Mvutano na mtifuano umekuwa mkubwa kiasi kwamba CC ya CCM inajuta kwa nini imerudisha maamuzi ya mgombea kwa mkutano wa wilaya ili kupiga kura tena. Hata hivyo makundi sasa yanamenyana na mtandao ulio kinyume na Sioi Sumari umemzushia kijana huyo propaganda chafu yenye kutia kinyaa. Habari zilizozagaa huko meru ni kuwa sioi hayuko sawa na amekuwa anafanya mchezo wa ajabu (watu wazima mtaelewa).
Kambi hiyo imeendeleza propaganda zaidi kwa kusema kuwa kitendo cha Sioi kuamua kugombea wakati hata marehemu baba yake hajatimiza 40 (tumbo halijapasuka) ni ishara kuwa kijana huyu amemfanyia kitu baba yake.
Yote haya yamekuwa yakirushwa ili kujenga mazingira ya sioi sumari apigwe chini na Sarakikya apitishwe. Habari ni kuwa sababu zilizotolewa za kumpiga chini Sioi zilikosa mashiko na hivyo CC ikaona irudishe kura za maoni tena na hapo sasa propaganda ya nguvu ipigwe ili kupunguza kura za sioi na kusaka kura zilizokuwa za Elishilia na Elirehema.
Kambi hiyo imeendeleza propaganda zaidi kwa kusema kuwa kitendo cha Sioi kuamua kugombea wakati hata marehemu baba yake hajatimiza 40 (tumbo halijapasuka) ni ishara kuwa kijana huyu amemfanyia kitu baba yake.
Yote haya yamekuwa yakirushwa ili kujenga mazingira ya sioi sumari apigwe chini na Sarakikya apitishwe. Habari ni kuwa sababu zilizotolewa za kumpiga chini Sioi zilikosa mashiko na hivyo CC ikaona irudishe kura za maoni tena na hapo sasa propaganda ya nguvu ipigwe ili kupunguza kura za sioi na kusaka kura zilizokuwa za Elishilia na Elirehema.