Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,291
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute
Jamaa kaamka asubuhi kajikuta kageuka mdudu. Hii hapa simulizi yake, Die Verwandlung, imefasiriwa kwa Kiswahili. Ilichapishwa kwa Kijeremani mwaka 1915, mwandishi akiwa Franz Kafka.
Asubuhi fulani, wakati Grego Samsa akiamka toka kwenye ndoto za kutisha, alibaini kwamba hapohapo kitandani alipo, amekwisha kubadilishwa kuwa lidudu kubwa, baya.
Alilalia mgongo wake mgumu mithili ya deraya, akiinua kidogo kichwa chake, tumbo lake la kahawia, likijigawa vipandevipande kuwa visehemu mithili ya pinde. Kutoka urefu huu liliko blanketi, likiwa karibia kabisa kudondoka toka mwilini mwake, alipata shida kubakia alipo. Miguu yake mingi, myembamba vya kusikitisha ukilinganisha na mzingo wa mwili wake, ilijitikisa huku na kule akiitizama.
“Kimenisibu nini,” aliwaza. Haikuwa ndoto. Chumba chake, chumba hasa kwa ajili ya binadamu, japo kidogo sana, kilitulia baina ya kuta nne alizozifahamu vyema. Juu ya meza, ambako kulikuwa na rundo la bidhaa za nguo (Samsa alikuwa ni mfanyabiashara asafiriye) palining’inia picha ambayo alikuwa ameikata toka kwenye jarida la mapicha muda mchache uliokuwa umepita na kuwekwa kwenye fremu ya rangi ya dhahabu. Ilikuwa ni picha ya mwanamke mmoja aliyevaa kofia ya ngozi na kitambaa kizito cha kufunika shingo. Alikaa wima, akiinua uelekeo wa mtazamaji ngozi yenye manyoya mazito ambamo mkono wake wote ulikuwa umezama.
Kisha macho ya Grego yakaelekea dirishani. Hali ya hewa ilikuwa mbaya (matone ya mvua yalidondokea kingo za dirisha kwa kelele) ilimfanya ajihisi ni mwenye huzuni. “Kwa nini silali kwa muda mwingine wa ziada kidogo na kusahau wehu huu wote,” aliwaza. Lakini hili lilikuwa haliwezekani aslani, kwa vile alikuwa na mazoea ya kulalia upande wake wa kulia, na kwa hali yake ya sasa hangeweza kujigeuzia upande wake wa kulia. Hata alipojirusha kwa nguvu zake zote ageukie upande wa kulia, mara zote aliviringika na kurudi chali.
INAENDELEA
Jamaa kaamka asubuhi kajikuta kageuka mdudu. Hii hapa simulizi yake, Die Verwandlung, imefasiriwa kwa Kiswahili. Ilichapishwa kwa Kijeremani mwaka 1915, mwandishi akiwa Franz Kafka.
Asubuhi fulani, wakati Grego Samsa akiamka toka kwenye ndoto za kutisha, alibaini kwamba hapohapo kitandani alipo, amekwisha kubadilishwa kuwa lidudu kubwa, baya.
Alilalia mgongo wake mgumu mithili ya deraya, akiinua kidogo kichwa chake, tumbo lake la kahawia, likijigawa vipandevipande kuwa visehemu mithili ya pinde. Kutoka urefu huu liliko blanketi, likiwa karibia kabisa kudondoka toka mwilini mwake, alipata shida kubakia alipo. Miguu yake mingi, myembamba vya kusikitisha ukilinganisha na mzingo wa mwili wake, ilijitikisa huku na kule akiitizama.
“Kimenisibu nini,” aliwaza. Haikuwa ndoto. Chumba chake, chumba hasa kwa ajili ya binadamu, japo kidogo sana, kilitulia baina ya kuta nne alizozifahamu vyema. Juu ya meza, ambako kulikuwa na rundo la bidhaa za nguo (Samsa alikuwa ni mfanyabiashara asafiriye) palining’inia picha ambayo alikuwa ameikata toka kwenye jarida la mapicha muda mchache uliokuwa umepita na kuwekwa kwenye fremu ya rangi ya dhahabu. Ilikuwa ni picha ya mwanamke mmoja aliyevaa kofia ya ngozi na kitambaa kizito cha kufunika shingo. Alikaa wima, akiinua uelekeo wa mtazamaji ngozi yenye manyoya mazito ambamo mkono wake wote ulikuwa umezama.
Kisha macho ya Grego yakaelekea dirishani. Hali ya hewa ilikuwa mbaya (matone ya mvua yalidondokea kingo za dirisha kwa kelele) ilimfanya ajihisi ni mwenye huzuni. “Kwa nini silali kwa muda mwingine wa ziada kidogo na kusahau wehu huu wote,” aliwaza. Lakini hili lilikuwa haliwezekani aslani, kwa vile alikuwa na mazoea ya kulalia upande wake wa kulia, na kwa hali yake ya sasa hangeweza kujigeuzia upande wake wa kulia. Hata alipojirusha kwa nguvu zake zote ageukie upande wa kulia, mara zote aliviringika na kurudi chali.
INAENDELEA