Elections 2010 Chenge apata pigo jingine Nec

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Chenge apata pigo jingine NEC

Fredy Azzah


TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetoa ufafanuzi wa viti sita vinavyosubiri uchaguzi wa majimbo saba unaotarajiwa kufanyika Jumapili ijayo, huku majina ya wanawake na watoto wa vigogo yakiachwa.

Kwa mujibu wa Nec, viti hivyo vimegawanywa kwa vyama vitatu; CCM, Chadema na CUF kila chama kikipewa viti viwili na kwamba, hali hiyo inaweza kubadilishwa na tofauti ya kura za uchaguzi huo.

Kulingana na taarifa hiyo, CCM ina viti 67, Chadema 25 na CUF 10 na kuongeza kuwa, idadi ya wabunge wa viti maalum wa CUF iliyotangazwa juzi ilikosewa hivi sasa watapata viti vinane wakisubiri matokeo ya Jumapili.

Baadhi ya wanawake wa CCM ambao walipitishwa na orodha ya Nec imewatupa ni mke wa Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, Tinner, Kaslida Mgeni, Mboni Mhita na Janet Masaburi. Kwa mujibu wa Mwanasheria wa Nec, Venosa Mkwizu, kwa sasa CCM imepewa wabunge 65, Chadema 23 na CUF vinane, huku viti viwili kwa kila chama vikiachwa wazi kusubiri matokeo ya majimbo saba ambayo uchaguzi wake iliahirishwa kutokana na kasoro mbalimbali zilizokuwa kwenye karatasi za kupiga kura.

"Majina mawili kwa kila chama, hatujayatoa kwa sababu tunasubiri matokeo ya majimbo hayo, tumefanya hivyo kwa sababu inawezakana kura zikabadilisha hesabu zetu…lakini kama haitoathiri basi, kila chama kitapata hao wabunge niliowaambia," alisema Mkwizu. Wabunge kutoka CCM ambao wametangazwa na Nec ni Lucy Owenya, Esther Matiko, Muhonga Ruhwanya, Anna Mallac, Paulina Gekul na Conjesta Rwamlaza. Wengine ni Suzan Kiwanga, Grace Kiwelu, Suzan Lyimo, Regia Mtema, Christowaja Mtinda, Anna Komu, Mwanamrisho Abama, Joyce Mukya, Leticia Nyerere na Naomi Kaihula.

Majina mengine ni Chiku Abwao, Rose Kamili, Christina Lissu, Raya Ibrahim Hamis, Philipa Mturano, Mariam Msabaha na Rachel Mashishanga. Nec iliwataja wabunge wa CCM kuwa ni viongozi wakuu wawili wa Jumuiya ya Wanawake wa chama hicho (UWT), Sophia Simba na katibu wake, Amina Nassoro Makilagi. Wengine ni Gaudentia Mugosi Kabaka, Ummi Ally Mwalimu, Agnes Elias Hokororo, Martha Jachi Umbulla, Lucy Thomas Mayenga na Faida Mohamed Bakari.

Walioteuliwa wengine ni Felista Bura, Kidawa Hamid Saleh, Stellah Manyanya, Maria Hewa, Hilda Cynthia Ngoye, Josephine Genzabuke na Esther Midimu. Wengine ni Maida Hamad Abdallah, Asha Mshimba Jecha, Zarina Madabida, Namalok Edward Sokoine, Munde Tambwe Abdallah, Benardetha Mushashu, Vicky Kamata, Pindi Chana, Fatuma Mikidadi, Gertrude Rwakatare, Betty Machangu, Diana Chilolo, Fakharia Shomari Khamis, Zaynabu Vulu, Abia Muhama Nyabakari, Pudenciana Kikwembe na Lediana Mng'ong'o.

Wengine ni Sarah Msafiri, Catherine Magige, Ester Bulaya, Neema Hamid, Tauhida Cassian, Asha Mohamed Omari, Rita Mlaki, Anna Abdallah, Fenella Mukangara, Terezya Huvisa, Al-Shaymaa Kwegir na Margreth Mkanga. Angellah Kairuki, Zainab Kawawa, Mwanakhamis Kassim Said, Riziki Lulida, Devotha Likokola, Christina Ishengoma, Mariam Mfaki, Margreth Sitta, Subira Mgalu, Rita Kabati, Martha Mlata, Maua Daftari na Elizabeth Batenga. Wamo pia, Azza Hillal Hamad, Mary Mwanjelwa, Josephine Chengula, Bahati Ali Abeid, Kumbwa Makame Mbaraka, Rosweeter Kasikila, Anastazia Wambura na Mary Chatanda.
Chanzo: Mwananchi
 
Wabunge kutoka CCM ambao wametangazwa na Nec ni Lucy Owenya, Esther Matiko, Muhonga Ruhwanya, Anna Mallac, Paulina Gekul na Conjesta Rwamlaza. Wengine ni Suzan Kiwanga, Grace Kiwelu, Suzan Lyimo, Regia Mtema, Christowaja Mtinda, Anna Komu, Mwanamrisho Abama, Joyce Mukya, Leticia Nyerere na Naomi Kaihula.

Majina mengine ni Chiku Abwao, Rose Kamili, Christina Lissu, Raya Ibrahim Hamis, Philipa Mturano, Mariam Msabaha na Rachel Mashishanga. Nec iliwataja wabunge wa CCM kuwa ni viongozi wakuu wawili wa Jumuiya ya Wanawake wa chama hicho (UWT), Sophia Simba na katibu wake, Amina Nassoro Makilagi. Wengine ni Gaudentia Mugosi Kabaka, Ummi Ally Mwalimu, Agnes Elias Hokororo, Martha Jachi Umbulla, Lucy Thomas Mayenga na Faida Mohamed Bakari.

Walioteuliwa wengine ni Felista Bura, Kidawa Hamid Saleh, Stellah Manyanya, Maria Hewa, Hilda Cynthia Ngoye, Josephine Genzabuke na Esther Midimu. Wengine ni Maida Hamad Abdallah, Asha Mshimba Jecha, Zarina Madabida, Namalok Edward Sokoine, Munde Tambwe Abdallah, Benardetha Mushashu, Vicky Kamata, Pindi Chana, Fatuma Mikidadi, Gertrude Rwakatare, Betty Machangu, Diana Chilolo, Fakharia Shomari Khamis, Zaynabu Vulu, Abia Muhama Nyabakari, Pudenciana Kikwembe na Lediana Mng'ong'o.
Chanzo: Mwananchi
Nadhani mwandishi alikosea waiotajwa mwanzo sio kutoka CCM.
 
Tume ya Uchaguzi ya Taifa ni horrible - kwa maana hii kabla hata ya kura kupigwa na wananchi wao tayari wamekwisha panga matokeo. Kwa nini wasisubiri mpaka kura zihesabiwe na kuachana na ubashiri wao. Ni sawa na referee kutabiri mshindi wa mechi atakayochezesha yeye mwenyewe!
 
Back
Top Bottom