Cheo, Madaraka na mabadiliko ya tabia; Kwa nini tuna mtizamo tofauti?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1574255454593.png
Ushawahi kuona mtu akiwa na tabia fulani (safi?) baadae akapata cheo au madaraka, akabadilika na akawa na tabia ambayo hukuwahi kuitarajia?

Ukweli ni kwamba cheo au madaraka humsababishia mtu mazingira ambayo ni rahisi sana kumbadilisha tabia. Kwa bahati mbaya, uwezekano wa cheo kumbadili mtu mwenye tabia nzuri kuwa mtu mbaya ni mkubwa wakati uwezekano wa kumbadili mtu mbaya kuwa mzuri ni kama haupo.

Ndio maana sisi wengine ijapokuwa hatueleweki kwa wepesi; tumekuwa tukishawishi kwamba ikiwa watanzania tunaamini juu ya Tanzania bora ya kesho, tunachotakiwa ni kushungulika zaidi na watu wa kawaida kuliko walioko madarakani. Msingi ni kwamba, ni rahisi kutengeneza watu wema wakiwa hawana cheo na siku wakipata cheo baadhi yao watabadilika kuwa watu wabaya lakini kwa kuwa tayari watakuwa ni wengi angalau kundi kubwa watabakia kuwa watu wema.

Lakini kama ukishindwa kujiadabisha au kumuaadabisha mtu akiwa hana cheo, uwezekano wa kuji/kum ‘Shape’ akiwa na cheo ni mdogo sana. Hii ni kwa sababu cheo humfanya mtu aangalie dunia na kujiangalia yeye mwenyewe kutokea kwenye ‘Angle’ ya tofauti kabisa.

Lakini pia suala la kujiuliza, kama tunafikiri sawasawa; kwa nini tusubiri kwamba eti tukishapata vyeo eti ndio tuanze kujifunza kuwa watu positive au ndio tuanze kuwafundisha waliopata kuwa watu positive?

Sasa hebu tujiulize maswali haya;


  • Ni nani miongoni mwetu akipata cheo, na akawa na uhakika akitumia njia fulani atabaki na cheo chake kwa muda wote anaotaka bila yoyote kumfanya kitu, na akaacha kutumia njia hiyo eti tu kwa sababu anaamini sio ‘fair’?

  • Hapo ulipo, ushawahi kufanya mambo mangapi ‘ya kiraia tu’ kusaidia wengine? Kama hujafanya au hufanyi, siku ukiwa kwenye ‘dilemma’ ya kuchagua kuwafanyia wengine wema wewe udhurike, au uwafanyie uovu upate maslahi, utachagua nini?

  • Ni nani miongoni mwetu akipewa salio kidogo hawezi kukana anachoamini? Lakini kabla ya huko kote ni nani ambaye anaamini kitu fulani ambacho hakimsaidii yeye binafsi na yuko tayari kukutetea bila malipo?

  • Ni nani ambaye yuko tayari kutumia akili, mwili na ikibidi mali kwa jambo lisilomnufaisha binafsi au bila malipo?

  • Ni nani akipewa kazi ya kusimamia mabilioni ya pesa ambazo sio zake, na anajua hata akichukua bilioni chache hakuna wa kumfanya kitu, lakini ataacha kwa sababu tu anaamini kufanya hivyo sio ‘Fair’?

  • Fikiria kama unakuta sasa hivi tu mtu hana cheo chochote ila anapenda kusikia habari za wengine kukwama au kudhalilika kuliko anavyopenda maendeleo yake mwenyewe, fikiria siku akiwa na cheo nini kitatokea?
Wakuu, hatukatai kwamba Watanzania hatuna changamoto la! Tunachosema ni kwamba, mambo yanayotokea sasa ni matokeo ya maandalizi yaliyofanyika au kutofanyika miaka kadhaa nyuma huko. Kwa mantiki hiyo, ikiwa kweli tuna dhamira ya mabadiliko; badala ya kutumia muda mwingi kulaumu na kulalamikia kile kinachotokea kwa dakika hii, ni vyema kujikita kwenye kuandaa mazingira rafiki ya mbeleni ili ikifika huko tusije kulamika zaidi ya tunavyolalamika leo.
 
Kuna watu wanazungumza mara kwa mara kuhusu katiba na sheria; ni kweli Katiba na sheria ni vitu muhimu, lakini tabia ya binadamu ni kitu kikubwa sana, na tabia ni hujengeka hatua kwa hatua na vile vile hubadilika taratibu na hasa hasa tabia positive. Sio jambo la kulala ukiamka tayari.
 
Kuna watu wanazungumza mara kwa mara kuhusu katiba na sheria; ni kweli Katiba na sheria ni vitu muhimu, lakini tabia ya binadamu ni kitu kikubwa sana, na tabia ni hujengeka hatua kwa hatua na vile vile hubadilika taratibu na hasa hasa tabia positive. Sio jambo la kulala ukiamka tayari.
Katiba na sheria (nzuri) humlazimisha binaadamu mwenye hulka za kiajabu kuenenda kwa mujibu wa taratibu nzuri mlizojiwekea.

Wakati katiba mbaya na sheria mbovu humtengeneza mungumtu wa duniani.
 
Katiba na sheria (nzuri) humlazimisha binaadamu mwenye hulka za kiajabu kuenenda kwa mujibu wa taratibu nzuri mlizojiwekea.

Wakati katiba mbaya na sheria mbovu humtengeneza mungumtu wa duniani.
Kuna mambo mbalimbali ambayo si mazuri ila kuna watu kulingana na sababu mbali mbali wanaweza wakayafanya bila kuwa controled. Kwa hiyo hatusemi hivyo visiwepo ila kitu cha muhimu kuliko vyote ni busara za viongozi na busara za viongozi ni matokeo ya tabia nao ni zao la jamii
 
Back
Top Bottom