hello...wana jamvini.!! kuna huu ugonjwa unaitwa CHEMBE CHA MOYO. nimejaribu kuliza marafiki,ndugu na jamaa chanzo chake na jinsi ya kuutiibu.. wote wananipa njia za asili.
swali nililonalo, akuna njia za kisayansi za kutibu huu ugonjwa?? pia vitu gani vina sababisha??!.
naomba help...kuna friend wangu anasumbuliwa.
Mamndenyi, mmasai alitibu na ndoa? LOL!
Chembe ya moyo kwa haraka zaidi huwa inasababishwa na acid indigestion. Mie nilitumia omeprazole tabs for two months nikasahau hiyo habari. Nakushauri uende hosp kwa general physician, atakuangalia na kukushauri.
Wadau hivi majuzi nilishikwa na kama kichomi fulani hapa juu ya tumbo yani katikati ya tumbo na kifua sikulala kabisa usiku wake.
Sikuwahi kutokewa na hali hii hiyo ndiyo ilikua mara ya kwanza.
Hata hivyo sikuweza kwenda hospitali kwa sababu nilikua na safari ya muhimu sana. Nilijaribu kuwauliza watu mbali mbali wakawa wananiambia ni chembe ya moyo lakini mimi sijui chochote kuhusu hiyo chembe ya moyo yenyewe.
Naombeni msaada wenu wadau.
chembe ya moyo ni sharp pain chini ya sternum (hapo mbavu zinapoishia kuungana na tumbo kuanzia,panabonyezeka).inasababishwa na acid indigestion,ni kama dalili za mwanzo za ulcers. lakini kama maumivu ni chini ya titi la kushoto maybe uonane na daktari,inaweza kuwa shida ya moyo (broken heart hahaha)
Nina mdogo wangu anasumbuliwa na kitu ambacho nimeelezwa kuwa ni chembe ya moyo.Anajisikia kubanwa sehemu ya kifua kinapoishia na tumbo linapo anzia kushuka chini kwenye chembe ya moyo.sana sana sehemu hiyo huanza kubana pale anapo chelewa kula.ninaomba msaada wenu tafadhari.
mnaishi wapi?
inabidi mwende hosp. vigumu kujua kama ni tumbo au moyo, maelezo yako hayatoselezi na huyomdogo wako hajulikani umri wake!!!!h