Uchaguzi 2020 Chief Kalumuna: Mgombea Ubunge pekee wa CHADEMA atayeitikisa CCM kwa Kanda ya Ziwa

Ni meya msitaafu wa manispaa ya Bukoba kwa akina Rwetabangula,Rweikiza ,etc

Kusema ukweli jamaa ana ushawishi wa kisiasa hatari, angekuwa mtumishi wa Jehova nafikiri hata shetani angetubu na kuacha ushetani wake.

Ikumbukwe kuwa,Chief Kalumuna mpaka alipofikia hapo ni malezi na taaluma nzuri aliyoipata akiwa CCM japo siku za nyuma Mwaka 2015 watu wachache ndani ya CCM walitaka kumharibia future yake ndipo alipokimbilia CHADEMA na hatimae akawa Meya.

Kwa jimbo la Bukoba Mjini bado ni sintofahamu kama upinzani utapoteza au la,maana jamaa ametia nia na ni asilimia kubwa anaweza kuchukua labda DJ zero akate jina lake maana hata kwenye uchaguzi ndani ya chama chao ngazi ya kanda alikuwa amemchapa fimbo za kutosha Wenje ila DJ zero kama kawaida akabadili gia angani jamaa akapolwa haki yake.


"Stay tuned BK is unpredictable"
Kwani kampeni zimeshafunguliwa?
 
Kuhusu, kukata jina lake usipende kuwa kama Mwanamke ..

Ila ukweli chadema kwa Bukoba chief yuko na nguvu kubwa ..pia nimtu anayemjua Mungu sana . .kama kweli jina lake wakilikata basi naamia CCM.
Hivi mbona mnawadharau Sana wanawake?
 
Kalumuna jina kubwa sana Bukoba nilifanya Kaka yake kaz Dar ,alimfania mke wake akitembea na DVO wa kinondoni kipindi cha JK na kumuacha bila kumwambia lolote wala kumdhuru mbaya wake..ni watu wa dini sana .
Hicho chuma ndicho kimemkimbiza Rwakatare, akijichanganya tu na yeye kinampiga kwenye kura, bora awaachie wengine akwepe aibu!
 
Hicho chuma ndicho kimemkimbiza Rwakatare, akijichanganya tu na yeye kinampiga kwenye kura, bora awaachie wengine akwepe aibu!
Halafu siasa za bk kihistoria ni za tofauti Sana ,huwa hawaangalii chama, ndio maana nahofia chama changu pendwa kisije pigwa chini tena
 
Halafu siasa za bk kihistoria ni za tofauti Sana ,huwa hawaangalii chama, ndio maana nahofia chama changu pendwa kisije pigwa chini tena
Chama chako kipi, CCM? Hiyo ndio nitolee tena, unafikri kwa Chief Kalumuna watafanyaje?
 
Kifupi ni wachawi wa maendeleo
Yawezekana keani ccm ina tabia kama za klabu ya simba wakihisi mtu kuwa tishio kwao umuonga ela kumchukua na kisha kumpoteza kama madiwan wa chadema wa shinyanga na wa mbeya ambao mpaka sasa hawajielewi
 
Chama chako kipi, CCM? Hiyo ndio nitolee tena, unafikri kwa Chief Kalumuna watafanyaje?
Lakini alikuwa kwetu sema tu kuna mzee mmoja alikuwaga diwani katika kata yake siku za nyuma ndiye aliyemvuruga hadi akakimbilia kwa wazungusha mikono
 
Hiyo ni danganya toto tu ,yule mzee hana time na siasa tena


Hata akigombea kupitia Ccm lwakatare sahivi watu wamemchoka kwa kufukuzwa chadema ,pia kama unakumbukumbu vzr chief alivyohama kutoka ccm ndo alileta nguvu kubwa sana chadema bukoba mjini... Mimi naishi Bukoba Mjini nakuambia chief hadi mama yangu nimwenyrkiti wa UWT Bukoba ,lakini anamkubari chief sana.
 
Back
Top Bottom