Elections 2010 Chenge inabidi ajiuzulu

politiki

JF-Expert Member
Sep 2, 2010
2,376
1,507
KUFUATIA TAARIFA YA SFO KUHUSIANA NA ISSUE YA RADAR KUWA UCHUNGUZI UNAENDELEA NA HAKUNA CONCLUSION ILIYOFIKIWA HUU NDIO NDIO INABIDI UWE MSUMARI WA MWISHO KWA JENEZA LA HOSEA. JK AKIENDELEA KUMGANGANIA AENDELEE TU LAKINI PCCB ITAKUWA NI TAASISI KAMA TAASISI ZINGINE ZINAZOPOTEZA PESA ZA WALIPA KODI YA WATANZANIA LAKINI HAZINA MCHANGO WOWOTE KTK KUBADILISHA MAISHA YA WATU.
Ili kurudisha imani kwa wananchi kwa taasisi nyeti kama hii basi taasisi
hii aiwezi kuendelea kuendeshwa na watu wasio makini kama Hosea.
kwanza aliwasafisha watu wa Richmond ikaja kugundulika kuwa ni bomu ambalo hata kipofu ilibidi alione. ikaja kwenye swala la kuakiki usajili wa Richmond akasema ni kampuni safi ilisajiliwa marekani lakini ikaja kugundulika Bwana Hosea alichakachua issue richmond dev. haijawahi kusajiliwa na wala haijulikani wakati huo huo Hosea alitumia mamilioni ya walipa kodi kuisafisha richmond. Kitendo cha Hosea kuwa na kazi hii mpaka leo ni maajabu ya kushangaza. Hosea huyuhuyu leo anakuja kumsafisha mtu kabla hata uchunguzi haujamilizika na bila hata kutoa ufafanuzi wowote kuhusiana na mamilioni ya dola za chenge zilizokutwa kwenye account yake uingereza ambao yeye mwenyewe alitoa maelezo chungu mzima ya kujikanyaga na pesa hizo ambazo SFO ilisema kuwa zilikuwa na connection na issue hiyo ya radar. alikamata watu wengi wakati wa uchaguzi lakni mpaka leo ameshindwa kuwafikisha mahakamani asilimia 90 ya watuhumiwa kwa kutumia endless investigation kama excuse ya kutowafikisha wahusika mahakamani.kwa kwa mtaji huu bwana hosea ameshindwa kuwa ni kiongozi effective kwahivyo inabidi AJIUZURU ili angalau kurudisha imani ya wananchi kwa chombo hiki ambacho mimi binafsi itanichukua muda mrefu sana kuanza tena kuwaamini.
 
Sorry wadau nilikuwa namaanisha hosea ndio inabidi ajiuzuru na chenge siyo tu ajiuzuru bali afunguliwe
mashitaka kwa kuhujumu uchumi na pia kumiliki account ya fedha za kigeni nje ya nchi bila kutoa taarifa bot.
 
Huyu Hosea anakinga ya Ikulu kama yule Mrema wa TANROADS.
Suluhisho la kudumu ni kuivunja TUKUKURU na kuwastaafisha maafisa watendaji wake wote.
 
Hebu tujaribu kuangalia hivi...kuwa Hosea ni kiongozi wetu wananchi....anatakiwa afanye kazi kwa ajili ya maslahi yetu...Sasa yeye anafanya kazi kwa maslahi ya nani?

Kwa sisi wananchi, twaona kuwa Hosea, hakututendea haki, ametudanganya...basi inabidi awajibike....AJIUZULU arudi kwao akaishi na familia yake....
 
Huyu Hosea anakinga ya Ikulu kama yule Mrema wa TANROADS.
Suluhisho la kudumu ni kuivunja TUKUKURU na kuwastaafisha maafisa watendaji wake wote.
Kabla ya kukurupuka kutoa post zenye harufu ya ush.uzi kama hii jiulize
1. Nani aivunje?
2. Kwa sheria ipi
3. Nani aunde mpya?
4. Hiyo mpya itaundwa kwa sheria ipi?
5. Sheria na Muundaji vitaweza kuifanya Takukuru iwe kama unavyohitaji?
 
Kabla ya kukurupuka kutoa post zenye harufu ya ush.uzi kama hii jiulize
1. Nani aivunje?
2. Kwa sheria ipi
3. Nani aunde mpya?
4. Hiyo mpya itaundwa kwa sheria ipi?
5. Sheria na Muundaji vitaweza kuifanya Takukuru iwe kama unavyohitaji?

What is your point brother?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom