Chid Benz amchana Bab Tale, alinifuata mwenyewe kisha ananitangaza nimeshindikana?

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,725
18,620
Msanii aliyekuwa ameathirika na madawa Chid Benz akiwa anahojiwa Clouds amemdiss meneja wa WCB Bab Tale kwenda kumtangaza ameshindikana na amerudia tena madawa
Amesema kama alimuona anafanya jambo ambalo sio angemuambia na sio kukaa kimya kisha kwenda kuongea mbovu

 
Msanii aliyekuwa ameathirika na madawa Chid Benz akiwa anahojiwa Clouds amemdiss meneja wa WCB Bab Tale kwenda kumtangaza ameshindikana na amerudia tena madawa
Amesema kama alimuona anafanya jambo ambalo sio angemuambia na sio kukaa kimya kisha kwenda kuongea mbovu


HAKIKA kijana ameeleza ukweli,Mungu atamsaidia atasimama upya,kwanza ameonyesha kuwa sasa anajitambua, Babu Tale anastahili KUMUOMBA radhi Chid Benz,HAKIKA amemdhalilisha, Tale anatakiwa KUWA kama Dr,anapoona AIBU ya mgonjwa sio vema kuiweka hadharani,ni inhumanity !
Pole Chid,binadamu sharti ajifunze kwa makosa wakati mwingine,naamini umejifunza na umefuzu ,JIPANGE upya jamii imekusamehe kwa makosa yako binafsi!
 
Huyu Mgonjwa wa akili ana fikiri tunahitaji kufanya utafiti kugundua alishindikana? alipo anza kutibiwa tulimuona na aliporejea kwenye hali yake nzuri tulimuona na alipo rudi tulimuona.
Huyu mgonjwa bado hajapona na wanao amini amepona wanahitaji kuusubiri muda uwambie...
Ni mjinga pekee anaweza kushindwa kuelewa mchango wa Tale na WCB kumrudisha kwenye hali yake nzuri ugonjwa bado unasumbua ubongo wake....

Mgonjwa ni mgonjwa tuu
 
Chid Benz kama kweli karudia madawa basi naweza kuamini kuwa madawa hayawezi KUMUACHA mtu salama
 
Nilivyosikia akiongea nilidhan ni TID baada ya kumtaja jina nikajua kumbe ni Chid Benz ..... kweli ngada hatari sana
 
Chidu hajaanza ujinga leo alianzia Mafinga Secondary wakati wa Headmaster Usangira walimgonga suspension za kutosha hazikusaidia baadae akatimuliwa tu mwaka 2000 & 2001 wakati huo akijiita Chid Boy na wenzake akina Simple F...Sioni jipya kwake aache tu muziki
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom