Makyomwango
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 322
- 79
Mbunge wa Nachingwea Bw Chikawe, alipopata habari kuwa kizaazaa cha M4C kilicholeta maafa makubwa kwa CCM Mkoani Mtwara kitaingia Wilayani kwake leo J'5 likitokea Wilayani Nanyumbu Mkoani Mtwara, basi jana nzima alikuwa akihaha kwenye Misikiti mbalimbali kama vile Misikiti ya Kata za Namapuya, Nditi, Mtonda, Nachingwea nk akigawa Sanda za kuzikia Maiti kwa biidii! Ingawa matangazo ya mikutano ya leo yalishaanza kutolewa, lakini inasemekana Convoy hilo la M4C limebadilisha ratiba na ruti yake hivyo halitafika Nachingwea leo, bali litafika baada ya siku 3 au 4 hivi likitokea Lindi Mjini, hivyo atakuwa amepata nafasi zaidi kwenda kufungasha Sanda nyingine zaidi za kugawa katika Misikiti ya Kata zilizobakia!
Nawashauri wana bodi waliopo Nachingwea wa printi maoni ya thread hii na kusambazwa kwa watu mbalimbali wa huko, zinaweza kuwaamsha zaidi.