Katika hali yenye kutia mashaka,
Yamekuwepo maelekezo makali juu ya ununuzi wa Vifaa vya ujenzi (TOFALI)sehemu moja ambayo ni kwa mzabuni mmoja aitwaye RWAIKONDO,
huyu jamaa ndio anakula na hawa vigogo wa wilaya,
Mbali na kuwepo wazabuni wengi ambao wapo jiran kabisa na shule nyingi yanapojengwa madarasa bado wamebanwa wasitoe huduma pamoja na kulipa kodi serikalini na ni watanzania.
Cha kushangaza hadi sasa tenda imeshamuelemea,
Tofali hamna site, mafundi wanasubiri hadi siku 5, na zikifika zinakuwa mbichi, zinavunjika tu.
Pili kwa sasa yametolewa maelekezo ya kwamba mabati, madirisha ya aluminium, mbao, rangi
Vitaletwa toka kwa mzabuni mmoja ambaye vigogo wa wilayan tayari wameshapanga ulaji wao kwa ununuzi wa Vifaa hivyo wilaya nzima, uroho wa namna hii ni hatari.
Nini maana ya kuwepo kamati za ujenzi mashuleni,
Nini maana ya pesa kuelekezwa mashuleni moja kwa moja. (Hapa mwendazake alijua huu upigaji)
IKUMBUKWE: Ni majuzi tu TAKUKURU walifanya kazi nzuri ya kuwadhibiti MKURUGENZI H/WILAYA YA CHATO NA MAAFISA ELIMU ambapo walikula njama na kuagiza mabati feki geji 30 badala ya geji 28 yaliyotakiwa kusambazwa kwenye ujenzi wa madarasa, vituo vya zahanati nk.
Bahati nzuri wote hawapo kwa sasa.
Nitoe rai yangu kwa serikali,
Kwa kuwa tupo kwenye soko huria,
Pesa za serikali zinapotolewa wafanyabiashara wote wenye vigezo wapewe fursa sawa ya kutoa huduma sio kuwabeba wale waliotoa rushwa tu kwa vigogo.
Mwisho naomba mamlaka zinazohusika kuanzia TAKUKURU, nk wafanyie kazi maelezo hayo kwa ujenzi wa TANZANIA BORA.
Yamekuwepo maelekezo makali juu ya ununuzi wa Vifaa vya ujenzi (TOFALI)sehemu moja ambayo ni kwa mzabuni mmoja aitwaye RWAIKONDO,
huyu jamaa ndio anakula na hawa vigogo wa wilaya,
Mbali na kuwepo wazabuni wengi ambao wapo jiran kabisa na shule nyingi yanapojengwa madarasa bado wamebanwa wasitoe huduma pamoja na kulipa kodi serikalini na ni watanzania.
Cha kushangaza hadi sasa tenda imeshamuelemea,
Tofali hamna site, mafundi wanasubiri hadi siku 5, na zikifika zinakuwa mbichi, zinavunjika tu.
Pili kwa sasa yametolewa maelekezo ya kwamba mabati, madirisha ya aluminium, mbao, rangi
Vitaletwa toka kwa mzabuni mmoja ambaye vigogo wa wilayan tayari wameshapanga ulaji wao kwa ununuzi wa Vifaa hivyo wilaya nzima, uroho wa namna hii ni hatari.
Nini maana ya kuwepo kamati za ujenzi mashuleni,
Nini maana ya pesa kuelekezwa mashuleni moja kwa moja. (Hapa mwendazake alijua huu upigaji)
IKUMBUKWE: Ni majuzi tu TAKUKURU walifanya kazi nzuri ya kuwadhibiti MKURUGENZI H/WILAYA YA CHATO NA MAAFISA ELIMU ambapo walikula njama na kuagiza mabati feki geji 30 badala ya geji 28 yaliyotakiwa kusambazwa kwenye ujenzi wa madarasa, vituo vya zahanati nk.
Bahati nzuri wote hawapo kwa sasa.
Nitoe rai yangu kwa serikali,
Kwa kuwa tupo kwenye soko huria,
Pesa za serikali zinapotolewa wafanyabiashara wote wenye vigezo wapewe fursa sawa ya kutoa huduma sio kuwabeba wale waliotoa rushwa tu kwa vigogo.
Mwisho naomba mamlaka zinazohusika kuanzia TAKUKURU, nk wafanyie kazi maelezo hayo kwa ujenzi wa TANZANIA BORA.