Chato: Msanii wa nyimbo za asili aliyemtumkana Rais Samia ahukumiwa miaka 6 jela

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Jul 21, 2021
1,125
4,168
Msanii wa Nyimbo za asili ya Kisukuma, Dawa Juma mkazi wa Kijiji cha Makurugusi wilayani Chato mkoani Geita, amehukumiwa kifungo cha miaka sita jela au kulipa faini ya Tsh. Milioni 10 baada ya kupatikana na hatia ya kumtukana rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa mahakama ya wilaya Chato, Amalia Mushi, baada ya mshitakiwa kukiri kosa mbele ya mahakama hiyo.

Awali mwendesha mashitaka wakili mwandamizi wa serikali, Robert Magige, ameiambia mahakama hiyo kuwa mshitakiwa alitunga wimbo wenye lengo la kumtukana matusi rais Samia Suluhu Hassan, licha ya kujua wazi kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Amesema akiwa na nia ovu alirekodi wimbo huo na kuusambaza kwenye mitandao ya kijamii ili kupeleka ujumbe wake kwa umma huku akijinadi kuwa haogopi kukamatwa.

Mwendesha mashitaka huyo, amesema kitendo cha kuchapisha taarifa za uongo na matusi kisha kuyasambaza kwenye mitandao ya kijamii (You tube) ni kinyume na kifungu cha 16 cha sheria ya makosa ya mtandao,sheria namba 14 ya mwaka 2015.

Hata hivyo mshitakiwa baada ya kusomewa mashitaka yanayo mkabili amekiri kutenda kosa hilo, licha ya kudai kuwa hakuwa na nia mbaya kwa kuwa alikusudia kuonyesha hali ilivyo mbaya kwa jamii baada ya bidhaa kupanda bei.

Aidha baada ya mshitakiwa kukiri kosa, wakiri wa serikali Magige ameiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye lengo la kumtukana rais kutokana na sababu zao binafsi.

Akitoa hukumu, Hakimu wa mahakama hiyo, amedai kuwa kwa kuzingatia kuwa mshitakiwa hakuisumbua mahakama hiyo, kwa kukiri kosa kwa kinywa chake mwenyewe mahakama inamhukumu kifungo cha miaka sita jela au kulipa faini ya shilingi milioni 10.

Hata hivyo mshitakiwa amepelekwa gerezani kuanza kutumikia kifungo chake baada ya kushindwa kulipa faini iliyoelekezwa na mahakama hiyo

Chanzo: Dima Online

=======

Wimbo huo kwa tafsiri ya Kiswahili;

Dawa Dawa

Ubeti wa 1
Leo naongea na Rais mwenye ushungi, Kwanini huvui ushungi?
Au Kichwa chako kina mapunye? Tuambie
Bei ya mafuta ya Kula imepanda, sabuni za kufulia nazo zimepanda bei
Niuze Mkaa nikamatwe, Rais gani huyu Watanzania? Au kwa kuwa hatukumchagua?

Urais kaupata kwa kurithi, punguza bei ya sabuni
Bora Magufuli, alikuwa anatutetea Wanyonge
Tunaomba Rais upunguze bei ya mafuta tuanze hata kununua ya Tsh 100/= na sabuni irudi kwenye bei yake ya Tsh. 300/=
Mimi naitwa Dawa, siogopi kumsema Rais

We Rais wetu ni Mshamba, mwaka kesho hatukuchagui
Umedharauliwa hadi na wanawake kwa sababu umepandisha bei ya bidhaa
Nimeona pia kwa vijana, tusikae tu vijiweni, tukubali kushinda mashambani, tusiombe ombe misaada
Urithi wa mashamba utaendelea kutumaliza

Ubeti wa 2
Muhudumu tupe pombe, pombe pombe bia tamu, wanawake ni watamu, yaani tamu tamu tamuuu
Mke wangu tukilala, yaani nipe ile tamu
Sasa narudi kwenu wasanii, mnaojiita wasanii wakubwa
Mnatuona sisi kama wadogo kama sio wasanii vile
Eleweni sasa kwamba na sisi ni watu, ipo siku tutajulikana pia
Mnajidai sana kwa kuwa ninyi ni wasanii wakubwa, tutambueni na sisi

Bei ya mafuta ya kula imepanda, sabuni za kufulia nazo zimepanda bei
Niuze mkaa nikamatwe, Rais gani huyu Watanzania? Au kwa kuwa hatukumchagua?
Urais kaupata kwa kurithi, punguza bei ya sabuni
Bora Magufuli, alikuwa anatutetea Wanyonge

