IROKOS
JF-Expert Member
- Aug 13, 2011
- 10,184
- 7,819
Wana JF hivi hili suala la kuasili mtoto (nadhani ndicho kiswahili chake? i stand to be corrected) au adoption kwa Kiingereza kwa hapa kwetu hali ikoje? sheria/sera (kama zipo) zinasemaje? Je linafanyika? Is it something which is becoming popular nowadays?
Nimeomba mawazo yenu kwa sababu utaratibu huu ni common huko kwa wenzetu kama tulivyoona kwa staa madona kumuasili yule mtoto Banda, na wengine wengi tuu. Hivi kwa kungalia mila zetu na desturi zetu, dini na mambo mengine hii kitu ina changomoto gani?
Nimelileta hili suala hapa jukwaani kwa sababu wote ni mashahidi jinsi watoto wanavyotupwa, kuuwawa na kutelekezwa kwa upande mmoja lakini pia kwa upande wa pili tumeshuhudia jinsi ambavyo ndoa nyingi zilivyo kwenye misukosuko kama siyo kuvunjika kabisa kwa kukosa watoto.
Yaani Wewe unamtupa mtoto wakati wenzio wamemaliza mahospitali na waganga wa jadi kutafuta!! Je Kali kuasili kukiwekwa wazi na watu wakaelewa haiwezi kupunguza hili tatizo kwa kila upande kufaidika?? Samahani kama mada hii ilishawahi kujadiliwa humu kabla sijajiunga.
Naomba kuwasilisha.
Nimeomba mawazo yenu kwa sababu utaratibu huu ni common huko kwa wenzetu kama tulivyoona kwa staa madona kumuasili yule mtoto Banda, na wengine wengi tuu. Hivi kwa kungalia mila zetu na desturi zetu, dini na mambo mengine hii kitu ina changomoto gani?
Nimelileta hili suala hapa jukwaani kwa sababu wote ni mashahidi jinsi watoto wanavyotupwa, kuuwawa na kutelekezwa kwa upande mmoja lakini pia kwa upande wa pili tumeshuhudia jinsi ambavyo ndoa nyingi zilivyo kwenye misukosuko kama siyo kuvunjika kabisa kwa kukosa watoto.
Yaani Wewe unamtupa mtoto wakati wenzio wamemaliza mahospitali na waganga wa jadi kutafuta!! Je Kali kuasili kukiwekwa wazi na watu wakaelewa haiwezi kupunguza hili tatizo kwa kila upande kufaidika?? Samahani kama mada hii ilishawahi kujadiliwa humu kabla sijajiunga.
Naomba kuwasilisha.