Chenji ya Rada Ipelekwe Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu - HESLB

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Jul 1, 2008
10,564
7,973
Salam wadau,

Kwa muda mrefu nimekuwa nikitafakari kuhusu zogo la wanafunzi wengi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu hapa nchini mwaka huu walivyokosa mikopo kutoka bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu(HESLB).

Bodi imejitetea kwamba sababu kubwa ya wanafunzi wengi kukosa mikopo ni ufinyu wa bajeti. Kwa hiyo katika bajeti ya mwaka 2011/2012 serikali haikutenga fungu la kutosha kwa ajili ya kukopesha wanafunzi. Na baadhi ya wanafunzi waliokosa mikopo wamekuwa wanahangaika kuonana na wahusika mbalimbali ili kuona kama wanaweza kufanikiwa kupata mikopo na hatimaye waweze kutimiza ndoto zao. Nimeambiwa wamefikisha ujumbe wao kwa raisi Kikwete naye amewaahidi kwamba suala lao linashughulikiwa, ingawa kwa upande wa pili waziri Kawambwa ameanza kupiga mkwara wa kuwafukuza vyuoni na kuwanyima mikopo wanafunzi wote watakaoshiriki kwa namna yoyote kugoma ama kuandamana kwa ajili ya kudai mikopo.

Wakati tukiendelea kuumiza vichwa ni jinsi gani tutaondokana na jinamizi la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, imekuja taarifa rasmi ya serikali kupitia kwa waziri wa mambo ya nje kwamba hatimaye BAE system wamekubali kuirudishia serikali ya Tanzania chenji ya rada kiasi cha pauni 29 milioni sawa na shilingi 70 bilioni za Tanzania. Kwakuwa tuna matatizo ya fedha za kukopesha watanzania waliodahiliwa katika taasisi zetu za elimu ya juu, nikadhani mojawapo ya matumizi mazuri ya fedha hizi itakuwa ni kuzielekeza bodi ya mikopo ili wanafunzi wote wenye uhitaji waweze kukopeshwa na hivyo kubaki na kazi moja tu ya kusoma. Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa sana kuepusha migomo na maandamano yanayoweza kutokea kufuatia wanafunzi wengi kukosa mikopo na huku wakiwa na sifa stahiki za kupatiwa mikopo.

Naomba kutoa hoja, mawazo yenu tafadhali.
 
mwaka huu serikal yetu imepata fedha nying san ikiwamo msaada wa fedha kutoka ufaransa, 2mesamehewa den na korea ili litumike kwenye elimu, Nadhani 2liokosa mikopo imani ya kupata bado ipo, nanyinyi bodi mbona hamkupeleka bajet kubwa bungen ikataliwe, tena mlipeleka bajet mkitarajia kupokea maomb elfu 60, leo hii baada ya bajet kupitishwa mnatusalit, kwanini?
 
Wazo zuri....

Na ile tozo tutaipata wapi hv kuilipa. Maana mahakama ishatoa maamuzi.
 
mwaka huu serikal yetu imepata fedha nying san ikiwamo msaada wa fedha kutoka ufaransa, 2mesamehewa den na korea ili litumike kwenye elimu, Nadhani 2liokosa mikopo imani ya kupata bado ipo, nanyinyi bodi mbona hamkupeleka bajet kubwa bungen ikataliwe, tena mlipeleka bajet mkitarajia kupokea maomb elfu 60, leo hii baada ya bajet kupitishwa mnatusalit, kwanini?

Wizara ya elimu imetengewa bajeti kubwa sana, nadhani itakuwa ni ya tatu kwa ukubwa wa bajeti ikitanguliwa na miundombinu pamoja nja nishati na madini.

Kwahiyo wanaposema wanashindwa kukopesha wanafunzin wengi kwa sababu ya ufinyu wa bajeti inakuwa vigumu kuwaelewa.

Hata hivyo fedha zimepatikana, wazielekeze huko bodi wanafunzi wakopeshwe na waendelee na masomo yao.
 
Wazo zuri....

Na ile tozo tutaipata wapi hv kuilipa. Maana mahakama ishatoa maamuzi.

Hiyo tozo ya dowans itabidi wale waliosaini mkataba wachangishane na kulipa. Hatutakubali pesa yetu iendelee kuchezewa.
 
Nina wasiwasi mkubwa fedha hiyo inaweza kutumika kulipia 'deni' la Tanesco linayodaiwa na Dowans...na tena bado itatakiwa watafute sh karibu bilion 41 kutoka vyanzo vyengine! CCM hoyee......RA hoyee....JK hoyeee...!!!! Tanzania, Ziiiiiii......!
 
Tuombe mungu wawe na mawazo kama haya japokuwa kwa taarifa waliyoitoa ni kuwa fedha hizo ni kwel zitaelekezwa ktk secta ya elimu lkn co upande wa mikopo ni ujenzi wa nyumba za walimu na misaada kwa shule hasa sekondary....!mungu ibariki tanzania na vongoz wake!
 
Nina wasiwasi mkubwa fedha hiyo inaweza kutumika kulipia 'deni' la Tanesco linayodaiwa na Dowans...na tena bado itatakiwa watafute sh karibu bilion 41 kutoka vyanzo vyengine! CCM hoyee......RA hoyee....JK hoyeee...!!!! Tanzania, Ziiiiiii......!

Wasiwasi wa hiyo chenji kulipa dowans ni mkubwa sana, lakini naamini wananchi tukikomaa itabidi hiyo pesa ielekezwe maeneo mengine ya maendeleo hususan kwenye elimu. Na hapo nio napendekeza zipelekwe bodi ya mikopo, wadogo zetu wengi watashindwa kupata elimu ya juu.
 
Back
Top Bottom