Ubeti wa 3
Mimi nimeanza kuja kitofauti, wala msiulize huyu anaimbaje
Wengine wanahoji, hivi huyu dawa ana akili kweli?
Mi nawajibu sina akili, nina nyimbo tu
Chuchumaa chuchumaa
Halafu wasanii wengine wanashinda siku nzima pasipo hata kusikilizwa wimbo mmoja, lakini kazi yao kubwa kujisifu

Wasanii imbeni nyimbo za kuelimisha
Msiwe kama Msanii Madaso wa Chato anayenuka, kila alikoenda kuimba alikuwa anaiba wake za watu,
Inakuwaje watu wanakushabikia lakini wewe unaiba wake zao?
Ndio maana hata usanii wake umekufa, mimi namueleza ukweli
Sasa tambueni dawa kali nimeanza kuimba japo sikuwa msanii mwanzo
Mashabiki wangu endeeleni kunisikiliza mimi msanii wenu dawa
Nipo tayari kuwatetea ndugu zangu maana mnahangaika mno

Ubeti wa 4
Leo nimekuja kuzungumza na Rais Samia, huyo mwenye ushungi
Jamani ndugu zangu tunateswa mno, watu wanaokata mkaa wanakamatwa ovyo mno
Ukiwaza hao askari wanaowakatama wanaupeleka wapi huo mkaa, ni uonevu tu
Nimechunguza nikabaini na wao huwa wanaenda kuuza huo mkaa
Sasa huo sio uonevu?

Wewe Rais mwenye mashavu yako wewe
Niite dawa kali mimi huwa situkani mtu asiye na hatia
Naongea mambo ya kweli
Simuogopi Rais, kama mnaweza njooni mnikamate lakini tayari nimeshazungumza ukweli
Dawa kali mwenyewe mimi ni jeshi, tembea

Ubeti wa 5
Maisha yamekuwa magumu mno, sisi tusio na kazi tulidhani kaja mwanamke atatutetea
Kumbe ni ovyo tu, msimbe huyu
Magufuli alipokufa haikupita hata wiki, ndege 3 zilipotea
Ndege hizo ilitambulika kazipoteza Mkuu wa Majeshi
Ulitaka uzipeleke wapi, wewe mvaa ushungi nakuuliza, nijibu

Yaani tangu uingie madarakani hata mwaka haujamaliza unaiba ndege?
Ulikuwa unazipeleka wapi? Au hakuwahi kupanda ndege kabla?
Nipo radhi kutetea raia wanaoteseka, kuliko kumtetea Rais mwenye ushungi anayetutesa vibaya
Hela zimekuwa ngumu mpaka dada zetu wanajiuza
Wanajiuza sababu ya ugumu wa Maisha, kwani kama hela zinamwagika nani atajiuza?

Ubeti wa Mwisho
DJ simamisha niongee na Mhe. Rais Samia, mbona Mhe. Samia vitu vimepanda bei?
Nataka uniambie ukweli mimi dawa
Au unataka ututoe kafara?

(HAPA SAUTI YA SAMIA INACHEZWA YENYE MANENO YA “WEWE NI KIJANA MIMI NI MAMA, UKINIZINGUA TUTAZINGUANA”)

Huu ndio ujinga sasa ambao mimi naukataa, nakuambia ushushe bei lakini wewe unasema mambo ya kuzinguana?
Hatuogopi kusema sababu hata kura tunapiga sisi, sasa tuogope nini?
Bila sisi utaweza kukalia kiti cha Urais?
Sema sasa wewe mtu mwenye mashavu makubwa, nakuuliza
Siimbi kwa kujificha kwamba nitakamatwa, nikamatwe vipi?
Shusha bei ya mafuta ya kula tupate hata ya Tsh 100/-
Bei ya sabuni irudi kwenye Tsh. 200/-

Hii ndio Audio ya wimbo.

 
Kule ufaransa jamaa alimtandika macron kofi la aina ya UTANITAMBUA na akafungwa miaka 3

nyie tusi hilo miaka 6

KUNA HAJA YA KATIBA MPYA KUONDOA SHERIA KANDAMIZI, RAISI WA TANZANIA NI MUNGU WA PILI KWA KATIBA HII

nawaza kama Jamaa angemtandika kofi samia si angeuuawa
 
Duh...

Sasa hii poor soul ni ya kufunga jela kweli?
Wimbo wenyewe wa kilugha

wanampa kijana ummarufu asiostahili.

Kutukana mtu Tanzania ni kosa kisheria na unafungwa jela?

Dear Madam president, hawa watu ni wakusamehe bure....
 
Back
Top Bottom