Chiligati apasua mafisadi CCM asema Mwakani mwisho wa mafisadi dagaa

Hawa ni mafisadi wakubwa CCM,Hawafai hata machoni mwa Mungu laana inawasumbua ya watanzania,hawa ni mbwa mwitu wakubwa.
 
huu ni mkutano au kikao? cz iyo idadi ya watu aingi akilini kwangu kama uwo ni mkutano

hiyo picha imepigwa kwa nyuma,, wewe mbona ukienda kwenye vikao vya dr slaa unakaa huko ulipopiga picha? Mbona mna staili ile ile ya ccm ya zamani?
 
Kumbe wana muda kula, hadi mwakani? Watakuwa washa'Chukua Chao Mapemaa!
 
hapo sidhani kama kuna watu
hata kwenye magazeti yao hakuna picha za hii mikutano
hapa wanazuga tu
 
Ni ngumu kwa ccm kuondoa mafisadi, atabaki nani? chama kimejengwa kifisadi/kiwizi kuanzia m/kiti taifa hadi m/kiti s/mitaa, sasa wanaimba kwamba mafisadi wajiondoe wenyewe.
Kuondoa ufisadi, dhuluma na kuleta ukombozi wa Mtanzania anayeteseka kwa muda mrefu bila kufaidi matunda ya uhuru wa Tanganyika, ni kuing'oa ccm madarakani tu, hakuna ukombozi mwingine.
Shime wananchi tuunge mkono wanaharakati wanaopigania ukombozi wa kweli wa Tanzania wakiongozwa na CDM.
 

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Taifa na mbunge wa Manyoni Mashariki John Chiligati


Thursday, 12 May 2011 19:11 newsroom


* Mwakani mwisho wa mafisadi dagaa
* Asema CCM itabaki na waadilifu tu
NA BASHIR NKOROMO, SINGIDA
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kitatumia uchaguzi mkuu wake kuwaengua viongozi wote wasio waadilifu na mafisadi. Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika baadaye mwakani na kwamba, utatumika kusafisha masalia ya watuhumiwa wa ufisadi, ambao watakuwa bado hawajajiondoa. CCM imewataka watuhumiwa wa ufisadi kujiondoa wenyewe, vinginevyo nguvu itatumika wakati wa kikao cha NEC ya CCM, kinachotarajiwa kuketi Julai au Agosti, mwaka huu. Hata hivyo, CCM imesema kuwa ikilazimu kinaweza kuitisha mkutano wa dharura na kutekeleza agizo hilo kwa maslahi ya Chama na Watanzania kwa jumla. Hayo yalisemwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), John Chiligati, wakati akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoani hapa katika Ukumbi wa
FDC, jana. Chiligati, ambaye alikuwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi katika Sekretarieti iliyopita, alisema CCM imedhamiria kuwasafisha wanachama na viongozi wasio waadilifu. Alisema, hiyo ni miongoni mwa mikakati ya wazi iliyopitishwa na CCM mjini Dodoma, wakati ikiwa katika mchakato wa kujivua gamba kulikosababisha Kamati Kuu na Sekretarieti yote kujiuzulu na kuundwa mpya.
Chiligati alisisitiza kuwa watuhumiwa wa ufisadi ndani ya CCM wajitafakari wenyewe na kuchukua hatua, kinyume na hapo watang’olewa. Pia, alisema ikionekana muda wa kufikia kikao kingine cha NEC ni mbali, mkutano wa dharura unaweza kuitishwa ili hatua za haraka zichukuliwe ili kukiacha Chama kikiwa safi mbele ya jamii. Alisema CCM imedhamiria kuwa na wanachama na viongozi wenye maadili safi mbele ya jamii na ndiyo, msingi wa kujivua gamba ili kusafisha wachafu. “Hatutawavumilia wanachama na viongozi wachafu wanaotumia mgongo wa CCM na vyeo walivyonavyo ndani ya Chama na serikali kujilimbikizia mali,” alisema.
Alisema ili kufikia malengo hayo, NEC ilipitisha uamuzi wa kuwepo kamati maalum ya udhibiti ili kurejesha nidhamu ndani ya Chama na kwamba, itakuwa na jukumu la kuzuia mpasuko wakati wa uchaguzi. Kuhusu kura za maoni, alisema zitakuwa zikipigwa na wananchi mapema ili kupata muda wa kusikiliza malalamiko, rufani, uchaguzi uliopita CCM haikuwa na muda wa kutosha ndiyo sababu zilijitokeza kasoro nyingi.
Pia, alisema uchaguzi huo utakuwa na uchujaji wa awali, na kwamba si kila anayechukua fomu atagombea, kwani itakuwa nafasi moja kwa watu watatu, anayeshinda lazima apate nusu ya kura.
Katika hatua nyingine, Chiligati aliongeza kuwa CCM imepitisha utaratibu wa kutoruhusu mwanachama wake kuwa na vyeo vingi kiutendaji, kwani hali hiyo imesababisha kasoro nyingi.
Chiligati yupo mkoani hapa katika ziara ya kuitambulisha Sekretarieti mpya ya CCM, ambapo amefuatana na Katibu wa NEC, Itikati na Uenezi, Nape Nnauye, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba na Katibu wa NEC, Oganaizesheni Asha Juma Abdallah.
Hizo porojo zenu haziingii kichwani hata kwa watoto wadogo wa chekechea.Mmeshindwa kuwaondoa magamba papa sasa mnakuja na hili la magamba dagaa,"Kwa kawaida katika taasisi au serikali yoyote makini inayozingatia sheria na maadili inachukua hatua maramoja ziwe za kinidhamu au kisheria inapoona au kugundua kua kuna uvunjwaji wa sheria katika serikali au taasisi husika"Katika chama tawala na serikali yake pamoja na Rais wanautaratibu mwingine wa kiuongozi,ambao nadhani haupo katika nchi nyingine yoyote Ulimwewnguni-Labda ya Kusadikika-Chama na serikalini kumejaa viongozi wasio na maadili ya uongozi (MAFISADI)wala rushwa, wazembe Rais CCM na wanachi wote wanafahamu hivyo,lakini badala ya hatua za kisheria kufuatwa kuwaondoa watu hawa tunasikia kauli za viongozi wa CCM na serikali zikikiri na kusema wajiondoe wenyewe!!!!!!Kauli hii isingekua ya kushangaza kama tungeisikia kutoka vyama vya upinzani na wananchi.Kama mabo ndiyo haya naona tufute mahakama na vyombo vyote vya sheria tutoe kauli ya kua yoyote anadhaniana makosa aende gerezani mwenyewe na atakaposhindwa kufanya hivyo vyombo vya sheria vichukue mkondo wake!!!!!Hili niwazi inafahamika katika SERIKALI YA JK na CCM VIONGOZI NI HAOHAO,WALARUSHWA NI HAOHAO,MAFISADI NI HAOHAO=MATOKEO NIHAYOHAYO.Katika hali kama hii NGUVU YA UMMA NDIYO SULUHISHO LA TATIZO HILI.
 
