Chihendo na MweneMwana 23/07/016 Kwaheri Baba Wa Siasa Afrika JK

Twalb zubeir

Senior Member
Feb 23, 2015
143
51
4a37a27b6428d2120b3f04f7238e74f4.jpg
 
Hahahahaha ilikuwa ofisi ndogo Lumumba hiyo Na mwenye mwana ndiyo yeye
 
Ni ukweli mchungu sana kwa wana CCM, walizoea malezi mazuri na ya kimahaba kutoka kwa baba yao kipenzi wa karne mzee Jakaya Mrisho Kikwete. Walizoea kauli nzuri na za busara kutoka kwake. Hatimaye tarehe 23 July ataondoka rasmi kwenye siasa na kurudi kabisa kuwafuata wazee wenzake. Hatasikika kwa mazoea kama ilivyozoeleka.

Wana CCM hapo July 23 watakuwa na kazi kubwa mbili. Kazi ya kwanza itakuwa kuagwa na hotuba nzuri iliyojaa busara na upendo wa kila namna, hotuba ambayo kwa kweli watai-miss sana. Kisha watakuwa na shughuli pevu ya kukaribishwa kwa "chuma" watashuhudia maneno makali na yasiyo na mzaha kutoka kwa rais John Magufuli. Maneno ambayo wengi wao hawajayazoea.

Huu ndiyo ukweli, wana CCM watakapokuwa wakizilinganisha hotuba mbili na kisha koana uhalisi wa mbeleni; Wengi wao watajikuta wakiwa kama wakiwa! Wakijikuta kuyakabili malezi mapya yasiyo ya "kimapenzi" kama aliyokuwa nayo JK.

Ukweli mchungu ni kuwa Magufuli yule wa ikulu ndiye Magufuli atakayeshika husukani ndani ya CCM. Itakuwa ni CCM isiyokuwa na uhakika wa kesho yao!

Mnyonge tulimnyonga weeee lakini ukweli wa haki yake upo! Nani asiyeziona busara za JK kwa kila jambo? Nani asiyeuona walau ule usikivu wa JK masikioni mwake?

Sisi makabwela kwakweli tunammiss kwelikweli, alikuwa anasikia anashuka! Laiti angekuwepo tusingekuwa tumeshalipuuza bunge letu tukufu! Ndani ya miezi nane ya utawala wa rais Magufuli kwa mara ya kwanza katika historia "SIJAWAHI KUANGALIA BUNGE" zaidi ya ile siku ya kwanza wabunge walipoapishwa! Ni kwa sababu sioni mjadala utakaonifanya nione kama nitapata chochote ndani ya bunge. Yapo mengi ya kusema lakini........

Nenda JK njoo Magufuli kamata usukani mpya Tuendelee kuuenzi ule wimbo maarufu kwenye kampeni zetu mwaka jana
Iringa ni ileileee...... wahehe mnasemajeeeee... tumejipangaaa mwaka huu tumejipangaaa... tumejipangaaa acha waisome nambaaaa
 
Tulieni mnyolewe enyi wanadamu, mlizoea kukenuliwa meno wakati huo huo mkimtukama JK, kawaletea chuma sasa.
 
Nakumbuka JK akimtambulisha Magufuli kwa wana CCM baada ya Magufuli kuteuliwa kugombea Uraisi kwa tiketi ta CCM alisema hivi:

" Hii ngoma ni ya mwali, na mwenye mwali ni mimi basi niachieni mimi" kilichofuata hapo ni Kampeni ya Kihistoria na ya kistaarabu iliyomuingiza Magufuli Ikulu bila hata kurusha bomu moja la machozi kwa Wapinzani.

Kwa heri baba JK, Hakuna tena mwanasiasa atakayekuja kupata kura asilimia 80 katika mazingira haya ya vyama vingi kama wewe Muheshimiwa.

Umelitendea taifa Makubwa, mabarabara, shule za kata, umeme wa REA, Taasisi ya moyo, Daraja la Kigamboni, Malagarasi, Dawa za ARV bure, Diplomasia ya hali ya juu, Jeshi bora lenye zana za Kisasa, Uhuru wa Habari na Demokrasia pana, Mishahara ya wafanyakazi iliyoboreshwa, Kada ya Wajasiriamali wadogowadogo, bodaboda, bajaji, mpesa, tigopesa, Umetujengea kituo cha michezo cha Kikwete Complex, Umeletea maji kutoka Ruvu chini hivi sasa shida ya maji DSM itakuwa ni historia, Mzee umetuwejea mradi wa Magari yaendayo Kasi DSM.

Asante sana baba JK, Tunakukumbuka na tutakukumbuka sana
 
tuliwa kwa mjomba, sasa tunarudi kwa baba JPM! MOLA akutetee milele JPM
 
CCM isiyo na gamba inaenda kuzaliwa, sina hakika gamba gumu vimagamba, upupu na fangasimagamba vitarukia wapi.Ninachoamini ni kuzaliwa kwa CCM mpya imara na yenye maono.Najaribu kuitafuta kadi yangu ya TANU nijikumbushe ukawa kaa chonjo saa ya ukombozi ni sasa.
 
Hiyo hotuba iandikwe kwa mantiki kiasi kwamba imsafishe kwa sababu yote yanayojiri yanajaribu kuonyesha kuwa hakufanya kazi nzuri wakati kuna mengi tu mazuri alifanya. Anayejenga msingi, anayejenga kuta na anayejenga paa wote wameijenga hiyo nyumba. maana yake ni kuwa ukiweza kuezeka ujue aliyejenga msingi hakujenga vizuri lakini ukiona paa linagoma hapo ujue watangulizi walikuwa na shida. wenye akili wajiulize kama paa linajengeka au la!
 
Kuna mengi ambayo nayakumbuka kila nisomapo sehemu na kuona ametajwa. Nakumbuka na kuheshimu kila alichoongea. Alionyesha kutupenda na kukipenda chama chake. Nina mengi sana lakini naahidi kuandika siku tutakapo muaga JK
 
Nakumbuka JK akimtambulisha Magufuli kwa wana CCM baada ya Magufuli kuteuliwa kugombea Uraisi kwa tiketi ta CCM alisema hivi:

" Hii ngoma ni ya mwali, na mwenye mwali ni mimi basi niachieni mimi" kilichofuata hapo ni Kampeni ya Kihistoria na ya kistaarabu iliyomuingiza Magufuli Ikulu bila hata kurusha bomu moja la machozi kwa Wapinzani.

Kwa heri baba JK, Hakuna tena mwanasiasa atakayekuja kupata kura asilimia 80 katika mazingira haya ya vyama vingi kama wewe Muheshimiwa.

Umelitendea taifa Makubwa, mabarabara, shule za kata, umeme wa REA, Taasisi ya moyo, Daraja la Kigamboni, Malagarasi, Dawa za ARV bure, Diplomasia ya hali ya juu, Jeshi bora lenye zana za Kisasa, Uhuru wa Habari na Demokrasia pana, Mishahara ya wafanyakazi iliyoboreshwa, Kada ya Wajasiriamali wadogowadogo, bodaboda, bajaji, mpesa, tigopesa, Umetujengea kituo cha michezo cha Kikwete Complex, Umeletea maji kutoka Ruvu chini hivi sasa shida ya maji DSM itakuwa ni historia, Mzee umetuwejea mradi wa Magari yaendayo Kasi DSM.

Asante sana baba JK, Tunakukumbuka na tutakukumbuka sana
Mbona Shein alikwisha kuvunja record yake, si alipata asilima 99.9
Sema tu hakuna mwanasi-hasa ambaye anapata kama za sheni ulimwengu mzima mpaka Duniani inaisha.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom