukisema walitokea Bara unakuwa haupo specific kwa sababu watu waliotokea bara na kuja Pwani ni waswahili. Wazaramo siyo waswahili.
Kitaalamu; Coastal zones as including the Land Area of within 60 Km of adjacent near shore waters, well inaweza kuwa hata zaidi but still ni pwani! kule kwao Musoma wanaita Mwibara.Kangi Lugora ndo mbunge! ilikuwa ni sehemu ya Ukerewe baadaye wakabadili ikaitwa Kibara. hii ina apply kotekote Bahari na Ziwa.

Moro/ main land to Dar /coastal area = Land area within ni 178 Km, kwa umbali huu Bado ni specific reasonable distance ya kuwa Bara, kumbuka Sultani alitawala visiwani na kuongezea Km 25 kutoka pwani ya EA. kutoka pwani ya Msumbiji mpaka Lamu. if my memory serve me well!!!! kwa hiyo Urugulu kwenda ndani zaidi bado ni Bara tu!

kiswahili (Wabantu)ndiyo Lugha ya Biashara iliyotumika kwa mawasiliano Bara na Pwani, kiswahili chenye lafudhi yenye radha safi iko ukanda wa pwani ya EA Mombasa, Tanga, Wazaramo, Wakwere, nk!

Kiswahili ni Kibantu, -Nilotics siyo wabantu, ukisema Wazaramo siyo Waswahili, ina maana Zaramo people siyo wabantu, hapa si kweli hata kidogo!!. Au prove!!!! Rejea ''wimbo wa shabani Madobe''
 
Kitaalamu; Coastal zones as including the Land Area of within 60 Km of adjacent near shore waters, well inaweza kuwa hata zaidi but still ni pwani! kule kwao Musoma wanaita Mwibara.Kangi Lugora ndo mbunge! ilikuwa ni sehemu ya Ukerewe baadaye wakabadili ikaitwa Kibara. hii ina apply kotekote Bahari na Ziwa.

Moro/ main land to Dar /coastal area = Land area within ni 178 Km, kwa umbali huu Bado ni specific reasonable distance ya kuwa Bara, kumbuka Sultani alitawala visiwani na kuongezea Km 25 kutoka pwani ya EA. kutoka pwani ya Msumbiji mpaka Lamu. if my memory serve me well!!!! kwa hiyo Urugulu kwenda ndani zaidi bado ni Bara tu!

kiswahili (Wabantu)ndiyo Lugha ya Biashara iliyotumika kwa mawasiliano Bara na Pwani, kiswahili chenye lafudhi yenye radha safi iko ukanda wa pwani ya EA Mombasa, Tanga, Wazaramo, Wakwere, nk!

Kiswahili ni Kibantu, -Nilotics siyo wabantu, ukisema Wazaramo siyo Waswahili, ina maana Zaramo people siyo wabantu, hapa si kweli hata kidogo!!. Au prove!!!! Rejea ''wimbo wa shabani Madobe''
Labda ni kutoelewana.

Ukisema wazaramo asili yao ni watu kutoka bara, unakuwa too general na haugusii asili hasa ya wazaramo. Hata ukitumia lugha na tamaduni bado theory ya wazaramo na waluguru ina hold water by far kuliko kuleta dhana kuwa wajita na wazanaki labda walikuja wakawa wazaramo.

Ila wajita na wazanaki kuwa waswahili, hilo linawezekana kwa sababu watu waliotokea bara kwa namna au muda wowote, wakaloea pwani waligeuka na kuwa waswahili. Nazungumzia uswahili kama mfumo wa maisha. Kwa mfano. wasukuma waliohamia Dar/Pwani kutahiri watoto wao. Sizungumzii kuingia jando la kizaramo, ila kutahiriwa na daktari au ngariba wa mtaani kwa sababu tu ya assimilation.

Na sizungumzii Geography ya Pwani kwa sababu kuna wamakonde wa Pwani na wa bara, hata wazaramo wa kibaha mimi siwaiti watu wa pwani. Ila kuondoa generosity, wazaramo ni waluguru na hiyo kwangu siyo tu kwa kusoma maandiko ya wataalam, bali mpaka babu yangu mimi ana ndugu zake wa damu kabisa tena wengi uzaramoni. Hapa namaanisha kutembea mpaka uzaramoni kuona wajomba zake.
 
Back
Top Bottom