hahaha.....wacha nikoroge kahawa hapa...huu mkutano au ni nini
 
The most interesting party of this comedy is that hata ukimuuliza leo hii Chiligati hao
watuhumiwa wa ufisadi ni nani atakwambia HAWAJUI. CCM wanakimbia kivuli chao.
Kama kweli wana nia ya kupigana na ufisadi waanike hadharani majina ya watuhumiwa
wa ufisadi ili wajifahamu na ndipo wajipime.

Tumemsikia Chenge mwenyewe akisema kwamba HAJIFAHAMU KAMA YEYE NI GAMBA.
List ya watuhumiwa wa ufisadi ambayo watanzania wote wanaifahamu ni ile iliyotolewa
na Dr. Slaa. CCM haijawahi kuwa na list ya watuhumiwa wa ufisadi na imekuwa ikikanusha
siku zote kuwa ndani ya CCM hakuna mafisadi.

CCM acheni kutudanganya leteni kwanza list ya mafisadi ili wajijue na watanzania tuwafahamu
halafu ndiyo muendelee na vita yenu. Je inaingia akilini kweli kupigana vita na ADUI usiyemfahamu?!

Ndiyo madhara hayo ya kudandia hoja za CDM, kama anavyofanya sasa hivi Nape Nnaye kuwa Dr. Slaa
anachukua mshahara wa 7.5 milioni @ month, Wakati katibu wake Mukama anakula 11 milioni @ month
huku CCM ikiwa imesimamisha kulipa watendaji wake kwenye wilaya na Kata baada ya ruzuku kupungua
kufuatia matokeo ya uchaguzi wa 2010.

Nape umeingia kwenye mtego ule ule wa Makamba aliyemtuhumu Dr. Slaa kwamba ni mwizi wa wake za watu. Yeye (Makamba) alipoulizwa atueleze ni kwanini alifukuzwa ualimu wa primary school akaingia mitini. Nina uhakika na wewe Nape utaingia mitini baada ya siku 90, tatizo la Nape hajifahamu kwamba
anatumika. For CCM the writting is already on the wall. You don't need to be a rocket engineer to figure out.
 
Hao wananchi wachache hivyo ni mkutano au mambo ya balozi nyumba kumikumi,inawezekana hao wanakijiji walitishiwa kubambuliwa na mabalozi wao Kama hawataenda ktk mkutano.
 
Back
Top Bottom