Chilligati: Alipozidisha kusifu akaishia kukashifu

Bikirembwe

JF-Expert Member
Feb 13, 2008
250
7
Kama kuna alosikilia na kuona tukio la Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano anaweza kukubaliana nami kuwa Mama Asha alitoa hotuba nzuri ilogusia mambo muhimu ambayo Umoja wa Mataifa unashughulika nayo kwa sasa na mchango wa Tanzania katika hilo.

Nia ya thread hii si kuijadili hiyo hotuba ila ni tukio lililofata, pale Spika alipomkaribisha Mheshimiwa John Chilligati atoe shukrani kwa mgeni wao kwa niaba ya Serikali na Bunge - kama kawaida ilikuwa kumpongeza lakini naona kama waswahili wanavyosema kuwa viungo vinapokuwa vingi huharibu mchuzi na kwa maoni yangu ndio ilivyotokea, kwani katika kutaka kuzidisha sifa na kumhakikishia Mama Migiro kuwa Watanzania wanamuunga mkono alimtoa wasi wasi kuwa anaweza kutembea "kifua wazi" kwani Watanzania wako nyuma yake.

Sasa ninalotaka muchangie ni jee hiyo ni sifa au kashfa na kama ni kashfa au kukosea hakutakiwa kuomba radhi? au ndio kuwa msamiati wa kumradhi haupo tena katika jamii ya kitanzania?
 
labda alimaanisha kutembea "kifua mbele"... watu huponyoka ulimi. It is just a gaffe and nothing more. Sasa ukijiuma ulimi kwa kauli kama hiyo what do you say next au unaicha iende tu? Of course unaiacha iende. I'll cut him some slacks unless unataka kusema alimaanisha atembee kifua wazi bila sidiria watu waone "alichojaliwa". I don't think so.
 
BiKirembwe,

Nadhani hilo haliwezi kukufanya ukose usingizi.

Pia nafikiri hata Dr Asha Migiro alikwishaelewa palepale maana ya neno hilo lilipotolewa.
 
Hahahaha yule jamaa huwa anatetemeka mara nyingi akitoa matamko au hata akijibu maswali nadhani tumuelewe...tu ila nae anakuwa kama Chemical ally....Propaganda Master in Saddam Regimme...bado tunamkumbuka............
 
Ila sisi waTanzania tunapenda sana sifa na kisha tunazilewa sana na tukianza kumsifia mtu mmmh!
 
Kutembea "kifua wazi" ni tamathali ya semi katika lugha ya kiswahili ikiwa na maana kutembea kwa majivuno na kwa kujiamini pasipo woga. Hicho ndo alitaka watu au wasikilizaji waelewe. Kwa vile ilikuwa ikimlenga mwanamke, inaweza kuonekana kana kwamba alimaanisha jambo jingine la kudhalilisha. Lakini, kwangu mimi ndivyo ninavyolielewa.
 
Bikirembwe, halafu nimesoma sana nikagundua hata kama alikuwa anamaanisha alichosema sidhani kama in reality ingekuwa vibaya.. maana umesema hivi:
utaka kuzidisha sifa na kumhakikishia Mama Migiro kuwa Watanzania wanamuunga mkono alimtoa wasi wasi kuwa anaweza kutembea "kifua wazi" kwani Watanzania wako nyuma yake.

so nimechora picha kichwani kwamba kama mama anatembea kifua wazi, na sisi tuko nyuma yake, sidhani kutakuwa kumeharibika kitu.
 
Bikirembwe, halafu nimesoma sana nikagundua hata kama alikuwa anamaanisha alichosema sidhani kama in reality ingekuwa vibaya.. maana umesema hivi:


so nimechora picha kichwani kwamba kama mama anatembea kifua wazi, na sisi tuko nyuma yake, sidhani kutakuwa kumeharibika kitu.

Mkuu mwanakijiji,

Tayari umechora picha kwahio inabakia kuwa ni mawazo tu tu na sio reality.

LOL!
 
Back
Top Bottom