CHATO: Mwanafunzi kufanya mitihani 9 kwa siku moja. Je, Shule ya sekondari Mujumuzi- ina mamlaka?

Tetra

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
1,520
764
Wanajamii, hii imekaaje?

Leo nimepigiwa simu na jamaa yangu yupo Chato, amekuta wanafunzi wa shule ya sekondari Mujumuzi (ya binafsi) wameandamana barabarani wakidai baadhi walimu wao kurudishwa kazini baada ya walimu hao kupinga utaratibu wa shule hiyo kuwafanyisha mitihani 9 kwa siku moja.

Yaani kuanzia saa tisa usiku hadi saa tano usiku. Wakati mwingine bila ratiba! Jamani hizi private schools zina nguvu kubwa hivo? Hivi kitaaluma inakubalika kweli?
 
Wanajamii, hii imekaaje?

Leo nimepigiwa simu na jamaa yangu yupo Chato, amekuta wanafunzi wa shule ya sekondari Mujumuzi (ya binafsi) wameandamana barabarani wakidai baadhi walimu wao kurudishwa kazini baada ya walimu hao kupinga utaratibu wa shule hiyo kuwafanyisha mitihani 9 kwa siku moja.

Yaani kuanzia saa tisa usiku hadi saa tano usiku. Wakati mwingine bila ratiba! Jamani hizi private schools zina nguvu kubwa hivo? Hivi kitaaluma inakubalika kweli?
Mmiliki wa shule ni nani?
Au ni kutoka familia ya yacobo wa agono jipya
 
Mwalimu mkuu ana Uhuru wa kuendesha shule atakavyo ili mradi havunji sheria za nchi, Ndio maana kabla hujachagua shule unasoma vigezo na masharti, ukikubaliana Ndio unajiunga.
Kisaikolojia sio vizuri lakini bado Kama Ni kuanzia saa 9usiku Hadi saa 5 asubuhi bado unaweza kukomaa, sidhani Kama mitihani Ni ya masaa 3,zitakuwa test tu za muda mfupi, Kuna tofauti kubwa Kati ya mtihani na jaribio. Hao watakuwa wanafanya majaribio tu.
 
Mzigo mzito mpe msukuma, huko chato kuna wasukuma wengi, haina shida
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom