CHATO tena Vita ya kibiashara na Muleba

KHALFANI 86

Member
May 16, 2020
14
24
Halmashauri ya Wilaya ya Chato kwa hiki kinachoendelea sasa ni unyanyasaji wa wazi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba. Hii kunyatia kulipora soko la Magarini kwa mazao ya Ziwani na kutaka soko hilo liende Muganza ni mabavu ambayo hayana maana kwa sasa. Sifa za kulipora soko hilo hakuna kwa Chato na wanaojaribu hawafikirii hata uwiano wa vyanzo katika maeneo hayo mawili.

Halmashauri ya Wilaya Muleba wanazo kata 5 majini na kata hizo ndio mtaji wa kuendesha soko hilo la Magarini na kuikuza Bandari hiyo ya Magarini. Lakini Chato wao wanayo kata moja tu nayo ni Rubondo iliyoko kwenye hifadhi ambako hawatakiwi kuvuna chochote. Sasa jeuri ya kulazimisha soko kuwa Muganza wanaipata wapi?

Ipo haja ya kukataa hizi mambo waziwazi .hatuwezi kukubali huu uporaji wa Soko la kibiashara hasa kuporwa na watu ambao hawana sifa za kuwa na soko hilo. Muleba ina kila sababu kutokana na kuwa inazo kata tano majini na visiwa visivyo pungua 30.

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba wanatakiwa kuamka na kupambana vilivyo ili kuhakikisha walio na hila na Soko hilo la Magarini wanashindwa mapema sana na hila zao. Hili Soko la Magarini ndio chanzo kikubwa kwa sasa cha Halmashauri ya Wilaya ya Muleba. Chato watulie kwanza

Kata ambazo zinaibeba Muleba iendelee kuwa imara na kuendesha Bandari ya Magarini ni 5 nazo ni
1.Kata Ikuza
2.Kata Mazinga
3.Kata Bumbile
4.Kata Kerebe
5.Kata Goziba .
 
Hujaeleweka kupora soko kivipi?
Kuna Soko liko Magarini ambalo liko Wilaya ya Muleba, sasa Chato wanalifanyia fugisu lifungwe lwa lengo la kutumia soko la Muganza ambayo iko chato . Huo ndio uporaji wenyewe na hali Wao hawana nguvu kubwa kama ilivyo Muleba
 
Awamu ya Giza chato ilikuwa midomoni mwa watu ikizungumzwa kila siku kwa upendeleo wa wazi,kupelekewa vitu ambavyo haistahili.
Watu walivumilia sababu walikuwa hawana namna mana wenye mamlaka walilazimisha.
Sasa hadi kipindi hichi ambacho haki,uhuru na demokrasia vimetamalaki bado mnalia lia tu kwa kuonewa?
Mtakuwa wajinga sana kama mtaruhusu na hilo litokee.haki haiombwi bali inapiganiwa.
 
Awamu ya Giza chato ilikuwa midomoni mwa watu ikizungumzwa kila siku kwa upendeleo wa wazi,kupelekewa vitu ambavyo haistahili.
Watu walivumilia sababu walikuwa hawana namna mana wenye mamlaka walilazimisha.
Sasa hadi kipindi hichi ambacho haki,uhuru na demokrasia vimetamalaki bado mnalia lia tu kwa kuonewa?
Mtakuwa wajinga sana kama mtaruhusu na hilo litokee.haki haiombwi bali inapiganiwa.
Umeongea kama inavyotakiwa iwe hakuna kupelekeshwa pelekeshwa hata kwa mambo yasiyowezekana
 
Isijekuwa ni CCM Wilaya ya Muleba imeuza bandari kwa CCM Wilaya ya Chato
 
Kuna Soko liko Magarini ambalo liko Wilaya ya Muleba, sasa Chato wanalifanyia fugisu lifungwe lwa lengo la kutumia soko la Muganza ambayo iko chato . Huo ndio uporaji wenyewe na hali Wao hawana nguvu kubwa kama ilivyo Muleba
Ninachojua muganza Kuna soko kuu la kimataifa la mazao ya ziwani.
Ila pia ni mpango wa muda mrefu. So kabla hujaanza uchonganishi ujue kwanza utaratibu wa serikali na mipango yake.
 
Back
Top Bottom