Chekechea graduation

Natty Bongoman

JF-Expert Member
Oct 10, 2008
403
191
Ni siku ya mwisho kwa watoto wa chekechea moja. Watoto walimletea mwalimu wao zawadi...

Mtoto wa muuza maua akampa kajibunda:
Mwalimu (akitabasamu): "Aaahsante! Mie nahisi, umineletea maua"
Mtoto akishangaa: "We umejuaje?"
Mwalimu (bado akitabasamu): "Aaah, nimebahatisha tu."

Kisha, Mtoto wa muuza mapombe (makonyagi na mawhisky) akampa kajibunda. Hicho kibunda kilikua kinavuja kidogo. Mwalimu naye akagusa mvujo, na akanyonya kidole chake akionja…

Mwalimu (akitabasamu): "Aaahsante! Hivi umineletea mvinyo?"
Mwanafunzi (akisisimka): "Hapana"
Mwalimu naye akarudia kuonja tena… :
Mwalimu: "Haya sasa mie nimeshindwa kubunia, hebu niambie ulichoneletea."
Mwanafunzi (msisimko ukimfanya aruke-ruke): "Chiboa! Mtoto wa mbwa wetu."
 
Natty_Bongoman
Teh teh teh Ina maana yale majimaji niliyolamba nimkonyagi ama Chiboa alikuwa amerekebisha mambo?
 
Duh, huyo teacher alikuwa mlevi kweli! Yaani hata harufu ya mkojo wa mbwa kashindwa kuing'amua? Au alidhani ni harufu ya aina mpya ya mvinyo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom